< Hesabu 15 >

1 Bwana akamwambia Mose,
And Jehovah speaketh unto Moses, saying,
2 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Baada ya ninyi kuingia katika nchi ninayowapa kama nyumbani,
'Speak unto the sons of Israel, and thou hast said unto them, When ye come in unto the land of your dwellings, which I am giving to you,
3 nanyi mkitoa sadaka za kuteketezwa kwa moto, kutoka makundi ya ngʼombe au kondoo, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, ikiwa ni sadaka za kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum ama sadaka ya hiari au sadaka ya sikukuu zenu,
then ye have prepared a fire-offering to Jehovah, a burnt-offering, or a sacrifice, at separating a vow or free-will-offering, or in your appointed things, to make a sweet fragrance to Jehovah, out of the herd, or out of the flock.
4 ndipo yeye aletaye sadaka yake ataiweka mbele za Bwana sadaka ya nafaka, sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta.
'And he who is bringing near his offering to Jehovah hath brought near a present of flour, a tenth deal, mixed with a fourth of the hin of oil;
5 Pamoja na kila mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, andaa robo ya hini ya divai kwa sadaka ya kinywaji.
and wine for a libation, a fourth of the hin thou dost prepare for the burnt-offering or for a sacrifice, for the one lamb;
6 “‘Pamoja na kondoo dume andaa sadaka ya nafaka ya sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na theluthi moja ya hini ya mafuta,
or for a ram thou dost prepare a present of flour, two-tenth deals, mixed with oil, a third of the hin;
7 na theluthi moja ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Vitoe kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
and wine for a libation, a third part of the hin, thou dost bring near — a sweet fragrance to Jehovah.
8 “‘Unapoandaa fahali mchanga kama sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum au sadaka ya amani kwa Bwana,
'And when thou makest a son of the herd a burnt-offering or a sacrifice, at separating a vow or peace-offerings to Jehovah,
9 leta pamoja na huyo fahali sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na nusu ya hini ya mafuta.
then he hath brought near for the son of the herd a present of flour, three-tenth deals, mixed with oil, a half of the hin;
10 Pia utaleta nusu ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Itakuwa sadaka iliyoteketezwa kwa moto, harufu nzuri inayompendeza Bwana.
and wine thou bringest near for a libation, a half of the hin — a fire-offering of sweet fragrance to Jehovah;
11 Kila fahali au kondoo dume, kila mwana-kondoo au mbuzi mchanga, atatayarishwa kwa njia hii.
thus it is done for the one ox, or for the one ram, or for a lamb of the sheep or of the goats.
12 Fanyeni hivi kwa ajili ya kila mmoja, kwa kadiri ya wingi wa mtakavyoandaa.
'According to the number that ye prepare, so ye do to each, according to their number;
13 “‘Kila mmoja ambaye ni mzawa ni lazima afanye vitu hivi kwa njia hii hapo aletapo sadaka ya kuteketezwa kwa moto kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
every native doth thus with these, at bringing near a fire-offering of sweet fragrance to Jehovah;
14 Kwa vizazi vijavyo, wakati wowote mgeni au mtu mwingine yeyote anayeishi miongoni mwenu aletapo sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana, ni lazima afanye sawasawa kabisa na jinsi mnavyofanya ninyi.
and when a sojourner sojourneth with you, or whoso [is] in your midst to your generations, and he hath made a fire-offering of sweet fragrance to Jehovah, as ye do so he doth.
15 Jumuiya itakuwa na sheria hizo hizo kwenu na kwa mgeni aishiye miongoni mwenu; hii ni amri ya kudumu kwa vizazi vijavyo. Ninyi na mgeni mtakuwa sawa mbele za Bwana:
'One statute is for you of the congregation and for the sojourner who is sojourning, a statute age-during to your generations: as ye [are] so is the sojourner before Jehovah;
16 Sheria hizo hizo na masharti hayo hayo hayo, yatawahusu ninyi na mgeni aishiye miongoni mwenu.’”
one law and one ordinance is to you and to the sojourner who is sojourning with you.'
17 Bwana akamwambia Mose,
And Jehovah speaketh unto Moses, saying,
18 “Sema na Waisraeli na uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapeleka
'Speak unto the sons of Israel, and thou hast said unto them, In your coming in unto the land whither I am bringing you in,
19 nanyi mkala chakula cha nchi hiyo, toeni sehemu ya chakula hicho kama sadaka kwa Bwana.
then it hath been, in your eating of the bread of the land, ye heave up a heave-offering to Jehovah;
20 Toeni andazi kutoka kwa malimbuko ya chakula chenu kitokacho katika ardhi, na mkitoe kama sadaka kutoka sakafu ya kupuria nafaka.
the beginning of your dough a cake ye heave up — a heave-offering; as the heave-offering of a threshing-floor, so ye do heave it.
21 Kwa vizazi vyote vijavyo hamna budi kutoa sadaka hii kwa Bwana kutoka kwa malimbuko ya unga wenu.
Of the beginning of your dough ye do give to Jehovah a heave-offering — to your generations.
