< Hesabu 22 >
1 Kisha Waisraeli wakasafiri katika tambarare za Moabu na kupiga kambi kando ya Mto Yordani, ngʼambo ya Yeriko.
and to set out son: descendant/people Israel and to camp in/on/with Plains (of Moab) (Plains of) Moab from side: beyond to/for Jordan Jericho
2 Basi Balaki mwana wa Sipori, aliona mambo yale yote ambayo Israeli aliwatendea Waamori,
and to see: see Balak son: child Zippor [obj] all which to make: do Israel to/for Amorite
3 Moabu aliogopa, kwa kuwa walikuwepo watu wengi sana. Hakika, Moabu alijawa na hofu kubwa kwa sababu ya Waisraeli.
and to dread Moab from face: because [the] people much for many he/she/it and to loathe Moab from face: because son: descendant/people Israel
4 Wamoabu wakawaambia wazee wa Midiani, “Umati huu wa watu unakwenda kuramba kila kitu kinachotuzunguka, kama maksai arambavyo majani ya shambani.” Kwa hiyo Balaki mwana wa Sipori, ambaye alikuwa mfalme wa Moabu wakati huo,
and to say Moab to(wards) old: elder Midian now to lick [the] assembly [obj] all around us like/as to lick [the] cattle [obj] green [the] land: country and Balak son: child Zippor king to/for Moab in/on/with time [the] he/she/it
5 akatuma wajumbe kwenda kumwita Balaamu mwana wa Beori, ambaye alikuwa huko Pethori, karibu na Mto Frati, katika nchi yake ya kuzaliwa. Balaki akasema: “Taifa limekuja kutoka Misri, nao wamefunika uso wa nchi, nao wametua karibu nami.
and to send: depart messenger to(wards) Balaam son: child Beor Pethor [to] which upon [the] River land: country/planet son: descendant/people people his to/for to call: call to to/for him to/for to say behold people to come out: come from Egypt behold to cover [obj] eye: before(the eyes) [the] land: country/planet and he/she/it to dwell from opposite me
6 Sasa uje kuwalaani watu hawa, kwa kuwa wana nguvu sana kuniliko. Kisha huenda nikaweza kuwashinda na kuwatoa nje ya nchi. Kwa kuwa ninajua kwamba, wale unaowabariki wanabarikiwa na wale unaowalaani wanalaaniwa.”
and now to go: come! [emph?] please to curse [emph?] to/for me [obj] [the] people [the] this for mighty he/she/it from me perhaps be able to smite in/on/with him and to drive out: drive out him from [the] land: country/planet for to know [obj] which to bless to bless and which to curse to curse
7 Wazee wa Moabu na wa Midiani wakaondoka, wakiwa wamechukua ada ya uaguzi. Walipokwenda kwa Balaamu, wakamweleza kile Balaki alikuwa amesema.
and to go: went old: elder Moab and old: elder Midian and divination in/on/with hand: power their and to come (in): come to(wards) Balaam and to speak: speak to(wards) him word Balak
8 Balaamu akawaambia, “Mlale hapa usiku huu, nami nitawaletea jibu lile Bwana atakalonipa.” Kwa hiyo wakuu wa Moabu wakakaa naye.
and to say to(wards) them to lodge here [the] night and to return: return [obj] you word like/as as which to speak: speak LORD to(wards) me and to dwell ruler Moab with Balaam
9 Mungu akamjia Balaamu na kumuuliza, “Watu gani hawa walio pamoja nawe?”
and to come (in): come God to(wards) Balaam and to say who? [the] human [the] these with you
10 Balaamu akamwambia Mungu, “Balaki mwana wa Sipori, mfalme wa Moabu, alinipelekea ujumbe huu:
and to say Balaam to(wards) [the] God Balak son: child Zippor king Moab to send: depart to(wards) me
11 ‘Taifa ambalo limekuja kutoka Misri limefunika uso wa nchi. Sasa uje unilaanie hao watu. Kisha huenda nitaweza kupigana nao na kuwafukuza.’”
behold [the] people [the] to come out: come from Egypt and to cover [obj] eye: before(the eyes) [the] land: country/planet now to go: come! [emph?] to curse [emph?] to/for me [obj] him perhaps be able to/for to fight in/on/with him and to drive out: drive out him
12 Lakini Bwana akamwambia Balaamu, “Usiende pamoja nao. Hupaswi kulaani watu hao, kwa kuwa wamebarikiwa.”
and to say God to(wards) Balaam not to go: went with them not to curse [obj] [the] people for to bless he/she/it
13 Asubuhi iliyofuata Balaamu akaamka, akawaambia wakuu wa Balaki, “Rudini katika nchi yenu, kwa kuwa Bwana amenikataza nisiende pamoja nanyi.”
