< Hesabu 19 >

1 Bwana akamwambia Mose na Aroni:
Le Seigneur parla encore à Moïse et à Aaron, disant:
2 “Hivi ndivyo sheria ambayo Bwana ameagiza itakavyo: Waambie Waisraeli wakuletee mtamba mwekundu asiye na dosari wala waa, na ambaye hajapata kufungwa nira.
Voici la cérémonie de la victime qu’a déterminée le Seigneur. Ordonne aux enfants d’Israël qu’ils t’amènent une vache rousse, dans l’intégrité de l’âge, en laquelle il n’y ait aucune tache, et qui n’ait point porté le joug;
3 Mpeni kuhani Eleazari huyo mtamba; naye atatolewa nje ya kambi na kuchinjwa mbele yake huyo kuhani.
Et vous la livrerez à Eléazar, le prêtre, qui après l’avoir menée hors du camp, l’immolera en présence de tous;
4 Kisha kuhani Eleazari atachukua baadhi ya damu yake kwenye kidole chake na kuinyunyiza mara saba kuelekea upande wa mbele ya Hema la Kukutania.
Et, trempant le doigt dans son sang, il fera l’aspersion contre la porte du tabernacle par sept fois.
5 Wakati angali akitazama, mtamba huyo atateketezwa: ngozi yake, nyama yake, damu na sehemu zake za ndani.
Puis il la brûlera, tous le voyant, en livrant aux flammes tant sa peau et sa chair, que son sang et sa fiente.
6 Kuhani atachukua kuni za mti wa mwerezi, hisopo na sufu nyekundu, na kuvitupa kwenye huyo mtamba anayeungua.
Le prêtre jettera aussi du bois de cèdre, de l’hysope et de l’écarlate deux fois teinte, dans la flamme qui brûle la vache.
7 Baada ya hayo, kuhani lazima afue nguo zake, na aoge mwili wake kwa maji. Kisha anaweza kurudi kambini, lakini atakuwa najisi kwa kawaida ya ibada mpaka jioni.
Et alors enfin, ses vêtements et son corps lavés, il entrera dans le camp et il sera souillé jusqu’au soir.
8 Mtu amchomaye huyo mtamba lazima naye pia afue nguo zake na kuoga kwa maji, naye pia atakuwa najisi mpaka jioni.
Mais celui aussi qui l’aura brûlée, lavera ses vêtements et son corps, et il sera impur jusqu’au soir.
9 “Mtu ambaye ni safi atakusanya majivu ya mtamba huyo na kuyaweka mahali ambapo ni safi nje ya kambi kwa taratibu za kiibada. Yatahifadhiwa na jumuiya ya Kiisraeli kwa matumizi katika maji ya utakaso; ni kwa ajili ya kutakasa kutoka dhambini.
Et un homme pur recueillera les cendres de la vache, et les déposera hors du camp dans un lieu très net, afin qu’elles soient à la garde de la multitude des enfants d’Israël, et qu’elles servent pour une eau d’aspersion; parce que c’est pour le péché que la vache a été brûlée.
10 Mtu akusanyaye majivu ya huyo mtamba ni lazima pia afue nguo zake, kadhalika naye pia atakuwa najisi hadi jioni. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa Waisraeli na kwa wageni wanaoishi miongoni mwao.
Et lorsque celui qui avait porté les cendres de la vache, aura lavé ses vêtements, il sera impur jusqu’au soir. Les enfants d’Israël et les étrangers qui habitent parmi eux tiendront cette ordonnance pour sainte par un droit perpétuel.
11 “Mtu yeyote agusaye maiti ya mtu yeyote atakuwa najisi kwa siku saba.
Celui qui aura touché le cadavre d’un homme, et qui pour cela sera impur pendant sept jours,
12 Ni lazima ajitakase mwenyewe kwa maji katika siku ya tatu na siku ya saba, ndipo atakuwa safi. Lakini kama hatajitakasa mwenyewe katika siku ya tatu na ya saba, hatakuwa safi.
Sera aspergé de cette eau au troisième et au septième jour, et c’est ainsi qu’il sera purifié. Si au troisième jour il n’a pas été aspergé, au septième il ne pourra être purifié.
