< Hesabu 18 >
1 Bwana akamwambia Aroni, “Wewe, wanao na jamaa ya baba yako mtawajibika kwa makosa dhidi ya mahali patakatifu, na wewe na wanao peke yenu ndio mtakaowajibika kwa makosa dhidi ya ukuhani.
Alors l'Éternel dit à Aaron: Toi et tes fils, et la maison de ton père avec toi, vous porterez l'iniquité du sanctuaire; et toi, et tes fils avec toi, vous porterez l'iniquité de votre sacerdoce.
2 Walete Walawi wenzako kutoka kabila la baba zako ili waungane nanyi na kuwasaidia wakati wewe na wanao mnapohudumu mbele ya Hema la Ushuhuda.
Fais aussi approcher avec toi tes frères, la tribu de Lévi, la tribu de ton père, qu'ils se joignent à toi et qu'ils te servent; et toi et tes fils avec toi, vous serez devant le tabernacle du Témoignage.
3 Watawajibika kwenu na watafanya kazi zote za Hema, lakini kamwe wasisogelee vifaa vya patakatifu au madhabahu, la sivyo wao na ninyi mtakufa.
Ils observeront ce que tu leur ordonneras, et ce qui concerne tout le tabernacle; seulement ils n'approcheront point des objets sacrés, ni de l'autel, de peur qu'ils ne meurent et vous avec eux.
4 Watajiunga nanyi na watawajibika kwa utunzaji wa Hema la Kukutania, yaani kazi zote kwenye Hema, wala hakuna mtu mwingine yeyote atakayeweza kusogea karibu hapo mlipo.
Ils te seront donc adjoints, et ils observeront ce qui concerne le tabernacle d'assignation, pour tout le service du tabernacle, et nul étranger n'approchera de vous.
5 “Mtawajibika katika utunzaji wa mahali patakatifu na madhabahu, ili kwamba ghadhabu isiwaangukie Waisraeli tena.
Et vous observerez ce qui concerne le sanctuaire et l'autel, afin qu'il n'y ait plus d'indignation contre les enfants d'Israël.
6 Mimi mwenyewe nimewachagua Walawi wenzenu kutoka miongoni mwa Waisraeli kama zawadi kwenu, waliowekwa wakfu kwa Bwana ili kufanya kazi katika Hema la Kukutania.
Quant à moi, voici, j'ai pris vos frères les Lévites, du milieu des enfants d'Israël; ils vous sont donnés en don pour l'Éternel, pour faire le service du tabernacle d'assignation.
7 Lakini ni wewe tu na wanao mtakaoweza kutumika kama makuhani kuhusiana na kila kitu kwenye madhabahu na ndani ya pazia. Ninawapa utumishi wa ukuhani kama zawadi. Mtu mwingine yeyote atakayekaribia mahali patakatifu ni lazima auawe.”
Mais toi, et tes fils avec toi, vous vous acquitterez avec soin de votre sacerdoce, en tout ce qui concerne l'autel et ce qui est en dedans du voile; et vous y ferez le service. Je vous donne le sacerdoce en office de pur don; et l'étranger qui en approchera, sera puni de mort.
8 Kisha Bwana akamwambia Aroni, “Mimi mwenyewe nimekuweka kuwa mwangalizi wa sadaka zote zitakazotolewa kwangu; matoleo yote matakatifu Waisraeli wanayonipa ninakupa wewe na wanao kama sehemu yenu na fungu lenu la kawaida.
L'Éternel dit encore à Aaron: Voici, je t'ai donné la garde de mes offrandes prélevées sur toutes les choses consacrées par les enfants d'Israël; je te les ai données, et à tes enfants, par ordonnance perpétuelle, comme droit conféré par l'onction.
9 Mtachukua sehemu ya yale matoleo matakatifu sana ambayo hayateketezwi kwa moto. Kutoka kwa matoleo yote wanayoniletea kama sadaka takatifu sana, ziwe za nafaka, au za dhambi, au za makosa, sehemu ile itakuwa yako na wanao.
Ceci t'appartiendra, d'entre les choses très saintes qui ne sont pas consumées: toutes leurs offrandes, dans toutes leurs oblations, dans tous leurs sacrifices pour le péché, et dans tous leurs sacrifices pour le délit, qu'ils m'apporteront; ces choses très saintes seront pour toi et pour tes enfants.
10 Mtaila kama kitu kilicho kitakatifu sana; kila mwanaume ataila. Ni lazima mtaiheshimu kama takatifu.
Tu les mangeras dans le lieu très-saint; tout mâle en mangera; ce sera pour toi une chose sacrée.
