< Hesabu 15 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Gospod je spregovoril Mojzesu, rekoč:
2 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Baada ya ninyi kuingia katika nchi ninayowapa kama nyumbani,
»Spregovori Izraelovim otrokom in jim reci: ›Ko boste prišli v deželo svojih prebivališč, ki vam jo dajem
3 nanyi mkitoa sadaka za kuteketezwa kwa moto, kutoka makundi ya ngʼombe au kondoo, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, ikiwa ni sadaka za kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum ama sadaka ya hiari au sadaka ya sikukuu zenu,
in boste naredili daritev z ognjem Gospodu, žgalno daritev ali žrtvovanje z izpolnjevanjem zaobljube ali s prostovoljnim darovanjem ali na vaše slovesne praznike, da naredite prijeten vonj Gospodu, od črede ali od tropa,
4 ndipo yeye aletaye sadaka yake ataiweka mbele za Bwana sadaka ya nafaka, sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta.
potem bo tisti, ki daruje svoj dar Gospodu, prinesel jedilno daritev desetinke moke, umešane s četrtino vrča olja.
5 Pamoja na kila mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, andaa robo ya hini ya divai kwa sadaka ya kinywaji.
Pripravil boš četrtino vrča vina za pitno daritev, z žgalno daritvijo ali žrtvovanjem, za vsako jagnje.
6 “‘Pamoja na kondoo dume andaa sadaka ya nafaka ya sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na theluthi moja ya hini ya mafuta,
Ali za ovna boš pripravil za jedilno daritev dve desetinki moke, umešane s tretjino vrča olja.
7 na theluthi moja ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Vitoe kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
Za pitno daritev boš pripravil tretjino vrča vina, za prijeten vonj Gospodu.
8 “‘Unapoandaa fahali mchanga kama sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum au sadaka ya amani kwa Bwana,
Ko pripravljaš bikca za žgalno daritev ali za klavno daritev v izpolnjevanju obljube ali mirovnih daritev Gospodu,
9 leta pamoja na huyo fahali sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na nusu ya hini ya mafuta.
potem bo z bikcem jedilne daritve prinesel tri desetinke moke, umešane s polovico vrča olja.
10 Pia utaleta nusu ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Itakuwa sadaka iliyoteketezwa kwa moto, harufu nzuri inayompendeza Bwana.
Za pitno daritev boš prinesel polovico vrča vina, za ognjeno daritev, prijetnega vonja Gospodu.
11 Kila fahali au kondoo dume, kila mwana-kondoo au mbuzi mchanga, atatayarishwa kwa njia hii.
Tako bo to storjeno za enega bikca ali za enega ovna ali za jagnje ali kozlička.
12 Fanyeni hivi kwa ajili ya kila mmoja, kwa kadiri ya wingi wa mtakavyoandaa.
Glede na število, ki ga boste pripravili, tako boste storili vsakemu glede na njihovo število.
13 “‘Kila mmoja ambaye ni mzawa ni lazima afanye vitu hivi kwa njia hii hapo aletapo sadaka ya kuteketezwa kwa moto kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
Vsi, ki so rojeni iz dežele, bodo te stvari storili na ta način, z darovanjem ognjene daritve, prijetnega vonja Gospodu.
14 Kwa vizazi vijavyo, wakati wowote mgeni au mtu mwingine yeyote anayeishi miongoni mwenu aletapo sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana, ni lazima afanye sawasawa kabisa na jinsi mnavyofanya ninyi.
Če tujec začasno prebiva z vami ali kdorkoli je med vami v vaših rodovih in bo daroval ognjeno daritev prijetnega vonja Gospodu; kakor počnete vi, tako bo storil on.
15 Jumuiya itakuwa na sheria hizo hizo kwenu na kwa mgeni aishiye miongoni mwenu; hii ni amri ya kudumu kwa vizazi vijavyo. Ninyi na mgeni mtakuwa sawa mbele za Bwana:
Ena odredba naj bo tako za vas iz skupnosti, kakor tudi za tujca, ki začasno biva z vami, odredba na veke za vaše rodove. Kakor ste vi, tako naj bo tujec pred Gospodom.
