< Hesabu 15 >

1 Bwana akamwambia Mose,
و خداوند موسی را خطاب کرده، گفت:۱
2 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Baada ya ninyi kuingia katika nchi ninayowapa kama nyumbani,
«بنی‌اسرائیل را خطاب کرده، به ایشان بگو: چون به زمین سکونت خود که من آن را به شما می‌دهم داخل شوید،۲
3 nanyi mkitoa sadaka za kuteketezwa kwa moto, kutoka makundi ya ngʼombe au kondoo, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, ikiwa ni sadaka za kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum ama sadaka ya hiari au sadaka ya sikukuu zenu,
و می‌خواهیدهدیه آتشین برای خداوند بگذرانید، چه قربانی سوختنی و چه ذبیحه وفای نذر، یا برای نافله یادر عیدهای خود، برای گذرانیدن هدیه خوشبوبجهت خداوند، خواه از رمه و خواه از گله،۳
4 ndipo yeye aletaye sadaka yake ataiweka mbele za Bwana sadaka ya nafaka, sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta.
آنگاه کسی‌که هدیه خود را می‌گذراند، برای هدیه آردی یک عشر ایفه آرد نرم مخلوط شده بایک ربع هین روغن بجهت خداوند بگذراند.۴
5 Pamoja na kila mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, andaa robo ya hini ya divai kwa sadaka ya kinywaji.
وبرای هدیه ریختنی یک ربع هین شراب با قربانی سوختنی یا برای ذبیحه بجهت هر بره حاضرکن.۵
6 “‘Pamoja na kondoo dume andaa sadaka ya nafaka ya sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na theluthi moja ya hini ya mafuta,
«یا بجهت قوچ برای هدیه آردی دو عشرایفه آرد نرم مخلوط شده با یک ثلث هین روغن حاضرکن.۶
7 na theluthi moja ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Vitoe kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
و بجهت هدیه ریختنی یک ثلث هین شراب برای خوشبویی بجهت خداوندحاضرکن.۷
8 “‘Unapoandaa fahali mchanga kama sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum au sadaka ya amani kwa Bwana,
«و چون گاوی برای قربانی سوختنی یاذبیحه‌ای برای ادای نذر یا برای ذبیحه سلامتی بجهت خداوند حاضر می‌کنی،۸
9 leta pamoja na huyo fahali sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na nusu ya hini ya mafuta.
آنگاه بجهت هدیه آردی، سه عشر آرد نرم مخلوط شده بانصف هین روغن با گاو بگذراند.۹
10 Pia utaleta nusu ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Itakuwa sadaka iliyoteketezwa kwa moto, harufu nzuri inayompendeza Bwana.
و برای هدیه ریختنی نصف هین شراب بگذران تا هدیه آتشین خوشبو برای خداوند بشود.۱۰
11 Kila fahali au kondoo dume, kila mwana-kondoo au mbuzi mchanga, atatayarishwa kwa njia hii.
«همچنین برای هر گاو و برای هر قوچ وبرای هر بره نرینه و هر بزغاله کرده شود.۱۱
12 Fanyeni hivi kwa ajili ya kila mmoja, kwa kadiri ya wingi wa mtakavyoandaa.
برحسب شماره‌ای که حاضر کنید بدین قسم برای هریک، موافق شماره آنها عمل نمایید.۱۲
13 “‘Kila mmoja ambaye ni mzawa ni lazima afanye vitu hivi kwa njia hii hapo aletapo sadaka ya kuteketezwa kwa moto kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
«هر متوطن چون هدیه آتشین خوشبو برای خداوند می‌گذراند، این اوامر را به اینطور بجابیاورد.۱۳
14 Kwa vizazi vijavyo, wakati wowote mgeni au mtu mwingine yeyote anayeishi miongoni mwenu aletapo sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana, ni lazima afanye sawasawa kabisa na jinsi mnavyofanya ninyi.