11 “Hiki pia ni chako: chochote kilichotengwa kutoka kwenye matoleo yote ya sadaka za kuinuliwa za Waisraeli. Ninakupa wewe haya, wana na binti zako kama sehemu yenu ya kawaida. Kila mmoja wa nyumba yako ambaye ni safi kwa taratibu za ibada anaweza kuyala.
Ceci aussi t'appartiendra: l'offrande prélevée de leurs dons, sur toutes les offrandes agitées des enfants d'Israël; je te les ai données, à toi, à tes fils et à tes filles avec toi, par ordonnance perpétuelle. Quiconque sera pur dans ta maison en mangera.
12 “Ninawapa mafuta ya zeituni yaliyo bora kuliko yote, na divai mpya iliyo bora kuliko zote na nafaka wanazompa Bwana kama malimbuko katika mavuno yao.
Je t'ai donné aussi leurs prémices qu'ils offriront à l'Éternel, tout le meilleur de l'huile, et tout le meilleur du moût et du froment.
13 Malimbuko yote ya nchi ambayo wanamletea Bwana yatakuwa yenu. Kila mmoja nyumbani kwako ambaye ni safi kwa taratibu za Ibada anaweza kula.
Les premiers fruits de tout ce que leur terre produira, et qu'ils apporteront à l'Éternel, t'appartiendront; quiconque sera pur dans ta maison en mangera.
14 “Kila kitu katika Israeli ambacho kimetolewa kwa Bwana ni chenu.
Tout ce qui sera dévoué par interdit en Israël t'appartiendra.
15 Kila mzaliwa wa kwanza wa mwanadamu na wa mnyama, ambaye ametolewa kwa Bwana ni wenu. Lakini ni lazima mtamkomboa kila mwana mzaliwa wa kwanza na kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa wanyama wasio safi.
Tout premier-né, de toute chair, qu'ils offriront à l'Éternel, soit des hommes soit des bêtes, t'appartiendra; seulement, tu rachèteras le premier-né de l'homme; tu rachèteras aussi le premier-né d'une bête impure.
16 Watakapokuwa na umri wa mwezi mmoja, ni lazima mtawakomboa kwa bei ya ukombozi iliyowekwa, kwa shekeli tano za fedha, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, yenye uzito wa gera ishirini.
Quant à son rachat, tu le rachèteras depuis l'âge d'un mois, d'après ton estimation, au prix de cinq sicles d'argent, selon le sicle du sanctuaire, qui est de vingt oboles.
17 “Lakini kamwe usimkomboe mzaliwa wa kwanza wa maksai, kondoo au mbuzi; hawa ni watakatifu. Nyunyizia damu yao juu ya madhabahu na uchome mafuta yao kama sadaka itolewayo kwa moto, harufu nzuri inayompendeza Bwana.
Mais tu ne rachèteras point le premier-né de la vache, ni le premier-né de la brebis, ni le premier-né de la chèvre; ce sont des choses sacrées. Tu répandras leur sang sur l'autel, et tu feras fumer leur graisse en sacrifice fait par le feu, d'agréable odeur à l'Éternel.
18 Nyama zao zitakuwa chakula chenu, kama ilivyokuwa kidari cha kuinuliwa na paja la mguu wa kulia.
Et leur chair t'appartiendra; elle t'appartiendra comme la poitrine qu'on agite, et comme la jambe droite.
19 Chochote kitakachotengwa kutoka sadaka takatifu ambazo Waisraeli wanamtolea Bwana, ninakupa wewe, wanao na binti zako kama fungu lenu la kawaida. Ni Agano la milele la chumvi mbele za Bwana kwako na watoto wako.”
Je t'ai donné toutes les offrandes prélevées sur les choses sacrées que les enfants d'Israël offriront à l'Éternel, à toi, à tes fils, et à tes filles avec toi, par ordonnance perpétuelle; c'est une alliance incorruptible, perpétuelle devant l'Éternel, pour toi et pour ta postérité avec toi.
20 Bwana akamwambia Aroni, “Hutakuwa na urithi wowote katika nchi yao, wala hutakuwa na sehemu miongoni mwao; Mimi ni fungu lako na urithi wako miongoni mwa Waisraeli.
Puis l'Éternel dit à Aaron: Tu n'auras point d'héritage en leur pays; tu n'auras point de portion au milieu d'eux; je suis ta portion et ton héritage au milieu des enfants d'Israël.
21 “Ninawapa Walawi zaka yote katika Israeli kama urithi wao kuwa kama malipo kwa kazi wanayoifanya wakati wanapohudumu katika Hema la Kukutania.
