< Hesabu 19 >
1 Bwana akamwambia Mose na Aroni:
L'Éternel parla encore à Moïse et à Aaron, en disant:
2 “Hivi ndivyo sheria ambayo Bwana ameagiza itakavyo: Waambie Waisraeli wakuletee mtamba mwekundu asiye na dosari wala waa, na ambaye hajapata kufungwa nira.
Voici l'ordonnance de la loi que l'Éternel a commandée, en disant: Parle aux enfants d'Israël, et qu'ils t'amènent une vache rousse, intacte, qui n'ait point de défaut et qui n'ait point porté le joug.
3 Mpeni kuhani Eleazari huyo mtamba; naye atatolewa nje ya kambi na kuchinjwa mbele yake huyo kuhani.
Puis vous la donnerez à Éléazar, le sacrificateur, qui la mènera hors du camp, et on l'égorgera en sa présence.
4 Kisha kuhani Eleazari atachukua baadhi ya damu yake kwenye kidole chake na kuinyunyiza mara saba kuelekea upande wa mbele ya Hema la Kukutania.
Ensuite Éléazar, le sacrificateur, prendra de son sang avec son doigt, et il fera sept fois aspersion de son sang, sur le devant du tabernacle d'assignation.
5 Wakati angali akitazama, mtamba huyo atateketezwa: ngozi yake, nyama yake, damu na sehemu zake za ndani.
Et on brûlera la vache devant ses yeux; on brûlera sa peau, sa chair et son sang, avec ses excréments.
6 Kuhani atachukua kuni za mti wa mwerezi, hisopo na sufu nyekundu, na kuvitupa kwenye huyo mtamba anayeungua.
Et le sacrificateur prendra du bois de cèdre, de l'hysope et du cramoisi, et les jettera au milieu du feu où brûlera la vache.
7 Baada ya hayo, kuhani lazima afue nguo zake, na aoge mwili wake kwa maji. Kisha anaweza kurudi kambini, lakini atakuwa najisi kwa kawaida ya ibada mpaka jioni.
Puis le sacrificateur lavera ses vêtements et sa chair dans l'eau, et après cela il rentrera au camp; et le sacrificateur sera souillé jusqu'au soir.
8 Mtu amchomaye huyo mtamba lazima naye pia afue nguo zake na kuoga kwa maji, naye pia atakuwa najisi mpaka jioni.
Et celui qui l'aura brûlée lavera ses vêtements dans l'eau et baignera sa chair dans l'eau, et il sera souillé jusqu'au soir.
9 “Mtu ambaye ni safi atakusanya majivu ya mtamba huyo na kuyaweka mahali ambapo ni safi nje ya kambi kwa taratibu za kiibada. Yatahifadhiwa na jumuiya ya Kiisraeli kwa matumizi katika maji ya utakaso; ni kwa ajili ya kutakasa kutoka dhambini.
Et un homme pur ramassera la cendre de la vache, et la déposera hors du camp dans un lieu pur; et on la gardera pour l'assemblée des enfants d'Israël, pour en faire l'eau de purification. C'est une purification pour le péché.
10 Mtu akusanyaye majivu ya huyo mtamba ni lazima pia afue nguo zake, kadhalika naye pia atakuwa najisi hadi jioni. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa Waisraeli na kwa wageni wanaoishi miongoni mwao.
Et celui qui aura ramassé la cendre de la vache lavera ses vêtements, et il sera souillé jusqu'au soir; et ce sera une ordonnance perpétuelle pour les enfants d'Israël et pour l'étranger séjournant au milieu d'eux.
11 “Mtu yeyote agusaye maiti ya mtu yeyote atakuwa najisi kwa siku saba.
Celui qui touchera un corps mort, de quelque personne que ce soit, sera souillé sept jours.
12 Ni lazima ajitakase mwenyewe kwa maji katika siku ya tatu na siku ya saba, ndipo atakuwa safi. Lakini kama hatajitakasa mwenyewe katika siku ya tatu na ya saba, hatakuwa safi.
Il se purifiera avec cette eau le troisième jour, et au septième jour il sera pur; que s'il ne se purifie pas au troisième jour ni au septième jour, il ne sera pas pur.
