< Hesabu 25 >

1 Israeli alipokuwa akikaa Shitimu, wanaume wa Israeli walianza kuzini na wanawake wa Kimoabu,
While the Israelis were camped at a place called Acacia [Grove], some of the men caused themselves to become unacceptable to God by having sex with some of the women of the Moab [people-group who lived in that area].
2 ambao waliwaalika kushiriki katika kutoa kafara kwa miungu yao. Watu wakala na kusujudu mbele ya miungu hii.
Then those women invited the men to come when the sacrifices were being offered to their gods. The Israeli men [accepted]. They went to the feasts with the women and worshiped the gods of the Moab people-group.
3 Kwa hiyo Israeli akaungana katika kumwabudu Baali wa Peori. Hasira ya Bwana ikawaka dhidi yao.
By doing that, those Israeli people joined the women in worshiping the god Baal [add] the Moab people-group thought lived on Peor Mountain. That caused Yahweh to become very angry with his people.
4 Bwana akamwambia Mose, “Uwachukue viongozi wote wa watu hawa, uwaue na uwaweke hadharani mchana peupe mbele za Bwana, ili hasira kali ya Bwana iweze kuondoka kwa Israeli.”
Yahweh said this to Moses/me: “Seize all the leaders of those men who are doing this and execute them while I am watching. Do that in the daytime. After you do that, I will no longer be angry with the Israeli people.”
5 Kwa hiyo Mose akawaambia waamuzi wa Israeli, “Kila mmoja wenu lazima awaue wale wanaume wenu, walioshiriki katika kumwabudu Baali wa Peori.”
So Moses/I said to the other Israeli leaders, “Each of you must execute your men who have joined [others] in worshiping Baal.”
6 Ndipo mwanaume wa Kiisraeli akamleta mwanamke wa Kimidiani katika jamaa yake palepale mbele ya Mose na mkutano wote wa Israeli walipokuwa wakilia kwenye lango la Hema la Kukutania.
[But later], while Moses/I and many [HYP] other people were crying at the entrance of the Sacred Tent, while they/we were watching, one of the Israeli men brought a woman from the Midian people-group into his tent [and started to have sex with her].
7 Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, alipoona jambo hili, akaondoka kwenye kusanyiko, akachukua mkuki mkononi mwake,
When Phinehas, who was the grandson of Aaron, saw that, he grabbed a spear
8 akamfuata yule Mwisraeli ndani ya hema. Akawachoma mkuki wote wawili kwa pamoja, ukapenya kwenye mwili wa yule Mwisraeli na mwili wa yule mwanamke. Ndipo tauni iliyokuwepo dhidi ya Waisraeli ikakoma.
and rushed into the man’s tent. He thrust the spear completely through the man’s body and into the woman’s belly [and killed both of them]. When he did that, the (plague/serious illness) [that had started to strike the Israelis] stopped.
9 Lakini wale waliokufa kwa hiyo tauni walikuwa watu 24,000.
But 24,000 people had already died [from that plague].
10 Bwana akamwambia Mose,
Then Yahweh said to Moses/me,
11 “Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, amegeuza hasira yangu mbali na Waisraeli, kwa sababu alikuwa na wivu kama nilio nao kwa heshima yangu miongoni mwao, hata kwamba kwa wivu wangu sikuwaangamiza.
“Phinehas has caused me to stop being angry with the Israeli people, by being as eager as I am [to stop this sinful behavior]. I was ready to get rid of all the Israeli people because I was extremely angry, but Phinehas has prevented me from doing that.
12 Kwa hiyo mwambie Finehasi ninafanya Agano langu la amani naye.
Now tell him that I am making a special peace agreement with him.
13 Yeye pamoja na wazao wake watakuwa na Agano la ukuhani milele, kwa sababu alikuwa na wivu kwa ajili ya heshima ya Mungu wake, na akafanya upatanisho kwa Waisraeli.”
In this agreement, I am promising to give to him and to his descendants the right/authority to be priests. I am doing this because [he showed that] he was very eager to honor me, his God, by stopping this sinful behavior. He has caused the Israeli people to become acceptable to me again by causing them to be forgiven for their sin.”
14 Jina la Mwisraeli ambaye aliuawa pamoja na mwanamke wa Kimidiani ni Zimri mwana wa Salu, kiongozi wa jamaa ya Simeoni.
The Israeli man who was killed with the woman of the Moab people-group was named Zimri. He was the son of Salu, who was the leader of a family from the tribe of Simeon.
15 Jina la mwanamke wa Kimidiani aliyeuawa ni Kozbi binti wa Suri, aliyekuwa mkuu wa kabila la jamaa ya Wamidiani.
The woman’s name was Cozbi. She was the daughter of Zur, who was the leader of one of the clans of the Midian people-group.
16 Bwana akamwambia Mose,
Then Yahweh said to Moses/me,
17 “Watendeeni Wamidiani kama adui na mwaue,
“[Take your men and] attack the Midian people-group and kill them.
18 kwa sababu wao waliwatendea kama adui wakati waliwadanganya katika tukio la Peori na dada yao Kozbi, binti wa kiongozi wa Kimidiani, mwanamke ambaye aliuawa wakati tauni ilikuja kama matokeo ya tukio la Peori.”
They have become your enemies, because they tricked you Israeli people and induced/persuaded many of you to worship Baal, and because [one of your men had sex with] Cozbi, who was the daughter of a leader of the Midian people-group. She was killed at the time the plague [started because the people sinned] at Peor [Mountain].”

< Hesabu 25 >