< Hesabu 21 >

1 Mfalme wa Kikanaani wa Aradi aliyeishi huko Negebu aliposikia kwamba Waisraeli walikuwa wanakuja kwa njia ya Atharimu, aliwashambulia Waisraeli na kuwateka baadhi yao.
And when king Arad the Chanaanite, who dwelt towards the south, had heard this, to wit, that Israel was come by the way of the spies, he fought against them, and overcoming them carried off their spoils.
2 Ndipo Israeli akaweka nadhiri hii kwa Bwana: “Ikiwa utawatia watu hawa mikononi mwetu, tutaiangamiza kabisa miji yao.”
But Israel binding himself by vow to the Lord, said: It thou wilt deliver this people into my hand, I will utterly destroy their cities.
3 Bwana akasikiliza ombi la Waisraeli, naye akawapa ushindi juu ya Wakanaani. Wakawaangamiza kabisa na miji yao; hivyo mahali pale pakaitwa Horma.
And the Lord heard the prayers of Israel, and delivered up the Chanaanite, and they cut them off and destroyed their cities: and they called the name of that place Horma, that is to say, Anathema.
4 Waisraeli wakasafiri kutoka mlima Hori kupitia njia inayoelekea Bahari ya Shamu, kuizunguka Edomu. Lakini watu wakakosa uvumilivu njiani,
And they marched from mount Hor, by the way that leadeth to the Red Sea, to compass the land of Edom. And the people began to be weary of their journey and labour:
5 wakamnungʼunikia Mungu na Mose, wakisema, “Kwa nini umetupandisha kutoka Misri ili tufe jangwani? Hakuna mkate! Hakuna maji! Nasi tunachukia sana chakula hiki duni!”
And speaking against God and Moses, they said: Why didst thou bring us out of Egypt, to die in the wilderness? There is no bread, nor have we any waters: our soul now loatheth this very light food.
6 Ndipo Bwana akapeleka nyoka wenye sumu katikati yao; wakawauma watu, nao Waisraeli wengi wakafa.
Wherefore the Lord sent among the people fiery serpents, which bit them and killed many of them.
7 Watu wakamjia Mose na kusema, “Tumetenda dhambi wakati tuliponena dhidi ya Bwana na dhidi yako. Mwombe Bwana ili atuondolee hawa nyoka.” Hivyo Mose akawaombea hao watu.
Upon which they came to Moses, and said: We have sinned, because we have spoken against the Lord and thee: pray that he may take away these serpents from us. And Moses prayed for the people.
8 Bwana akamwambia Mose, “Tengeneza nyoka wa shaba na umweke juu ya mti; yeyote aliyeumwa na nyoka anaweza kumtazama na akaishi tena.”
And the Lord said to him: Make brazen serpent, and set it up for a sign: whosoever being struck shall look on it, shall live.
9 Kwa hiyo Mose akatengeneza nyoka wa shaba na kumweka juu ya mti. Kisha wakati mtu yeyote aliumwa na nyoka, naye akamtazama yule nyoka wa shaba, aliishi.
Moses therefore made a brazen serpent, and set it up for a sign: which when they that were bitten looked upon, they were healed.
10 Waisraeli waliendelea na safari yao na wakapiga kambi huko Obothi.
And the children of Israel setting forwards camped in Oboth.
11 Kisha wakaondoka Obothi na kupiga kambi huko Iye-Abarimu, katika jangwa linalotazamana na Moabu kuelekea mawio ya jua.
And departing thence they pitched their tents in Jeabarim, in the wilderness, that faceth Moab toward the east.
12 Kutoka hapo waliendelea mbele wakapiga kambi kwenye Bonde la Zeredi.
And removing from thence, they came to the torrent Zared:
13 Wakasafiri kutoka hapo na kupiga kambi kando ya Mto Arnoni, ambao uko katika jangwa lililoenea hadi nchi ya Waamori. Arnoni ni mpaka wa Moabu, kati ya Moabu na Waamori.
Which they left and encamped over against Arnon, which is in the desert and standeth out on the borders of the Amorrhite. For Arnon is the border of Moab, dividing the Moabites and the Amorrhites.
14 Ndiyo sababu Kitabu cha Vita vya Bwana kinasema: “…Mji wa Wahebu nchini Seifa na mabonde ya Arnoni,
Wherefore it is said in the book of the wars of the Lord: As he did in the Red Sea, so will he do in the streams of Amen.
15 na miteremko ya mabonde inayofika hadi mji wa Ari na huelekea mpakani mwa Moabu.”
The rocks of the torrents were bowed down that they might rest in Ar, and lie down in the borders of the Moabites.
16 Kutoka hapo waliendelea mbele hadi kisima cha Beeri; kwenye kisima ambacho Bwana alimwambia Mose, “Wakusanye watu pamoja, nami nitawapa maji.”
When they went from that place, the well appeared whereof the Lord said to Moses: Gather the people together, and I will give them water.
17 Kisha Israeli akaimba wimbo huu: “Bubujika, ee kisima! Imba kuhusu maji,
Then Israel sung this song: Let the well spring up. They sung thereto:
18 kuhusu kisima ambacho kilichimbwa na wakuu, ambacho watu mashuhuri walikifukua, watu mashuhuri wakiwa na fimbo za utawala na bakora.” Kisha wakatoka jangwani kwenda Matana,
The well, which the princes dug, and the chiefs of the people prepared by the direction of the lawgiver, and with their staves. And they marched from the wilderness to Mathana.
