< Hesabu 20 >

1 Katika mwezi wa kwanza jumuiya yote ya Kiisraeli ilifika kwenye Jangwa la Sini, nao wakakaa Kadeshi. Miriamu akafa huko na kuzikwa.
And the sons of Israel, and the entire multitude, went into the desert of Sin, in the first month. And the people stayed at Kadesh. And Miriam died there, and she was buried in the same place.
2 Mahali hapo hapakuwa na maji kwa ajili ya jumuiya hiyo, nao wakakusanyika ili kumpinga Mose na Aroni.
And when the people were in need of water, they came together against Moses and Aaron.
3 Watu wakagombana na Mose, na kusema, “Laiti tungelikufa wakati ndugu zetu walipoanguka na kufa mbele za Bwana!
And as it turned into sedition, they said: “If only we had perished among our brothers in the sight of the Lord.
4 Kwa nini mmeileta jumuiya ya Bwana kwenye jangwa hili, ili tufe humu, sisi na mifugo yetu?
Why have you led away the Church of the Lord, into the wilderness, so that both we and our cattle would die?
5 Kwa nini mmetupandisha kutoka Misri mpaka mahali hapa pa kutisha? Hapa hakuna nafaka wala tini, zabibu au makomamanga. Wala hapa hakuna maji ya kunywa!”
Why did you cause us to ascend from Egypt, and why have you led us into this most wretched place, which is not able to be sown, which does not produce figs, or vines, or pomegranates, and which, moreover, does not even have water to drink?”
6 Mose na Aroni wakaondoka pale kwenye kusanyiko mpaka kwenye mlango wa Hema la Kukutania na kuanguka kifudifudi, nao utukufu wa Bwana ukawatokea.
And Moses and Aaron, dismissing the multitude, entered the tabernacle of the covenant, and they fell prone on the ground, and they cried out to the Lord, and they said: “O Lord God, listen to the outcry of this people, and open for them, from your storehouse, a fountain of living water, so that, being satisfied, their murmuring may cease.” And the glory of the Lord appeared over them.
7 Bwana akamwambia Mose,
And the Lord spoke to Moses, saying:
8 “Chukua ile fimbo, na wewe na ndugu yako Aroni mkusanye kusanyiko pamoja. Nena na ule mwamba mbele ya macho yao, nao utatoa maji yake. Utatoa maji kutoka huo mwamba kwa ajili ya jumuiya ili wao na mifugo yao waweze kunywa.”
“Take the rod, and gather the people, you and your brother Aaron, and speak to the rock before them, and it shall bestow waters. And when you have brought forth water from the rock, the entire multitude and their cattle shall drink.”
9 Kwa hiyo Mose akaichukua hiyo fimbo kutoka pale ilipokuwa mbele za Bwana kama alivyomwagiza.
Therefore, Moses took the rod, which was in the sight of the Lord, just as he had instructed him.
10 Mose na Aroni wakakusanya kusanyiko pamoja mbele ya huo mwamba, naye Mose akawaambia, “Sikilizeni, enyi waasi. Je, ni lazima tuwatoleeni maji kutoka mwamba huu?”
And having gathered the multitude before the rock, he said to them: “Listen, you who are rebellious and unbelieving. Would we be able to cast out water from this rock?”
11 Ndipo Mose akainua mkono wake na kuupiga mwamba mara mbili kwa fimbo yake. Maji yakabubujika, nayo jumuiya na mifugo yao wakanywa.
And when Moses had lifted up his hand, striking the stone twice with the rod, very great waters went forth, so much so that the people and their cattle were able to drink.
12 Lakini Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Kwa sababu hamkuniamini mimi kiasi cha kuniheshimu kama mtakatifu machoni pa Waisraeli, hamtaiingiza jumuiya hii katika nchi ninayowapa.”
And the Lord said to Moses and Aaron, “Because you did not believe me, so as to sanctify me before the sons of Israel, you shall not lead this people into the land, which I will give to them.”
13 Haya yalikuwa maji ya Meriba, mahali pale ambapo Waisraeli waligombana na Bwana, naye akajionyesha mwenyewe huko kuwa mtakatifu katikati yao.
This is the Water of Contradiction, where the sons of Israel were quarreling against the Lord, and he was sanctified in them.
14 Mose akawatuma wajumbe kutoka Kadeshi kwenda kwa mfalme wa Edomu, akisema: “Hili ndilo ndugu yako Israeli asemalo: Wewe unafahamu juu ya taabu zote ambazo zimetupata.
