< Hesabu 2 >

1 Bwana aliwaambia Mose na Aroni:
And the Lord spak to Moises and to Aaron, and seide,
2 “Waisraeli watapiga kambi zao kuzunguka Hema la Kukutania kwa umbali fulani kutoka kwenye hema, kila mwanaume chini ya alama yake pamoja na bendera ya jamaa yake.”
Alle men of the sones of Israel schulen sette tentis bi the cumpenyes, signes, and baneris, and housis of her kynredis, bi the cumpas of the tabernacle of boond of pees.
3 Kwa upande wa mashariki kuelekea mawio ya jua, kambi ya makundi ya Yuda watapiga kambi chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Yuda ni Nashoni mwana wa Aminadabu.
At the est Judas schal sette tentis, bi the cumpenyes of his oost; and Naason, the sone of Amynadab, schal be prince of the sones of Juda;
4 Kundi lake lina watu 74,600.
and al the summe of fiyteris of his kynrede, foure and seuenty thousynde and sixe hundrid.
5 Kabila la Isakari watapiga kambi karibu na Yuda. Kiongozi wa watu wa Isakari ni Nethaneli mwana wa Suari.
Men of the lynage of Ysachar settiden tentis bysydis hym, of whiche the prince was Nathanael, the sone of Suar;
6 Kundi lake lina watu 54,400.
and al the noumbre of hise fiyteris, foure and fifti thousynde and foure hundrid.
7 Kabila la Zabuloni litafuata. Kiongozi wa watu wa Zabuloni ni Eliabu mwana wa Heloni.
Eliab, the sone of Elon, was prince of the lynage of Zabulon;
8 Kundi lake lina watu 57,400.
al the oost of fiyteris of his kynrede, seuene and fifti thousynde and foure hundrid.
9 Wanaume wote walio katika kambi ya Yuda, kufuatana na makundi yao, ni 186,400. Wao watatangulia kuondoka.
Alle that weren noumbrid in the castels of Judas, weren an hundrid thousynde `foure scoore thousynde and sixe and foure hundrid; and thei schulen go out the firste bi her cumpanyes.
10 Kwa upande wa kusini kutakuwa kambi ya makundi ya Reubeni chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Reubeni ni Elisuri mwana wa Shedeuri.
In the castels of the sones of Ruben, at the south coost, Elisur, the sone of Sedeur, schal be prince; and al the oost of hise fiyteris,
11 Kundi lake lina watu 46,500.
that weren noumbrid, sixe and fourti thousynde and fyue hundrid.
12 Kabila la Simeoni watapiga kambi karibu na Reubeni. Kiongozi wa watu wa Simeoni ni Shelumieli mwana wa Surishadai.
Men of the lynage of Symeon settiden tentis bisidis hym, of whiche the prince was Salamyhel, the sone of Surisaddai; and al the oost of hise fiyteris,
13 Kundi lake lina watu 59,300.
that weren noumbrid, nyne and fifty thousynde and thre hundrid.
14 Kabila la Gadi litafuata. Kiongozi wa watu wa Gadi ni Eliasafu mwana wa Deueli.
Eliasaph, sone of Duel, was prince in the lynage of Gad; and al the oost of his fiyteris,
15 Kundi lake lina watu 45,650.
that weren noumbrid, fyue and fourti thousynde sixe hundrid and fifti.
16 Wanaume wote walio katika kambi ya Reubeni, kufuatana na makundi yao, ni 151,450. Nao watakuwa nafasi ya pili kuondoka.
Alle that weren noumbrid in the castels of Ruben, an hundrid thousynde fifty thousinde and a thousinde foure hundrid and fifty; thei schulen go forth in the secounde place bi her cumpenyes.
17 Kisha Hema la Kukutania na kambi ya Walawi vitakuwa katikati ya kambi zote. Wao watasafiri kwa utaratibu ule ule kama walivyopiga kambi, kila mmoja mahali pake mwenyewe chini ya alama yake.
Sotheli the tabernacle of witnessyng schal be reisid bi the offices of dekenes, and bi the cumpenyes `of hem; as it schal be reisid, so and it schal be takun doun; alle schulen go forth bi her places and ordris.
