< Hesabu 18 >

1 Bwana akamwambia Aroni, “Wewe, wanao na jamaa ya baba yako mtawajibika kwa makosa dhidi ya mahali patakatifu, na wewe na wanao peke yenu ndio mtakaowajibika kwa makosa dhidi ya ukuhani.
HERREN sagde til Aron: Du tillige med dine Sønner og dit Fædrenehus skal have Ansvaret for Helligdommen, og du tillige med dine Sønner skal have Ansvaret for eders Præstetjeneste.
2 Walete Walawi wenzako kutoka kabila la baba zako ili waungane nanyi na kuwasaidia wakati wewe na wanao mnapohudumu mbele ya Hema la Ushuhuda.
Men også dine Brødre, Levis Stamme, din Fædrenestamme, skal du lade træde frem sammen med dig, og de skal holde sig til dig og gå dig til Hånde, når du tillige med dine Sønner gør Tjeneste foran Vidnesbyrdets Telt;
3 Watawajibika kwenu na watafanya kazi zote za Hema, lakini kamwe wasisogelee vifaa vya patakatifu au madhabahu, la sivyo wao na ninyi mtakufa.
og de skal tage Vare på, hvad du har at varetage, og på alt, hvad der er at varetage ved Teltet, men de må ikke komme de hellige Ting eller Alteret nær, at ikke både de og I skal dø.
4 Watajiunga nanyi na watawajibika kwa utunzaji wa Hema la Kukutania, yaani kazi zote kwenye Hema, wala hakuna mtu mwingine yeyote atakayeweza kusogea karibu hapo mlipo.
De skal holde sig til dig og tage Vare på, hvad der er at varetage ved Åbenbaringsteltet, alt Arbejdet derved, men ingen Lægmand må der komme eder nær.
5 “Mtawajibika katika utunzaji wa mahali patakatifu na madhabahu, ili kwamba ghadhabu isiwaangukie Waisraeli tena.
Men I skal tage Vare på, hvad der er at varetage ved Helligdommen og Alteret, for at der ikke atter skal komme Vrede over Israelitterne.
6 Mimi mwenyewe nimewachagua Walawi wenzenu kutoka miongoni mwa Waisraeli kama zawadi kwenu, waliowekwa wakfu kwa Bwana ili kufanya kazi katika Hema la Kukutania.
Se, jeg har selv udtaget eders Brødre Leviterne af Israelitternes Midte som en Gave til eder, de er givet HERREN til at udføre Arbejdet ved Åbenbaringsteltet.
7 Lakini ni wewe tu na wanao mtakaoweza kutumika kama makuhani kuhusiana na kila kitu kwenye madhabahu na ndani ya pazia. Ninawapa utumishi wa ukuhani kama zawadi. Mtu mwingine yeyote atakayekaribia mahali patakatifu ni lazima auawe.”
Men du tillige med dine Sønner skal tage Vare på eders Præstegerning i alt, hvad der angår Alteret og det, der er inden for Forhænget, og udføre Arbejdet derved. Som en Gave skænker jeg eder Præstedømmet; men enhver Lægmand, der trænger sig ind deri, skal lide Døden.
8 Kisha Bwana akamwambia Aroni, “Mimi mwenyewe nimekuweka kuwa mwangalizi wa sadaka zote zitakazotolewa kwangu; matoleo yote matakatifu Waisraeli wanayonipa ninakupa wewe na wanao kama sehemu yenu na fungu lenu la kawaida.
HERREN talede fremdeles til Aron: Se, jeg giver dig, hvad der skal lægges til Side af mine Offerydelser; alle Israelitternes Helliggaver giver jeg dig og dine Sønner som eders Del, en evig gyldig Rettighed.
9 Mtachukua sehemu ya yale matoleo matakatifu sana ambayo hayateketezwi kwa moto. Kutoka kwa matoleo yote wanayoniletea kama sadaka takatifu sana, ziwe za nafaka, au za dhambi, au za makosa, sehemu ile itakuwa yako na wanao.
Følgende skal tilfalde dig af det højhellige, fraregnet hvad der opbrændes: Alle deres Offergaver, der falder ind under Afgrødeofre, Syndofre og Skyldofre, som de bringer mig til Erstatning; som højhelligt skal dette tilfalde dig og dine Sønner.
10 Mtaila kama kitu kilicho kitakatifu sana; kila mwanaume ataila. Ni lazima mtaiheshimu kama takatifu.
På et højhelligt Sted skal du spise det, og alle af Mandkøn må spise deraf; det skal være dig helligt.
