< Hesabu 15 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Then Yahweh spoke to Moses. He said,
2 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Baada ya ninyi kuingia katika nchi ninayowapa kama nyumbani,
“Speak to the people of Israel and say to them, 'When you go into the land where you will live, which Yahweh will give to you,
3 nanyi mkitoa sadaka za kuteketezwa kwa moto, kutoka makundi ya ngʼombe au kondoo, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, ikiwa ni sadaka za kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum ama sadaka ya hiari au sadaka ya sikukuu zenu,
you are to prepare an offering by fire to Yahweh, either a burnt offering or a sacrifice to fulfill a vow or a freewill offering, or an offering at your feasts, to produce a pleasing aroma for Yahweh from the herd or the flock.
4 ndipo yeye aletaye sadaka yake ataiweka mbele za Bwana sadaka ya nafaka, sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta.
You must offer to Yahweh a burnt offering as well as a grain offering of a tenth of an ephah of fine flour mixed with one-fourth of a hin of oil.
5 Pamoja na kila mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, andaa robo ya hini ya divai kwa sadaka ya kinywaji.
You must also offer with the burnt offering, or for the sacrifice, one-fourth of a hin of wine for the drink offering for each lamb.
6 “‘Pamoja na kondoo dume andaa sadaka ya nafaka ya sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na theluthi moja ya hini ya mafuta,
If you are offering a ram, you must prepare as a grain offering two-tenths of an ephah of fine flour mixed with a third of a hin of oil.
7 na theluthi moja ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Vitoe kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
For the drink offering, you must offer a third of a hin of wine. It will produce a sweet aroma for Yahweh.
8 “‘Unapoandaa fahali mchanga kama sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum au sadaka ya amani kwa Bwana,
When you prepare a bull as a burnt offering or as a sacrifice to fulfill a vow, or as a fellowship offering to Yahweh,
9 leta pamoja na huyo fahali sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na nusu ya hini ya mafuta.
then you must offer with the bull a grain offering of three-tenths of an ephah of fine flour mixed with half a hin of oil.
10 Pia utaleta nusu ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Itakuwa sadaka iliyoteketezwa kwa moto, harufu nzuri inayompendeza Bwana.
You must offer as the drink offering half a hin of wine, as an offering made by fire, to produce a sweet aroma for Yahweh.
11 Kila fahali au kondoo dume, kila mwana-kondoo au mbuzi mchanga, atatayarishwa kwa njia hii.
It must be done this way for each bull, for each ram, and for each of the male lambs or young goats.
12 Fanyeni hivi kwa ajili ya kila mmoja, kwa kadiri ya wingi wa mtakavyoandaa.
Every sacrifice that you prepare and offer must be done as described here.
13 “‘Kila mmoja ambaye ni mzawa ni lazima afanye vitu hivi kwa njia hii hapo aletapo sadaka ya kuteketezwa kwa moto kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
All who are native-born Israelites must do these things in this way, when anyone brings an offering made by fire, to produce an aroma that is pleasing to Yahweh.
14 Kwa vizazi vijavyo, wakati wowote mgeni au mtu mwingine yeyote anayeishi miongoni mwenu aletapo sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana, ni lazima afanye sawasawa kabisa na jinsi mnavyofanya ninyi.
If a foreigner is staying with you, or whoever may live among you throughout your people's generations, he must make an offering made by fire, to produce a sweet aroma for Yahweh. He must act as you act.
15 Jumuiya itakuwa na sheria hizo hizo kwenu na kwa mgeni aishiye miongoni mwenu; hii ni amri ya kudumu kwa vizazi vijavyo. Ninyi na mgeni mtakuwa sawa mbele za Bwana:
There must be the same law for the community and for the foreigner who stays with you, a permanent law throughout your people's generations. As you are, so also must be the traveler staying with you. He must act as you act before Yahweh.
16 Sheria hizo hizo na masharti hayo hayo hayo, yatawahusu ninyi na mgeni aishiye miongoni mwenu.’”
The same law and decree must apply to you and to the foreigner who is staying with you.'”
17 Bwana akamwambia Mose,
Again Yahweh spoke to Moses. He said,
18 “Sema na Waisraeli na uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapeleka
“Speak to the people of Israel and say to them, 'When you come into the land where I will take you,
19 nanyi mkala chakula cha nchi hiyo, toeni sehemu ya chakula hicho kama sadaka kwa Bwana.
when you eat the food produced in the land, you must offer an offering and present it to me.
20 Toeni andazi kutoka kwa malimbuko ya chakula chenu kitokacho katika ardhi, na mkitoe kama sadaka kutoka sakafu ya kupuria nafaka.
From the first of your dough you must offer a loaf to raise it up as a raised offering from the threshing floor. You must raise it up in this way.
21 Kwa vizazi vyote vijavyo hamna budi kutoa sadaka hii kwa Bwana kutoka kwa malimbuko ya unga wenu.
You must give to me a raised offering throughout your people's generations from the first of your dough.
