< Hesabu 2 >

1 Bwana aliwaambia Mose na Aroni:
And the LORD spoke unto Moses and unto Aaron, saying,
2 “Waisraeli watapiga kambi zao kuzunguka Hema la Kukutania kwa umbali fulani kutoka kwenye hema, kila mwanaume chini ya alama yake pamoja na bendera ya jamaa yake.”
Every man of the children of Israel shall pitch by his own standard, with the explicit sign of their father's house: far off about the tabernacle of the congregation shall they pitch.
3 Kwa upande wa mashariki kuelekea mawio ya jua, kambi ya makundi ya Yuda watapiga kambi chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Yuda ni Nashoni mwana wa Aminadabu.
And on the east side toward the rising of the sun shall they of the standard of the camp of Judah pitch throughout their armies: and Nahshon the son of Amminadab shall be captain of the children of Judah.
4 Kundi lake lina watu 74,600.
And his host, and those that were numbered of them, were threescore and fourteen thousand and six hundred.
5 Kabila la Isakari watapiga kambi karibu na Yuda. Kiongozi wa watu wa Isakari ni Nethaneli mwana wa Suari.
And those that do pitch next unto him shall be the tribe of Issachar: and Nethaneel the son of Zuar shall be captain of the children of Issachar.
6 Kundi lake lina watu 54,400.
And his host, and those that were numbered thereof, were fifty and four thousand and four hundred.
7 Kabila la Zabuloni litafuata. Kiongozi wa watu wa Zabuloni ni Eliabu mwana wa Heloni.
Then the tribe of Zebulun: and Eliab the son of Helon shall be captain of the children of Zebulun.
8 Kundi lake lina watu 57,400.
And his host, and those that were numbered thereof, were fifty and seven thousand and four hundred.
9 Wanaume wote walio katika kambi ya Yuda, kufuatana na makundi yao, ni 186,400. Wao watatangulia kuondoka.
All that were numbered in the camp of Judah were an hundred thousand and fourscore thousand and six thousand and four hundred, throughout their armies. These shall first set forth.
10 Kwa upande wa kusini kutakuwa kambi ya makundi ya Reubeni chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Reubeni ni Elisuri mwana wa Shedeuri.
On the south side shall be the standard of the camp of Reuben according to their armies: and the captain of the children of Reuben shall be Elizur the son of Shedeur.
11 Kundi lake lina watu 46,500.
And his host, and those that were numbered thereof, were forty and six thousand and five hundred.
12 Kabila la Simeoni watapiga kambi karibu na Reubeni. Kiongozi wa watu wa Simeoni ni Shelumieli mwana wa Surishadai.
And those which pitch by him shall be the tribe of Simeon: and the captain of the children of Simeon shall be Shelumiel the son of Zurishaddai.
13 Kundi lake lina watu 59,300.
And his host, and those that were numbered of them, were fifty and nine thousand and three hundred.
14 Kabila la Gadi litafuata. Kiongozi wa watu wa Gadi ni Eliasafu mwana wa Deueli.
Then the tribe of Gad: and the captain of the sons of Gad shall be Eliasaph the son of Reuel.
15 Kundi lake lina watu 45,650.
And his host, and those that were numbered of them, were forty and five thousand and six hundred and fifty.
16 Wanaume wote walio katika kambi ya Reubeni, kufuatana na makundi yao, ni 151,450. Nao watakuwa nafasi ya pili kuondoka.
All that were numbered in the camp of Reuben were an hundred thousand and fifty and one thousand and four hundred and fifty, throughout their armies. And they shall set forth in the second rank.
17 Kisha Hema la Kukutania na kambi ya Walawi vitakuwa katikati ya kambi zote. Wao watasafiri kwa utaratibu ule ule kama walivyopiga kambi, kila mmoja mahali pake mwenyewe chini ya alama yake.
