< Hesabu 17 >

1 Bwana akamwambia Mose,
And Jehovah spoke to Moses, saying,
2 “Sema na Waisraeli, na ujipatie fimbo kumi na mbili kutoka kwao, moja kutoka kwa kila mmoja wa viongozi wa kabila za baba zao. Andika jina la kila mtu kwenye fimbo yake.
Speak unto the children of Israel, and take of them a staff, a staff for each father's house, of all their princes according to the houses of their fathers, twelve staves: thou shalt write each one's name upon his staff.
3 Kwenye fimbo ya Lawi andika jina la Aroni, kwa maana ni lazima iwepo fimbo moja kwa kila kiongozi kwa ajili ya kila kabila la baba zao.
And Aaron's name shalt thou write upon the staff of Levi; for one staff shall be for [each] head of their fathers' houses.
4 Ziweke hizo fimbo ndani ya Hema la Kukutania mbele ya Sanduku la Ushuhuda, mahali nikutanapo nawe.
And thou shalt lay them up in the tent of meeting before the testimony, where I meet with you.
5 Fimbo ya mtu nitakayemchagua itachipuka, nami mwenyewe nitayakomesha haya manungʼuniko ya mara kwa mara ya Waisraeli dhidi yako.”
And it shall come to pass, that the man whom I shall choose, his staff shall bud forth; and I will make to cease from before me the murmurings of the children of Israel, that they murmur against you.
6 Hivyo Mose akasema na Waisraeli, nao viongozi wao wakampa fimbo kumi na mbili, fimbo moja kwa ajili ya kila kabila la baba zao, nayo fimbo ya Aroni ikiwa miongoni mwa hizo.
And Moses spoke to the children of Israel, and all their princes gave him a staff, one staff for each prince according to their fathers' houses, twelve staves, and the staff of Aaron was among their staves.
7 Mose akaziweka hizo fimbo mbele za Bwana ndani ya Hema la Ushuhuda.
And Moses laid the staves before Jehovah in the tent of the testimony.
8 Siku iliyofuata Mose aliingia kwenye Hema la Ushuhuda akaona ile fimbo ya Aroni ambayo iliwakilisha jamaa ya Lawi haikuwa tu imechipuka, bali pia ilikuwa imetoa machipukizi, kuchanua maua na kuzaa malozi.
And it came to pass, when on the morrow Moses went into the tent of the testimony, behold, the staff of Aaron for the house of Levi had budded, and brought forth buds, and bloomed blossoms, and ripened almonds.
9 Ndipo Mose akaleta zile fimbo zote kwa Waisraeli wote kutoka mbele za Bwana. Wakaziangalia, na kila mtu akaichukua fimbo yake mwenyewe.
And Moses brought out all the staves from before Jehovah to all the children of Israel, and they looked and took each one his staff.
10 Bwana akamwambia Mose, “Rudisha fimbo ya Aroni mbele ya Sanduku la Ushuhuda, ili ihifadhiwe kama alama kwa waasi. Hili litakomesha manungʼuniko yao dhidi yangu, ili kwamba wasife.”
And Jehovah said to Moses, Bring Aaron's staff again before the testimony, to be kept as a token for the sons of rebellion, that thou mayest put an end to their murmurings before me, that they may not die.
11 Mose akafanya kama Bwana alivyomwamuru.
And Moses did so: as Jehovah had commanded him, so did he.
12 Waisraeli wakamwambia Mose, “Tutakufa! Tumepotea, sote tumepotea!
And the children of Israel spoke to Moses, saying, Lo, we expire, we perish, we all perish.
13 Yeyote akaribiaye Maskani ya Bwana atakufa. Je, sisi sote tutakufa?”
Every one that comes at all near to the tabernacle of Jehovah shall die: shall we then expire altogether?

< Hesabu 17 >