< Hesabu 21 >

1 Mfalme wa Kikanaani wa Aradi aliyeishi huko Negebu aliposikia kwamba Waisraeli walikuwa wanakuja kwa njia ya Atharimu, aliwashambulia Waisraeli na kuwateka baadhi yao.
Le Chananéen, roi d'Arad, qui habitait le Négeb, apprit qu'Israël venait par le chemin d'Atharim. Il livra bataille à Israël et lui fit des prisonniers.
2 Ndipo Israeli akaweka nadhiri hii kwa Bwana: “Ikiwa utawatia watu hawa mikononi mwetu, tutaiangamiza kabisa miji yao.”
Alors Israël fit un vœu à Yahweh, en disant: « Si vous livrez ce peuple entre mes mains, je dévouerai ses villes à l'anathème. »
3 Bwana akasikiliza ombi la Waisraeli, naye akawapa ushindi juu ya Wakanaani. Wakawaangamiza kabisa na miji yao; hivyo mahali pale pakaitwa Horma.
Yahweh entendit la voix d'Israël et livra les Chananéens; on les dévoua à l'anathème, eux et leurs villes, et on nomma ce lieu Horma.
4 Waisraeli wakasafiri kutoka mlima Hori kupitia njia inayoelekea Bahari ya Shamu, kuizunguka Edomu. Lakini watu wakakosa uvumilivu njiani,
Ils partirent de la montagne de Hor par le chemin de la mer Rouge, pour tourner le pays d'Edom. Le peuple perdit patience dans ce chemin,
5 wakamnungʼunikia Mungu na Mose, wakisema, “Kwa nini umetupandisha kutoka Misri ili tufe jangwani? Hakuna mkate! Hakuna maji! Nasi tunachukia sana chakula hiki duni!”
et il parla contre Dieu et contre Moïse: « Pourquoi nous avez-vous fait monter d'Egypte, pour que nous mourions dans le désert? Il n'y a point de pain, il n'y a point d'eau, et notre âme a pris en dégoût cette misérable nourriture. »
6 Ndipo Bwana akapeleka nyoka wenye sumu katikati yao; wakawauma watu, nao Waisraeli wengi wakafa.
Alors Yahweh envoya contre le peuple les serpents brûlants; ils mordirent le peuple, et il mourut beaucoup de gens en Israël.
7 Watu wakamjia Mose na kusema, “Tumetenda dhambi wakati tuliponena dhidi ya Bwana na dhidi yako. Mwombe Bwana ili atuondolee hawa nyoka.” Hivyo Mose akawaombea hao watu.
Le peuple vint à Moïse et dit: « Nous avons péché, car nous avons parlé contre Yahweh et contre toi. Prie Yahweh, afin qu'il éloigne de nous ces serpents. » Moïse pria pour le peuple.
8 Bwana akamwambia Mose, “Tengeneza nyoka wa shaba na umweke juu ya mti; yeyote aliyeumwa na nyoka anaweza kumtazama na akaishi tena.”
Et Yahweh dit à Moïse: « Fais-toi un serpent brûlant et place-le sur un poteau; quiconque aura été mordu et le regardera, conservera la vie. »
9 Kwa hiyo Mose akatengeneza nyoka wa shaba na kumweka juu ya mti. Kisha wakati mtu yeyote aliumwa na nyoka, naye akamtazama yule nyoka wa shaba, aliishi.
Moïse fit un serpent d'airain et le plaça sur un poteau, et, si quelqu'un était mordu par un serpent, il regardait le serpent d'airain, et il vivait.
10 Waisraeli waliendelea na safari yao na wakapiga kambi huko Obothi.
Les enfants d'Israël partirent, et ils campèrent à Oboth.
11 Kisha wakaondoka Obothi na kupiga kambi huko Iye-Abarimu, katika jangwa linalotazamana na Moabu kuelekea mawio ya jua.
Ils partirent d'Oboth, et ils campèrent à Jeabarim, dans le désert qui est vis-à-vis de Moab, vers le soleil levant.
