< Hesabu 14 >

1 Usiku ule watu wote wa jumuiya walipaza sauti zao na kulia kwa sauti kuu.
Toute l’assemblée éleva la voix et poussa des cris, et le peuple pleura pendant cette nuit-là.
2 Waisraeli wote wakanungʼunika dhidi ya Mose na Aroni, nalo kusanyiko lote wakawaambia, “Laiti tungekuwa tumefia humo nchi ya Misri! Au humu kwenye hili jangwa!
Tous les enfants d’Israël murmurèrent contre Moïse et Aaron, et toute l’assemblée leur dit: « Que ne sommes-nous morts dans le pays d’Égypte, ou que ne sommes-nous morts dans ce désert?
3 Kwa nini Bwana anatuleta katika nchi hii ili tufe kwa upanga? Wake zetu na watoto wetu watachukuliwa kama nyara. Je, isingekuwa bora kwetu kurudi Misri?”
Pourquoi Yahweh nous fait-il aller dans ce pays, pour que nous tombions par l’épée? Nos femmes et nos enfants deviendront une proie. Ne vaut-il pas mieux pour nous retourner en Égypte? »
4 Wakasemezana wao kwa wao, “Inatupasa kumchagua kiongozi na kurudi Misri.”
Et ils se dirent les uns aux autres: « Nommons un chef, et retournons en Égypte. »
5 Ndipo Mose na Aroni wakaanguka kifudifudi mbele ya kusanyiko lote la Kiisraeli lililokusanyika hapo.
Moïse et Aaron tombèrent sur leur visage en présence de toute l’assemblée réunie des enfants d’Israël.
6 Yoshua mwana wa Nuni na Kalebu mwana wa Yefune, waliokuwa miongoni mwa watu wale waliokwenda kuipeleleza nchi, wakararua nguo zao,
Josué, fils de Nun, et Caleb, fils de Jéphoné, deux de ceux qui avaient exploré le pays, déchirèrent leurs vêtements
7 wakasema na kusanyiko lote la Kiisraeli, wakawaambia, “Nchi tuliyopita katikati yake na kuipeleleza ni nzuri sana sana.
et ils parlèrent ainsi à toute l’assemblée des enfants d’Israël: « Le pays que nous avons parcouru pour l’explorer est un excellent pays.
8 Ikiwa Bwana anapendezwa nasi, atatuongoza kuingia katika nchi ile, nchi itiririkayo maziwa na asali, naye atatupa nchi hiyo.
Si Yahweh nous est favorable, il nous fera entrer dans ce pays et nous le donnera; c’est un pays où coulent le lait et le miel.
9 Ila tu msimwasi Bwana. Wala msiwaogope watu wa nchi hiyo, kwa sababu tutawameza. Ulinzi wao umeondoka, lakini Bwana yupo pamoja nasi. Msiwaogope.”
Seulement ne vous mettez pas en rébellion contre Yahweh, et ne craignez point les hommes de ce pays, car ils seront pour nous une pâture; leur abri s’est retiré d’eux, et Yahweh est avec nous, ne les craignez point. »
10 Lakini kusanyiko lote likazungumza juu ya kuwapiga kwa mawe. Ndipo utukufu wa Bwana ukaonekana katika Hema la Kukutania kwa Waisraeli wote.
Toute l’assemblée parlait de les lapider, lorsque la gloire de Yahweh apparut sur la tente de réunion, devant tous les enfants d’Israël.
11 Bwana akamwambia Mose, “Watu hawa watanidharau mpaka lini? Wataendelea kukataa kuniamini mimi mpaka lini, ingawa nimetenda ishara za miujiza miongoni mwao?
Et Yahweh dit à Moïse: « Jusques à quand ce peuple me méprisera-t-il? Jusques à quand ne croira-t-il pas en moi, malgré tous les prodiges que j’ai faits au milieu de lui?
12 Nitawapiga kwa tauni na kuwaangamiza, lakini nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa lenye nguvu kuliko wao.”
Je le frapperai par la peste et je le détruirai, et je ferai de toi une nation plus grande et plus puissante que lui. »
13 Mose akamwambia Bwana, “Ndipo Wamisri watasikia juu ya jambo hili! Kwa uweza wako uliwapandisha watu hawa kutoka miongoni mwao.
Moïse dit à Yahweh: « Les Égyptiens ont appris que, par votre puissance, vous avez fait monter ce peuple du milieu d’eux, et ils l’ont dit aux habitants de ce pays.
14 Nao watawaambia wenyeji wa nchi hii jambo hili. Wao tayari wameshasikia kwamba wewe, Ee Bwana, upo pamoja na watu hawa, na kuwa wewe, Ee Bwana, umeonekana uso kwa uso, nalo wingu lako hukaa juu yao. Tena wewe unawatangulia kwa nguzo ya wingu mchana na kwa nguzo ya moto usiku.
Tous ont appris que vous, Yahweh, vous êtes au milieu de ce peuple; que vous vous montrez face à face, vous, Yahweh; que votre nuée se tient sur eux, et que vous marchez devant eux le jour dans une colonne de nuée, et la nuit dans une colonne de feu.
