< Hesabu 25 >

1 Israeli alipokuwa akikaa Shitimu, wanaume wa Israeli walianza kuzini na wanawake wa Kimoabu,
Israeliterne slog sig derpå ned i Sjitim. Men Folket begyndte at bedrive Hor med de moabitiske Kvinder;
2 ambao waliwaalika kushiriki katika kutoa kafara kwa miungu yao. Watu wakala na kusujudu mbele ya miungu hii.
og da de indbød Folket til deres Guders Slagtofre, spiste Folket deraf og tilbad deres Guder.
3 Kwa hiyo Israeli akaungana katika kumwabudu Baali wa Peori. Hasira ya Bwana ikawaka dhidi yao.
Og Israel holdt til med Bål Peor; derover blussede HERRENs Vrede op mod Israel,
4 Bwana akamwambia Mose, “Uwachukue viongozi wote wa watu hawa, uwaue na uwaweke hadharani mchana peupe mbele za Bwana, ili hasira kali ya Bwana iweze kuondoka kwa Israeli.”
og HERREN sagde til Moses: "Kald alle Folkets Overhoveder sammen og hæng dem op for HERREN under åben Himmel, for at HERRENs Vrede må vige fra Israel!"
5 Kwa hiyo Mose akawaambia waamuzi wa Israeli, “Kila mmoja wenu lazima awaue wale wanaume wenu, walioshiriki katika kumwabudu Baali wa Peori.”
Og Moses sagde til Israeliternes Dommere: "Enhver af eder skal slå dem af sine Mænd ihjel, der har holdt til med Ba'al Peor!"
6 Ndipo mwanaume wa Kiisraeli akamleta mwanamke wa Kimidiani katika jamaa yake palepale mbele ya Mose na mkutano wote wa Israeli walipokuwa wakilia kwenye lango la Hema la Kukutania.
Og se, en af Israeliterne kom og førte en midjanitisk Kvinde hen til sine Landsmænd lige for Øjnene af Moses og hele Israeliternes Menighed, medens de stod og græd ved Indgangen til Åbenbaringsteltet.
7 Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, alipoona jambo hili, akaondoka kwenye kusanyiko, akachukua mkuki mkononi mwake,
Da nu Pinehas, Præsten Arons Søn Eleazars Søn, så det, trådte han frem af Menighedens Midte, greb et Spyd,
8 akamfuata yule Mwisraeli ndani ya hema. Akawachoma mkuki wote wawili kwa pamoja, ukapenya kwenye mwili wa yule Mwisraeli na mwili wa yule mwanamke. Ndipo tauni iliyokuwepo dhidi ya Waisraeli ikakoma.
fulgte den israelitiske Mand ind i Sengekammeret og gennemborede dem begge, både den israelitiske Mand og Kvinden, hende gennem Underlivet. Da standsede Plagen blandt Israeliterne.
9 Lakini wale waliokufa kwa hiyo tauni walikuwa watu 24,000.
Men Tallet på dem, Plagen havde kostet Livet, løb op til 24000.
10 Bwana akamwambia Mose,
Da talede HERREN således til Moses:
11 “Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, amegeuza hasira yangu mbali na Waisraeli, kwa sababu alikuwa na wivu kama nilio nao kwa heshima yangu miongoni mwao, hata kwamba kwa wivu wangu sikuwaangamiza.
Pinehas, Præsten Arons Søn Eleazars Søn, har vendt min Vrede fra Israeliterne, idet han var nidkær iblandt dem med min Nidkærhed, så at jeg ikke tilintetgjorde Israeliterne i min Nidkærhed.
12 Kwa hiyo mwambie Finehasi ninafanya Agano langu la amani naye.
Derfor skal du sige: Se, jeg giver ham min Fredspagt!
13 Yeye pamoja na wazao wake watakuwa na Agano la ukuhani milele, kwa sababu alikuwa na wivu kwa ajili ya heshima ya Mungu wake, na akafanya upatanisho kwa Waisraeli.”
Et evigt Præstedømmes Pagt skal blive hans og efter ham hans Efterkommeres Lod, til Løn for at han var nidkær for sin Gud og skaffede Israeliterne Soning."
14 Jina la Mwisraeli ambaye aliuawa pamoja na mwanamke wa Kimidiani ni Zimri mwana wa Salu, kiongozi wa jamaa ya Simeoni.
Den dræbte Israelit, han, der dræbtes sammenmed den midjanitiske kvinde, hed Zimri, Salus Søn, og var Øverste for et Fædrenehus blandt Simeoniterne;
15 Jina la mwanamke wa Kimidiani aliyeuawa ni Kozbi binti wa Suri, aliyekuwa mkuu wa kabila la jamaa ya Wamidiani.
og den dræbte midjanitiske Kvinde hed Hozbi og var en Datter af Zur, der var Stammehøvding for et Fædrenehus blandt Midjaniterne,
16 Bwana akamwambia Mose,
HERREN talede fremdeles til Moses og sagde:
17 “Watendeeni Wamidiani kama adui na mwaue,
"Fald over Midjaniterne og slå dem;
18 kwa sababu wao waliwatendea kama adui wakati waliwadanganya katika tukio la Peori na dada yao Kozbi, binti wa kiongozi wa Kimidiani, mwanamke ambaye aliuawa wakati tauni ilikuja kama matokeo ya tukio la Peori.”
thi de faldt over eder med de Rænker, de spandt imod eder i den Sag med Peor og med Hozbi, den midjanitiske Høvdings Datter, deres Landsmandinde, der dræbtes, den Dag Plagen brød løs for Peors Skyld."

< Hesabu 25 >