< Hesabu 15 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Ja Herra puhui Moosekselle sanoen:
2 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Baada ya ninyi kuingia katika nchi ninayowapa kama nyumbani,
"Puhu israelilaisille ja sano heille: Kun te tulette siihen maahan, jonka minä annan teille asuinsijaksi,
3 nanyi mkitoa sadaka za kuteketezwa kwa moto, kutoka makundi ya ngʼombe au kondoo, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, ikiwa ni sadaka za kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum ama sadaka ya hiari au sadaka ya sikukuu zenu,
ja uhraatte Herralle uhrin, poltto-tai teurasuhrin, joko lupausta täyttääksenne tai vapaaehtoisena lahjana tai juhlissanne, valmistaaksenne Herralle suloisen tuoksun raavaista tai lampaista,
4 ndipo yeye aletaye sadaka yake ataiweka mbele za Bwana sadaka ya nafaka, sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta.
niin se, joka tuo uhrin, tuokoon lahjanansa Herralle ruokauhriksi kymmenenneksen lestyjä jauhoja, sekoitettuna neljännekseen hiin-mittaa öljyä;
5 Pamoja na kila mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, andaa robo ya hini ya divai kwa sadaka ya kinywaji.
ja juomauhriksi, polttouhrin tai teurasuhrin lisäksi, uhraa neljännes hiin-mittaa viiniä kutakin karitsaa kohti.
6 “‘Pamoja na kondoo dume andaa sadaka ya nafaka ya sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na theluthi moja ya hini ya mafuta,
Mutta oinaan lisäksi uhraa ruokauhrina kaksi kymmenennestä lestyjä jauhoja, sekoitettuna kolmannekseen hiin-mittaa öljyä,
7 na theluthi moja ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Vitoe kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
ja juomauhriksi tuo kolmannes hiin-mittaa viiniä suloiseksi tuoksuksi Herralle.
8 “‘Unapoandaa fahali mchanga kama sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum au sadaka ya amani kwa Bwana,
Mutta kun uhraat mullikan poltto-tai teurasuhriksi, joko lupausta täyttääksesi tai yhteysuhriksi Herralle,
9 leta pamoja na huyo fahali sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na nusu ya hini ya mafuta.
niin tuotakoon mullikan lisäksi ruokauhrina kolme kymmenennestä lestyjä jauhoja, sekoitettuna puoleen hiin-mittaa öljyä,
10 Pia utaleta nusu ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Itakuwa sadaka iliyoteketezwa kwa moto, harufu nzuri inayompendeza Bwana.
ja juomauhriksi tuo puoli hiin-mittaa viiniä suloisesti tuoksuvaksi uhriksi Herralle.
11 Kila fahali au kondoo dume, kila mwana-kondoo au mbuzi mchanga, atatayarishwa kwa njia hii.
Näin tehtäköön kutakin härkää tai oinasta tai karitsaa tai vohlaa uhrattaessa.
12 Fanyeni hivi kwa ajili ya kila mmoja, kwa kadiri ya wingi wa mtakavyoandaa.
Niin monta kuin uhrieläimiä on, niin tehkää näin kullekin, niin monta kuin niitä on.
13 “‘Kila mmoja ambaye ni mzawa ni lazima afanye vitu hivi kwa njia hii hapo aletapo sadaka ya kuteketezwa kwa moto kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
Jokainen maassa syntynyt tehköön näin, tuodessaan suloisesti tuoksuvan uhrin Herralle.
14 Kwa vizazi vijavyo, wakati wowote mgeni au mtu mwingine yeyote anayeishi miongoni mwenu aletapo sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana, ni lazima afanye sawasawa kabisa na jinsi mnavyofanya ninyi.
Ja jos muukalainen, joka asuu teidän luonanne tai on ainiaaksi asettunut teidän keskuuteenne, tahtoo uhrata suloisesti tuoksuvan uhrin Herralle, niin hän tehköön, niinkuin tekin teette.
