< Hesabu 2 >
1 Bwana aliwaambia Mose na Aroni:
And he spoke Yahweh to Moses and to Aaron saying.
2 “Waisraeli watapiga kambi zao kuzunguka Hema la Kukutania kwa umbali fulani kutoka kwenye hema, kila mwanaume chini ya alama yake pamoja na bendera ya jamaa yake.”
Everyone at standard his with [the] signs of [the] house of ancestors their they will encamp [the] people of Israel from before around [the] tent of meeting they will encamp.
3 Kwa upande wa mashariki kuelekea mawio ya jua, kambi ya makundi ya Yuda watapiga kambi chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Yuda ni Nashoni mwana wa Aminadabu.
And those [who] encamp east-ward east-ward [will be] [the] standard of [the] camp of Judah to military groups their and [the] leader of [the] descendants of Judah [was] Nahshon [the] son of Amminadab.
4 Kundi lake lina watu 74,600.
And military group his and enrolled [men] their [were] four and seventy thousand and six hundred.
5 Kabila la Isakari watapiga kambi karibu na Yuda. Kiongozi wa watu wa Isakari ni Nethaneli mwana wa Suari.
And those [who] encamp on him [will be] [the] tribe of Issachar and [the] leader of [the] descendants of Issachar [was] Nethanel [the] son of Zuar.
6 Kundi lake lina watu 54,400.
And military group his and enrolled [men] his [were] four and fifty thousand and four hundred.
7 Kabila la Zabuloni litafuata. Kiongozi wa watu wa Zabuloni ni Eliabu mwana wa Heloni.
[the] tribe of Zebulun and [the] leader of [the] descendants of Zebulun [was] Eliab [the] son of Helon.
8 Kundi lake lina watu 57,400.
And military group his and enrolled [men] his [were] seven and fifty thousand and four hundred.
9 Wanaume wote walio katika kambi ya Yuda, kufuatana na makundi yao, ni 186,400. Wao watatangulia kuondoka.
All those enrolled of [the] camp of Judah [were] one hundred thousand and eighty thousand and six thousand and four hundred to military groups their first they will set out.
10 Kwa upande wa kusini kutakuwa kambi ya makundi ya Reubeni chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Reubeni ni Elisuri mwana wa Shedeuri.
[the] standard of [the] camp of Reuben [will be] south-ward to military groups their and [the] leader of [the] descendants of Reuben [was] Elizur [the] son of Shedeur.
11 Kundi lake lina watu 46,500.
And military group his and enrolled [men] his [were] six and forty thousand and five hundred.
12 Kabila la Simeoni watapiga kambi karibu na Reubeni. Kiongozi wa watu wa Simeoni ni Shelumieli mwana wa Surishadai.
And those [who] encamp on him [will be] [the] tribe of Simeon and [the] leader of [the] descendants of Simeon [was] Shelumiel [the] son of Zuri-shaddai.
13 Kundi lake lina watu 59,300.
And military group his and enrolled [men] their [were] nine and fifty thousand and three hundred.
14 Kabila la Gadi litafuata. Kiongozi wa watu wa Gadi ni Eliasafu mwana wa Deueli.
And [the] tribe of Gad and [the] leader of [the] descendants of Gad [was] Eliasaph [the] son of Reuel.
15 Kundi lake lina watu 45,650.
And military group his and enrolled [men] their [were] five and forty thousand and six hundred and fifty.
16 Wanaume wote walio katika kambi ya Reubeni, kufuatana na makundi yao, ni 151,450. Nao watakuwa nafasi ya pili kuondoka.
All those enrolled of [the] camp of Reuben [were] one hundred thousand and one and fifty thousand and four hundred and fifty to military groups their and second they will set out.
17 Kisha Hema la Kukutania na kambi ya Walawi vitakuwa katikati ya kambi zote. Wao watasafiri kwa utaratibu ule ule kama walivyopiga kambi, kila mmoja mahali pake mwenyewe chini ya alama yake.
And it will set out [the] tent of meeting [the] camp of the Levites [will be] in [the] middle of the camps just as they will encamp so they will set out each on hand his to standards their.