Then the tabernacle of the congregation shall set forward with the camp of the Levites in the midst of the camp: as they camp, so shall they set forward, every man in his place by their standards.
18 Upande wa magharibi kutakuwepo na kambi ya makundi ya Efraimu chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Efraimu ni Elishama mwana wa Amihudi.
On the west side shall be the standard of the camp of Ephraim according to their armies: and the captain of the sons of Ephraim shall be Elishama the son of Ammihud.
19 Kundi lake lina watu 40,500.
And his host, and those that were numbered of them, were forty thousand and five hundred.
20 Kabila la Manase litafuata baada ya Efraimu. Kiongozi wa watu wa Manase ni Gamalieli mwana wa Pedasuri.
And by him shall be the tribe of Manasseh: and the captain of the children of Manasseh shall be Gamaliel the son of Pedahzur.
21 Kundi lake lina watu 32,200.
And his host, and those that were numbered of them, were thirty and two thousand and two hundred.
22 Kabila la Benyamini litafuata baada ya Manase. Kiongozi wa watu wa Benyamini ni Abidani mwana wa Gideoni.
Then the tribe of Benjamin: and the captain of the sons of Benjamin shall be Abidan the son of Gideoni.
23 Kundi lake lina watu 35,400.
And his host, and those that were numbered of them, were thirty and five thousand and four hundred.
24 Wanaume wote walio katika kambi ya Efraimu kufuatana na makundi yao ni 108,100. Nao watakuwa nafasi ya tatu kuondoka.
All that were numbered of the camp of Ephraim were an hundred thousand and eight thousand and an hundred, throughout their armies. And they shall go forward in the third rank.
25 Upande wa kaskazini kutakuwa na makundi ya kambi ya Dani, chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Dani ni Ahiezeri mwana wa Amishadai.
The standard of the camp of Dan shall be on the north side by their armies: and the captain of the children of Dan shall be Ahiezer the son of Ammishaddai.
26 Kundi lake lina watu 62,700.
And his host, and those that were numbered of them, were threescore and two thousand and seven hundred.
27 Kabila la Asheri watapiga kambi karibu na Dani. Kiongozi wa watu wa Asheri ni Pagieli mwana wa Okrani.
And those that camp by him shall be the tribe of Asher: and the captain of the children of Asher shall be Pagiel the son of Ocran.
28 Kundi lake lina watu 41,500.
And his host, and those that were numbered of them, were forty and one thousand and five hundred.
29 Kabila la Naftali litafuata. Kiongozi wa watu wa Naftali ni Ahira mwana wa Enani.
Then the tribe of Naphtali: and the captain of the children of Naphtali shall be Ahira the son of Enan.
30 Kundi lake lina watu 53,400.
And his host, and those that were numbered of them, were fifty and three thousand and four hundred.
31 Wanaume wote walio katika kambi ya Dani ni 157,600. Wao watakuwa wa mwisho kuondoka chini ya alama yao.
All they that were numbered in the camp of Dan were an hundred thousand and fifty and seven thousand and six hundred. They shall go hindmost with their standards.
32 Hawa ndio Waisraeli, wakiwa wamehesabiwa kufuatana na jamaa zao. Wote walio kambini kwa makundi yao ni watu 603,550.
These are those which were numbered of the children of Israel by the house of their fathers: all those that were numbered of the camps throughout their hosts were six hundred thousand and three thousand and five hundred and fifty.
33 Hata hivyo, Walawi hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
But the Levites were not numbered among the children of Israel; as the LORD commanded Moses.
34 Kwa hiyo Waisraeli wakafanya kila kitu Bwana alichomwamuru Mose. Hivyo ndivyo walivyopiga kambi chini ya alama zao, pia hivyo ndivyo walivyoondoka, kila mmoja akiwa na ukoo wake na jamaa yake.
And the children of Israel did according to all that the LORD commanded Moses: so they pitched by their standards, and so they set forward, every one after their families, according to the house of their fathers.

< Hesabu 2 >