< Hesabu 20 >
1 Katika mwezi wa kwanza jumuiya yote ya Kiisraeli ilifika kwenye Jangwa la Sini, nao wakakaa Kadeshi. Miriamu akafa huko na kuzikwa.
Then the children of Israel came with ye whole Congregation to the desert of Zin in the first moneth, and the people abode at Cadesh: where Miriam died, and was buried there.
2 Mahali hapo hapakuwa na maji kwa ajili ya jumuiya hiyo, nao wakakusanyika ili kumpinga Mose na Aroni.
But there was no water for the Congregation, and they assembled them selues against Moses and against Aaron.
3 Watu wakagombana na Mose, na kusema, “Laiti tungelikufa wakati ndugu zetu walipoanguka na kufa mbele za Bwana!
And the people chode with Moses, and spake, saying, Would God we had perished, when our brethren died before the Lord.
4 Kwa nini mmeileta jumuiya ya Bwana kwenye jangwa hili, ili tufe humu, sisi na mifugo yetu?
Why haue ye thus brought the Congregation of the Lord vnto his wildernesse, that both we, and our cattell should die there?
5 Kwa nini mmetupandisha kutoka Misri mpaka mahali hapa pa kutisha? Hapa hakuna nafaka wala tini, zabibu au makomamanga. Wala hapa hakuna maji ya kunywa!”
Wherefore nowe haue yee made vs to come vp from Egypt, to bring vs into this miserable place, which is no place of seede, nor figges, nor vines, nor pomegranates? neither is there any water to drinke.
6 Mose na Aroni wakaondoka pale kwenye kusanyiko mpaka kwenye mlango wa Hema la Kukutania na kuanguka kifudifudi, nao utukufu wa Bwana ukawatokea.
Then Moses and Aaron went from the assemblie vnto the doore of the Tabernacle of the Congregation, and fell vpon their faces: and the glory of the Lord appeared vnto them.
And the Lord spake vnto Moses, saying,
8 “Chukua ile fimbo, na wewe na ndugu yako Aroni mkusanye kusanyiko pamoja. Nena na ule mwamba mbele ya macho yao, nao utatoa maji yake. Utatoa maji kutoka huo mwamba kwa ajili ya jumuiya ili wao na mifugo yao waweze kunywa.”
Take the rod, and gather thou and thy brother Aaron the Congregation together, and speake yee vnto the rocke before their eyes, and it shall giue foorth his water, and thou shalt bring them water out of the rocke: so thou shalt giue the Congregation, and their beastes drinke.
9 Kwa hiyo Mose akaichukua hiyo fimbo kutoka pale ilipokuwa mbele za Bwana kama alivyomwagiza.
Then Moses tooke the rod from before the Lord, as he had commanded him.
10 Mose na Aroni wakakusanya kusanyiko pamoja mbele ya huo mwamba, naye Mose akawaambia, “Sikilizeni, enyi waasi. Je, ni lazima tuwatoleeni maji kutoka mwamba huu?”
And Moses and Aaron gathered the Congregation together before the rocke, and Moses sayd vnto them, Heare nowe, ye rebels: shall we bring you water out of this rocke?
11 Ndipo Mose akainua mkono wake na kuupiga mwamba mara mbili kwa fimbo yake. Maji yakabubujika, nayo jumuiya na mifugo yao wakanywa.
Then Moses lift vp his hande, and with his rod he smote the rocke twise, and the water came out aboundantly: so the Congregation, and their beastes dranke.
12 Lakini Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Kwa sababu hamkuniamini mimi kiasi cha kuniheshimu kama mtakatifu machoni pa Waisraeli, hamtaiingiza jumuiya hii katika nchi ninayowapa.”
Againe the Lord spake vnto Moses, and to Aaron, Because ye beleeued me not, to sanctifie mee in the presence of the children of Israel, therefore ye shall not bring this Congregation into the land which I haue giuen them.
13 Haya yalikuwa maji ya Meriba, mahali pale ambapo Waisraeli waligombana na Bwana, naye akajionyesha mwenyewe huko kuwa mtakatifu katikati yao.
This is the water of Meribah, because the children of Israel stroue with the Lord, and hee was sanctified in them.
14 Mose akawatuma wajumbe kutoka Kadeshi kwenda kwa mfalme wa Edomu, akisema: “Hili ndilo ndugu yako Israeli asemalo: Wewe unafahamu juu ya taabu zote ambazo zimetupata.