22 “‘Basi kama pasipo kukusudia umeshindwa kushika mojawapo katika amri hizi ambazo Bwana alimpa Mose,
'And when ye err, and do not all these commands which Jehovah hath spoken unto Moses,
23 amri yoyote ya Bwana kwenu kupitia Mose, tangu siku ile Bwana alipowapa na inaendelea hadi vizazi vyote vijavyo;
the whole that Jehovah hath charged upon you by the hand of Moses, from the day that Jehovah hath commanded, and henceforth, to your generations,
24 ikiwa hili limefanyika pasipo kukusudia bila jumuiya kuwa na habari nalo, basi jumuiya yote itatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya kuteketezwa ikiwa harufu nzuri inayompendeza Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka na ya kinywaji zilizoamriwa kwayo, na mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
then it hath been, if from the eyes of the company it hath been done in ignorance, that all the company have prepared one bullock, a son of the herd, for a burnt-offering, for sweet fragrance to Jehovah, and its present, and its libation, according to the ordinance, and one kid of the goats for a sin-offering.
25 Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya jumuiya yote ya Kiisraeli, nao watasamehewa, kwa kuwa haikuwa makusudi nao wamemletea Bwana sadaka iliyoteketezwa kwa moto na sadaka ya dhambi kwa ajili ya kosa lao.
'And the priest hath made atonement for all the company of the sons of Israel, and it hath been forgiven them, for it [is] ignorance, and they — they have brought in their offering, a fire-offering to Jehovah, even their sin-offering before Jehovah for their ignorance;
26 Jumuiya yote ya Kiisraeli pamoja na wageni waishio miongoni mwao watasamehewa, kwa sababu watu wote walihusika katika kosa lile lisilokusudiwa.
and it hath been forgiven to all the company of the sons of Israel, and to the sojourner who is sojourning in their midst; for to all the company [it is done] in ignorance.
27 “‘Lakini kama mtu mmoja peke yake akitenda dhambi pasipo kukusudia, ni lazima alete mbuzi mke wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
'And if one person sin in ignorance, then he hath brought near a she-goat, daughter of a year, for a sin-offering;
28 Kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule aliyekosa kwa kufanya dhambi pasipo kukusudia, upatanisho utakapofanywa kwa ajili yake, atasamehewa.
and the priest hath made atonement for the person who is erring, in his sinning in ignorance before Jehovah, by making atonement for him, and it hath been forgiven him;
29 Sheria hiyo moja itamhusu kila mmoja ambaye ametenda dhambi pasipo kukusudia, awe Mwisraeli mzawa ama mgeni.
for the native among the sons of Israel, and for the sojourner who is sojourning in their midst — one law is to you, for him who is doing [anything] through ignorance.
30 “‘Lakini yeyote ambaye amefanya dhambi kwa dharau awe mzawa au mgeni, anamkufuru Bwana, naye mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
'And the person who doth [aught] with a high hand — of the native or of the sojourner — Jehovah he is reviling, and that person hath been cut off from the midst of his people;
31 Kwa sababu amelidharau neno la Bwana na kuvunja amri zake, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali; hatia yake inabaki juu yake.’”
because the word of Jehovah he despised, and His command hath broken — that person is certainly cut off; his iniquity [is] on him.'
32 Waisraeli walipokuwa jangwani, mtu mmoja alikutwa akikusanya kuni siku ya Sabato.
And the sons of Israel are in the wilderness, and they find a man gathering wood on the sabbath-day,
33 Wale waliomkuta akikusanya kuni wakamleta kwa Mose, Aroni na kusanyiko lote,
and those finding him gathering wood bring him near unto Moses, and unto Aaron, and unto all the company,
34 nao wakamweka kifungoni, kwa sababu haikufahamika kwa wazi kwamba afanyiwe nini.
and they place him in ward, for it [is] not explained what is [to be] done to him.
35 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Huyo mtu ni lazima afe. Kusanyiko lote lazima limpige mawe nje ya kambi.”
And Jehovah saith unto Moses, 'The man is certainly put to death, all the company stoning him with stones, at the outside of the camp.'
36 Hivyo kusanyiko likamtoa nje ya kambi na kumpiga mawe hadi akafa, kama Bwana alivyomwamuru Mose.
And all the company bring him out unto the outside of the camp, and stone him with stones, and he dieth, as Jehovah hath commanded Moses.
37 Bwana akamwambia Mose,
And Jehovah speaketh unto Moses, saying,
38 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Kwa vizazi vyote vijavyo jifanyieni vifundo katika pindo za mavazi yenu vikiwa na uzi wa buluu kwenye kila kifundo.
'Speak unto the sons of Israel, and thou hast said unto them, and they have made for themselves fringes on the skirts of their garments, to their generations, and they have put on the fringe of the skirt a ribbon of blue,
39 Mtakuwa mkivitazama vifundo hivyo ili mpate kukumbuka amri zote za Bwana, ili mpate kuzitii msije mkajitia uzinzi wenyewe kwa kuzifuata tamaa za mioyo yenu na za macho yenu.
and it hath been to you for a fringe, and ye have seen it, and have remembered all the commands of Jehovah, and have done them, and ye search not after your heart, and after your eyes, after which ye are going a-whoring;
40 Ndipo mtakumbuka kuzitii amri zangu zote nanyi mtawekwa wakfu kwa Mungu wenu.
so that ye remember and have done all My commands, and ye have been holy to your God;
41 Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa Misri niwe Mungu wenu. Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu.’”
I [am] Jehovah your God, who hath brought you out from the land of Egypt to become your God; I, Jehovah, [am] your God.'

< Hesabu 15 >