13 Mtu yeyote agusaye maiti ya mtu yeyote na kushindwa kujitakasa mwenyewe hunajisi Maskani ya Bwana. Mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na Israeli. Kwa sababu hajanyunyiziwa maji ya utakaso, yeye ni najisi; unajisi wake unabaki juu yake.
Quiconque aura touché le corps mort du ne âme humaine, et n’aura pas été aspergé de cette eau ainsi mêlée, souillera le tabernacle du Seigneur, et périra du milieu d’Israël: parce qu’il n’a pas été aspergé d’eau d’expiation, il sera impur et son impureté demeurera sur lui.
14 “Hii ndiyo sheria itumikayo wakati mtu amekufa ndani ya hema: Yeyote aingiaye ndani ya hema hilo na yeyote aliye ndani yake watakuwa najisi kwa muda wa siku saba,
Voici la loi de l’homme qui meurt dans une tente: Tous ceux qui entrent dans sa tente, et tous les vases qui y sont, seront souillés pendant sept jours.
15 nacho kila chombo kisicho na kifuniko juu yake kitakuwa najisi.
Un vase qui n’aurait point de couvercle, ni d’attache par-dessus, sera impur.
16 “Mtu yeyote aliyeko nje mahali pa wazi agusaye mtu aliyeuawa kwa upanga au mtu aliyekufa kwa kifo cha kawaida, au mtu yeyote agusaye mfupa wa mtu aliyekufa au kaburi, atakuwa najisi kwa siku saba.
Si quelqu’un dans un champ touche le cadavre d’un homme tué, ou mort de lui-même, ou bien un de ses os, ou son sépulcre, il sera impur pendant sept jours.
17 “Kwa mtu aliye najisi, weka majivu ya sadaka ya utakaso wa dhambi ndani ya chombo, umimine maji safi juu yao.
On prendra des cendres de la combustion et du péché, et l’on mettra de l’eau vive sur ces cendres dans un vase;
18 Kisha mtu aliye safi kwa kawaida za kiibada atachukua hisopo, achovye ndani ya maji, na kunyunyizia hema na vifaa vyote pamoja na watu ambao walikuwamo. Pia ni lazima amnyunyizie mtu yeyote ambaye amegusa mfupa wa mtu aliyekufa, au kaburi, au mtu ambaye ameuawa, au mtu ambaye amekufa kifo cha kawaida.
Et un homme pur y ayant trempé de l’hysope, il en aspergera toute la tente, tous les meubles et tous les hommes souillés par un tel contact
19 Mtu ambaye ni safi ndiye atakayemnyunyizia yeyote ambaye ni najisi siku ya tatu na siku ya saba, na katika siku ya saba atamtakasa mtu huyo. Mtu ambaye ametakaswa lazima afue nguo zake na kuoga kwa maji, na jioni ile atakuwa safi.
Et de cette manière le pur purifiera l’impur au troisième et au septième jour; et celui qui aura été purifié au septième jour, se lavera, lui et ses vêtements, et il sera impur jusqu’au soir.
20 Lakini ikiwa mtu ambaye ni najisi hakujitakasa mwenyewe, ni lazima akatiliwe mbali na jumuiya, kwa sababu ameinajisi Maskani ya Bwana. Maji ya utakaso hayajanyunyizwa juu yake, naye ni najisi.
Si quelqu’un n’est pas purifié selon ce rite, son âme périra du milieu de l’assemblée, parce qu’il a souillé le sanctuaire du Seigneur, et qu’il n’a pas été aspergé d’eau de purification.
21 Hii ni sheria ya kudumu kwao. “Mtu yeyote ambaye ananyunyiza yale maji ya utakaso lazima pia afue nguo zake, na yeyote ambaye hugusa maji ya utakaso atakuwa najisi mpaka jioni.
Cette ordonnance sera une loi perpétuelle. Celui aussi qui aura fait les aspersions de l’eau, lavera ses vêtements. Quiconque aura touché l’eau de l’expiation sera impur jusqu’au soir.
22 Kitu chochote anachogusa mtu aliye najisi kitakuwa najisi, na yeyote akigusaye huwa najisi mpaka jioni.”
Tout ce que touchera un impur, il le rendra impur: et l’homme qui touchera quelqu’une de ces choses, sera impur jusqu’au soir.

< Hesabu 19 >