12 Kutoka hapo waliendelea mbele wakapiga kambi kwenye Bonde la Zeredi.
Ils partirent de là, et campèrent dans la vallée de Zared.
13 Wakasafiri kutoka hapo na kupiga kambi kando ya Mto Arnoni, ambao uko katika jangwa lililoenea hadi nchi ya Waamori. Arnoni ni mpaka wa Moabu, kati ya Moabu na Waamori.
Ils partirent de là, et campèrent au-delà de l'Arnon, qui coule dans le désert, en sortant du territoire des Amorrhéens; car l'Arnon est la frontière de Moab, entre Moab et les Amorrhéens.
14 Ndiyo sababu Kitabu cha Vita vya Bwana kinasema: “…Mji wa Wahebu nchini Seifa na mabonde ya Arnoni,
C'est pourquoi il est dit dans le livre des Guerres de Yahweh: « Yahweh a pris Vaheb, dans sa course impétueuse, et les torrents de l'Arnon,
15 na miteremko ya mabonde inayofika hadi mji wa Ari na huelekea mpakani mwa Moabu.”
et la pente des torrents qui s'étend vers le site d'Ar et s'appuie à la frontière de Moab. »
16 Kutoka hapo waliendelea mbele hadi kisima cha Beeri; kwenye kisima ambacho Bwana alimwambia Mose, “Wakusanye watu pamoja, nami nitawapa maji.”
De là ils allèrent à Beer. C'est le puits à propos duquel Yahweh dit à Moïse: « Rassemble le peuple, et je leur donnerai de l'eau. »
17 Kisha Israeli akaimba wimbo huu: “Bubujika, ee kisima! Imba kuhusu maji,
Alors Israël chanta ce cantique: Monte, puits! Acclamez-le!
18 kuhusu kisima ambacho kilichimbwa na wakuu, ambacho watu mashuhuri walikifukua, watu mashuhuri wakiwa na fimbo za utawala na bakora.” Kisha wakatoka jangwani kwenda Matana,
Le puits, que des princes ont creusé, que les grands du peuple ont ouvert, avec le sceptre, avec leurs bâtons! Du désert ils allèrent à Matthana;
19 kutoka Matana wakafika Nahalieli, kutoka Nahalieli wakafika Bamothi,
de Matthana à Nahaliel; de Nahaliel, à Bamoth;
20 na kutoka Bamothi wakafika kwenye bonde lililoko Moabu, mahali ambapo kilele cha Pisga kinatazamana na nyika.
de Bamoth, à la vallée qui est dans les champs de Moab, au sommet du Phasga, qui domine le désert.
21 Israeli akawatuma wajumbe kumwambia Sihoni mfalme wa Waamori:
Israël envoya des messagers à Séhon, roi des Amorrhéens, pour lui dire:
22 “Uturuhusu tupite katika nchi yako. Hatutageuka kando kwenda katika mashamba au mashamba ya mizabibu, ama kunywa maji kutoka kisima chochote. Tutasafiri kwenye njia kuu ya mfalme hata tutakapokuwa tumekwisha kupita katika nchi yako.”
« Laisse-moi passer par ton pays; nous ne nous écarterons ni dans les champs, ni dans les vignes, et nous ne boirons pas l'eau des puits; nous suivrons la route royale, jusqu'à ce que nous ayons franchi ton territoire. »
23 Lakini Sihoni hakumruhusu Israeli apite katika nchi yake. Alilikutanisha jeshi lake lote, wakaondoka kwenda jangwani ili kupigana na Israeli. Alipofika huko Yahazi, akapigana na Israeli.
Séhon ne permit pas à Israël de passer sur son territoire; il rassembla tout son peuple et, étant sorti à la rencontre d'Israël dans le désert, il vint à Jasa et livra bataille à Israël.
24 Hata hivyo, Israeli alimshinda kwa upanga na kuiteka ardhi yake kutoka Arnoni mpaka Yaboki, lakini ni hadi kufikia nchi ya Waamoni tu, kwa sababu mipaka yake ilikuwa imezungushwa ukuta.