Et quant aux enfants de Lévi, voici, je leur ai donné pour héritage toutes les dîmes d'Israël, en échange du service qu'ils font, le service du tabernacle d'assignation.
22 Kuanzia sasa, kamwe Waisraeli wasisogelee karibu na Hema la Kukutania, la sivyo watabeba matokeo ya dhambi zao, nao watakufa.
Et les enfants d'Israël n'approcheront plus du tabernacle d'assignation, de peur qu'ils ne se chargent d'un péché et qu'ils ne meurent.
23 Ni Walawi watakaofanya kazi katika Hema la Kukutania na kubeba wajibu wa makosa dhidi yake. Hili ni agizo la kudumu kwa vizazi vijavyo. Hawatapokea urithi wowote miongoni mwa Waisraeli.
Mais ce sont les Lévites qui feront le service du tabernacle d'assignation, et ce sont eux qui porteront leur iniquité; ce sera une ordonnance perpétuelle dans vos générations; et ils ne posséderont point d'héritage au milieu des enfants d'Israël.
24 Badala yake, ninawapa Walawi zaka zote zinazotolewa na Waisraeli kama sadaka kwa Bwana kuwa urithi wao. Hiyo ndiyo sababu nimesema hivi kuhusu wao: ‘Hawatakuwa na urithi miongoni mwa Waisraeli.’”
Car j'ai donné pour héritage aux Lévites les dîmes des enfants d'Israël, qu'ils prélèveront pour l'Éternel en offrande; c'est pourquoi, j'ai dit d'eux: Ils ne posséderont point d'héritage au milieu des enfants d'Israël.
25 Bwana akamwambia Mose,
Puis l'Éternel parla à Moïse, en disant:
26 “Sema na Walawi na uwaambie: ‘Mtakapopokea zaka kutoka kwa Waisraeli ambayo ninawapa kama urithi wenu kutoka kwao, ni lazima mtoe sehemu ya kumi ya hiyo zaka kama sadaka kwa Bwana, iwe zaka ya hiyo zaka.
Tu parleras aussi aux Lévites, et tu leur diras: Quand vous aurez reçu des enfants d'Israël la dîme que je vous ai donnée sur eux pour votre héritage, vous en prélèverez l'offrande de l'Éternel, la dîme de la dîme.
27 Sadaka yenu itahesabiwa kwenu kama nafaka kutoka sakafu ya kupuria, au divai kutoka kwenye shinikizo la kukamulia zabibu.
Et votre offrande prélevée vous sera comptée comme le froment de l'aire et comme l'abondance de la cuve.
28 Kwa njia hii, ninyi pia mtatoa sadaka kwa Bwana kutoka zaka zote mtakazopokea kutoka kwa Waisraeli. Kutoka kwenye zaka hizi, ni lazima mtoe sehemu ya Bwana kwa Aroni, kuhani.
Ainsi, vous prélèverez, vous aussi, l'offrande de l'Éternel sur toutes vos dîmes, que vous recevrez des enfants d'Israël; et vous en donnerez l'offrande de l'Éternel à Aaron, le sacrificateur.
29 Ni lazima mtoe kama sehemu ya Bwana iliyo nzuri sana tena ile sehemu iliyo takatifu sana kuliko zote ya kile kitu mlichopewa.’
Vous prélèverez toute l'offrande de l'Éternel, sur toutes les choses qui vous seront données; sur tout ce qu'il y aura de meilleur, vous prélèverez la portion consacrée.
30 “Waambie Walawi: ‘Mtakapotoa sehemu zilizo bora sana, itahesabiwa kwenu kama mazao ya sakafu ya kupuria nafaka, au ya shinikizo la kukamulia zabibu.
Et tu leur diras: Quand vous aurez prélevé le meilleur de la dîme, elle sera comptée aux Lévites comme le revenu de l'aire et comme le revenu de la cuve.
31 Ninyi na watu wa nyumbani mwenu mnaweza kula sehemu iliyobaki mahali popote, kwani ndio ujira wenu kwa ajili ya kazi yenu katika Hema la Kukutania.
Et vous la mangerez en un lieu quelconque, vous et votre famille; car c'est votre salaire, en échange de votre service dans le tabernacle d'assignation.
32 Kwa kutoa sehemu zake zilizo bora sana, hamtakuwa na hatia katika jambo hili; ndipo hamtatia unajisi sadaka takatifu za Waisraeli, nanyi hamtakufa.’”
Et par là vous ne vous chargerez d'aucun péché, quand vous en aurez prélevé ce qu'il y a de meilleur, et vous ne profanerez point les choses sacrées des enfants d'Israël, et vous ne mourrez point.