Meanwhile, Moses sent messengers from Kadesh to the king of Edom. They said: “Your brother Israel says this: You know of all the hardships which have overtaken us,
15 Baba zetu walishuka Misri, nasi tumeishi huko miaka mingi. Wamisri walitutesa sisi na baba zetu,
how our fathers descended into Egypt, and we lived there for a long time, and the Egyptians afflicted both us and our fathers,
16 lakini tulipomlilia Bwana, alisikia kilio chetu na akamtuma malaika akatutoa Misri. “Sasa tupo hapa Kadeshi, mji ulio mpakani mwa nchi yako.
and how we cried out to the Lord, and he heeded us and sent an Angel, who led us away from Egypt. Behold, we are situated in the city of Kadesh, which is at the extremity of your borders.
17 Tafadhali turuhusu tupite katika nchi yako. Hatutapita katika shamba lolote, wala shamba la mizabibu, au kunywa maji kutoka kwenye kisima chochote. Tutasafiri kufuata njia kuu ya mfalme, na hatutageuka kulia wala kushoto mpaka tuwe tumeshapita nchi yako.”
And we beg you to permit us to cross through your land. We will not go through the fields, nor through the vineyards; we will not drink the waters of your wells, but we will travel by the public ways, neither turning aside to the right, nor to the left, until we have passed your borders.”
18 Lakini mfalme wa Edomu akajibu: “Hamtapita hapa; kama mkijaribu kupita, tutatoka na kuwashambulia kwa upanga.”
Edom responded to them: “You shall not cross through me, otherwise, I will meet you armed.”
19 Waisraeli wakajibu: “Sisi tutafuata njia kuu; tena ikiwa sisi au mifugo yetu tutakunywa tone la maji yenu, tutalilipia. Sisi tunataka tu kupita kwa miguu, wala si kitu kingine chochote.”
And the sons of Israel said: “We will travel by the well-trodden path. And if we or our cattle drink from your waters, we will give you what is just. There shall be no difficulty in the price, only let us cross through quickly.”
20 Watu wa Edomu wakajibu tena: “Hamwezi kupita hapa.” Ndipo watu wa Edomu wakatoka dhidi ya Waisraeli, jeshi kubwa lenye nguvu.
But he answered, “You shall not cross.” And immediately he went out to meet them with a countless multitude and a strong hand;
21 Kwa kuwa Waedomu waliwakatalia Waisraeli kupita katika nchi yao, Israeli wakageuka, wakawaacha.
neither was he willing to agree to their petition to concede passage through his borders. For this reason, Israel diverted away from him.
22 Jumuiya yote ya Kiisraeli ikaondoka kutoka Kadeshi, wakafika kwenye Mlima Hori.
And when they had moved the camp from Kadesh, they arrived at mount Hor, which is at the borders of the land of Edom,
23 Kwenye Mlima Hori, karibu na mpaka wa Edomu, Bwana akamwambia Mose na Aroni,
where the Lord spoke to Moses:
24 “Aroni atakusanywa pamoja na watu wake. Hataingia katika nchi ninayowapa Waisraeli, kwa sababu ninyi wawili mliasi dhidi ya agizo langu kwenye maji ya Meriba.
“Let Aaron,” he said, “go to his people. For he shall not enter into the land which I have given to the sons of Israel, because he did not believe my mouth at the Waters of Contradiction.
25 Watwae Aroni na Eleazari mwanawe, na uwapandishe juu katika Mlima wa Hori.
Take Aaron, and his son with him, and lead them on to mount Hor.
26 Mvue Aroni mavazi yake, na umvike Eleazari mwanawe, kwa maana Aroni atakusanywa pamoja na watu wake; atakufa huko.”
And when you have stripped the father of his vestments, you shall put them on Eleazar, his son. Aaron shall be gathered and shall die there.”
27 Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza: Wakapanda Mlima Hori mbele ya macho ya jumuiya yote ya Kiisraeli.
Moses did just as the Lord had instructed. And they ascended mount Hor, in the sight of the entire multitude.
28 Mose akamvua Aroni mavazi yake na kumvika mwanawe Eleazari mavazi hayo. Naye Aroni akafia pale juu ya mlima. Kisha Mose na Eleazari wakateremka kutoka mlimani.
And when he had despoiled Aaron of his vestments, he clothed his son Eleazar with them. And when Aaron had died at the top of the mountain, Moses came down with Eleazar.
29 Jumuiya yote ilipofahamu kwamba Aroni amekufa, jamaa yote ya Kiisraeli wakamwomboleza kwa siku thelathini.
And the entire multitude, seeing that Aaron lay dead, wept over him for thirty days, throughout all their families.

< Hesabu 20 >