16 Sheria hizo hizo na masharti hayo hayo hayo, yatawahusu ninyi na mgeni aishiye miongoni mwenu.’”
Ena postava in en način bo za vas in za tujca, ki začasno biva z vami.‹«
17 Bwana akamwambia Mose,
Gospod je spregovoril Mojzesu, rekoč:
18 “Sema na Waisraeli na uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapeleka
»Govori Izraelovim otrokom in jim reci: ›Ko pridete v deželo, kamor vas privedem,
19 nanyi mkala chakula cha nchi hiyo, toeni sehemu ya chakula hicho kama sadaka kwa Bwana.
potem bo, ko jeste od kruha dežele, da boste darovali vzdigovalno daritev Gospodu.
20 Toeni andazi kutoka kwa malimbuko ya chakula chenu kitokacho katika ardhi, na mkitoe kama sadaka kutoka sakafu ya kupuria nafaka.
Kolač svojega prvega testa boste darovali za vzdigovalno daritev. Kakor delate vzdigovalno daritev od mlatišča, tako boste to vzdignili.
21 Kwa vizazi vyote vijavyo hamna budi kutoa sadaka hii kwa Bwana kutoka kwa malimbuko ya unga wenu.
Od svojega prvega testa boste dali Gospodu vzdigovalno daritev v vaših rodovih.
22 “‘Basi kama pasipo kukusudia umeshindwa kushika mojawapo katika amri hizi ambazo Bwana alimpa Mose,
Če pa zaidete in ne obeležujete vseh teh zapovedi, ki jih je Gospod govoril Mojzesu,
23 amri yoyote ya Bwana kwenu kupitia Mose, tangu siku ile Bwana alipowapa na inaendelea hadi vizazi vyote vijavyo;
celó vse, kar vam je po Mojzesovi roki zapovedal Gospod, od dneva, ko je Gospod zapovedal Mojzesu in odslej med vašimi rodovi,
24 ikiwa hili limefanyika pasipo kukusudia bila jumuiya kuwa na habari nalo, basi jumuiya yote itatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya kuteketezwa ikiwa harufu nzuri inayompendeza Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka na ya kinywaji zilizoamriwa kwayo, na mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
potem bo to, če bo storjeno z nevednostjo, brez védenja skupnosti, da bo vsa skupnost darovala enega mladega bikca za žgalno daritev, v prijeten vonj Gospodu, z njegovo jedilno daritvijo in njegovo pitno daritvijo, glede na določen način in enega kozlička od koz za daritev za greh.
25 Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya jumuiya yote ya Kiisraeli, nao watasamehewa, kwa kuwa haikuwa makusudi nao wamemletea Bwana sadaka iliyoteketezwa kwa moto na sadaka ya dhambi kwa ajili ya kosa lao.
Duhovnik bo opravil spravo za vso skupnost Izraelovih otrok in to jim bo odpuščeno, kajti to je nevednost. Prinesli bodo svojo daritev, žrtvovanje, narejeno z ognjem Gospodu in njihovo daritev za greh pred Gospoda, za njihovo nevednost.
26 Jumuiya yote ya Kiisraeli pamoja na wageni waishio miongoni mwao watasamehewa, kwa sababu watu wote walihusika katika kosa lile lisilokusudiwa.
To bo odpuščeno vsem otrokom Izraelove skupnosti in tujcu, ki začasno biva med njimi, glede na to, da je bilo vse ljudstvo v nevednosti.
27 “‘Lakini kama mtu mmoja peke yake akitenda dhambi pasipo kukusudia, ni lazima alete mbuzi mke wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
Če katerakoli duša greši zaradi nevednosti, potem bo privedel kozo prvega leta za daritev za greh.
28 Kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule aliyekosa kwa kufanya dhambi pasipo kukusudia, upatanisho utakapofanywa kwa ajili yake, atasamehewa.
