< Hesabu 21 >

1 Mfalme wa Kikanaani wa Aradi aliyeishi huko Negebu aliposikia kwamba Waisraeli walikuwa wanakuja kwa njia ya Atharimu, aliwashambulia Waisraeli na kuwateka baadhi yao.
And when king Arad the Canaanite, who was living toward the south, had heard this, namely, that Israel had arrived by the way of spies, he fought against them. And proving to be the victor, he led away prey from them.
2 Ndipo Israeli akaweka nadhiri hii kwa Bwana: “Ikiwa utawatia watu hawa mikononi mwetu, tutaiangamiza kabisa miji yao.”
But Israel, obliging himself by a vow to the Lord, said: “If you deliver this people into my hand, I will wipe away their cities.”
3 Bwana akasikiliza ombi la Waisraeli, naye akawapa ushindi juu ya Wakanaani. Wakawaangamiza kabisa na miji yao; hivyo mahali pale pakaitwa Horma.
And the Lord heard the prayers of Israel, and he delivered the Canaanite, whom they put to death, overthrowing his cities. And they called the name of that place Hormah, that is, Anathema.
4 Waisraeli wakasafiri kutoka mlima Hori kupitia njia inayoelekea Bahari ya Shamu, kuizunguka Edomu. Lakini watu wakakosa uvumilivu njiani,
Then they set out from mount Hor, by the way that leads to the Red Sea, to circle around the land of Edom. And the people began to tire of their journey and hardships.
5 wakamnungʼunikia Mungu na Mose, wakisema, “Kwa nini umetupandisha kutoka Misri ili tufe jangwani? Hakuna mkate! Hakuna maji! Nasi tunachukia sana chakula hiki duni!”
And speaking against God and Moses, they said: “Why did you lead us away from Egypt, so as to die in the wilderness? Bread is lacking; there are no waters. Our soul is now nauseous over this very light food.”
6 Ndipo Bwana akapeleka nyoka wenye sumu katikati yao; wakawauma watu, nao Waisraeli wengi wakafa.
For this reason, the Lord sent fiery serpents among the people, which wounded or killed many of them.
7 Watu wakamjia Mose na kusema, “Tumetenda dhambi wakati tuliponena dhidi ya Bwana na dhidi yako. Mwombe Bwana ili atuondolee hawa nyoka.” Hivyo Mose akawaombea hao watu.
And so they went to Moses, and they said: “We have sinned, because we have spoken against the Lord and against you. Pray, so that he may take away these serpents from us.” And Moses prayed for the people.
8 Bwana akamwambia Mose, “Tengeneza nyoka wa shaba na umweke juu ya mti; yeyote aliyeumwa na nyoka anaweza kumtazama na akaishi tena.”
And the Lord said to him: “Make a bronze serpent, and place it as a sign. Whoever, having been struck, gazes upon it, shall live.”
9 Kwa hiyo Mose akatengeneza nyoka wa shaba na kumweka juu ya mti. Kisha wakati mtu yeyote aliumwa na nyoka, naye akamtazama yule nyoka wa shaba, aliishi.
Therefore, Moses made a bronze serpent, and he placed it as a sign. When those who had been struck gazed upon it, they were healed.
10 Waisraeli waliendelea na safari yao na wakapiga kambi huko Obothi.
And the sons of Israel, setting out, made camp at Oboth.
11 Kisha wakaondoka Obothi na kupiga kambi huko Iye-Abarimu, katika jangwa linalotazamana na Moabu kuelekea mawio ya jua.
Having departed from there, they pitched their tents at Iye-abarim, in the wilderness, which looks out toward Moab, opposite the eastern region.
12 Kutoka hapo waliendelea mbele wakapiga kambi kwenye Bonde la Zeredi.
And moving from there, they arrived at the Torrent of Zared.
13 Wakasafiri kutoka hapo na kupiga kambi kando ya Mto Arnoni, ambao uko katika jangwa lililoenea hadi nchi ya Waamori. Arnoni ni mpaka wa Moabu, kati ya Moabu na Waamori.
Having left that place behind, they then made camp opposite Arnon, which is in the desert, and which juts out at the borders of the Amorite. For certainly Arnon is at the limit of Moab, dividing the Moabites and the Amorites.
14 Ndiyo sababu Kitabu cha Vita vya Bwana kinasema: “…Mji wa Wahebu nchini Seifa na mabonde ya Arnoni,
About this place, it is said in the book of the wars of the Lord: “As he did at the Red Sea, so will he do at the Torrents of Arnon.”
15 na miteremko ya mabonde inayofika hadi mji wa Ari na huelekea mpakani mwa Moabu.”
The stones of the torrents were bent, so that they might rest in Ar and lie back within the borders of the Moabites.
16 Kutoka hapo waliendelea mbele hadi kisima cha Beeri; kwenye kisima ambacho Bwana alimwambia Mose, “Wakusanye watu pamoja, nami nitawapa maji.”
Beyond that place appeared a well, about which the Lord said to Moses: “Gather the people together, and I will give them water.”
17 Kisha Israeli akaimba wimbo huu: “Bubujika, ee kisima! Imba kuhusu maji,
Then Israel sang this verse: “Let the well rise up.” They sang:
18 kuhusu kisima ambacho kilichimbwa na wakuu, ambacho watu mashuhuri walikifukua, watu mashuhuri wakiwa na fimbo za utawala na bakora.” Kisha wakatoka jangwani kwenda Matana,
“The well, the leaders dug it, and the commanders of the multitude prepared it, at the direction of the lawgiver, and with their staffs.”
