< Hesabu 15 >

1 Bwana akamwambia Mose,
RAB Musa'ya şöyle dedi:
2 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Baada ya ninyi kuingia katika nchi ninayowapa kama nyumbani,
“İsrail halkına de ki, ‘Yerleşmek için size vereceğim ülkeye girince,
3 nanyi mkitoa sadaka za kuteketezwa kwa moto, kutoka makundi ya ngʼombe au kondoo, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, ikiwa ni sadaka za kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum ama sadaka ya hiari au sadaka ya sikukuu zenu,
RAB'bi hoşnut eden bir koku yapmak için yakmalık sunu, özel adak kurbanı, gönülden verilen sunu ya da bayram sunusu gibi yakılan sunu olarak RAB'be sığır ya da davar sunacaksınız.
4 ndipo yeye aletaye sadaka yake ataiweka mbele za Bwana sadaka ya nafaka, sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta.
Sunu sunan kişi RAB'be tahıl sunusu olarak dörtte bir hin zeytinyağıyla yoğrulmuş onda bir efa ince un sunacak.
5 Pamoja na kila mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, andaa robo ya hini ya divai kwa sadaka ya kinywaji.
Yakmalık sunu ya da kurban için, her kuzuya dökmelik sunu olarak dörtte bir hin şarap hazırla.
6 “‘Pamoja na kondoo dume andaa sadaka ya nafaka ya sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na theluthi moja ya hini ya mafuta,
“‘Koç sunarken tahıl sunusu olarak üçte bir hin zeytinyağıyla yoğrulmuş onda iki efa ince un hazırla.
7 na theluthi moja ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Vitoe kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
Dökmelik sunu olarak da üçte bir hin şarap sun. Bunları RAB'bi hoşnut eden koku olarak sunacaksın.
8 “‘Unapoandaa fahali mchanga kama sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum au sadaka ya amani kwa Bwana,
RAB'be yakmalık sunu, özel adak kurbanı ya da esenlik sunusu olarak bir boğa sunduğunda,
9 leta pamoja na huyo fahali sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na nusu ya hini ya mafuta.
boğayla birlikte tahıl sunusu olarak yarım hin zeytinyağıyla yoğrulmuş onda üç efa ince un sun.
10 Pia utaleta nusu ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Itakuwa sadaka iliyoteketezwa kwa moto, harufu nzuri inayompendeza Bwana.
Ayrıca dökmelik sunu olarak yarım hin şarap sun. Yakılan bu sunu RAB'bi hoşnut eden bir koku olacak.
11 Kila fahali au kondoo dume, kila mwana-kondoo au mbuzi mchanga, atatayarishwa kwa njia hii.
Sığır, koç, davar –kuzu ya da keçi– böyle hazırlanacak.
12 Fanyeni hivi kwa ajili ya kila mmoja, kwa kadiri ya wingi wa mtakavyoandaa.
Kaç hayvan sunacaksan her biri için aynı şeyleri yapacaksın.
13 “‘Kila mmoja ambaye ni mzawa ni lazima afanye vitu hivi kwa njia hii hapo aletapo sadaka ya kuteketezwa kwa moto kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
“‘Her İsrail yerlisi RAB'bi hoşnut eden koku olarak yakılan bir sunu sunarken bunları aynen yapmalıdır.
14 Kwa vizazi vijavyo, wakati wowote mgeni au mtu mwingine yeyote anayeishi miongoni mwenu aletapo sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana, ni lazima afanye sawasawa kabisa na jinsi mnavyofanya ninyi.
Kuşaklar boyunca aranızda yaşayan bir yabancı ya da yerli olmayan bir konuk, RAB'bi hoşnut eden koku olarak yakılan bir sunu sunarken, sizin uyguladığınız kuralları uygulamalıdır.