و اگر غریبی که در میان شما ماواگزیند، هرکه در قرنهای شما در میان شما باشد، می‌خواهد هدیه آتشین خوشبو برای خداوندبگذراند، به نوعی که شما عمل می‌نمایید، او نیزعمل نماید.۱۴
15 Jumuiya itakuwa na sheria hizo hizo kwenu na kwa mgeni aishiye miongoni mwenu; hii ni amri ya kudumu kwa vizazi vijavyo. Ninyi na mgeni mtakuwa sawa mbele za Bwana:
برای شما که اهل جماعت هستیدو برای غریبی که نزد شما ماوا گزیند یک فریضه باشد، فریضه ابدی در نسلهای شما؛ مثل شما به حضور خداوند مثل غریب است.۱۵
16 Sheria hizo hizo na masharti hayo hayo hayo, yatawahusu ninyi na mgeni aishiye miongoni mwenu.’”
یک قانون ویک حکم برای شما و برای غریبی که در میان شما ماوا گزیند، خواهد بود.»۱۶
17 Bwana akamwambia Mose,
و خداوند موسی را خطاب کرده، گفت:۱۷
18 “Sema na Waisraeli na uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapeleka
«بنی‌اسرائیل را خطاب کرده، به ایشان بگو: چون به زمینی که من شما را در آن درمی آورم داخل شوید،۱۸
19 nanyi mkala chakula cha nchi hiyo, toeni sehemu ya chakula hicho kama sadaka kwa Bwana.
و از محصول زمین بخورید، آنگاه هدیه افراشتنی برای خداوند بگذرانید.۱۹
20 Toeni andazi kutoka kwa malimbuko ya chakula chenu kitokacho katika ardhi, na mkitoe kama sadaka kutoka sakafu ya kupuria nafaka.
از خمیر اول خود گرده‌ای بجهت هدیه افراشتنی بگذرانید؛ مثل هدیه افراشتنی خرمن، همچنان آن را بگذرانید.۲۰
21 Kwa vizazi vyote vijavyo hamna budi kutoa sadaka hii kwa Bwana kutoka kwa malimbuko ya unga wenu.
از خمیر اول خود، هدیه افراشتنی در قرنهای خود برای خداوند بگذرانید.۲۱
22 “‘Basi kama pasipo kukusudia umeshindwa kushika mojawapo katika amri hizi ambazo Bwana alimpa Mose,
«و هرگاه سهو خطا کرده، جمیع این اوامررا که خداوند به موسی گفته است، بجا نیاورده باشید،۲۲
23 amri yoyote ya Bwana kwenu kupitia Mose, tangu siku ile Bwana alipowapa na inaendelea hadi vizazi vyote vijavyo;
یعنی هرچه خداوند به واسطه موسی شما را امر فرمود، از روزی که خداوند امر فرمودو از آن به بعد در قرنهای شما.۲۳
24 ikiwa hili limefanyika pasipo kukusudia bila jumuiya kuwa na habari nalo, basi jumuiya yote itatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya kuteketezwa ikiwa harufu nzuri inayompendeza Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka na ya kinywaji zilizoamriwa kwayo, na mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
پس اگر این کارسهو و بدون اطلاع جماعت کرده شد، آنگاه تمامی جماعت یک گاو جوان برای قربانی سوختنی و خوشبویی بجهت خداوند با هدیه آردی و هدیه ریختنی آن، موافق رسم بگذرانند، و یک بز نر بجهت قربانی گناه.۲۴
25 Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya jumuiya yote ya Kiisraeli, nao watasamehewa, kwa kuwa haikuwa makusudi nao wamemletea Bwana sadaka iliyoteketezwa kwa moto na sadaka ya dhambi kwa ajili ya kosa lao.
و کاهن برای تمامی جماعت بنی‌اسرائیل کفاره نماید، و ایشان آمرزیده خواهندشد، زیراکه آن کار سهو شده است، و ایشان قربانی خود را بجهت هدیه آتشین خداوند و قربانی گناه خود را بجهت سهوخویش، به حضور خداوند گذرانیده‌اند.۲۵
26 Jumuiya yote ya Kiisraeli pamoja na wageni waishio miongoni mwao watasamehewa, kwa sababu watu wote walihusika katika kosa lile lisilokusudiwa.
وتمامی جماعت بنی‌اسرائیل و غریبی که در میان ایشان ساکن باشد، آمرزیده خواهند شد، زیراکه به تمامی جماعت سهو شده بود.۲۶
27 “‘Lakini kama mtu mmoja peke yake akitenda dhambi pasipo kukusudia, ni lazima alete mbuzi mke wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
«و اگر یک نفر سهو خطا کرده باشد، آنگاه بز ماده‌یک ساله برای قربانی گناه بگذراند.۲۷
28 Kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule aliyekosa kwa kufanya dhambi pasipo kukusudia, upatanisho utakapofanywa kwa ajili yake, atasamehewa.
