< Hesabu 17 >

1 Bwana akamwambia Mose,
And the Lord spake vnto Moses, saying,
2 “Sema na Waisraeli, na ujipatie fimbo kumi na mbili kutoka kwao, moja kutoka kwa kila mmoja wa viongozi wa kabila za baba zao. Andika jina la kila mtu kwenye fimbo yake.
Speake vnto the children of Israel, and take of euery one of them a rod, after the house of their fathers, of all their princes according to the familie of their fathers, euen twelue rods: and thou shalt write euery mans name vpon his rod.
3 Kwenye fimbo ya Lawi andika jina la Aroni, kwa maana ni lazima iwepo fimbo moja kwa kila kiongozi kwa ajili ya kila kabila la baba zao.
And write Aarons name vpon the rod of Leui: for euery rodde shalbe for the head of the house of their fathers.
4 Ziweke hizo fimbo ndani ya Hema la Kukutania mbele ya Sanduku la Ushuhuda, mahali nikutanapo nawe.
And thou shalt put them in the Tabernacle of the Congregation, before the Arke of the Testimonie, where I wil declare my selfe to you.
5 Fimbo ya mtu nitakayemchagua itachipuka, nami mwenyewe nitayakomesha haya manungʼuniko ya mara kwa mara ya Waisraeli dhidi yako.”
And the mans rod, whome I chuse, shall blossome: and I will make cease from mee the grudgings of the children of Israel, which grudge against you.
6 Hivyo Mose akasema na Waisraeli, nao viongozi wao wakampa fimbo kumi na mbili, fimbo moja kwa ajili ya kila kabila la baba zao, nayo fimbo ya Aroni ikiwa miongoni mwa hizo.
Then Moses spake vnto the children of Israel, and al their princes gaue him a rod, one rod for euery Prince, according to the houses of their fathers, euen twelue rods, and the rod of Aaron was among their roddes.
7 Mose akaziweka hizo fimbo mbele za Bwana ndani ya Hema la Ushuhuda.
And Moses layde the rods before the Lord in the Tabernacle of the Testimonie.
8 Siku iliyofuata Mose aliingia kwenye Hema la Ushuhuda akaona ile fimbo ya Aroni ambayo iliwakilisha jamaa ya Lawi haikuwa tu imechipuka, bali pia ilikuwa imetoa machipukizi, kuchanua maua na kuzaa malozi.
And when Moses on the morow went into the Tabernacle of the Testimonie, beholde, the rod of Aaron for the house of Leui was budded, and brought forth buddes, and brought forth blossoms, and bare ripe almondes.
9 Ndipo Mose akaleta zile fimbo zote kwa Waisraeli wote kutoka mbele za Bwana. Wakaziangalia, na kila mtu akaichukua fimbo yake mwenyewe.
Then Moses brought out all the rods from before the Lord vnto all the children of Israel: and they looked vpon them, and tooke euery man his rodde.
10 Bwana akamwambia Mose, “Rudisha fimbo ya Aroni mbele ya Sanduku la Ushuhuda, ili ihifadhiwe kama alama kwa waasi. Hili litakomesha manungʼuniko yao dhidi yangu, ili kwamba wasife.”
After, the Lord said vnto Moses, Bring Aarons rod againe before the Testimonie to bee kept for a token to the rebellious children, and thou shalt cause their murmurings to cease from me, that they dye not.
11 Mose akafanya kama Bwana alivyomwamuru.
So Moses did as the Lord had commanded him: so did he.
12 Waisraeli wakamwambia Mose, “Tutakufa! Tumepotea, sote tumepotea!
And the children of Israel spake vnto Moses, saying, Behold, we are dead, we perish, we are all lost:
13 Yeyote akaribiaye Maskani ya Bwana atakufa. Je, sisi sote tutakufa?”
Whosoeuer commeth neere, or approcheth to the Tabernacle of the Lord, shall dye: shall we be consumed and dye?

< Hesabu 17 >