Israël le frappa du tranchant de l'épée, et se rendit maître de son pays depuis l'Arnon jusqu'au Jaboc, jusqu'aux enfants d'Ammon; car la frontière des enfants d'Ammon était forte.
25 Israeli akaiteka miji yote ya Waamori na kuikalia, pamoja na Heshboni na makazi yote yanayoizunguka.
Israël prit toutes ces villes et Israël s'établit dans toutes les villes des Amorrhéens, à Hésebon et dans toutes les villes de son ressort.
26 Heshboni ulikuwa mji wa Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alikuwa amepigana dhidi ya mfalme wa Moabu aliyetangulia na akawa amechukua ardhi yake yote mpaka Arnoni.
Car Hésebon était la ville de Séhon, roi des Amorrhéens, qui avait fait la guerre au précédent roi de Moab et lui avait enlevé tout son pays jusqu'à l'Arnon.
27 Ndiyo sababu watunga mashairi husema: “Njoo Heshboni na ujengwe tena; mji wa Sihoni na ufanywe upya.
C'est pourquoi les poètes disent: Venez à Hésebon! Que la ville de Séhon soit rebâtie et fortifiée!
28 “Moto uliwaka kutoka Heshboni, mwali wa moto kutoka mji wa Sihoni. Uliteketeza Ari ya Moabu, raiya wa mahali pa Arnoni palipoinuka.
Car il est sorti un feu de Hésebon, une flamme de la ville de Séhon; elle a dévoré Ar-Moab. Les maîtres des hauteurs de l'Arnon.
29 Ole wako, ee Moabu! Umeharibiwa, enyi watu wa Kemoshi! Amewatoa wanawe kuwa wakimbizi, na binti zake kama mateka kwa Mfalme Sihoni wa Waamori.
Malheur à toi, Moab! Tu es perdu, peuple de Chamos! Il a livré ses fils fugitifs et ses filles captives à Séhon, roi des Amorrhéens.
30 “Lakini tumewashinda; Heshboni umeharibiwa hadi Diboni. Tumebomoa hadi kufikia Nofa, ulioenea hadi Medeba.”
Et nous avons lancé sur eux nos traits; Hésebon est détruite jusqu'à Dibon; nous avons dévasté jusqu'à Nophé, avec le feu jusqu'à Médaba.
31 Kwa hiyo Israeli akaishi katika nchi ya Waamori.
Israël s'établit dans le pays des Amorrhéens.
32 Baada ya Mose kutuma wapelelezi kwenda mji wa Yazeri, Waisraeli waliteka viunga vya mji huo na kuwafukuza Waamori waliokuwa wanaishi huko.
Moïse envoya reconnaître Jaser; et ils prirent les villes de son ressort, et expulsèrent les Amorrhéens qui y étaient.
33 Kisha wakageuka na kwenda katika njia inayoelekea Bashani, naye Ogu mfalme wa Bashani pamoja na jeshi lake lote wakatoka kupigana nao huko Edrei.
Puis, changeant de direction, ils montèrent par le chemin de Basan. Og, roi de Basan, sortit à leur rencontre, avec tout son peuple, pour les combattre à Edraï.
34 Bwana akamwambia Mose, “Usimwogope Ogu, kwa sababu nimeshamkabidhi mikononi mwako, pamoja na jeshi lake lote na nchi yake. Mtendee kama ulivyomtendea Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni.”
Yahweh dit à Moïse: « Ne le crains point, car je le livre entre tes mains, lui, tout son peuple et son pays; tu le traiteras comme tu as traité Séhon, roi des Amorrhéens, qui habitait à Hésebon. »
35 Kwa hiyo wakamuua, pamoja na wanawe na jeshi lake lote, bila ya kumwacha hata mtu mmoja hai. Nao wakaimiliki nchi yake.
Et ils le battirent, lui et ses fils, et tout son peuple, jusqu'à ne pas lui laisser de survivant, et ils s'emparèrent de son pays.

< Hesabu 21 >