18 Upande wa magharibi kutakuwepo na kambi ya makundi ya Efraimu chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Efraimu ni Elishama mwana wa Amihudi.
The castels of the sones of Effraym schulen be at the west coost, of whiche the prince was Elisama, the sone of Amyud;
19 Kundi lake lina watu 40,500.
and al the oost of his fiyteris, that weren noumbrid, fourti thousynde and fyue hundrid.
20 Kabila la Manase litafuata baada ya Efraimu. Kiongozi wa watu wa Manase ni Gamalieli mwana wa Pedasuri.
And with hem was the lynage of `the sones of Manasses, of whiche the prince was Gamaliel, the sone of Fadassur;
21 Kundi lake lina watu 32,200.
al the oost of hise fiyteris, that weren noumbrid, two and thretti thousande and two hundrid.
22 Kabila la Benyamini litafuata baada ya Manase. Kiongozi wa watu wa Benyamini ni Abidani mwana wa Gideoni.
In the lynage of the sones of Beniamyn the prince was Abidan, the sone of Gedeon;
23 Kundi lake lina watu 35,400.
and al the oost of hise fiyteris, that weren noumbrid, fyue and thretti thousynde and foure hundrid.
24 Wanaume wote walio katika kambi ya Efraimu kufuatana na makundi yao ni 108,100. Nao watakuwa nafasi ya tatu kuondoka.
Alle that weren noumbrid in the castels of Effraym weren an hundrid thousynde and eiyte thousynde and oon hundrid; thei schulen go forth `the thridde bi her cumpenyes.
25 Upande wa kaskazini kutakuwa na makundi ya kambi ya Dani, chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Dani ni Ahiezeri mwana wa Amishadai.
At the `part of the north the sones of Dan settiden tentis, of whiche the prince was Abiezer, the sone of Amysaddai;
26 Kundi lake lina watu 62,700.
al the oost of hise fiyteris, that weren noumbrid, two and sixti thousynde and seuene hundrid.
27 Kabila la Asheri watapiga kambi karibu na Dani. Kiongozi wa watu wa Asheri ni Pagieli mwana wa Okrani.
Men of the lynage of Aser settiden tentis bisidis hym, of whiche the prince was Fegiel, the sone of Ochran;
28 Kundi lake lina watu 41,500.
and al the oost of hise fiyteris, that weren noumbrid, fourti thousynde `and a thousynde and fyue hundrid.
29 Kabila la Naftali litafuata. Kiongozi wa watu wa Naftali ni Ahira mwana wa Enani.
Of the lynage of the sones of Neptalym the prince was Ahira, the sone of Henam; and al the oost of hise fiyteris,
30 Kundi lake lina watu 53,400.
thre and fifti thousynde and foure hundrid.
31 Wanaume wote walio katika kambi ya Dani ni 157,600. Wao watakuwa wa mwisho kuondoka chini ya alama yao.
Alle that weren noumbrid in the castels of Dan weren an hundrid thousynde seuene and fifti thousynde and sixe hundrid; thei schulen go forth the laste.
32 Hawa ndio Waisraeli, wakiwa wamehesabiwa kufuatana na jamaa zao. Wote walio kambini kwa makundi yao ni watu 603,550.
This is the noumbre of the sones of Israel, bi the housis of her kynredis, and bi cumpenyes of the oost departid, sixe hundrid thousynde thre thousynde fyue hundrid and fifti.
33 Hata hivyo, Walawi hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Sotheli the dekenes weren not noumbrid among the sones of Israel; for God comaundide so to Moises.
34 Kwa hiyo Waisraeli wakafanya kila kitu Bwana alichomwamuru Mose. Hivyo ndivyo walivyopiga kambi chini ya alama zao, pia hivyo ndivyo walivyoondoka, kila mmoja akiwa na ukoo wake na jamaa yake.
And the sones of Israel diden bi alle thingis whiche the Lord comaundide; thei settiden tentis bi her cumpenyes, and yeden forth bi the meynees, and housis of her fadris.

< Hesabu 2 >