< Hesabu 25 >
1 Israeli alipokuwa akikaa Shitimu, wanaume wa Israeli walianza kuzini na wanawake wa Kimoabu,
Now Israel, at that time, dwelt in Shittim, and the people were fornicating with the daughters of Moab,
2 ambao waliwaalika kushiriki katika kutoa kafara kwa miungu yao. Watu wakala na kusujudu mbele ya miungu hii.
who called them to their sacrifices. And they ate, and they adored their gods.
3 Kwa hiyo Israeli akaungana katika kumwabudu Baali wa Peori. Hasira ya Bwana ikawaka dhidi yao.
And Israel was initiated into Baal of Peor. And so the Lord, being angry,
4 Bwana akamwambia Mose, “Uwachukue viongozi wote wa watu hawa, uwaue na uwaweke hadharani mchana peupe mbele za Bwana, ili hasira kali ya Bwana iweze kuondoka kwa Israeli.”
said to Moses, “Take all the leaders of the people, and hang them on gallows against the sun, so that my fury may be averted from Israel.”
5 Kwa hiyo Mose akawaambia waamuzi wa Israeli, “Kila mmoja wenu lazima awaue wale wanaume wenu, walioshiriki katika kumwabudu Baali wa Peori.”
And Moses said to the judges of Israel, “Let each one kill his neighbors, who have been initiated into Baal of Peor.”
6 Ndipo mwanaume wa Kiisraeli akamleta mwanamke wa Kimidiani katika jamaa yake palepale mbele ya Mose na mkutano wote wa Israeli walipokuwa wakilia kwenye lango la Hema la Kukutania.
And behold, one of the sons of Israel entered, in the sight of his brothers, to a prostitute of Midian, within view of Moses and of all the crowd of the sons of Israel, who were weeping before the door of the tabernacle.
7 Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, alipoona jambo hili, akaondoka kwenye kusanyiko, akachukua mkuki mkononi mwake,
And when Phinehas the son of Eleazar, the son of Aaron the priest, had seen it, he rose up from the midst of the multitude, and, seizing a dagger,
8 akamfuata yule Mwisraeli ndani ya hema. Akawachoma mkuki wote wawili kwa pamoja, ukapenya kwenye mwili wa yule Mwisraeli na mwili wa yule mwanamke. Ndipo tauni iliyokuwepo dhidi ya Waisraeli ikakoma.
he entered after the Israelite man, into the brothel, and he pierced both of them at the same time, specifically, the man and the woman at the location of their genitals. And the scourge ceased from among the sons of Israel.
9 Lakini wale waliokufa kwa hiyo tauni walikuwa watu 24,000.
And there were slain twenty-four thousand men.
10 Bwana akamwambia Mose,
And the Lord said to Moses:
11 “Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, amegeuza hasira yangu mbali na Waisraeli, kwa sababu alikuwa na wivu kama nilio nao kwa heshima yangu miongoni mwao, hata kwamba kwa wivu wangu sikuwaangamiza.
“Phinehas the son of Eleazar, the son of Aaron the priest, has averted my wrath from the sons of Israel. For he was moved against them by my zeal, so that I myself, in my zeal, might not wipe away the sons of Israel.
12 Kwa hiyo mwambie Finehasi ninafanya Agano langu la amani naye.
Because of this, say to him: Behold, I give to him the peace of my covenant.
13 Yeye pamoja na wazao wake watakuwa na Agano la ukuhani milele, kwa sababu alikuwa na wivu kwa ajili ya heshima ya Mungu wake, na akafanya upatanisho kwa Waisraeli.”
And the covenant of the everlasting priesthood shall be as much for him as for his offspring. For he was zealous on behalf of his God, and he has made expiation for the wickedness of the sons of Israel.”
14 Jina la Mwisraeli ambaye aliuawa pamoja na mwanamke wa Kimidiani ni Zimri mwana wa Salu, kiongozi wa jamaa ya Simeoni.
Now the name of the Israelite man, who was killed with the Midianite woman, was Zimri the son of Salu, a leader from the kinship and tribe of Simeon.
15 Jina la mwanamke wa Kimidiani aliyeuawa ni Kozbi binti wa Suri, aliyekuwa mkuu wa kabila la jamaa ya Wamidiani.
Moreover, the Midianite woman, who was put to death together with him, was called Cozbi the daughter of Zur, a most noble leader among the Midianites.
16 Bwana akamwambia Mose,
And the Lord spoke to Moses, saying:
17 “Watendeeni Wamidiani kama adui na mwaue,
“Let the Midianites perceive you as enemies, and strike them down,
18 kwa sababu wao waliwatendea kama adui wakati waliwadanganya katika tukio la Peori na dada yao Kozbi, binti wa kiongozi wa Kimidiani, mwanamke ambaye aliuawa wakati tauni ilikuja kama matokeo ya tukio la Peori.”
for they, too, have behaved with hostility against you, and they have deceived you insidiously by means of the idol Peor, and by Cozbi, the daughter of a commander of Midian, their sister, who was struck down in the day of the scourge because of the sacrilege of Peor.”