< Hesabu 19 >

1 Bwana akamwambia Mose na Aroni:
And the Lord spak to Moises and to Aaron,
2 “Hivi ndivyo sheria ambayo Bwana ameagiza itakavyo: Waambie Waisraeli wakuletee mtamba mwekundu asiye na dosari wala waa, na ambaye hajapata kufungwa nira.
and seide, This is the religioun of sacrifice, which the Lord ordeynede. Comaunde thou to the sones of Israel, that thei brynge to thee a reed cow of hool age, in which is no wem, nether sche hath bore yok.
3 Mpeni kuhani Eleazari huyo mtamba; naye atatolewa nje ya kambi na kuchinjwa mbele yake huyo kuhani.
And ye schulen bitake hir to Eleazar, preest, which schal offre `the cow, led out of the tentis, in the siyt of alle men.
4 Kisha kuhani Eleazari atachukua baadhi ya damu yake kwenye kidole chake na kuinyunyiza mara saba kuelekea upande wa mbele ya Hema la Kukutania.
And he schal dippe his fyngur in the blood therof, and schal sprynge seuene sithis ayens the yatis of the tabernacle.
5 Wakati angali akitazama, mtamba huyo atateketezwa: ngozi yake, nyama yake, damu na sehemu zake za ndani.
And he schal brenne that cow, while alle men sien; and he schal yyue as wel the skyn and fleischis therof as the blood and dung to flawme.
6 Kuhani atachukua kuni za mti wa mwerezi, hisopo na sufu nyekundu, na kuvitupa kwenye huyo mtamba anayeungua.
Also the preest schal `sende a tre of cedre, and ysope, and reed threed died twies, into the flawme that deuourith the cow.
7 Baada ya hayo, kuhani lazima afue nguo zake, na aoge mwili wake kwa maji. Kisha anaweza kurudi kambini, lakini atakuwa najisi kwa kawaida ya ibada mpaka jioni.
And thanne at the laste, whanne hise clothis `and bodi ben waischun, he schal entre in to the tentis, and he schal be defoulid `til to euentid.
8 Mtu amchomaye huyo mtamba lazima naye pia afue nguo zake na kuoga kwa maji, naye pia atakuwa najisi mpaka jioni.
But also he that brente the cow, schal waische hise clothis, and bodi, and he schal be vncleene `til to euentid.
9 “Mtu ambaye ni safi atakusanya majivu ya mtamba huyo na kuyaweka mahali ambapo ni safi nje ya kambi kwa taratibu za kiibada. Yatahifadhiwa na jumuiya ya Kiisraeli kwa matumizi katika maji ya utakaso; ni kwa ajili ya kutakasa kutoka dhambini.
Forsothe a cleene man schal gadere the aischis of the cow, and schal schede out tho with out the tentis, in a place moost cleene, that tho be to the multitude of the sones of Israel in to keping, and in to watir of spryngyng; for the cow is brent for synne.
10 Mtu akusanyaye majivu ya huyo mtamba ni lazima pia afue nguo zake, kadhalika naye pia atakuwa najisi hadi jioni. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa Waisraeli na kwa wageni wanaoishi miongoni mwao.
And whanne he that bar the aischis of the cow, hath waische hise clothis, he schal be vncleene `til to euentid. And the sones of Israel, and comelyngis that dwellen among hem, schulen haue this hooli bi euerlastynge lawe.
11 “Mtu yeyote agusaye maiti ya mtu yeyote atakuwa najisi kwa siku saba.
He that touchith a deed bodi of man, and is vncleene for this bi seuene daies,
12 Ni lazima ajitakase mwenyewe kwa maji katika siku ya tatu na siku ya saba, ndipo atakuwa safi. Lakini kama hatajitakasa mwenyewe katika siku ya tatu na ya saba, hatakuwa safi.
schal be spreynt of this watir in the thridde, and in the seuenthe dai; and so he schal be clensid. If he is not spreynt in the thridde dai, he schal not mow be clensid in the seuenthe dai.
13 Mtu yeyote agusaye maiti ya mtu yeyote na kushindwa kujitakasa mwenyewe hunajisi Maskani ya Bwana. Mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na Israeli. Kwa sababu hajanyunyiziwa maji ya utakaso, yeye ni najisi; unajisi wake unabaki juu yake.
