< Hesabu 15 >

1 Bwana akamwambia Mose,
And the Lord spak to Moises, and seide, Speke thou to the sones of Israel,
2 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Baada ya ninyi kuingia katika nchi ninayowapa kama nyumbani,
and thou schalt seie to hem, Whanne ye han entrid in to the lond of youre abitacioun which Y schal yyue to you,
3 nanyi mkitoa sadaka za kuteketezwa kwa moto, kutoka makundi ya ngʼombe au kondoo, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, ikiwa ni sadaka za kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum ama sadaka ya hiari au sadaka ya sikukuu zenu,
and ye make an offryng to the Lord in to brent sacrifice, ether a pesible sacrifice, and ye payen auowis, ethir offren yiftis bi fre wille, ethir in youre solempnytees ye brennen odour of swetnesse to the Lord, of oxun, ether of scheep;
4 ndipo yeye aletaye sadaka yake ataiweka mbele za Bwana sadaka ya nafaka, sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta.
who euer offrith the slayn sacrifice, schal offre a sacrifice of flour, the tenthe part of ephi, spreynt togidere with oile, which oil schal haue a mesure the fourthe part of hyn;
5 Pamoja na kila mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, andaa robo ya hini ya divai kwa sadaka ya kinywaji.
and he schal yyue wyn to fletynge sacrifices to be sched, of the same mesure, in to brent sacrifice, and slayn sacrifice.
6 “‘Pamoja na kondoo dume andaa sadaka ya nafaka ya sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na theluthi moja ya hini ya mafuta,
Bi ech loomb and ram schal be the sacrifice of flour, of twey tenthe partis, which schal be spreynt togidere with oile, of the thridde part of hyn;
7 na theluthi moja ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Vitoe kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
and he schal offre wyn to the fletynge sacrifice, of the thridde part of the same mesure, in to odour of swetnesse to the Lord.
8 “‘Unapoandaa fahali mchanga kama sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum au sadaka ya amani kwa Bwana,
Forsothe whanne thou makist a brent sacrifice, ethir an offryng of oxun, that thou fille avow, ethir pesible sacrifice, thou schalt yyue,
9 leta pamoja na huyo fahali sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na nusu ya hini ya mafuta.
bi ech oxe, thre tenthe partis of flour, spreynt togidere with oile, which schal haue the half of mesure of hyn;
10 Pia utaleta nusu ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Itakuwa sadaka iliyoteketezwa kwa moto, harufu nzuri inayompendeza Bwana.
and thou schalt yyue wyn to fletynge sacrifices to be sched, of the same mesure, in to offryng of the swettest odour to the Lord.
11 Kila fahali au kondoo dume, kila mwana-kondoo au mbuzi mchanga, atatayarishwa kwa njia hii.
So ye schulen do bi ech oxe, and ram,
12 Fanyeni hivi kwa ajili ya kila mmoja, kwa kadiri ya wingi wa mtakavyoandaa.
and lomb, and kide;
13 “‘Kila mmoja ambaye ni mzawa ni lazima afanye vitu hivi kwa njia hii hapo aletapo sadaka ya kuteketezwa kwa moto kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
as wel men borun in the lond,
14 Kwa vizazi vijavyo, wakati wowote mgeni au mtu mwingine yeyote anayeishi miongoni mwenu aletapo sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana, ni lazima afanye sawasawa kabisa na jinsi mnavyofanya ninyi.
as pilgrymys, schulen offre sacrifices bi the same custom;
15 Jumuiya itakuwa na sheria hizo hizo kwenu na kwa mgeni aishiye miongoni mwenu; hii ni amri ya kudumu kwa vizazi vijavyo. Ninyi na mgeni mtakuwa sawa mbele za Bwana:
o comaundement and doom schal be, as wel to you as to comelyngis of the lond.
16 Sheria hizo hizo na masharti hayo hayo hayo, yatawahusu ninyi na mgeni aishiye miongoni mwenu.’”
And the Lord spak to Moises,
17 Bwana akamwambia Mose,
and seide, Speke thou to the sones of Israel, and thou schalt seie to hem,
18 “Sema na Waisraeli na uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapeleka
Whanne ye comen in to the lond which Y schal yyue to you,
19 nanyi mkala chakula cha nchi hiyo, toeni sehemu ya chakula hicho kama sadaka kwa Bwana.
and `ye eten of the looues of that cuntrey, ye
20 Toeni andazi kutoka kwa malimbuko ya chakula chenu kitokacho katika ardhi, na mkitoe kama sadaka kutoka sakafu ya kupuria nafaka.
schulen departe the firste fruytis of youre metis to the Lord; as ye schulen departe the firste fruytis of corn flooris,
21 Kwa vizazi vyote vijavyo hamna budi kutoa sadaka hii kwa Bwana kutoka kwa malimbuko ya unga wenu.
so ye schulen yyue the firste fruytis also of sewis to the Lord.