Duhovnik bo opravil spravo za dušo, ki nevedno greši, ko z nevednostjo greši pred Gospodom, da zanjo opravi spravo; in to ji bo odpuščeno.
29 Sheria hiyo moja itamhusu kila mmoja ambaye ametenda dhambi pasipo kukusudia, awe Mwisraeli mzawa ama mgeni.
Imeli boste eno postavo za tistega, ki greši zaradi nevednosti, tako za tistega, ki je rojen med Izraelovimi otroki, kot za tujca, ki začasno biva med njimi.
30 “‘Lakini yeyote ambaye amefanya dhambi kwa dharau awe mzawa au mgeni, anamkufuru Bwana, naye mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
Toda duša, ki ravna prepotentno, ne glede na to, ali je rojena v deželi ali tujec, ta ista graja Gospoda; in ta duša bo iztrebljena izmed svojega ljudstva.
31 Kwa sababu amelidharau neno la Bwana na kuvunja amri zake, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali; hatia yake inabaki juu yake.’”
Ker je prezirala Gospodovo besedo in prelomila njegovo zapoved, bo ta duša popolnoma iztrebljena; njegova krivičnost bo nad njim.‹«
32 Waisraeli walipokuwa jangwani, mtu mmoja alikutwa akikusanya kuni siku ya Sabato.
Medtem ko so bili Izraelovi otroci v divjini, so našli moža, ki je na šabatni dan nabiral veje.
33 Wale waliomkuta akikusanya kuni wakamleta kwa Mose, Aroni na kusanyiko lote,
Tisti, ki so ga našli nabirati veje, so ga privedli k Mojzesu in Aronu in k vsej skupnosti.
34 nao wakamweka kifungoni, kwa sababu haikufahamika kwa wazi kwamba afanyiwe nini.
Dali so ga pod stražo, ker ni bilo oznanjeno kaj naj bi mu bilo storjeno.
35 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Huyo mtu ni lazima afe. Kusanyiko lote lazima limpige mawe nje ya kambi.”
Gospod je rekel Mojzesu: »Mož bo zagotovo usmrčen. Vsa skupnost ga bo zunaj tabora kamnala s kamenjem.«
36 Hivyo kusanyiko likamtoa nje ya kambi na kumpiga mawe hadi akafa, kama Bwana alivyomwamuru Mose.
In vsa skupnost ga je odvedla zunaj tabora in ga kamnala s kamenjem in ta je umrl, kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
37 Bwana akamwambia Mose,
Gospod je spregovoril Mojzesu, rekoč:
38 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Kwa vizazi vyote vijavyo jifanyieni vifundo katika pindo za mavazi yenu vikiwa na uzi wa buluu kwenye kila kifundo.
»Govori Izraelovim otrokom in jim naroči, da si delajo rese na robovih svojih oblek skozi njihove rodove in da na rese robov dajejo moder trak.
39 Mtakuwa mkivitazama vifundo hivyo ili mpate kukumbuka amri zote za Bwana, ili mpate kuzitii msije mkajitia uzinzi wenyewe kwa kuzifuata tamaa za mioyo yenu na za macho yenu.
Ta vam bo za obrobo, da boste lahko pogledali nanjo in se spomnili vseh Gospodovih zapovedi in jih izvrševali, in da ne boste tavali za svojim lastnim srcem in za svojimi lastnimi očmi, za katerimi ste se vlačugali,
40 Ndipo mtakumbuka kuzitii amri zangu zote nanyi mtawekwa wakfu kwa Mungu wenu.
da se boste lahko spomnili in izpolnjevali vse moje zapovedi in boste sveti svojemu Bogu.
41 Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa Misri niwe Mungu wenu. Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu.’”
Jaz sem Gospod, vaš Bog, ki vas je privedel iz egiptovske dežele, da bi bil vaš Bog. Jaz sem Gospod, vaš Bog.«

< Hesabu 15 >