15 Jumuiya itakuwa na sheria hizo hizo kwenu na kwa mgeni aishiye miongoni mwenu; hii ni amri ya kudumu kwa vizazi vijavyo. Ninyi na mgeni mtakuwa sawa mbele za Bwana:
Sizin ve aranızda yaşayan yabancılar için topluluk aynı kuralları uygulamalıdır. Kuşaklar boyunca kalıcı bir kural olacak bu. RAB'bin önünde siz nasılsanız, aranızda yaşayan yabancı da aynı olacak.
16 Sheria hizo hizo na masharti hayo hayo hayo, yatawahusu ninyi na mgeni aishiye miongoni mwenu.’”
Size de aranızda yaşayan yabancıya da aynı yasalar ve kurallar uygulanacak.’”
17 Bwana akamwambia Mose,
RAB Musa'ya şöyle dedi:
18 “Sema na Waisraeli na uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapeleka
“İsrail halkına de ki, ‘Sizi götüreceğim ülkeye girip
19 nanyi mkala chakula cha nchi hiyo, toeni sehemu ya chakula hicho kama sadaka kwa Bwana.
o ülkenin ekmeğinden yediğinizde, bir kısmını bana sunacaksınız.
20 Toeni andazi kutoka kwa malimbuko ya chakula chenu kitokacho katika ardhi, na mkitoe kama sadaka kutoka sakafu ya kupuria nafaka.
İlk tahılınızdan sunu olarak bir pide sunacaksınız; bunu harmanınızdan bir sunu olarak sunacaksınız.
21 Kwa vizazi vyote vijavyo hamna budi kutoa sadaka hii kwa Bwana kutoka kwa malimbuko ya unga wenu.
İlk tahılınızdan yapılmış bu sunuyu kuşaklar boyunca RAB'be sunacaksınız.’”
22 “‘Basi kama pasipo kukusudia umeshindwa kushika mojawapo katika amri hizi ambazo Bwana alimpa Mose,
“‘Eğer bilmeden günah işlediyseniz, RAB'bin Musa'ya verdiği buyruklardan herhangi birini –RAB'bin buyruk verdiği günden başlayarak Musa aracılığıyla size ve gelecek kuşaklara buyurduğu herhangi bir şeyi– yerine getirmediyseniz
23 amri yoyote ya Bwana kwenu kupitia Mose, tangu siku ile Bwana alipowapa na inaendelea hadi vizazi vyote vijavyo;
24 ikiwa hili limefanyika pasipo kukusudia bila jumuiya kuwa na habari nalo, basi jumuiya yote itatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya kuteketezwa ikiwa harufu nzuri inayompendeza Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka na ya kinywaji zilizoamriwa kwayo, na mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
ve bu günah bilmeden işlendiyse, bütün topluluk RAB'bi hoşnut eden koku sunmak için yakmalık sunu olarak istenilen tahıl ve dökmelik sunuyla birlikte bir boğa, günah sunusu olarak da bir teke sunacaktır.
25 Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya jumuiya yote ya Kiisraeli, nao watasamehewa, kwa kuwa haikuwa makusudi nao wamemletea Bwana sadaka iliyoteketezwa kwa moto na sadaka ya dhambi kwa ajili ya kosa lao.
Kâhin bütün İsrail topluluğunun günahını bağışlatacak, halk bağışlanacak. Çünkü bilmeyerek günah işlediler. İşledikleri günah yüzünden RAB için yakılan sunu olarak sunularını ve günah sunularını sundular.
26 Jumuiya yote ya Kiisraeli pamoja na wageni waishio miongoni mwao watasamehewa, kwa sababu watu wote walihusika katika kosa lile lisilokusudiwa.
Bütün İsrail topluluğu da aranızda yaşayan yabancılar da bağışlanacaktır. Çünkü halk bilmeyerek bu günahı işledi.
27 “‘Lakini kama mtu mmoja peke yake akitenda dhambi pasipo kukusudia, ni lazima alete mbuzi mke wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
“‘Eğer biri bilmeden günah işlerse, günah sunusu olarak bir yaşında bir dişi keçi getirmeli.