11 “Hiki pia ni chako: chochote kilichotengwa kutoka kwenye matoleo yote ya sadaka za kuinuliwa za Waisraeli. Ninakupa wewe haya, wana na binti zako kama sehemu yenu ya kawaida. Kila mmoja wa nyumba yako ambaye ni safi kwa taratibu za ibada anaweza kuyala.
Fremdeles skal følgende tilfalde dig som Offerydelse af deres Gaver: Alle Gaver fra Israelitterne, hvormed der udføres Svingning, giver jeg dig tillige med dine Sønner og Døtre som en evig gyldig Rettighed; enhver, som er ren i dit Hus, må spise deraf.
12 “Ninawapa mafuta ya zeituni yaliyo bora kuliko yote, na divai mpya iliyo bora kuliko zote na nafaka wanazompa Bwana kama malimbuko katika mavuno yao.
Alt det bedste af Olien, Mosten og Kornet, Førstegrøden deraf, som de giver HERREN, giver jeg dig.
13 Malimbuko yote ya nchi ambayo wanamletea Bwana yatakuwa yenu. Kila mmoja nyumbani kwako ambaye ni safi kwa taratibu za Ibada anaweza kula.
De første Frugter af alt, hvad der gror i deres Land, som de bringer HERREN, skal tilfalde dig; enhver, som er ren i dit Hus, må spise deraf.
14 “Kila kitu katika Israeli ambacho kimetolewa kwa Bwana ni chenu.
Alt, hvad der lægges Band på i Israel, skal tilfalde dig.
15 Kila mzaliwa wa kwanza wa mwanadamu na wa mnyama, ambaye ametolewa kwa Bwana ni wenu. Lakini ni lazima mtamkomboa kila mwana mzaliwa wa kwanza na kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa wanyama wasio safi.
Af alt Kød, som de bringer til HERREN, såvel af Mennesker som af Dyr, skal alt, hvad der åbner Moders Liv, tilfalde dig; dog skal du lade de førstefødte Mennesker udløse, og ligeledes skal du lade de førstefødte urene Dyr udløse.
16 Watakapokuwa na umri wa mwezi mmoja, ni lazima mtawakomboa kwa bei ya ukombozi iliyowekwa, kwa shekeli tano za fedha, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, yenye uzito wa gera ishirini.
Hine skal du lade udløse, når de er en Måned gamle eller derover, med en Vurderingssum af fem Sekel efter hellig Vægt, tyve Gera på en Sekel.
17 “Lakini kamwe usimkomboe mzaliwa wa kwanza wa maksai, kondoo au mbuzi; hawa ni watakatifu. Nyunyizia damu yao juu ya madhabahu na uchome mafuta yao kama sadaka itolewayo kwa moto, harufu nzuri inayompendeza Bwana.
Men de førstefødte Stykker Hornkvæg, Lam eller Geder må du ikke lade udløse; de er hellige, deres Blod skal du sprænge på Alteret, og Fedtet skal du bringe som Røgoffer, et Ildoffer til en liflig Duft for HERREN;
18 Nyama zao zitakuwa chakula chenu, kama ilivyokuwa kidari cha kuinuliwa na paja la mguu wa kulia.
men Kødet tilfalder dig; ligesom Svingningsbrystet og højre Kølle tilfalder det dig.
19 Chochote kitakachotengwa kutoka sadaka takatifu ambazo Waisraeli wanamtolea Bwana, ninakupa wewe, wanao na binti zako kama fungu lenu la kawaida. Ni Agano la milele la chumvi mbele za Bwana kwako na watoto wako.”
Al Offerydelse af Helliggaver, som Israelitterne yder HERREN, giver jeg dig tillige med dine Sønner og Døtre som en evig gyldig Rettighed; det skal være en evig gyldig Saltpagt for HERRENs Åsyn for dig tillige med dine Efterkommere.
20 Bwana akamwambia Aroni, “Hutakuwa na urithi wowote katika nchi yao, wala hutakuwa na sehemu miongoni mwao; Mimi ni fungu lako na urithi wako miongoni mwa Waisraeli.
HERREN sagde fremdeles til Aron: Du skal ingen Arvelod have i deres Land, og der skal ikke tilfalde dig nogen Lod iblandt dem; jeg selv er din Arvelod og Del blandt Israelitterne.
21 “Ninawapa Walawi zaka yote katika Israeli kama urithi wao kuwa kama malipo kwa kazi wanayoifanya wakati wanapohudumu katika Hema la Kukutania.