وکاهن بجهت آن کسی‌که سهو کرده است چونکه خطای او از نادانستگی بود، به حضور خداوندکفاره کند تا بجهت وی کفاره بشود و آمرزیده خواهد شد.۲۸
29 Sheria hiyo moja itamhusu kila mmoja ambaye ametenda dhambi pasipo kukusudia, awe Mwisraeli mzawa ama mgeni.
بجهت کسی‌که سهو خطا کند، خواه متوطنی از بنی‌اسرائیل و خواه غریبی که در میان ایشان ساکن باشد، یک قانون خواهدبود.۲۹
30 “‘Lakini yeyote ambaye amefanya dhambi kwa dharau awe mzawa au mgeni, anamkufuru Bwana, naye mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
«و اما کسی‌که به‌دست بلند عمل نماید، چه متوطن و چه غریب، او به خداوند کفر کرده باشد، پس آن شخص از میان قوم خود منقطع خواهد شد.۳۰
31 Kwa sababu amelidharau neno la Bwana na kuvunja amri zake, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali; hatia yake inabaki juu yake.’”
چونکه کلام خداوند را حقیرشمرده، حکم او را شکسته است، آن کس البته منقطع شود و گناهش بر وی خواهد بود.»۳۱
32 Waisraeli walipokuwa jangwani, mtu mmoja alikutwa akikusanya kuni siku ya Sabato.
و چون بنی‌اسرائیل در صحرا بودند، کسی را یافتند که در روز سبت هیزم جمع می‌کرد.۳۲
33 Wale waliomkuta akikusanya kuni wakamleta kwa Mose, Aroni na kusanyiko lote,
وکسانی که او را یافتند که هیزم جمع می‌کرد، او رانزد موسی و هارون و تمامی جماعت آوردند.۳۳
34 nao wakamweka kifungoni, kwa sababu haikufahamika kwa wazi kwamba afanyiwe nini.
و او را در حبس نگاه داشتند، زیراکه اعلام نشده بود که با وی چه باید کرد.۳۴
35 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Huyo mtu ni lazima afe. Kusanyiko lote lazima limpige mawe nje ya kambi.”
و خداوند به موسی گفت: «این شخص البته کشته شود، تمامی جماعت او را بیرون از لشکرگاه با سنگها سنگسارکنند.»۳۵
36 Hivyo kusanyiko likamtoa nje ya kambi na kumpiga mawe hadi akafa, kama Bwana alivyomwamuru Mose.
پس تمامی جماعت او را بیرون ازلشکرگاه آورده، او را سنگسار کردند و بمرد، چنانکه خداوند به موسی‌امر کرده بود.۳۶
37 Bwana akamwambia Mose,
و خداوند موسی را خطاب کرده، گفت:۳۷
38 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Kwa vizazi vyote vijavyo jifanyieni vifundo katika pindo za mavazi yenu vikiwa na uzi wa buluu kwenye kila kifundo.
«بنی‌اسرائیل را خطاب کرده، به ایشان بگو که: برای خود بر گوشه های رخت خویش در قرنهای خود صیصیت بسازند و رشته لاجوردی بر هرگوشه صیصیت بگذارند.۳۸
39 Mtakuwa mkivitazama vifundo hivyo ili mpate kukumbuka amri zote za Bwana, ili mpate kuzitii msije mkajitia uzinzi wenyewe kwa kuzifuata tamaa za mioyo yenu na za macho yenu.
و بجهت شماصیصیت خواهد بود تا برآن بنگرید و تمام اوامرخداوند را بیاد آورده، بجا آورید، و در‌پی دلها وچشمان خود که شما در‌پی آنها زنا می‌کنید، منحرف نشوید.۳۹
40 Ndipo mtakumbuka kuzitii amri zangu zote nanyi mtawekwa wakfu kwa Mungu wenu.
تا تمامی اوامر مرا بیاد آورده، بجا آورید، و بجهت خدای خود مقدس باشید.۴۰
41 Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa Misri niwe Mungu wenu. Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu.’”
من یهوه خدای شما هستم که شما را از زمین مصر بیرون آوردم تا خدای شما باشم. من یهوه خدای شما هستم.»۴۱

< Hesabu 15 >