< Hesabu 25 >

1 Israeli alipokuwa akikaa Shitimu, wanaume wa Israeli walianza kuzini na wanawake wa Kimoabu,
Or, en ce temps-là Israël demeurait à Settim, et le peuple forniqua avec les filles de Moab,
2 ambao waliwaalika kushiriki katika kutoa kafara kwa miungu yao. Watu wakala na kusujudu mbele ya miungu hii.
Qui les appelèrent à leurs sacrifices; et eux en mangèrent et ils adorèrent leurs dieux,
3 Kwa hiyo Israeli akaungana katika kumwabudu Baali wa Peori. Hasira ya Bwana ikawaka dhidi yao.
Et Israël fut initié au culte de Béelphégor; et le Seigneur irrité,
4 Bwana akamwambia Mose, “Uwachukue viongozi wote wa watu hawa, uwaue na uwaweke hadharani mchana peupe mbele za Bwana, ili hasira kali ya Bwana iweze kuondoka kwa Israeli.”
Dit à Moïse: Prends tous les princes du peuple, et suspends-les à des potences à la face du soleil, afin que ma fureur se détourne d’Israël.
5 Kwa hiyo Mose akawaambia waamuzi wa Israeli, “Kila mmoja wenu lazima awaue wale wanaume wenu, walioshiriki katika kumwabudu Baali wa Peori.”
Moïse dit donc aux juges d’Israël: Que chacun tue ses proches, qui ont été initiés au culte de Béelphégor.
6 Ndipo mwanaume wa Kiisraeli akamleta mwanamke wa Kimidiani katika jamaa yake palepale mbele ya Mose na mkutano wote wa Israeli walipokuwa wakilia kwenye lango la Hema la Kukutania.
Et voilà qu’un des enfants d’Israël entra devant ses frères chez une prostituée madianite, Moïse le voyant, ainsi que toute la multitude des enfants d’Israël, qui pleuraient devant la porte du tabernacle.
7 Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, alipoona jambo hili, akaondoka kwenye kusanyiko, akachukua mkuki mkononi mwake,
Ce qu’ayant vu Phinéès, fils d’Eléazar, fils d’Aaron, le prêtre, il se leva du milieu de la multitude, et, un poignard pris,
8 akamfuata yule Mwisraeli ndani ya hema. Akawachoma mkuki wote wawili kwa pamoja, ukapenya kwenye mwili wa yule Mwisraeli na mwili wa yule mwanamke. Ndipo tauni iliyokuwepo dhidi ya Waisraeli ikakoma.
Il entra après l’Israélite, dans la tente de prostitution, perça tous deux, c’est-à-dire l’homme et la femme dans les parties secrètes: et la plaie fut détournée des enfants d’Israël;
9 Lakini wale waliokufa kwa hiyo tauni walikuwa watu 24,000.
Or, vingt-quatre mille hommes furent tués.
10 Bwana akamwambia Mose,
Et le Seigneur dit à Moïse:
11 “Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, amegeuza hasira yangu mbali na Waisraeli, kwa sababu alikuwa na wivu kama nilio nao kwa heshima yangu miongoni mwao, hata kwamba kwa wivu wangu sikuwaangamiza.
Phinéès, fils d’Eléazar, fils d’Aaron, le prêtre, a détourné ma colère des enfants d’Israël, parce qu’il a été animé de mon zèle contre eux, afin que moi-même je ne détruisisse point les enfants d’Israël dans mon zèle.
12 Kwa hiyo mwambie Finehasi ninafanya Agano langu la amani naye.
C’est pourquoi dis-lui: Voici que je lui donne la paix de mon alliance;
13 Yeye pamoja na wazao wake watakuwa na Agano la ukuhani milele, kwa sababu alikuwa na wivu kwa ajili ya heshima ya Mungu wake, na akafanya upatanisho kwa Waisraeli.”
Et ce sera tant pour lui que pour sa postérité un pacte perpétuel de sacerdoce, parce qu’il a été zélé pour son Dieu, et qu’il a expié le crime des enfants d’Israël.
14 Jina la Mwisraeli ambaye aliuawa pamoja na mwanamke wa Kimidiani ni Zimri mwana wa Salu, kiongozi wa jamaa ya Simeoni.
Or le nom de l’homme Israélite, qui fut tué avec la Madianite, était Zambri, fils de Salu, chef de la parenté et de la tribu de Siméon.
15 Jina la mwanamke wa Kimidiani aliyeuawa ni Kozbi binti wa Suri, aliyekuwa mkuu wa kabila la jamaa ya Wamidiani.
Et la femme madianite qui pareillement fut tuée, s’appelait Cozbi, fille de Sur, prince très noble des Madianites.
16 Bwana akamwambia Mose,
Le Seigneur parla encore à Moïse, disant:
17 “Watendeeni Wamidiani kama adui na mwaue,
Que les Madianites sentent que vous êtes leurs ennemis, et frappez-les,
18 kwa sababu wao waliwatendea kama adui wakati waliwadanganya katika tukio la Peori na dada yao Kozbi, binti wa kiongozi wa Kimidiani, mwanamke ambaye aliuawa wakati tauni ilikuja kama matokeo ya tukio la Peori.”
Parce qu’eux-mêmes aussi vous ont traités hostilement, et vous ont trompés insidieusement par l’idole de Phogor, et par Cozbi, fille du chef de Madian, leur sœur, qui fut frappée au jour de la plaie, à cause du sacrilège de Phogor.

< Hesabu 25 >