< Hesabu 20 >

1 Katika mwezi wa kwanza jumuiya yote ya Kiisraeli ilifika kwenye Jangwa la Sini, nao wakakaa Kadeshi. Miriamu akafa huko na kuzikwa.
And the sones of Israel and al the multitude camen in to the deseert of Syn, in the firste monethe. And the puple dwellide in Cades; and Marie was deed there, and biried in the same place.
2 Mahali hapo hapakuwa na maji kwa ajili ya jumuiya hiyo, nao wakakusanyika ili kumpinga Mose na Aroni.
And whanne the puple hadde nede to watir, thei yeden togidere ayens Moises and Aaron; and thei weren turned in to dissensioun,
3 Watu wakagombana na Mose, na kusema, “Laiti tungelikufa wakati ndugu zetu walipoanguka na kufa mbele za Bwana!
and seiden, We wolden that we hadden perischid among oure britheren bifor the Lord.
4 Kwa nini mmeileta jumuiya ya Bwana kwenye jangwa hili, ili tufe humu, sisi na mifugo yetu?
Whi han ye led out the chirche of the Lord in to wildirnesse, that bothe we and oure beestis die?
5 Kwa nini mmetupandisha kutoka Misri mpaka mahali hapa pa kutisha? Hapa hakuna nafaka wala tini, zabibu au makomamanga. Wala hapa hakuna maji ya kunywa!”
Whi han ye maad vs to stie from Egipt, and han brouyt vs in to this werste place, which may not be sowun, which nether bryngith forth fige tre, nether vineris, nether pumgranatis, ferthermore and hath not watir to drynke?
6 Mose na Aroni wakaondoka pale kwenye kusanyiko mpaka kwenye mlango wa Hema la Kukutania na kuanguka kifudifudi, nao utukufu wa Bwana ukawatokea.
And whanne the multitude was left, Moises and Aaron entriden in to the tabernacle of boond of pees, and felden lowe to erthe, and crieden to God, and seiden, Lord God, here the cry of this puple, and opene to hem thi tresour, a welle of quyk watir, that whanne thei ben fillid, the grutchyng of hem ceesse. And the glorie of the Lord apperide on hem;
7 Bwana akamwambia Mose,
and the Lord spak to Moises,
8 “Chukua ile fimbo, na wewe na ndugu yako Aroni mkusanye kusanyiko pamoja. Nena na ule mwamba mbele ya macho yao, nao utatoa maji yake. Utatoa maji kutoka huo mwamba kwa ajili ya jumuiya ili wao na mifugo yao waweze kunywa.”
and seide, Take the yerde, and gadere the puple, thou, and Aaron thi brother; and speke ye to the stoon bifore hem, and it schal yyue watris. And whanne thou hast led watir out of the stoon, al the multitude schal drynke, and the beestis therof `schulden drynke.
9 Kwa hiyo Mose akaichukua hiyo fimbo kutoka pale ilipokuwa mbele za Bwana kama alivyomwagiza.
Therfor Moises took the yerde that was in the `siyt of the Lord, as the Lord comaundide to hym,
10 Mose na Aroni wakakusanya kusanyiko pamoja mbele ya huo mwamba, naye Mose akawaambia, “Sikilizeni, enyi waasi. Je, ni lazima tuwatoleeni maji kutoka mwamba huu?”
whanne the multitude was gaderid bifor the stoon; and he seide to hem, Here ye, rebel and vnbileueful; whether we moun brynge out of this stoon watir to you?
11 Ndipo Mose akainua mkono wake na kuupiga mwamba mara mbili kwa fimbo yake. Maji yakabubujika, nayo jumuiya na mifugo yao wakanywa.
And whanne Moises hadde reisid the hond, and hadde smyte the flynt twies with the yerde, largeste watris yeden out, so that the puple drank, and the beestis drunken.
12 Lakini Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Kwa sababu hamkuniamini mimi kiasi cha kuniheshimu kama mtakatifu machoni pa Waisraeli, hamtaiingiza jumuiya hii katika nchi ninayowapa.”
And the Lord seide to Moises and to Aaron, For ye bileueden not to me, that ye schulden halewe me bifor the sones of Israel, ye schulen not lede these puples in to the lond which Y schal yyue to hem.
13 Haya yalikuwa maji ya Meriba, mahali pale ambapo Waisraeli waligombana na Bwana, naye akajionyesha mwenyewe huko kuwa mtakatifu katikati yao.
This is the watir of ayenseiyng; there the sones of Israel stryueden ayens the Lord, and he was halewid in hem.
14 Mose akawatuma wajumbe kutoka Kadeshi kwenda kwa mfalme wa Edomu, akisema: “Hili ndilo ndugu yako Israeli asemalo: Wewe unafahamu juu ya taabu zote ambazo zimetupata.