28 Kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule aliyekosa kwa kufanya dhambi pasipo kukusudia, upatanisho utakapofanywa kwa ajili yake, atasamehewa.
Kâhin RAB'bin önünde, bilmeden günah işleyen kişinin günahını bağışlatacak. Bağışlatma yapılınca kişi bağışlanacak.
29 Sheria hiyo moja itamhusu kila mmoja ambaye ametenda dhambi pasipo kukusudia, awe Mwisraeli mzawa ama mgeni.
Bilmeden günah işleyen İsrail yerlisi için de aranızda yaşayan yabancı için de aynı yasayı uygulayacaksınız.
30 “‘Lakini yeyote ambaye amefanya dhambi kwa dharau awe mzawa au mgeni, anamkufuru Bwana, naye mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
“‘Yerli ya da yabancı biri bilerek günah işlerse, RAB'be saygısızlık etmiştir. Bu kişi halkının arasından atılmalı.
31 Kwa sababu amelidharau neno la Bwana na kuvunja amri zake, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali; hatia yake inabaki juu yake.’”
RAB'bin sözünü küçümsemiş, buyruklarına karşı gelmiştir. Bu nedenle o kişi halkının arasından kesinlikle atılacak, suçunun cezasını çekecektir.’”
32 Waisraeli walipokuwa jangwani, mtu mmoja alikutwa akikusanya kuni siku ya Sabato.
İsrailliler çöldeyken, Şabat Günü odun toplayan birini buldular.
33 Wale waliomkuta akikusanya kuni wakamleta kwa Mose, Aroni na kusanyiko lote,
Odun toplarken adamı bulanlar onu Musa'yla Harun'un ve bütün topluluğun önüne getirdiler.
34 nao wakamweka kifungoni, kwa sababu haikufahamika kwa wazi kwamba afanyiwe nini.
Adama ne yapılacağı belirlenmediğinden onu gözaltında tuttular.
35 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Huyo mtu ni lazima afe. Kusanyiko lote lazima limpige mawe nje ya kambi.”
Derken RAB Musa'ya, “O adam öldürülmeli. Bütün topluluk ordugahın dışında onu taşa tutsun” dedi.
36 Hivyo kusanyiko likamtoa nje ya kambi na kumpiga mawe hadi akafa, kama Bwana alivyomwamuru Mose.
Böylece topluluk adamı ordugahın dışına çıkardı. RAB'bin Musa'ya buyurduğu gibi, onu taşlayarak öldürdüler.
37 Bwana akamwambia Mose,
RAB Musa'ya şöyle dedi:
38 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Kwa vizazi vyote vijavyo jifanyieni vifundo katika pindo za mavazi yenu vikiwa na uzi wa buluu kwenye kila kifundo.
“İsrail halkına de ki, ‘Kuşaklar boyunca giysinizin dört yanına püskül dikeceksiniz. Her püskülün üzerine lacivert bir kordon koyacaksınız.
39 Mtakuwa mkivitazama vifundo hivyo ili mpate kukumbuka amri zote za Bwana, ili mpate kuzitii msije mkajitia uzinzi wenyewe kwa kuzifuata tamaa za mioyo yenu na za macho yenu.
Öyle ki, püskülleri gördükçe RAB'bin buyruklarını anımsayasınız. Böylelikle RAB'bin buyruklarına uyacak, yüreğinizin, gözünüzün istekleri ardınca gitmeyecek, hainlik etmeyeceksiniz.
40 Ndipo mtakumbuka kuzitii amri zangu zote nanyi mtawekwa wakfu kwa Mungu wenu.
Ta ki, bütün buyruklarımı anımsayıp tutasınız ve Tanrınız için kutsal olasınız.
41 Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa Misri niwe Mungu wenu. Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu.’”
Tanrınız olmak için sizi Mısır'dan çıkaran Tanrınız RAB benim. Tanrınız RAB benim.’”

< Hesabu 15 >