and to arise: rise Balaam in/on/with morning and to say to(wards) ruler Balak to go: went to(wards) land: country/planet your for to refuse LORD to/for to give: allow me to/for to go: went with you
14 Kwa hiyo wakuu wa Moabu wakarudi kwa Balaki na kumwambia, “Balaamu amekataa kuja pamoja nasi.”
and to arise: rise ruler Moab and to come (in): come to(wards) Balak and to say to refuse Balaam to go: come with us
15 Kisha Balaki akatuma wakuu wengine, wengi zaidi na wanaoheshimiwa zaidi kuliko wale wa kwanza.
and to add: again still Balak to send: depart ruler many and to honor: honour from these
16 Wakafika kwa Balaamu na kumwambia: “Balaki mwana wa Sipori amesema hivi: Usiruhusu kitu chochote kikuzuie kuja kwangu,
and to come (in): come to(wards) Balaam and to say to/for him thus to say Balak son: child Zippor not please to withhold from to go: come to(wards) me
17 kwa sababu nitakulipa vizuri sana na kufanya lolote usemalo. Njoo unilaanie watu hawa.”
for to honor: honour to honor: honour you much and all which to say to(wards) me to make: do and to go: come! [emph?] please to curse [emph?] to/for me [obj] [the] people [the] this
18 Lakini Balaamu akawajibu, “Hata kama Balaki angenipa jumba lake la kifalme likiwa limejazwa fedha na dhahabu, singeweza kufanya kitu chochote kikubwa au kidogo ili kutenda kitu nje ya agizo la Bwana Mungu wangu.
and to answer Balaam and to say to(wards) servant/slave Balak if to give: give to/for me Balak fullness house: home his silver: money and gold not be able to/for to pass: trespass [obj] lip: word LORD God my to/for to make: do small or great: large
19 Mlale hapa usiku huu kama wale wengine walivyofanya, nami nitatafuta ni nini kingine Bwana atakachoniambia.”
and now to dwell please in/on/with this also you(m. p.) [the] night and to know what? to add LORD to speak: speak with me
20 Usiku ule Bwana akamjia Balaamu na kumwambia, “Kwa kuwa watu hawa wamekuja kukuita wewe, nenda nao, lakini ufanye tu lile nitakalokuambia.”
and to come (in): come God to(wards) Balaam night and to say to/for him if to/for to call: call to to/for you to come (in): come [the] human to arise: rise to go: went with them and surely [obj] [the] word which to speak: speak to(wards) you [obj] him to make: do
21 Balaamu akaamka asubuhi, akatandika punda wake akaenda pamoja na wakuu wa Moabu.
and to arise: rise Balaam in/on/with morning and to saddle/tie [obj] she-ass his and to go: went with ruler Moab
22 Lakini Mungu alikasirika sana alipokwenda, naye malaika wa Bwana akasimama barabarani kumpinga. Balaamu alikuwa amepanda punda wake, na watumishi wake wawili walikuwa pamoja naye.
and to be incensed face: anger God for to go: went he/she/it and to stand messenger: angel LORD in/on/with way: journey to/for Satan to/for him and he/she/it to ride upon she-ass his and two youth his with him
23 Wakati punda alipomwona malaika wa Bwana akiwa amesimama barabarani akiwa na upanga uliofutwa mkononi mwake, punda akageukia upande kuelekea shambani. Balaamu akampiga ili amrudishe barabarani.
and to see: see [the] she-ass [obj] messenger: angel LORD to stand in/on/with way: road and sword his to draw in/on/with hand: power his and to stretch [the] she-ass from [the] way: road and to go: went in/on/with land: country and to smite Balaam [obj] [the] she-ass to/for to stretch her [the] way: road
24 Ndipo malaika wa Bwana akasimama katika njia nyembamba iliyo kati ya mashamba mawili ya mizabibu, yakiwa na kuta pande zote mbili.
and to stand: stand messenger: angel LORD in/on/with passage [the] vineyard wall from this and wall from this
25 Punda alipomwona malaika wa Bwana, alijisukumiza karibu na ukuta, na kugandamiza mguu wa Balaamu ukutani. Ndipo Balaamu akampiga tena punda.
and to see: see [the] she-ass [obj] messenger: angel LORD and to oppress to(wards) [the] wall and to oppress [obj] foot Balaam to(wards) [the] wall and to add: again to/for to smite her
26 Kisha malaika wa Bwana akaendelea mbele na kusimama mahali pembamba ambapo hapakuwepo nafasi ya kugeuka, upande wa kulia wala wa kushoto.
and to add messenger: angel LORD to pass and to stand: stand in/on/with place narrow which nothing way: journey to/for to stretch right and left
27 Punda alipomwona malaika wa Bwana, alilala chini Balaamu angali amempanda, naye Balaamu akakasirika na kumpiga kwa fimbo yake.
