< Hesabu 25 >

1 Israeli alipokuwa akikaa Shitimu, wanaume wa Israeli walianza kuzini na wanawake wa Kimoabu,
And Israel dwells in Shittim, and the people begin to go whoring to daughters of Moab,
2 ambao waliwaalika kushiriki katika kutoa kafara kwa miungu yao. Watu wakala na kusujudu mbele ya miungu hii.
and they call for the people to the sacrifices of their gods, and the people eat and bow themselves to their gods,
3 Kwa hiyo Israeli akaungana katika kumwabudu Baali wa Peori. Hasira ya Bwana ikawaka dhidi yao.
and Israel is joined to Ba‘al-Peor, and the anger of YHWH burns against Israel.
4 Bwana akamwambia Mose, “Uwachukue viongozi wote wa watu hawa, uwaue na uwaweke hadharani mchana peupe mbele za Bwana, ili hasira kali ya Bwana iweze kuondoka kwa Israeli.”
And YHWH says to Moses, “Take all the chiefs of the people and hang them before YHWH in sight of the sun; and the fierceness of the anger of YHWH turns back from Israel.”
5 Kwa hiyo Mose akawaambia waamuzi wa Israeli, “Kila mmoja wenu lazima awaue wale wanaume wenu, walioshiriki katika kumwabudu Baali wa Peori.”
And Moses says to [the] judges of Israel, “Each slays his men who are joined to Ba‘al-Peor.”
6 Ndipo mwanaume wa Kiisraeli akamleta mwanamke wa Kimidiani katika jamaa yake palepale mbele ya Mose na mkutano wote wa Israeli walipokuwa wakilia kwenye lango la Hema la Kukutania.
And behold, a man of the sons of Israel has come, and brings a Midianitess to his brothers before the eyes of Moses and before the eyes of all the congregation of the sons of Israel, who are weeping at the opening of the Tent of Meeting;
7 Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, alipoona jambo hili, akaondoka kwenye kusanyiko, akachukua mkuki mkononi mwake,
and Phinehas, son of Eleazar, son of Aaron the priest, sees, and rises from the midst of the congregation, and takes a javelin in his hand,
8 akamfuata yule Mwisraeli ndani ya hema. Akawachoma mkuki wote wawili kwa pamoja, ukapenya kwenye mwili wa yule Mwisraeli na mwili wa yule mwanamke. Ndipo tauni iliyokuwepo dhidi ya Waisraeli ikakoma.
and goes in after the man of Israel to the hollow place, and pierces them both, the man of Israel and the woman—to her belly, and the plague is restrained from the sons of Israel;
9 Lakini wale waliokufa kwa hiyo tauni walikuwa watu 24,000.
and the dead by the plague are twenty-four thousand.
10 Bwana akamwambia Mose,
And YHWH speaks to Moses, saying,
11 “Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, amegeuza hasira yangu mbali na Waisraeli, kwa sababu alikuwa na wivu kama nilio nao kwa heshima yangu miongoni mwao, hata kwamba kwa wivu wangu sikuwaangamiza.
“Phinehas, son of Eleazar, son of Aaron the priest, has turned back My fury from the sons of Israel by his being zealous with My zeal in their midst, and I have not consumed the sons of Israel in My zeal.
12 Kwa hiyo mwambie Finehasi ninafanya Agano langu la amani naye.
Therefore say, Behold, I am giving My covenant of peace to him,
13 Yeye pamoja na wazao wake watakuwa na Agano la ukuhani milele, kwa sababu alikuwa na wivu kwa ajili ya heshima ya Mungu wake, na akafanya upatanisho kwa Waisraeli.”
and it has been to him and to his seed after him [for] a covenant of a continuous priesthood, because that he has been zealous for his God, and makes atonement for the sons of Israel.”
14 Jina la Mwisraeli ambaye aliuawa pamoja na mwanamke wa Kimidiani ni Zimri mwana wa Salu, kiongozi wa jamaa ya Simeoni.
And the name of the man of Israel who is struck, who has been struck with the Midianitess, [is] Zimri son of Salu, prince of the house of a father of the Simeonite;
15 Jina la mwanamke wa Kimidiani aliyeuawa ni Kozbi binti wa Suri, aliyekuwa mkuu wa kabila la jamaa ya Wamidiani.
and the name of the woman who is struck, the Midianitess, [is] Cozbi daughter of Zur; he [is] head of peoples of a father’s house in Midian.
16 Bwana akamwambia Mose,
And YHWH speaks to Moses, saying,
17 “Watendeeni Wamidiani kama adui na mwaue,
“Distress the Midianites, and you have struck them,
18 kwa sababu wao waliwatendea kama adui wakati waliwadanganya katika tukio la Peori na dada yao Kozbi, binti wa kiongozi wa Kimidiani, mwanamke ambaye aliuawa wakati tauni ilikuja kama matokeo ya tukio la Peori.”
for they are adversaries to you with their frauds, [with] which they have acted fraudulently to you, concerning the matter of Peor and concerning the matter of Cozbi, daughter of a prince of Midian, their sister, who is struck in the day of the plague for the matter of Peor.”

< Hesabu 25 >