22 “‘Basi kama pasipo kukusudia umeshindwa kushika mojawapo katika amri hizi ambazo Bwana alimpa Mose,
That if bi ignoraunce ye passen ony of tho thingis whiche the Lord spak to Moyses,
23 amri yoyote ya Bwana kwenu kupitia Mose, tangu siku ile Bwana alipowapa na inaendelea hadi vizazi vyote vijavyo;
and comaundide bi hym to you, fro the dai in which he bigan to comaunde,
24 ikiwa hili limefanyika pasipo kukusudia bila jumuiya kuwa na habari nalo, basi jumuiya yote itatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya kuteketezwa ikiwa harufu nzuri inayompendeza Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka na ya kinywaji zilizoamriwa kwayo, na mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
and ouer, and the multitude hath foryete to do, it schal offre a calf of the drooue, brent sacrifice in to swettist odour to the Lord, and the sacrificis therof, and fletynge offryngis, as the cerymonyes therof axen; and it schal offre a `buc of geet for synne.
25 Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya jumuiya yote ya Kiisraeli, nao watasamehewa, kwa kuwa haikuwa makusudi nao wamemletea Bwana sadaka iliyoteketezwa kwa moto na sadaka ya dhambi kwa ajili ya kosa lao.
And the preest schal preie for al the multitude of the sones of Israel, and it schal be foryouun to hem, for thei synneden not wilfuli. And neuerthelesse thei schulen offre encense to the Lord for hemsilf, and for her synne and errour;
26 Jumuiya yote ya Kiisraeli pamoja na wageni waishio miongoni mwao watasamehewa, kwa sababu watu wote walihusika katika kosa lile lisilokusudiwa.
and it schal be foryouun to al the puple of the sones of Israel, and to comelyngis that ben pilgryms among hem, for it is the synne of al the multitude bi ignoraunce.
27 “‘Lakini kama mtu mmoja peke yake akitenda dhambi pasipo kukusudia, ni lazima alete mbuzi mke wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
That if a soule synneth vnwityngli, it schal offre a geet of o yeer for his synne; and the preest schal preye for that soule, for it synnede vnwityngli bifor the Lord;
28 Kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule aliyekosa kwa kufanya dhambi pasipo kukusudia, upatanisho utakapofanywa kwa ajili yake, atasamehewa.
and the preest schal gete foryyuenesse to it, and synne schal be foryouun to it.
29 Sheria hiyo moja itamhusu kila mmoja ambaye ametenda dhambi pasipo kukusudia, awe Mwisraeli mzawa ama mgeni.
As wel to men borun in the lond as to comelyngis, o lawe schal be of alle that synnen vnwityngli.
30 “‘Lakini yeyote ambaye amefanya dhambi kwa dharau awe mzawa au mgeni, anamkufuru Bwana, naye mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
Forsothe a man that doith ony synne bi pride, schal perische fro his puple, whether he be a citeseyn, ethir a pilgrym, for he was rebel ayens the Lord;
31 Kwa sababu amelidharau neno la Bwana na kuvunja amri zake, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali; hatia yake inabaki juu yake.’”
for he dispiside the word of the Lord, and made voide his comaundement; therfor he schal be doon awei, and schal bere his owne wickidnes.
32 Waisraeli walipokuwa jangwani, mtu mmoja alikutwa akikusanya kuni siku ya Sabato.
Forsothe it was doon, whanne the sones of Israel weren in wildirnesse, and hadde founde a man gaderynge woode in the `day of sabat,
33 Wale waliomkuta akikusanya kuni wakamleta kwa Mose, Aroni na kusanyiko lote,
thei brouyten hym to Moises, and to Aaron, and to al the multitude; whiche closiden hym in to prisoun,
34 nao wakamweka kifungoni, kwa sababu haikufahamika kwa wazi kwamba afanyiwe nini.
and wisten not what thei schulden do of hym.
35 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Huyo mtu ni lazima afe. Kusanyiko lote lazima limpige mawe nje ya kambi.”
And the Lord seide to Moises, This man die bi deeth; al the cumpeny oppresse hym with stoonus with out the tentis.
36 Hivyo kusanyiko likamtoa nje ya kambi na kumpiga mawe hadi akafa, kama Bwana alivyomwamuru Mose.
And whanne thei hadden led hym with out forth, thei oppressiden him with stoonus, and he was deed, as the Lord comaundide.
37 Bwana akamwambia Mose,
Also the Lord seide to Moises,
38 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Kwa vizazi vyote vijavyo jifanyieni vifundo katika pindo za mavazi yenu vikiwa na uzi wa buluu kwenye kila kifundo.
Speke thou to the sones of Israel, and thou schalt seye to hem, that thei make to hem hemmes bi foure corneris of mentils, and sette laces of iacynct `in tho;
39 Mtakuwa mkivitazama vifundo hivyo ili mpate kukumbuka amri zote za Bwana, ili mpate kuzitii msije mkajitia uzinzi wenyewe kwa kuzifuata tamaa za mioyo yenu na za macho yenu.
and whanne thei seen thoo, haue thei mynde of alle comaundementis of the Lord, lest thei suen her thouytis and iyen, doynge fornycacioun bi dyuerse thingis;
40 Ndipo mtakumbuka kuzitii amri zangu zote nanyi mtawekwa wakfu kwa Mungu wenu.
but more be thei myndeful of the `Lordis heestis, and do thei tho, and be thei hooli to her God.
41 Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa Misri niwe Mungu wenu. Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu.’”
Y am youre Lord God, which ledde you out of the lond of Egipt, that Y schulde be youre God.

< Hesabu 15 >