19 kutoka Matana wakafika Nahalieli, kutoka Nahalieli wakafika Bamothi,
They went from the wilderness to Mattanah, from Mattanah to Nahaliel, from Nahaliel to Bamoth,
20 na kutoka Bamothi wakafika kwenye bonde lililoko Moabu, mahali ambapo kilele cha Pisga kinatazamana na nyika.
from Bamoth, a valley in the region of Moab, to the top of Pisgah, which looks out opposite the desert.
21 Israeli akawatuma wajumbe kumwambia Sihoni mfalme wa Waamori:
Then Israel sent messengers to Sihon, the king of the Amorites, saying:
22 “Uturuhusu tupite katika nchi yako. Hatutageuka kando kwenda katika mashamba au mashamba ya mizabibu, ama kunywa maji kutoka kisima chochote. Tutasafiri kwenye njia kuu ya mfalme hata tutakapokuwa tumekwisha kupita katika nchi yako.”
“I beg you to permit me to cross through your land. We will not turn aside into the fields or the vineyards. We will not drink waters from the wells. We will travel by the royal way, until we have passed your borders.”
23 Lakini Sihoni hakumruhusu Israeli apite katika nchi yake. Alilikutanisha jeshi lake lote, wakaondoka kwenda jangwani ili kupigana na Israeli. Alipofika huko Yahazi, akapigana na Israeli.
And he was not willing to allow Israel to cross through his borders. But instead, gathering an army, he went out to meet them in the desert, and he arrived at Jahaz and fought against them.
24 Hata hivyo, Israeli alimshinda kwa upanga na kuiteka ardhi yake kutoka Arnoni mpaka Yaboki, lakini ni hadi kufikia nchi ya Waamoni tu, kwa sababu mipaka yake ilikuwa imezungushwa ukuta.
And he was struck down by them with the edge of the sword, and they possessed his land from Arnon, even to Jabbok and the sons of Ammon. For the borders of the Ammonites were held by a strong fortress.
25 Israeli akaiteka miji yote ya Waamori na kuikalia, pamoja na Heshboni na makazi yote yanayoizunguka.
Therefore, Israel took all his cities and lived in the cities of the Amorite, namely, in Heshbon and its villages.
26 Heshboni ulikuwa mji wa Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alikuwa amepigana dhidi ya mfalme wa Moabu aliyetangulia na akawa amechukua ardhi yake yote mpaka Arnoni.
Heshbon was the city of Sihon, the king of the Amorites, who fought against the king of Moab. And he took all the land, which had been under his sovereignty, as far as Arnon.
27 Ndiyo sababu watunga mashairi husema: “Njoo Heshboni na ujengwe tena; mji wa Sihoni na ufanywe upya.
About this, it is said in the proverb: “Enter into Heshbon. Let the city of Sihon be established and built.
28 “Moto uliwaka kutoka Heshboni, mwali wa moto kutoka mji wa Sihoni. Uliteketeza Ari ya Moabu, raiya wa mahali pa Arnoni palipoinuka.
A fire has gone forth from Heshbon, a flame from the town of Sihon, and it has devoured Ar of the Moabites, and the inhabitants of the heights of Arnon.
29 Ole wako, ee Moabu! Umeharibiwa, enyi watu wa Kemoshi! Amewatoa wanawe kuwa wakimbizi, na binti zake kama mateka kwa Mfalme Sihoni wa Waamori.
Woe to you, Moab! You are perishing, O people of Chemosh. He gave flight to his sons, and he gave the daughters into captivity, to the king of the Amorites, Sihon.
30 “Lakini tumewashinda; Heshboni umeharibiwa hadi Diboni. Tumebomoa hadi kufikia Nofa, ulioenea hadi Medeba.”
Their yoke has been scattered from Heshbon even to Dibon. They have passed through, wearily, into Nophah, and as far as Medeba.”
31 Kwa hiyo Israeli akaishi katika nchi ya Waamori.
And so Israel lived in the land of the Amorite.
32 Baada ya Mose kutuma wapelelezi kwenda mji wa Yazeri, Waisraeli waliteka viunga vya mji huo na kuwafukuza Waamori waliokuwa wanaishi huko.
And Moses sent some to explore Jazer. These captured its villages and possessed its inhabitants.
33 Kisha wakageuka na kwenda katika njia inayoelekea Bashani, naye Ogu mfalme wa Bashani pamoja na jeshi lake lote wakatoka kupigana nao huko Edrei.
And they turned themselves and ascended, along the way of Bashan. And Og, the king of Bashan, met them with all his people, to fight at Edrei.
34 Bwana akamwambia Mose, “Usimwogope Ogu, kwa sababu nimeshamkabidhi mikononi mwako, pamoja na jeshi lake lote na nchi yake. Mtendee kama ulivyomtendea Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni.”
And the Lord said to Moses: “Do not be afraid of him. For I have delivered him, and all his people, as well as his land, into your hand. And you shall do to him just as you did to Sihon, the king of the Amorites, the inhabitant of Heshbon.”
35 Kwa hiyo wakamuua, pamoja na wanawe na jeshi lake lote, bila ya kumwacha hata mtu mmoja hai. Nao wakaimiliki nchi yake.
Therefore, they struck him down also, with his sons, and all his people, even to utter destruction, and they possessed his land.

< Hesabu 21 >