15 Ikiwa utawaua watu hawa wote mara moja, mataifa ambayo yamesikia taarifa hii kukuhusu wewe watasema,
Si vous faites mourir ce peuple comme un seul homme, les nations qui ont entendu parler de vous diront:
16 ‘Bwana alishindwa kuwaingiza watu hawa katika nchi aliyowaahidi kwa kiapo; hivyo akawaua jangwani.’
Yahweh n’avait pas le pouvoir de faire entrer ce peuple dans le pays qu’il avait juré de leur donner; c’est pourquoi il les a fait périr dans le désert.
17 “Basi sasa nguvu za Bwana na zionekane, sawasawa na vile ulivyosema:
Maintenant que la puissance du Seigneur se montre grande, comme vous l’avez déclaré, en disant:
18 ‘Bwana si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo na mwenye kusamehe dhambi na uasi. Lakini haachi kumwadhibu mwenye hatia, huadhibu watoto kwa ajili ya dhambi ya baba zao hata kizazi cha tatu na cha nne.’
Yahweh est lent à la colère et riche en bonté, il pardonne l’iniquité et le péché; mais il ne tient pas le coupable pour innocent, et il punit l’iniquité des pères sur les enfants, sur ceux de la troisième et de la quatrième génération.
19 Kwa kadiri ya upendo wako mkuu, usamehe dhambi ya watu hawa, kama vile ulivyowasamehe tangu wakati walitoka Misri mpaka sasa.”
Pardonnez l’iniquité de ce peuple selon la grandeur de votre miséricorde, comme vous avez pardonné à ce peuple depuis l’Égypte jusqu’ici. »
20 Bwana akajibu, “Nimewasamehe kama ulivyoomba.
Et Yahweh dit: « Je pardonne, selon ta demande;
21 Hata hivyo, kwa hakika kama niishivyo, na kwa hakika kama utukufu wa Bwana uijazavyo dunia yote,
mais, — je suis vivant! et la gloire de Yahweh remplira toute la terre! —
22 hakuna hata mmoja wa watu hawa ambao waliuona utukufu wangu na ishara za miujiza niliyotenda huko Misri na huko jangwani, lakini ambaye hakunitii na akanijaribu mara hizi kumi,
tous les hommes qui ont vu ma gloire et les prodiges que j’ai faits en Égypte et dans le désert, qui m’ont tenté déjà dix fois et qui n’ont pas écouté ma voix,
23 hakuna hata mmoja wao atakayeona nchi niliyowaahidi baba zao kwa kiapo. Hakuna hata mmoja ambaye amenidharau atakayeiona.
tous ceux-là ne verront point le pays que j’ai promis avec serment à leurs pères. Aucun de ceux qui m’ont méprisé ne le verra.
24 Lakini kwa sababu mtumishi wangu Kalebu ana roho ya tofauti na ananifuata kwa moyo wote, nitamwingiza katika nchi aliyoiendea, nao wazao wake watairithi.
Mais mon serviteur Caleb, qui a été animé d’un autre esprit et s’est fidèlement attaché à moi, je le ferai entrer dans le pays où il est allé, et ses descendants le posséderont.
25 Kwa kuwa Waamaleki na Wakanaani wanaishi katika mabonde, kesho geukeni mwelekee jangwani kwa kufuata njia iendayo Bahari ya Shamu.”
L’Amalécite et le Chananéen habitent dans la vallée: demain retournez-vous, et partez pour le désert, sur le chemin de la mer Rouge. »
26 Bwana akamwambia Mose na Aroni:
Yahweh parla à Moïse et à Aaron, en disant:
27 “Jumuiya hii ovu itanungʼunika dhidi yangu hadi lini? Nimesikia malalamiko ya hawa Waisraeli wanaonungʼunika.
« Jusques à quand supporterai-je cette méchante assemblée qui murmure contre moi? J’ai entendu les murmures que les enfants d’Israël profèrent contre moi.
28 Hivyo waambie, ‘Hakika kama niishivyo, asema Bwana, nitawafanyia vitu vilevile nilivyosikia mkisema:
Dis-leur: Je suis vivant! dit Yahweh: je vous ferai selon que vous avez parlé à mes oreilles.
29 Kila mmoja wenu mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi ambaye alihesabiwa na amenungʼunika dhidi yangu, miili yenu itaanguka katika jangwa hili.
Vos cadavres tomberont dans ce désert. Vous tous, dont on a fait le recensement, en vous comptant depuis l’âge de vingt ans et au-dessus, et qui avez murmuré contre moi,
30 Hakuna hata mmoja wenu atakayeingia katika nchi niliyoapa kwa mkono ulioinuliwa kuwa makao yenu, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune, na Yoshua mwana wa Nuni.
vous n’entrerez point dans le pays où j’ai juré de vous établir, à l’exception de Caleb, fils de Jéphoné, et de Josué, fils de Nun.