22 “‘Basi kama pasipo kukusudia umeshindwa kushika mojawapo katika amri hizi ambazo Bwana alimpa Mose,
You will sometimes sin without intending to do so, when you do not obey all these commands that I have spoken to Moses—
23 amri yoyote ya Bwana kwenu kupitia Mose, tangu siku ile Bwana alipowapa na inaendelea hadi vizazi vyote vijavyo;
everything that I have commanded you through Moses from the day that I began to give you commands and onward throughout your people's generations.
24 ikiwa hili limefanyika pasipo kukusudia bila jumuiya kuwa na habari nalo, basi jumuiya yote itatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya kuteketezwa ikiwa harufu nzuri inayompendeza Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka na ya kinywaji zilizoamriwa kwayo, na mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
In the case of unintentional sin without the community's knowledge, then all the community must offer one young bull as a burnt offering to produce a sweet aroma for Yahweh. Along with this must be made a grain offering and drink offering, as commanded by the decree, and one male goat as a sin offering.
25 Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya jumuiya yote ya Kiisraeli, nao watasamehewa, kwa kuwa haikuwa makusudi nao wamemletea Bwana sadaka iliyoteketezwa kwa moto na sadaka ya dhambi kwa ajili ya kosa lao.
The priest must make atonement for all the community of the people of Israel. They will be forgiven because the sin was an error. They have brought their sacrifice, an offering made by fire to me. They have brought their sin offering before me for their error.
26 Jumuiya yote ya Kiisraeli pamoja na wageni waishio miongoni mwao watasamehewa, kwa sababu watu wote walihusika katika kosa lile lisilokusudiwa.
Then all the community of the people of Israel will be forgiven, and also the foreigners who are staying with them, because all the people committed the sin unintentionally.
27 “‘Lakini kama mtu mmoja peke yake akitenda dhambi pasipo kukusudia, ni lazima alete mbuzi mke wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
If a person sins unintentionally, then he must offer a female goat a year old as a sin offering.
28 Kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule aliyekosa kwa kufanya dhambi pasipo kukusudia, upatanisho utakapofanywa kwa ajili yake, atasamehewa.
The priest must make atonement before Yahweh for the person who sins unintentionally. That person will be forgiven when atonement has been made.
29 Sheria hiyo moja itamhusu kila mmoja ambaye ametenda dhambi pasipo kukusudia, awe Mwisraeli mzawa ama mgeni.
You must have the same law for the one who does anything unintentionally, the same law for the one who is native born among the people of Israel and for the foreigners who are staying among them.
30 “‘Lakini yeyote ambaye amefanya dhambi kwa dharau awe mzawa au mgeni, anamkufuru Bwana, naye mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
But the person who does anything in defiance, whether he is native born or a foreigner, blasphemes me. That person must be cut off from among his people.
31 Kwa sababu amelidharau neno la Bwana na kuvunja amri zake, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali; hatia yake inabaki juu yake.’”
Because he has despised my word and has broken my commandment, that person must be cut off completely. His sin will be on him.'”
32 Waisraeli walipokuwa jangwani, mtu mmoja alikutwa akikusanya kuni siku ya Sabato.
While the people of Israel were in the wilderness, they found a man gathering wood on the Sabbath day.
33 Wale waliomkuta akikusanya kuni wakamleta kwa Mose, Aroni na kusanyiko lote,
Those who found him brought him to Moses, Aaron, and all the community.
34 nao wakamweka kifungoni, kwa sababu haikufahamika kwa wazi kwamba afanyiwe nini.
They kept him in custody because it had not been declared what should be done with him.
35 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Huyo mtu ni lazima afe. Kusanyiko lote lazima limpige mawe nje ya kambi.”
Then Yahweh said to Moses, “The man must surely be put to death. All the community must stone him with stones outside the camp.”
36 Hivyo kusanyiko likamtoa nje ya kambi na kumpiga mawe hadi akafa, kama Bwana alivyomwamuru Mose.
So all the community brought him outside the camp and stoned him to death as Yahweh had commanded Moses.
37 Bwana akamwambia Mose,
Again Yahweh spoke to Moses. He said,
38 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Kwa vizazi vyote vijavyo jifanyieni vifundo katika pindo za mavazi yenu vikiwa na uzi wa buluu kwenye kila kifundo.
“Speak to the descendants of Israel and command them to make for themselves tassels to hang from the borders of their garments, to hang them from each border by a blue cord. They must do this throughout their people's generations.
39 Mtakuwa mkivitazama vifundo hivyo ili mpate kukumbuka amri zote za Bwana, ili mpate kuzitii msije mkajitia uzinzi wenyewe kwa kuzifuata tamaa za mioyo yenu na za macho yenu.
It will be a special reminder to you, when you may look at it, of all my commandments, to carry them out so that you do not look to your own heart and your own eyes and prostitute yourselves to them.
40 Ndipo mtakumbuka kuzitii amri zangu zote nanyi mtawekwa wakfu kwa Mungu wenu.
Do this so that you may call to mind and obey all my commandments, and so that you may be holy, reserved for me, your God.
41 Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa Misri niwe Mungu wenu. Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu.’”
I am Yahweh your God, who brought you out of the land of Egypt, to become your God. I am Yahweh your God.”

< Hesabu 15 >