< Hesabu 17 >
And the Lord said to Moses,
2 “Sema na Waisraeli, na ujipatie fimbo kumi na mbili kutoka kwao, moja kutoka kwa kila mmoja wa viongozi wa kabila za baba zao. Andika jina la kila mtu kwenye fimbo yake.
Say to the children of Israel that they are to give you rods, one for every family, for every chief, the head of his father's house, making twelve rods; let every man's name be placed on his rod.
3 Kwenye fimbo ya Lawi andika jina la Aroni, kwa maana ni lazima iwepo fimbo moja kwa kila kiongozi kwa ajili ya kila kabila la baba zao.
And let Aaron's name be placed on the rod of Levi: for there is to be one rod for the head of every family.
4 Ziweke hizo fimbo ndani ya Hema la Kukutania mbele ya Sanduku la Ushuhuda, mahali nikutanapo nawe.
And let them be stored up in the Tent of meeting, in front of the ark of witness where I come to you.
5 Fimbo ya mtu nitakayemchagua itachipuka, nami mwenyewe nitayakomesha haya manungʼuniko ya mara kwa mara ya Waisraeli dhidi yako.”
And the rod of that man who is marked out by me for myself will have buds on it; so I will put a stop to the outcries which the children of Israel make to me against you.
6 Hivyo Mose akasema na Waisraeli, nao viongozi wao wakampa fimbo kumi na mbili, fimbo moja kwa ajili ya kila kabila la baba zao, nayo fimbo ya Aroni ikiwa miongoni mwa hizo.
So Moses gave these orders to the children of Israel, and all their chiefs gave him rods, one for the head of every family, making twelve rods: and Aaron's rod was among them.
7 Mose akaziweka hizo fimbo mbele za Bwana ndani ya Hema la Ushuhuda.
And Moses put the rods before the Lord in the Tent of witness.
8 Siku iliyofuata Mose aliingia kwenye Hema la Ushuhuda akaona ile fimbo ya Aroni ambayo iliwakilisha jamaa ya Lawi haikuwa tu imechipuka, bali pia ilikuwa imetoa machipukizi, kuchanua maua na kuzaa malozi.
Now on the day after, Moses went into the Tent of witness; and he saw that Aaron's rod, the rod of the house of Levi, had put out buds, and was covered with buds and flowers and fruit.
9 Ndipo Mose akaleta zile fimbo zote kwa Waisraeli wote kutoka mbele za Bwana. Wakaziangalia, na kila mtu akaichukua fimbo yake mwenyewe.
Then Moses took out all the rods from before the Lord, and gave them back to the children of Israel: and they saw them, and every man took his rod.
10 Bwana akamwambia Mose, “Rudisha fimbo ya Aroni mbele ya Sanduku la Ushuhuda, ili ihifadhiwe kama alama kwa waasi. Hili litakomesha manungʼuniko yao dhidi yangu, ili kwamba wasife.”
And the Lord said to Moses, Put Aaron's rod back in front of the ark of witness, to be kept for a sign against this false-hearted people, so that you may put a stop to their outcries against me, and death may not overtake them.
11 Mose akafanya kama Bwana alivyomwamuru.
This Moses did: as the Lord gave orders, so he did.
12 Waisraeli wakamwambia Mose, “Tutakufa! Tumepotea, sote tumepotea!
And the children of Israel said to Moses, Truly, destruction has come on us; an evil fate has overtaken us all.
13 Yeyote akaribiaye Maskani ya Bwana atakufa. Je, sisi sote tutakufa?”
Death will overtake everyone who comes near, who comes near the House of the Lord: are we all to come to destruction?