Ech that touchith the deed bodi bi it silf of mannus soule, and is not spreynt with this medlyng, defoulith the `tabernacle of the Lord, and he schal perische fro Israel; for he is not spreynt with the wateris of clensyng, he schal be vncleene, and his filthe schal dwelle on hym.
14 “Hii ndiyo sheria itumikayo wakati mtu amekufa ndani ya hema: Yeyote aingiaye ndani ya hema hilo na yeyote aliye ndani yake watakuwa najisi kwa muda wa siku saba,
This is the lawe of a man that dieth in the tabernacle; alle that entren in to his tente, and alle vessels that ben there, schulen be defoulid bi seuene daies.
15 nacho kila chombo kisicho na kifuniko juu yake kitakuwa najisi.
A vessel that hath not an hilyng, nethir a byndyng aboue, schal be vncleene.
16 “Mtu yeyote aliyeko nje mahali pa wazi agusaye mtu aliyeuawa kwa upanga au mtu aliyekufa kwa kifo cha kawaida, au mtu yeyote agusaye mfupa wa mtu aliyekufa au kaburi, atakuwa najisi kwa siku saba.
If ony man touchith the deed bodi of man slayn in the feeld, ether deed bi hym silf, ether a boon, ether the sepulcre `of hym, he schal be vncleene bi seuene daies.
17 “Kwa mtu aliye najisi, weka majivu ya sadaka ya utakaso wa dhambi ndani ya chombo, umimine maji safi juu yao.
And thei schulen take `of the aischis of the brennyng, and of the synne, and thei schulen sende quyk watris in to a vessel on tho aischis;
18 Kisha mtu aliye safi kwa kawaida za kiibada atachukua hisopo, achovye ndani ya maji, na kunyunyizia hema na vifaa vyote pamoja na watu ambao walikuwamo. Pia ni lazima amnyunyizie mtu yeyote ambaye amegusa mfupa wa mtu aliyekufa, au kaburi, au mtu ambaye ameuawa, au mtu ambaye amekufa kifo cha kawaida.
in whiche whanne `a cleene man hath dippid ysope, he schal spreynge therof the tente, and al the purtenaunce of howshold, and men defoulid bi sich defoulyng.
19 Mtu ambaye ni safi ndiye atakayemnyunyizia yeyote ambaye ni najisi siku ya tatu na siku ya saba, na katika siku ya saba atamtakasa mtu huyo. Mtu ambaye ametakaswa lazima afue nguo zake na kuoga kwa maji, na jioni ile atakuwa safi.
And in this maner a cleene man schal clense an vncleene, in the thridde and in the seuenthe dai; and he schal be clensid in the seuenthe dai. And he schal waische hym silf, and hise clothis, and he schal be vncleene `til to euentid.
20 Lakini ikiwa mtu ambaye ni najisi hakujitakasa mwenyewe, ni lazima akatiliwe mbali na jumuiya, kwa sababu ameinajisi Maskani ya Bwana. Maji ya utakaso hayajanyunyizwa juu yake, naye ni najisi.
If ony man is not clensid bi this custom, the soule of hym schal perische fro the myddis of the chirche; for he defoulith the `seyntuarie of the Lord, and is not spreynt with the watir of clensyng.
21 Hii ni sheria ya kudumu kwao. “Mtu yeyote ambaye ananyunyiza yale maji ya utakaso lazima pia afue nguo zake, na yeyote ambaye hugusa maji ya utakaso atakuwa najisi mpaka jioni.
This comaundement schal be a lawful thing euerlastynge. Also he that schal sprenge the watris schal waische his clothis; ech man that touchith the watris of clensyng, schal be vncleene `til to euentid.
22 Kitu chochote anachogusa mtu aliye najisi kitakuwa najisi, na yeyote akigusaye huwa najisi mpaka jioni.”
What euer thing an vncleene man touchith, he schal make it vncleene; and a soule that touchith ony of these thingis `defoulid so, schal be vncleene `til to euentid.

< Hesabu 19 >