and to see: see [the] she-ass [obj] messenger: angel LORD and to stretch underneath: under Balaam and to be incensed face: anger Balaam and to smite [obj] [the] she-ass in/on/with rod
28 Kisha Bwana akakifungua kinywa cha punda, akamwambia Balaamu, “Nimekutendea nini kinachokufanya unipige mara hizi tatu?”
and to open LORD [obj] lip [the] she-ass and to say to/for Balaam what? to make: do to/for you for to smite me this three foot
29 Balaamu akamjibu punda, “Umenifanya mjinga! Kama ningelikuwa na upanga mkononi mwangu, ningelikuua sasa hivi.”
and to say Balaam to/for she-ass for to abuse in/on/with me if there sword in/on/with hand my for now to kill you
30 Punda akamwambia Balaamu, “Je, mimi si punda wako mwenyewe, ambaye umenipanda siku zote, hadi leo? Je, nimekuwa na tabia ya kufanya hivi kwako?” Akajibu, “Hapana.”
and to say [the] she-ass to(wards) Balaam not I she-ass your which to ride upon me from still your till [the] day [the] this be useful be useful to/for to make: do to/for you thus and to say not
31 Kisha Bwana akafungua macho ya Balaamu, naye akamwona malaika wa Bwana amesimama barabarani akiwa ameufuta upanga wake. Balaamu akainama, akaanguka kifudifudi.
and to reveal: uncover LORD [obj] eye Balaam and to see: see [obj] messenger: angel LORD to stand in/on/with way: journey and sword his to draw in/on/with hand his and to bow and to bow to/for face his
32 Malaika wa Bwana akamuuliza Balaamu, “Kwa nini umempiga punda wako mara tatu hizi? Nimekuja kukuzuia kwa sababu njia yako imepotoka mbele yangu.
and to say to(wards) him messenger: angel LORD upon what? to smite [obj] she-ass your this three foot behold I to come out: come to/for Satan for to push [the] way: conduct to/for before me
33 Punda aliniona na kunikwepa mara hizi tatu. Kama punda hangenikwepa, hakika ningekuwa nimeshakuua sasa, lakini ningemwacha punda hai.”
and to see: see me [the] she-ass and to stretch to/for face: before my this three foot perhaps to stretch from face: before my for now also [obj] you to kill and [obj] her to live
34 Balaamu akamwambia malaika wa Bwana, “Nimetenda dhambi. Sikutambua kuwa umesimama barabarani kunizuia. Basi kama haikupendezi, nitarudi.”
and to say Balaam to(wards) messenger: angel LORD to sin for not to know for you(m. s.) to stand to/for to encounter: toward me in/on/with way: road and now if be evil in/on/with eye: seeing your to return: return to/for me
35 Malaika wa Bwana akamwambia Balaamu, “Uende na watu hao, lakini useme tu lile nikuambialo.” Kwa hiyo Balaamu akaenda na wale wakuu wa Balaki.
and to say messenger: angel LORD to(wards) Balaam to go: went with [the] human and end [obj] [the] word which to speak: speak to(wards) you [obj] him to speak: speak and to go: went Balaam with ruler Balak
36 Balaki aliposikia kuwa Balaamu anakuja, akatoka kumlaki katika mji wa Moabu, katika mpaka wa Arnoni, ukingoni mwa nchi yake.
and to hear: hear Balak for to come (in): come Balaam and to come out: come to/for to encounter: meet him to(wards) city Moab which upon border: boundary Arnon which in/on/with end [the] border: boundary
37 Balaki akamwambia Balaamu, “Je, sikukupelekea jumbe za haraka? Kwa nini hukuja kwangu? Hivi kweli mimi siwezi kukulipa?”
and to say Balak to(wards) Balaam not to send: depart to send: depart to(wards) you to/for to call: call to to/for you to/for what? not to go: come to(wards) me truly not be able to honor: honour you
38 Balaamu akajibu, “Vema, sasa nimekuja kwako. Lakini kwani nina uwezo wa kusema tu chochote? Ni lazima niseme tu kile ambacho Mungu ataweka kinywani mwangu.”
and to say Balaam to(wards) Balak behold to come (in): come to(wards) you now be able be able to speak: speak anything [the] word which to set: put God in/on/with lip my [obj] him to speak: speak
39 Kisha Balaamu alikwenda na Balaki mpaka Kiriath-Husothi.
and to go: went Balaam with Balak and to come (in): come Kiriath-huzoth Kiriath-huzoth
40 Balaki akatoa dhabihu ya ngʼombe na kondoo; baadhi yake akampa Balaamu na wakuu waliokuwa pamoja naye.
and to sacrifice Balak cattle and flock and to send: depart to/for Balaam and to/for ruler which with him
41 Asubuhi iliyofuata Balaki akamchukua Balaamu mpaka Bamoth-Baali, na kutoka huko Balaamu akawaona baadhi ya watu.
and to be in/on/with morning and to take: take Balak [obj] Balaam and to ascend: establish him Bamoth (Bamoth)-baal and to see: see from there end [the] people