31 Lakini watoto wenu ambao mlisema watachukuliwa kama mateka, nitawaingiza humo ili waifurahie nchi ambayo ninyi mmeikataa.
Et vos petits enfants, dont vous avez dit: Ils deviendront une proie! je les y ferai entrer, et ils connaîtront le pays que vous avez dédaigné.
32 Lakini ninyi, miili yenu itaanguka katika jangwa hili.
Vos cadavres, à vous, tomberont dans le désert;
33 Watoto wenu watakuwa wachungaji wa mifugo hapa kwa miaka arobaini, wakiteseka kwa ajili ya kukosa uaminifu kwenu, hadi mwili wa mtu wenu wa mwisho ulale katika jangwa hili.
et vos fils mèneront leurs troupeaux dans le désert pendant quarante ans, et ils porteront la peine de vos infidélités, jusqu’à ce que vos cadavres soient consumés dans le désert.
34 Kwa miaka arobaini, mwaka mmoja kwa kila siku katika zile siku arobaini mlizoipeleleza nchi, mtateseka kwa ajili ya dhambi zenu, na kujua jinsi ilivyo vibaya kunifanya mimi kuwa adui yenu.’
Selon les quarante jours que vous avez mis à explorer le pays, — autant de jours, autant d’années — vous porterez vos iniquités quarante années, et vous saurez ce que c’est que mon éloignement.
35 Mimi Bwana nimesema, na hakika nitafanya mambo haya kwa jumuiya hii yote ovu, ambayo imefungamana pamoja dhidi yangu. Watakutana na mwisho wao katika jangwa hili; hapa ndipo watafia.”
Moi, Yahweh, j’ai parlé! Voilà ce que je ferai à cette méchante assemblée qui s’est ameutée contre moi: ils seront consumés dans ce désert, ils y mourront. »
36 Hivyo watu wale ambao Mose alikuwa amewatuma kuipeleleza nchi, waliorudi na kuifanya jumuiya nzima kunungʼunika dhidi ya Mose kwa kueneza taarifa mbaya kuhusu hiyo nchi:
Les hommes que Moïse avait envoyés pour explorer le pays et qui, à leur retour, avaient fait murmurer contre lui toute l’assemblée, en décrivant le pays,
37 watu hawa waliohusika kueneza taarifa mbaya kuhusu hiyo nchi walipigwa na kuanguka kwa tauni mbele za Bwana.
ces hommes, qui avaient décrié le pays, moururent frappés d’une plaie devant Yahweh.
38 Miongoni mwa watu waliokwenda kuipeleleza hiyo nchi, ni Yoshua mwana wa Nuni, na Kalebu mwana wa Yefune peke yao waliosalia.
Josué, fils de Nun, et Caleb, fils de Jéphoné, restèrent seuls vivants parmi ces hommes qui étaient allés explorer le pays.
39 Mose alipotoa taarifa hii kwa Waisraeli wote, waliomboleza kwa uchungu.
Moïse rapporta ces paroles à tous les enfants d’Israël, et le peuple fut en grande désolation.
40 Mapema asubuhi siku iliyofuata walipanda juu kuelekea kwenye nchi ya vilima virefu, wakasema, “Tumetenda dhambi. Tutakwea mpaka mahali Bwana alipotuahidi.”
S’étant levés de bon matin, ils montèrent vers le sommet de la montagne, en disant: « Nous voici! Nous monterons au lieu dont Yahweh a parlé, car nous avons péché. »
41 Lakini Mose akasema, “Kwa nini hamtii amri ya Bwana? Jambo hili halitafanikiwa!
Moïse dit: « Pourquoi transgressez-vous l’ordre de Yahweh? Cela ne vous réussira point.
42 Msipande juu, kwa kuwa Bwana hayupo pamoja nanyi. Mtashindwa na adui zenu,
Ne montez pas, car Yahweh n’est pas au milieu de vous! Ne vous faites pas battre par vos ennemis.
43 kwa kuwa Waamaleki na Wakanaani watapambana nanyi huko. Kwa sababu mmemwacha Bwana, hatakuwa pamoja nanyi, ninyi mtaanguka kwa upanga.”
Car l’Amalécite et le Chananéen sont là devant vous, et vous tomberiez par l’épée; parce qui vous vous êtes détournés de Yahweh, Yahweh ne sera pas avec vous. »
44 Hata hivyo, kwa kiburi chao walipanda juu kuelekea nchi ya vilima virefu, ijapokuwa Mose hakutoka kambini wala Sanduku la Agano la Bwana.
Ils s’obstinèrent à monter vers le sommet de la montagne; mais l’arche d’alliance de Yahweh et Moïse ne bougèrent pas du milieu du camp.
45 Ndipo Waamaleki na Wakanaani walioishi katika hiyo nchi ya vilima wakateremka na kuwashambulia, wakawapiga njia yote hadi Horma.
Alors l’Amalécite et le Chananéen qui habitaient cette montagne descendirent, les battirent et les taillèrent en pièces jusqu’à Horma.

< Hesabu 14 >