Men se, Levisønnerne giver jeg al Tiende i Israel som Arvelod til Løn for det Arbejde, de udfører ved Åbenbaringsteltet.
22 Kuanzia sasa, kamwe Waisraeli wasisogelee karibu na Hema la Kukutania, la sivyo watabeba matokeo ya dhambi zao, nao watakufa.
Israelitterne må herefter ikke komme Åbenbaringsteltet nær, for at de ikke skal pådrage sig Synd og dø;
23 Ni Walawi watakaofanya kazi katika Hema la Kukutania na kubeba wajibu wa makosa dhidi yake. Hili ni agizo la kudumu kwa vizazi vijavyo. Hawatapokea urithi wowote miongoni mwa Waisraeli.
kun Leviterne må udføre Arbejdet ved Åbenbaringsteltet, og de skal have Ansvaret derfor. Det skal være eder en evig gyldig Anordning fra Slægt til Slægt. Men nogen Arvelod skal de ikke have blandt Israelitterne;
24 Badala yake, ninawapa Walawi zaka zote zinazotolewa na Waisraeli kama sadaka kwa Bwana kuwa urithi wao. Hiyo ndiyo sababu nimesema hivi kuhusu wao: ‘Hawatakuwa na urithi miongoni mwa Waisraeli.’”
thi Tienden, Israelitterne yder HERREN som Offerydelse, giver jeg Leviterne til Arvelod. Derfor sagde jeg dem, at de ikke skal have nogen Arvelod blandt Israelitterne.
25 Bwana akamwambia Mose,
HERREN talede fremdeles til Moses og sagde:
26 “Sema na Walawi na uwaambie: ‘Mtakapopokea zaka kutoka kwa Waisraeli ambayo ninawapa kama urithi wenu kutoka kwao, ni lazima mtoe sehemu ya kumi ya hiyo zaka kama sadaka kwa Bwana, iwe zaka ya hiyo zaka.
Tal til Leviterne og sig til dem: Når I af Israelitterne modtager Tienden, som jeg har givet eder som den Arvelod, I skal have af dem, så skal I yde HERREN en Offerydelse deraf, Tiende af Tienden;
27 Sadaka yenu itahesabiwa kwenu kama nafaka kutoka sakafu ya kupuria, au divai kutoka kwenye shinikizo la kukamulia zabibu.
og denne eders Offerydelse skal ligestilles med Offerydelsen af Kornet fra Tærskepladsen og Overfloden fra Vinpersen.
28 Kwa njia hii, ninyi pia mtatoa sadaka kwa Bwana kutoka zaka zote mtakazopokea kutoka kwa Waisraeli. Kutoka kwenye zaka hizi, ni lazima mtoe sehemu ya Bwana kwa Aroni, kuhani.
Således skal også I yde HERREN en Offerydelse af al den Tiende, I modtager af Israelitterne, og denne HERRENs Offerydelse skal I give Præsten Aron.
29 Ni lazima mtoe kama sehemu ya Bwana iliyo nzuri sana tena ile sehemu iliyo takatifu sana kuliko zote ya kile kitu mlichopewa.’
Af alle de Gaver, I modtager, skal I yde HERRENs Offerydelse, af alt det bedste deraf, som hans Helliggave.
30 “Waambie Walawi: ‘Mtakapotoa sehemu zilizo bora sana, itahesabiwa kwenu kama mazao ya sakafu ya kupuria nafaka, au ya shinikizo la kukamulia zabibu.
Og sig til dem: Når I yder det bedste deraf, skal det ligestilles med Offerydelsen af, hvad der kommer fra Tærskepladsen og Vinpersen.
31 Ninyi na watu wa nyumbani mwenu mnaweza kula sehemu iliyobaki mahali popote, kwani ndio ujira wenu kwa ajili ya kazi yenu katika Hema la Kukutania.
I må spise det hvor som helst sammen med eders Familie, thi det er eders Løn for eders Arbejde ved Åbenbaringsteltet.
32 Kwa kutoa sehemu zake zilizo bora sana, hamtakuwa na hatia katika jambo hili; ndipo hamtatia unajisi sadaka takatifu za Waisraeli, nanyi hamtakufa.’”
Når I blot yder det bedste deraf, skal I ikke for den Sags Skyld pådrage eder Synd og ikke vanhellige Israelitternes Helliggaver og udsætte eder for at dø.

< Hesabu 18 >