19 kutoka Matana wakafika Nahalieli, kutoka Nahalieli wakafika Bamothi,
From Mathana unto Nahaliel: from Nahaliel unto Bamoth.
20 na kutoka Bamothi wakafika kwenye bonde lililoko Moabu, mahali ambapo kilele cha Pisga kinatazamana na nyika.
From Bamoth, is a valley in the country of Moab, to the top of Phasga, which looked towards the desert.
21 Israeli akawatuma wajumbe kumwambia Sihoni mfalme wa Waamori:
And Israel sent messengers to Sehon king of the Amorrhites, saying:
22 “Uturuhusu tupite katika nchi yako. Hatutageuka kando kwenda katika mashamba au mashamba ya mizabibu, ama kunywa maji kutoka kisima chochote. Tutasafiri kwenye njia kuu ya mfalme hata tutakapokuwa tumekwisha kupita katika nchi yako.”
I beseech thee that I may have leave to pass through thy land: we will not go aside into the fields or the vineyards, we will not drink waters of the wells, we will go the king’s highway, till we be past thy borders.
23 Lakini Sihoni hakumruhusu Israeli apite katika nchi yake. Alilikutanisha jeshi lake lote, wakaondoka kwenda jangwani ili kupigana na Israeli. Alipofika huko Yahazi, akapigana na Israeli.
And he would not grant that Israel should pass by his borders: but rather gathering an army, went forth to meet them in the desert, and came to Jasa, and fought against them.
24 Hata hivyo, Israeli alimshinda kwa upanga na kuiteka ardhi yake kutoka Arnoni mpaka Yaboki, lakini ni hadi kufikia nchi ya Waamoni tu, kwa sababu mipaka yake ilikuwa imezungushwa ukuta.
And he was slain by them with the edge of the sword, and they possessed his land from the Arnon unto the Jeboc, and to the confines of the children of Ammon: for the borders of the Ammonites, were kept with a strong garrison.
25 Israeli akaiteka miji yote ya Waamori na kuikalia, pamoja na Heshboni na makazi yote yanayoizunguka.
So Israel took all his cities, and dwelt in the cities of the Amorrhite, to wit, in Hesebon, and in the villages thereof.
26 Heshboni ulikuwa mji wa Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alikuwa amepigana dhidi ya mfalme wa Moabu aliyetangulia na akawa amechukua ardhi yake yote mpaka Arnoni.
Hesebon was the city of Sehon the king of the Amorrhites, who fought against the king of Moab: and took all the land, that had been of his dominions, as far as the Arnon.
27 Ndiyo sababu watunga mashairi husema: “Njoo Heshboni na ujengwe tena; mji wa Sihoni na ufanywe upya.
Therefore it is said in the proverb: Come into Hesebon, let the city of Sehon be built and set up:
28 “Moto uliwaka kutoka Heshboni, mwali wa moto kutoka mji wa Sihoni. Uliteketeza Ari ya Moabu, raiya wa mahali pa Arnoni palipoinuka.
A fire is gone out of Hesebon, a flame from the city of Sehon, and hath consumed Ar of the Moabites, and the inhabitants of the high places of the Arnon.
29 Ole wako, ee Moabu! Umeharibiwa, enyi watu wa Kemoshi! Amewatoa wanawe kuwa wakimbizi, na binti zake kama mateka kwa Mfalme Sihoni wa Waamori.
Woe to thee Moab: thou art undone, O people of Chamos. He hath given his sons to flight, and his daughters into captivity to Sehon the king of the Amorrhites.
30 “Lakini tumewashinda; Heshboni umeharibiwa hadi Diboni. Tumebomoa hadi kufikia Nofa, ulioenea hadi Medeba.”
Their yoke is perished from Hesebon unto Dibon, they came weary to Nophe, and unto Medaba.
31 Kwa hiyo Israeli akaishi katika nchi ya Waamori.
So Israel dwelt in the land of the Amorrhite.
32 Baada ya Mose kutuma wapelelezi kwenda mji wa Yazeri, Waisraeli waliteka viunga vya mji huo na kuwafukuza Waamori waliokuwa wanaishi huko.
And Moses sent some to take a view of Jazer: and they took the villages of it, and conquered the inhabitants.
33 Kisha wakageuka na kwenda katika njia inayoelekea Bashani, naye Ogu mfalme wa Bashani pamoja na jeshi lake lote wakatoka kupigana nao huko Edrei.
And they turned themselves, and went up by the way of Basan, and Og the king of Basan came against them with all his people, to fight in Edrai.
34 Bwana akamwambia Mose, “Usimwogope Ogu, kwa sababu nimeshamkabidhi mikononi mwako, pamoja na jeshi lake lote na nchi yake. Mtendee kama ulivyomtendea Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni.”
And the Lord said to Moses: Fear him not, for I have delivered him and all his people, and his country into thy hand: and thou shalt do to him as thou didst to Sehon the king of the Amorrhites, the inhabitant of Hesebon.
35 Kwa hiyo wakamuua, pamoja na wanawe na jeshi lake lote, bila ya kumwacha hata mtu mmoja hai. Nao wakaimiliki nchi yake.
So they slew him also with his sons, and all his people, not letting any one escape, and they possessed his land.

< Hesabu 21 >