Then Moses sent messengers from Kadesh vnto the king of Edom, saying, Thus sayth thy brother Israel, Thou knowest all the trauaile that we haue had,
15 Baba zetu walishuka Misri, nasi tumeishi huko miaka mingi. Wamisri walitutesa sisi na baba zetu,
How our fathers went downe into Egypt, and we dwelt in Egypt a long time, where the Egyptians handled vs euill and our fathers.
16 lakini tulipomlilia Bwana, alisikia kilio chetu na akamtuma malaika akatutoa Misri. “Sasa tupo hapa Kadeshi, mji ulio mpakani mwa nchi yako.
But when we cried vnto the Lord, he heard our voyce, and sent an Angel, and hath brought vs out of Egypt, and beholde, wee are in the citie Kadesh, in thine vtmost border.
17 Tafadhali turuhusu tupite katika nchi yako. Hatutapita katika shamba lolote, wala shamba la mizabibu, au kunywa maji kutoka kwenye kisima chochote. Tutasafiri kufuata njia kuu ya mfalme, na hatutageuka kulia wala kushoto mpaka tuwe tumeshapita nchi yako.”
I pray thee that we may passe through thy countrey: we will not goe through the fieldes nor the vineyardes, neither will we drinke of the water of the welles: we will goe by the kings way, and neither turne vnto the right hand nor to the left, vntill we be past thy borders.
18 Lakini mfalme wa Edomu akajibu: “Hamtapita hapa; kama mkijaribu kupita, tutatoka na kuwashambulia kwa upanga.”
And Edom answered him, Thou shalt not passe by mee, least I come out against thee with the sword.
19 Waisraeli wakajibu: “Sisi tutafuata njia kuu; tena ikiwa sisi au mifugo yetu tutakunywa tone la maji yenu, tutalilipia. Sisi tunataka tu kupita kwa miguu, wala si kitu kingine chochote.”
Then the children of Israel said vnto him, We will goe vp by the hie way: and if I and my cattell drinke of thy water, I will then pay for it: I will onely (without any harme) goe through on my feete.
20 Watu wa Edomu wakajibu tena: “Hamwezi kupita hapa.” Ndipo watu wa Edomu wakatoka dhidi ya Waisraeli, jeshi kubwa lenye nguvu.
Hee answered againe, Thou shalt not goe through. The Edom came out against him with much people, and with a mightie power.
21 Kwa kuwa Waedomu waliwakatalia Waisraeli kupita katika nchi yao, Israeli wakageuka, wakawaacha.
Thus Edom denyed to giue Israel passage through his countrey: wherefore Israel turned away from him.
22 Jumuiya yote ya Kiisraeli ikaondoka kutoka Kadeshi, wakafika kwenye Mlima Hori.
And when the children of Israel with al the Congregation departed from Kadesh, they came vnto the mount Hor.
23 Kwenye Mlima Hori, karibu na mpaka wa Edomu, Bwana akamwambia Mose na Aroni,
And the Lord spake vnto Moses and to Aaron in the mount Hor neere the coast of the land of Edom, saying,
24 “Aroni atakusanywa pamoja na watu wake. Hataingia katika nchi ninayowapa Waisraeli, kwa sababu ninyi wawili mliasi dhidi ya agizo langu kwenye maji ya Meriba.
Aaron shall be gathered vnto his people: for hee shall not enter into the lande, which I haue giuen vnto the children of Israel, because ye disobeyed my commandement at the water of Meribah.
25 Watwae Aroni na Eleazari mwanawe, na uwapandishe juu katika Mlima wa Hori.
Take Aaron and Eleazar his sonne, and bring them vp into the mount Hor,
26 Mvue Aroni mavazi yake, na umvike Eleazari mwanawe, kwa maana Aroni atakusanywa pamoja na watu wake; atakufa huko.”
And cause Aaron to put off his garmentes and put them vpon Eleazar his sonne: for Aaron shall be gathered to his fathers, and shall die there.
27 Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza: Wakapanda Mlima Hori mbele ya macho ya jumuiya yote ya Kiisraeli.
And Moses did as the Lord had commanded: and they went vp into the mount Hor, in the sight of all the Congregation.
28 Mose akamvua Aroni mavazi yake na kumvika mwanawe Eleazari mavazi hayo. Naye Aroni akafia pale juu ya mlima. Kisha Mose na Eleazari wakateremka kutoka mlimani.
And Moses put off Aarons clothes, and put them vpon Eleazar his sonne: so Aaron dyed there in the top of the mount: and Moses and Eleazar came downe from off the mount.
29 Jumuiya yote ilipofahamu kwamba Aroni amekufa, jamaa yote ya Kiisraeli wakamwomboleza kwa siku thelathini.
When al the Congregation sawe that Aaron was dead, al the house of Israel wept for Aaron thirtie dayes.