15 Jumuiya itakuwa na sheria hizo hizo kwenu na kwa mgeni aishiye miongoni mwenu; hii ni amri ya kudumu kwa vizazi vijavyo. Ninyi na mgeni mtakuwa sawa mbele za Bwana:
Seurakunnassa olkoon laki sama teillä kuin muukalaisellakin, joka asuu teidän luonanne. Tämä olkoon teille ikuinen säädös sukupolvesta sukupolveen. Se, mikä koskee teitä, koskekoon myös muukalaista Herran edessä.
16 Sheria hizo hizo na masharti hayo hayo hayo, yatawahusu ninyi na mgeni aishiye miongoni mwenu.’”
Sama laki ja sama oikeus olkoon sekä teillä että muukalaisella, joka asuu teidän luonanne."
17 Bwana akamwambia Mose,
Ja Herra puhui Moosekselle sanoen:
18 “Sema na Waisraeli na uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapeleka
"Puhu israelilaisille ja sano heille: Kun tulette siihen maahan, johon minä teidät vien,
19 nanyi mkala chakula cha nchi hiyo, toeni sehemu ya chakula hicho kama sadaka kwa Bwana.
niin syödessänne sen maan leipää antakaa Herralle anti.
20 Toeni andazi kutoka kwa malimbuko ya chakula chenu kitokacho katika ardhi, na mkitoe kama sadaka kutoka sakafu ya kupuria nafaka.
Ensimmäisistä jyvärouheistanne antakaa kakku anniksi; antakaa se, niinkuin puimatantereelta annatte annin.
21 Kwa vizazi vyote vijavyo hamna budi kutoa sadaka hii kwa Bwana kutoka kwa malimbuko ya unga wenu.
Ensimmäisistä jyvärouheistanne antakaa Herralle anti sukupolvesta sukupolveen.
22 “‘Basi kama pasipo kukusudia umeshindwa kushika mojawapo katika amri hizi ambazo Bwana alimpa Mose,
Mutta jos erehdyksestä jätätte täyttämättä jonkun näistä käskyistä, jotka Herra on Moosekselle puhunut,
23 amri yoyote ya Bwana kwenu kupitia Mose, tangu siku ile Bwana alipowapa na inaendelea hadi vizazi vyote vijavyo;
mitä hyvänsä, mistä Herra Mooseksen kautta on teille käskyn antanut, siitä päivästä lähtien, jolloin Herra antoi käskynsä, ja edelleen sukupolvesta sukupolveen,
24 ikiwa hili limefanyika pasipo kukusudia bila jumuiya kuwa na habari nalo, basi jumuiya yote itatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya kuteketezwa ikiwa harufu nzuri inayompendeza Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka na ya kinywaji zilizoamriwa kwayo, na mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
niin, jos rikkomus tapahtui seurakunnan tietämättä, erehdyksestä, uhratkoon koko seurakunta mullikan polttouhriksi, suloiseksi tuoksuksi Herralle, ynnä siihen kuuluvan ruoka-ja juomauhrin, niinkuin säädetty on, sekä kauriin syntiuhriksi.
25 Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya jumuiya yote ya Kiisraeli, nao watasamehewa, kwa kuwa haikuwa makusudi nao wamemletea Bwana sadaka iliyoteketezwa kwa moto na sadaka ya dhambi kwa ajili ya kosa lao.
Kun pappi sitten on toimittanut sovituksen kaikelle israelilaisten seurakunnalle, niin rikkomus annetaan heille anteeksi; sillä se on ollut erehdys ja he ovat tuoneet lahjansa uhriksi Herralle sekä syntiuhrinsa Herran eteen erehdyksensä vuoksi.
26 Jumuiya yote ya Kiisraeli pamoja na wageni waishio miongoni mwao watasamehewa, kwa sababu watu wote walihusika katika kosa lile lisilokusudiwa.
Se annetaan silloin anteeksi kaikelle israelilaisten seurakunnalle samoinkuin muukalaiselle, joka asuu heidän keskellänsä; sillä koko kansa on vastuunalainen erehdyksestä.
27 “‘Lakini kama mtu mmoja peke yake akitenda dhambi pasipo kukusudia, ni lazima alete mbuzi mke wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
Mutta jos joku yksityinen rikkoo erehdyksestä, tuokoon vuoden vanhan vuohen syntiuhriksi.