13 Mtu yeyote agusaye maiti ya mtu yeyote na kushindwa kujitakasa mwenyewe hunajisi Maskani ya Bwana. Mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na Israeli. Kwa sababu hajanyunyiziwa maji ya utakaso, yeye ni najisi; unajisi wake unabaki juu yake.
Quiconque aura touché un mort, une personne qui sera morte, et ne se sera point purifié, a souillé la Demeure de l'Éternel; cette personne sera retranchée d'Israël; puisque l'eau de purification n'a pas été répandue sur lui, il est souillé; sa souillure est encore sur lui.
14 “Hii ndiyo sheria itumikayo wakati mtu amekufa ndani ya hema: Yeyote aingiaye ndani ya hema hilo na yeyote aliye ndani yake watakuwa najisi kwa muda wa siku saba,
Voici la loi: Quand un homme mourra dans une tente, quiconque entrera dans la tente, et tout ce qui sera dans la tente, sera souillé sept jours.
15 nacho kila chombo kisicho na kifuniko juu yake kitakuwa najisi.
Et tout vase découvert, sur lequel il n'y a point de couvercle attaché, sera souillé.
16 “Mtu yeyote aliyeko nje mahali pa wazi agusaye mtu aliyeuawa kwa upanga au mtu aliyekufa kwa kifo cha kawaida, au mtu yeyote agusaye mfupa wa mtu aliyekufa au kaburi, atakuwa najisi kwa siku saba.
Et quiconque touchera, dans les champs, un homme tué par l'épée, ou un mort, ou des ossements humains, ou un tombeau, sera souillé sept jours.
17 “Kwa mtu aliye najisi, weka majivu ya sadaka ya utakaso wa dhambi ndani ya chombo, umimine maji safi juu yao.
Et on prendra, pour celui qui sera souillé, de la cendre de ce qui a été brûlé pour le péché, et on mettra dessus, dans un vase, de l'eau vive;
18 Kisha mtu aliye safi kwa kawaida za kiibada atachukua hisopo, achovye ndani ya maji, na kunyunyizia hema na vifaa vyote pamoja na watu ambao walikuwamo. Pia ni lazima amnyunyizie mtu yeyote ambaye amegusa mfupa wa mtu aliyekufa, au kaburi, au mtu ambaye ameuawa, au mtu ambaye amekufa kifo cha kawaida.
Et un homme pur prendra de l'hysope, et la trempera dans l'eau et en fera aspersion sur la tente, sur tous les vases et sur les personnes qui y sont, et sur celui qui a touché des ossements, ou un homme tué, ou un mort, ou un tombeau.
19 Mtu ambaye ni safi ndiye atakayemnyunyizia yeyote ambaye ni najisi siku ya tatu na siku ya saba, na katika siku ya saba atamtakasa mtu huyo. Mtu ambaye ametakaswa lazima afue nguo zake na kuoga kwa maji, na jioni ile atakuwa safi.
L'homme pur fera aspersion sur celui qui sera souillé, au troisième jour et au septième, et le purifiera le septième. Il lavera ses vêtements, et se lavera dans l'eau; et le soir il sera pur.
20 Lakini ikiwa mtu ambaye ni najisi hakujitakasa mwenyewe, ni lazima akatiliwe mbali na jumuiya, kwa sababu ameinajisi Maskani ya Bwana. Maji ya utakaso hayajanyunyizwa juu yake, naye ni najisi.
Mais quant à l'homme qui sera souillé et ne se purifiera point, cette personne sera retranchée du milieu de l'assemblée, car elle a souillé le sanctuaire de l'Éternel. L'eau de purification n'a pas été répandue sur lui, il est souillé.
21 Hii ni sheria ya kudumu kwao. “Mtu yeyote ambaye ananyunyiza yale maji ya utakaso lazima pia afue nguo zake, na yeyote ambaye hugusa maji ya utakaso atakuwa najisi mpaka jioni.
Et ce sera pour eux une ordonnance perpétuelle. Celui qui aura fait aspersion de l'eau de purification lavera ses vêtements; et celui qui touchera l'eau de purification sera souillé jusqu'au soir.
22 Kitu chochote anachogusa mtu aliye najisi kitakuwa najisi, na yeyote akigusaye huwa najisi mpaka jioni.”
Et tout ce que l'homme souillé touchera, sera souillé; et la personne qui le touchera, sera souillée jusqu'au soir.