< Hesabu 17 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Then spake Yahweh unto Moses, saying:
2 “Sema na Waisraeli, na ujipatie fimbo kumi na mbili kutoka kwao, moja kutoka kwa kila mmoja wa viongozi wa kabila za baba zao. Andika jina la kila mtu kwenye fimbo yake.
Speak unto the sons of Israel and take of them one staff each for an ancestral house of all their princes, by their ancestral houses, twelve staves, —each man’s name, shalt thou write upon his staff;
3 Kwenye fimbo ya Lawi andika jina la Aroni, kwa maana ni lazima iwepo fimbo moja kwa kila kiongozi kwa ajili ya kila kabila la baba zao.
and, Aaron’s name, shalt thou write upon the staff of Levi, —for, one staff, shall there be for the head of their ancestral house.
4 Ziweke hizo fimbo ndani ya Hema la Kukutania mbele ya Sanduku la Ushuhuda, mahali nikutanapo nawe.
Then shalt thou lay them up in the tent of meeting, —before the testimony, where I meet with you.
5 Fimbo ya mtu nitakayemchagua itachipuka, nami mwenyewe nitayakomesha haya manungʼuniko ya mara kwa mara ya Waisraeli dhidi yako.”
So shall it come to pass, that, the man whom I shall choose, his staff, shall bud, —so will I cause to cease from against me the murmurings of the sons of Israel, wherewith they, are murmuring against you.
6 Hivyo Mose akasema na Waisraeli, nao viongozi wao wakampa fimbo kumi na mbili, fimbo moja kwa ajili ya kila kabila la baba zao, nayo fimbo ya Aroni ikiwa miongoni mwa hizo.
And Moses spake unto the sons of Israel and every one of their princes gave unto him, a staff apiece, for each prince, by their ancestral houses, twelve staves, —and the staff of Aaron, was in the midst of their staves.
7 Mose akaziweka hizo fimbo mbele za Bwana ndani ya Hema la Ushuhuda.
So Moses laid up the staves before Yahweh, —in the tent of the testimony.
8 Siku iliyofuata Mose aliingia kwenye Hema la Ushuhuda akaona ile fimbo ya Aroni ambayo iliwakilisha jamaa ya Lawi haikuwa tu imechipuka, bali pia ilikuwa imetoa machipukizi, kuchanua maua na kuzaa malozi.
And it came to pass, on the morrow, that Moses entered into the tent of the testimony; and lo! the staff of Aaron for the house of Levi, had budded, —yea it had brought forth buds and bloomed blossoms, and borne ripe almonds.
9 Ndipo Mose akaleta zile fimbo zote kwa Waisraeli wote kutoka mbele za Bwana. Wakaziangalia, na kila mtu akaichukua fimbo yake mwenyewe.
So then Moses brought forth all the staves, from before Yahweh, unto all the sons of Israel, —and they saw and took, each man his own staff.
10 Bwana akamwambia Mose, “Rudisha fimbo ya Aroni mbele ya Sanduku la Ushuhuda, ili ihifadhiwe kama alama kwa waasi. Hili litakomesha manungʼuniko yao dhidi yangu, ili kwamba wasife.”
And Yahweh said unto Moses—Put back the rod of Aaron, before the testimony, to be kept as a sign unto such as are perverse, —that thou mayest bring to an end their murmurings against me that they die not.
11 Mose akafanya kama Bwana alivyomwamuru.
Thus did Moses, —as Yahweh commanded him, so, did he.
12 Waisraeli wakamwambia Mose, “Tutakufa! Tumepotea, sote tumepotea!
Then spake the sons of Israel unto Moses saying: Lo! we have breathed our last—we are lost, we are, all, lost:
13 Yeyote akaribiaye Maskani ya Bwana atakufa. Je, sisi sote tutakufa?”
whosoever draweth near—draweth near—unto the habitation of Yahweh, dieth, —are we ever to have made an end of breathing our last?

< Hesabu 17 >