In the meene tyme Moises sente messangeres fro Cades to the kyng of Edom, whiche seiden, Israel thi brother sendith these thinges. Thou knowist al the trauel that took vs,
15 Baba zetu walishuka Misri, nasi tumeishi huko miaka mingi. Wamisri walitutesa sisi na baba zetu,
hou oure fadris yeden doun in to Egipt, and we dwelliden there myche tyme, and Egipcians turmentiden vs and oure fadris; and hou we crieden to the Lord,
16 lakini tulipomlilia Bwana, alisikia kilio chetu na akamtuma malaika akatutoa Misri. “Sasa tupo hapa Kadeshi, mji ulio mpakani mwa nchi yako.
and he herde vs, and sente an aungel that ledde vs out of Egipt. And lo! we ben set in the citee of Cades, which is in thi laste coostis,
17 Tafadhali turuhusu tupite katika nchi yako. Hatutapita katika shamba lolote, wala shamba la mizabibu, au kunywa maji kutoka kwenye kisima chochote. Tutasafiri kufuata njia kuu ya mfalme, na hatutageuka kulia wala kushoto mpaka tuwe tumeshapita nchi yako.”
and we bisechen that it be leueful to vs to passe thorou thi lond; we schulen not go bi feeldis, nether bi vyneris, nether we schulen drynke watris of thi pittis; but we schulen go in the comyn weie, and we schulen not bowe to the riyt side, nether to the left side, til we passen thi termes.
18 Lakini mfalme wa Edomu akajibu: “Hamtapita hapa; kama mkijaribu kupita, tutatoka na kuwashambulia kwa upanga.”
To whom Edom answeride, Ye schulen not passe bi me, ellis Y schal be armed, and come ayens thee.
19 Waisraeli wakajibu: “Sisi tutafuata njia kuu; tena ikiwa sisi au mifugo yetu tutakunywa tone la maji yenu, tutalilipia. Sisi tunataka tu kupita kwa miguu, wala si kitu kingine chochote.”
And the sones of Israel seiden, We schulen go bi the weie comynli vsid, and if we and oure beestis drynken thi watris, we schulen yyue that that is iust; noon hardnesse schal be in prijs, onely passe we swiftli.
20 Watu wa Edomu wakajibu tena: “Hamwezi kupita hapa.” Ndipo watu wa Edomu wakatoka dhidi ya Waisraeli, jeshi kubwa lenye nguvu.
And he answeride, Ye schulen not passe. And anoon he yede out ayens Israel, with a multitude without noumbre, and `strong hond,
21 Kwa kuwa Waedomu waliwakatalia Waisraeli kupita katika nchi yao, Israeli wakageuka, wakawaacha.
nether he wolde assente to Israel bisechynge, that he schulde graunte passage bi hise coostis. Wherfor Israel turnede awey fro hym.
22 Jumuiya yote ya Kiisraeli ikaondoka kutoka Kadeshi, wakafika kwenye Mlima Hori.
And whanne thei hadden moued tentis fro Cades, thei camen in to the hil of Hor, which is in the endis of the lond of Edom;
23 Kwenye Mlima Hori, karibu na mpaka wa Edomu, Bwana akamwambia Mose na Aroni,
where the Lord spak to Moyses and seide, Aaron go to his puples;
24 “Aroni atakusanywa pamoja na watu wake. Hataingia katika nchi ninayowapa Waisraeli, kwa sababu ninyi wawili mliasi dhidi ya agizo langu kwenye maji ya Meriba.
for he schal not entre in to the lond which Y yaf to the sones of Israel, for he was vnbileueful to my mouth, at the watris of ayenseiyng.
25 Watwae Aroni na Eleazari mwanawe, na uwapandishe juu katika Mlima wa Hori.
Take thou Aaron, and his sone with hym, and thou schalt lede hem in to the hil of Hor;
26 Mvue Aroni mavazi yake, na umvike Eleazari mwanawe, kwa maana Aroni atakusanywa pamoja na watu wake; atakufa huko.”
and whanne thou hast maad nakid the fadir of his cloth, thou schalt clothe `with it Eleazar, his sone, and Aaron schal be gederid, and schal die there.
27 Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza: Wakapanda Mlima Hori mbele ya macho ya jumuiya yote ya Kiisraeli.
Moises dide as the Lord comaundide; and thei stieden in to the hil of Hor, bifor al the multitude.
28 Mose akamvua Aroni mavazi yake na kumvika mwanawe Eleazari mavazi hayo. Naye Aroni akafia pale juu ya mlima. Kisha Mose na Eleazari wakateremka kutoka mlimani.
And whanne he hadde maad nakid Aaron of hise clothis, he clothide with tho Eleazar, his sone. Sotheli whanne Aaron was deed in the `cop of the hil, Moises cam doun with Eleazar.
29 Jumuiya yote ilipofahamu kwamba Aroni amekufa, jamaa yote ya Kiisraeli wakamwomboleza kwa siku thelathini.
Sotheli al the multitude siy that Aaron was deed, and wepte on hym thretti daies, bi alle her meyness.

< Hesabu 20 >