< Hesabu 25 >
1 Israeli alipokuwa akikaa Shitimu, wanaume wa Israeli walianza kuzini na wanawake wa Kimoabu,
Israel stayed in Shittim, and the men began to prostitute themselves with women of Moab,
2 ambao waliwaalika kushiriki katika kutoa kafara kwa miungu yao. Watu wakala na kusujudu mbele ya miungu hii.
for the Moabites had invited the people to the sacrifices to their gods. So the people ate and bowed down to Moabite gods.
3 Kwa hiyo Israeli akaungana katika kumwabudu Baali wa Peori. Hasira ya Bwana ikawaka dhidi yao.
The men of Israel joined in worshiping Baal of Peor, and Yahweh's anger was kindled against Israel.
4 Bwana akamwambia Mose, “Uwachukue viongozi wote wa watu hawa, uwaue na uwaweke hadharani mchana peupe mbele za Bwana, ili hasira kali ya Bwana iweze kuondoka kwa Israeli.”
Yahweh said to Moses, “Kill all the leaders of the people and hang them up before me to expose them in the daylight, so that my fierce anger may turn away from Israel.”
5 Kwa hiyo Mose akawaambia waamuzi wa Israeli, “Kila mmoja wenu lazima awaue wale wanaume wenu, walioshiriki katika kumwabudu Baali wa Peori.”
So Moses said to Israel's leaders, “Each of you must execute his people who have joined in worshiping Baal of Peor.”
6 Ndipo mwanaume wa Kiisraeli akamleta mwanamke wa Kimidiani katika jamaa yake palepale mbele ya Mose na mkutano wote wa Israeli walipokuwa wakilia kwenye lango la Hema la Kukutania.
Then one of the men of Israel came and brought among his family members a Midianite woman. This happened in the sight of Moses and all the community of the people of Israel, while they were weeping at the entrance to the tent of meeting.
7 Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, alipoona jambo hili, akaondoka kwenye kusanyiko, akachukua mkuki mkononi mwake,
When Phinehas son of Eleazar son of Aaron the priest, saw that, he rose up from among the community and took a spear in his hand.
8 akamfuata yule Mwisraeli ndani ya hema. Akawachoma mkuki wote wawili kwa pamoja, ukapenya kwenye mwili wa yule Mwisraeli na mwili wa yule mwanamke. Ndipo tauni iliyokuwepo dhidi ya Waisraeli ikakoma.
He followed the Israelite man into the tent and thrust the spear through both of their bodies, both the Israelite man and the woman. So a plague that God had sent on the people of Israel stopped.
9 Lakini wale waliokufa kwa hiyo tauni walikuwa watu 24,000.
Those who died by the plague were twenty-four thousand in number.
10 Bwana akamwambia Mose,
Yahweh spoke to Moses and said,
11 “Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, amegeuza hasira yangu mbali na Waisraeli, kwa sababu alikuwa na wivu kama nilio nao kwa heshima yangu miongoni mwao, hata kwamba kwa wivu wangu sikuwaangamiza.
“Phinehas son of Eleazar son of Aaron the priest, has turned my rage away from the people of Israel because he was passionate with my zeal among them. So I have not consumed the people of Israel in my fierceness.
12 Kwa hiyo mwambie Finehasi ninafanya Agano langu la amani naye.
Therefore say, 'Yahweh says, “Look, I am giving to Phinehas my covenant of peace.
13 Yeye pamoja na wazao wake watakuwa na Agano la ukuhani milele, kwa sababu alikuwa na wivu kwa ajili ya heshima ya Mungu wake, na akafanya upatanisho kwa Waisraeli.”
For him and his descendants after him, it will be a covenant of an everlasting priesthood because he was zealous for me, his God. He has atoned for the people of Israel.”'”
14 Jina la Mwisraeli ambaye aliuawa pamoja na mwanamke wa Kimidiani ni Zimri mwana wa Salu, kiongozi wa jamaa ya Simeoni.
Now the name of the Israelite man who was killed with the Midianite woman was Zimri son of Salu, a leader of an ancestor's family among the Simeonites.
15 Jina la mwanamke wa Kimidiani aliyeuawa ni Kozbi binti wa Suri, aliyekuwa mkuu wa kabila la jamaa ya Wamidiani.
The name of the Midianite woman who was killed was Kozbi daughter of Zur, who was head of a tribe and family in Midian.
16 Bwana akamwambia Mose,
So Yahweh spoke to Moses and said,
17 “Watendeeni Wamidiani kama adui na mwaue,
“Treat the Midianites as enemies and attack them,
18 kwa sababu wao waliwatendea kama adui wakati waliwadanganya katika tukio la Peori na dada yao Kozbi, binti wa kiongozi wa Kimidiani, mwanamke ambaye aliuawa wakati tauni ilikuja kama matokeo ya tukio la Peori.”
for they treated you like enemies with their deceitfulness. They led you into evil in the case of Peor and in the case of their sister Kozbi, the daughter of a leader in Midian, who was killed on the day of the plague in the matter of Peor.”