28 Kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule aliyekosa kwa kufanya dhambi pasipo kukusudia, upatanisho utakapofanywa kwa ajili yake, atasamehewa.
Kun pappi on toimittanut sovituksen sille, joka on erehdyksestä, tahtomattaan, rikkonut Herraa vastaan, kun hän on toimittanut hänelle sovituksen, niin hänelle annetaan anteeksi.
29 Sheria hiyo moja itamhusu kila mmoja ambaye ametenda dhambi pasipo kukusudia, awe Mwisraeli mzawa ama mgeni.
Sama laki olkoon sekä maassa syntyneillä israelilaisilla että muukalaisella, joka asuu heidän keskellänsä, kun joku rikkoo erehdyksestä.
30 “‘Lakini yeyote ambaye amefanya dhambi kwa dharau awe mzawa au mgeni, anamkufuru Bwana, naye mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
Mutta se, joka tahallisesti tekee syntiä, olipa hän maassa syntynyt tai muukalainen, pilkkaa Herraa, ja hänet hävitettäköön kansastansa.
31 Kwa sababu amelidharau neno la Bwana na kuvunja amri zake, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali; hatia yake inabaki juu yake.’”
Sillä hän on pitänyt halpana Herran sanan ja rikkonut hänen käskynsä; hänet tuhottakoon, syntivelka painaa häntä."
32 Waisraeli walipokuwa jangwani, mtu mmoja alikutwa akikusanya kuni siku ya Sabato.
Israelilaisten oleskellessa erämaassa tavattiin mies kokoamassa puita sapatinpäivänä.
33 Wale waliomkuta akikusanya kuni wakamleta kwa Mose, Aroni na kusanyiko lote,
Niin ne, jotka hänet tapasivat puita kokoamasta, toivat hänet Mooseksen ja Aaronin ja koko seurakunnan eteen.
34 nao wakamweka kifungoni, kwa sababu haikufahamika kwa wazi kwamba afanyiwe nini.
Ja he panivat hänet vankeuteen, koska ei ollut vielä määrätty, mitä hänelle oli tehtävä.
35 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Huyo mtu ni lazima afe. Kusanyiko lote lazima limpige mawe nje ya kambi.”
Mutta Herra sanoi Moosekselle: "Se mies rangaistakoon kuolemalla, koko seurakunta kivittäköön hänet leirin ulkopuolella".
36 Hivyo kusanyiko likamtoa nje ya kambi na kumpiga mawe hadi akafa, kama Bwana alivyomwamuru Mose.
Silloin koko seurakunta vei hänet leirin ulkopuolelle, ja he kivittivät hänet kuoliaaksi, niinkuin Herra oli Moosekselle käskyn antanut.
37 Bwana akamwambia Mose,
Ja Herra puhui Moosekselle sanoen:
38 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Kwa vizazi vyote vijavyo jifanyieni vifundo katika pindo za mavazi yenu vikiwa na uzi wa buluu kwenye kila kifundo.
"Puhu israelilaisille ja sano heille, että heidän on sukupolvesta sukupolveen tehtävä itsellensä tupsut viittojensa kulmiin ja sidottava kulmien tupsuihin punasininen lanka.
39 Mtakuwa mkivitazama vifundo hivyo ili mpate kukumbuka amri zote za Bwana, ili mpate kuzitii msije mkajitia uzinzi wenyewe kwa kuzifuata tamaa za mioyo yenu na za macho yenu.
Ne tupsut olkoon teillä, että te, kun ne näette, muistaisitte kaikki Herran käskyt ja ne täyttäisitte ettekä seuraisi sydämenne ettekä silmienne himoja, jotka houkuttelevat teitä haureuteen;
40 Ndipo mtakumbuka kuzitii amri zangu zote nanyi mtawekwa wakfu kwa Mungu wenu.
niin muistakaa ja täyttäkää kaikki minun käskyni ja olkaa pyhät Jumalallenne.
41 Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa Misri niwe Mungu wenu. Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu.’”
Minä olen Herra, teidän Jumalanne, joka vein teidät pois Egyptin maasta ollakseni teidän Jumalanne. Minä olen Herra, teidän Jumalanne."

< Hesabu 15 >