< Hesabu 25 >

1 Israeli alipokuwa akikaa Shitimu, wanaume wa Israeli walianza kuzini na wanawake wa Kimoabu,
Alors Israël demeurait en Sittim, et le peuple commença à paillarder avec les filles de Moab.
2 ambao waliwaalika kushiriki katika kutoa kafara kwa miungu yao. Watu wakala na kusujudu mbele ya miungu hii.
Car elles convièrent le peuple aux sacrifices de leurs dieux, et le peuple y mangea, et se prosterna devant leurs dieux.
3 Kwa hiyo Israeli akaungana katika kumwabudu Baali wa Peori. Hasira ya Bwana ikawaka dhidi yao.
Et Israël s'accoupla à Bahal-Péhor; c'est pourquoi la colère de l'Eternel s'enflamma contre Israël.
4 Bwana akamwambia Mose, “Uwachukue viongozi wote wa watu hawa, uwaue na uwaweke hadharani mchana peupe mbele za Bwana, ili hasira kali ya Bwana iweze kuondoka kwa Israeli.”
Et l'Eternel dit à Moïse: Prends tous les chefs du peuple, et les fais pendre devant l'Eternel au soleil, et l'ardeur de la colère de l'Eternel se détournera d'Israël.
5 Kwa hiyo Mose akawaambia waamuzi wa Israeli, “Kila mmoja wenu lazima awaue wale wanaume wenu, walioshiriki katika kumwabudu Baali wa Peori.”
Moïse donc dit aux juges d'Israël: Que chacun de vous fasse mourir les hommes qui sont à sa charge, lesquels se sont joints à Bahal-Péhor.
6 Ndipo mwanaume wa Kiisraeli akamleta mwanamke wa Kimidiani katika jamaa yake palepale mbele ya Mose na mkutano wote wa Israeli walipokuwa wakilia kwenye lango la Hema la Kukutania.
Et voici, un homme des enfants d'Israël vint, et amena à ses frères une Madianite, devant Moïse et devant toute l'assemblée des enfants d'Israël, comme ils pleuraient à la porte du Tabernacle d'assignation.
7 Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, alipoona jambo hili, akaondoka kwenye kusanyiko, akachukua mkuki mkononi mwake,
Ce que Phinées, fils d'Eléazar, fils d'Aaron le Sacrificateur ayant vu, il se leva du milieu de l'assemblée, et prit une javeline en sa main.
8 akamfuata yule Mwisraeli ndani ya hema. Akawachoma mkuki wote wawili kwa pamoja, ukapenya kwenye mwili wa yule Mwisraeli na mwili wa yule mwanamke. Ndipo tauni iliyokuwepo dhidi ya Waisraeli ikakoma.
Et il entra vers l'homme Israélite dans la tente, et les transperça tous deux par le ventre, l'homme Israélite et la femme; et la plaie fut arrêtée de dessus les enfants d'Israël.
9 Lakini wale waliokufa kwa hiyo tauni walikuwa watu 24,000.
Or il y en eut vingt-quatre mille qui moururent de cette plaie.
10 Bwana akamwambia Mose,
Et l'Eternel parla à Moïse, en disant:
11 “Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, amegeuza hasira yangu mbali na Waisraeli, kwa sababu alikuwa na wivu kama nilio nao kwa heshima yangu miongoni mwao, hata kwamba kwa wivu wangu sikuwaangamiza.
Phinées, fils d'Eléazar, fils d'Aaron, le Sacrificateur, a détourné ma colère de dessus les enfants d'Israël, parce qu'il a été animé de mon zèle au milieu d'eux, et je n'ai point consumé les enfants d'Israël par mon ardeur.
12 Kwa hiyo mwambie Finehasi ninafanya Agano langu la amani naye.
C'est pourquoi, dis-lui: Voici, je lui donne mon alliance de paix.
13 Yeye pamoja na wazao wake watakuwa na Agano la ukuhani milele, kwa sababu alikuwa na wivu kwa ajili ya heshima ya Mungu wake, na akafanya upatanisho kwa Waisraeli.”
Et l'alliance de Sacrificature perpétuelle sera tant pour lui, que pour sa postérité après lui, parce qu'il a été animé de zèle pour son Dieu, et qu'il a fait propitiation pour les enfants d'Israël.
14 Jina la Mwisraeli ambaye aliuawa pamoja na mwanamke wa Kimidiani ni Zimri mwana wa Salu, kiongozi wa jamaa ya Simeoni.
Et le nom de l'homme Israélite tué, lequel fut tué avec la Madianite, était Zimri, fils de Salu, chef d'une maison de père des Siméonites.
15 Jina la mwanamke wa Kimidiani aliyeuawa ni Kozbi binti wa Suri, aliyekuwa mkuu wa kabila la jamaa ya Wamidiani.
Et le nom de la femme Madianite qui fut tuée était Cozbi, fille de Tsur, chef du peuple, et de maison de père en Madian.
16 Bwana akamwambia Mose,
L'Eternel parla aussi à Moïse, en disant:
17 “Watendeeni Wamidiani kama adui na mwaue,
Serrez de près les Madianites, et les frappez.
18 kwa sababu wao waliwatendea kama adui wakati waliwadanganya katika tukio la Peori na dada yao Kozbi, binti wa kiongozi wa Kimidiani, mwanamke ambaye aliuawa wakati tauni ilikuja kama matokeo ya tukio la Peori.”
Car ils vous ont serrés [les premiers] par leurs ruses, par lesquelles ils vous ont surpris dans le fait de Péhor, et dans le fait de Cozbi, fille d'un des principaux d'entre les Madianites, leur sœur, qui a été tuée le jour de la plaie arrivée pour le fait de Péhor.

< Hesabu 25 >