18 Upande wa magharibi kutakuwepo na kambi ya makundi ya Efraimu chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Efraimu ni Elishama mwana wa Amihudi.
[the] standard of [the] camp of Ephraim to military groups their [will be] west-ward and [the] leader of [the] descendants of Ephraim [was] Elishama [the] son of Ammihud.
19 Kundi lake lina watu 40,500.
And military group his and enrolled [men] their [were] forty thousand and five hundred.
20 Kabila la Manase litafuata baada ya Efraimu. Kiongozi wa watu wa Manase ni Gamalieli mwana wa Pedasuri.
And [will be] on him [the] tribe of Manasseh and [the] leader of [the] descendants of Manasseh [was] Gamaliel [the] son of Pedahzur.
21 Kundi lake lina watu 32,200.
And military group his and enrolled [men] their [were] two and thirty thousand and two hundred.
22 Kabila la Benyamini litafuata baada ya Manase. Kiongozi wa watu wa Benyamini ni Abidani mwana wa Gideoni.
And [the] tribe of Benjamin and [the] leader of [the] descendants Benjamin [was] Abidan [the] son of Gideoni.
23 Kundi lake lina watu 35,400.
And military group his and enrolled [men] their [were] five and thirty thousand and four hundred.
24 Wanaume wote walio katika kambi ya Efraimu kufuatana na makundi yao ni 108,100. Nao watakuwa nafasi ya tatu kuondoka.
All those enrolled of [the] camp of Ephraim [were] one hundred thousand and eight thousand and one hundred to military groups their and third they will set out.
25 Upande wa kaskazini kutakuwa na makundi ya kambi ya Dani, chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Dani ni Ahiezeri mwana wa Amishadai.
[the] standard of [the] camp of Dan [will be] north-ward to military groups their and [the] leader of [the] descendants of Dan [was] Ahiezer [the] son of Ammishaddai.
26 Kundi lake lina watu 62,700.
And military group his and enrolled [men] their [were] two and sixty thousand and seven hundred.
27 Kabila la Asheri watapiga kambi karibu na Dani. Kiongozi wa watu wa Asheri ni Pagieli mwana wa Okrani.
And those [who] encamp on him [will be] [the] tribe of Asher and [the] leader of [the] descendants of Asher [was] Pagiel [the] son of Ocran.
28 Kundi lake lina watu 41,500.
And military group his and enrolled [men] their [were] one and forty thousand and five hundred.
29 Kabila la Naftali litafuata. Kiongozi wa watu wa Naftali ni Ahira mwana wa Enani.
And [the] tribe of Naphtali and [the] leader of [the] descendants of Naphtali [was] Ahira [the] son of Enan.
30 Kundi lake lina watu 53,400.
And military group his and enrolled [men] their [were] three and fifty thousand and four hundred.
31 Wanaume wote walio katika kambi ya Dani ni 157,600. Wao watakuwa wa mwisho kuondoka chini ya alama yao.
All those enrolled of [the] camp of Dan [were] one hundred thousand and seven and fifty thousand and six hundred to the last they will set out to standards their.
32 Hawa ndio Waisraeli, wakiwa wamehesabiwa kufuatana na jamaa zao. Wote walio kambini kwa makundi yao ni watu 603,550.
These [were] [the] [men] enrolled of [the] people of Israel to [the] house of ancestors their all [those] enrolled of the camps to military groups their [were] six hundred thousand and three thousand and five hundred and fifty.
33 Hata hivyo, Walawi hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
And the Levites not they were enrolled in among [the] people of Israel just as he had commanded Yahweh Moses.
34 Kwa hiyo Waisraeli wakafanya kila kitu Bwana alichomwamuru Mose. Hivyo ndivyo walivyopiga kambi chini ya alama zao, pia hivyo ndivyo walivyoondoka, kila mmoja akiwa na ukoo wake na jamaa yake.
And they did [the] people of Israel according to all that he had commanded Yahweh Moses so they camped to standards their and so they set out everyone to clans his on [the] house of ancestors his.