< Hesabu 13 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Yahweh parla à Moïse, en disant:
2 “Watume baadhi ya watu wakaipeleleze nchi ya Kanaani, ambayo ninawapa Waisraeli. Kutoka kwa kila kabila la baba zao, tuma mmoja wa viongozi wao.”
« Envoie des hommes pour explorer le pays de Chanaan, que je donne aux enfants d'Israël. Vous enverrez un homme par chacune des tribus patriarcales; que tous soient des princes parmi eux. »
3 Hivyo kwa agizo la Bwana Mose akawatuma kutoka Jangwa la Parani. Wote walikuwa viongozi wa Waisraeli.
Moïse les envoya du désert de Pharan, selon l'ordre de Yahweh; tous ces hommes étaient des chefs des enfants d'Israël.
4 Haya ndiyo majina yao: kutoka kabila la Reubeni, Shamua mwana wa Zakuri;
Voici leurs noms: pour la tribu de Ruben, Sammua, fils de Zéchur;
5 kutoka kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori;
pour la tribu de Siméon, Saphat, fils de Huri;
6 kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune;
pour la tribu de Juda, Caleb, fils de Jéphoné;
7 kutoka kabila la Isakari, Igali mwana wa Yosefu;
pour la tribu d'Issachar, Igal, fils de Joseph;
8 kutoka kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Nuni;
pour la tribu d'Ephraïm, Osée, fils de Nun;
9 kutoka kabila la Benyamini, Palti mwana wa Rafu;
pour la tribu de Benjamin, Phalti, fils de Raphu;
10 kutoka kabila la Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi,
pour la tribu de Zabulon, Geddiel, fils de Sodi;
11 kutoka kabila la Manase (kabila la Yosefu), Gadi mwana wa Susi;
pour la tribu de Joseph, la tribu de Manassé, Gaddi, fils de Susi;
12 kutoka kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemali;
pour la tribu de Dan, Ammiel, fils de Gemalli;
13 kutoka kabila la Asheri, Sethuri mwana wa Mikaeli;
pour la tribu d'Aser, Sthur, fils de Michaël;
14 kutoka kabila la Naftali, Nabi mwana wa Wofsi;
pour la tribu de Nephthali, Nahabi, fils de Vapsi;
15 kutoka kabila la Gadi, Geueli mwana wa Maki.
pour la tribu de Gad, Guel, fils de Machi. —
16 Haya ndiyo majina ya watu ambao Mose aliwatuma kuipeleleza nchi. (Mose akampa Hoshea mwana wa Nuni jina Yoshua.)
Tels sont les noms des hommes que Moïse envoya pour explorer le pays. Moïse donna à Osée, fils de Nun, le nom de Josué.
17 Mose alipowatuma wakaipeleleze Kanaani, alisema, “Pandeni kupitia Negebu, mwende mpaka nchi ya vilima.
Moïse les envoya pour explorer le pays de Chanaan; il leur dit: « Montez là par le Négeb; et vous monterez sur la montagne.
18 Mwone nchi ni ya namna gani, na kama watu waishio humo wana nguvu au ni wadhaifu, iwapo ni wachache au wengi.
Vous examinerez le pays, ce qu'il est, et le peuple qui l'habite, s'il est fort ou faible, peu nombreux ou considérable;
19 Wanaishi katika nchi ya namna gani? Je, ni nzuri au mbaya? Wanaishi katika miji ya namna gani? Je, haina kuta au ngome?
ce qu'est le pays où il habite, s'il est bon ou mauvais; ce que sont les villes où il habite, si elles sont ouvertes ou fortifiées;
20 Ardhi iko aje? Ina rutuba au la? Je, kuna miti ndani yake au la? Jitahidini kadiri mwezavyo kuleta baadhi ya matunda ya nchi.” (Ulikuwa msimu wa kuiva zabibu za kwanza.)
ce qu'est le sol, s'il est gras ou maigre, s'il y a des arbres ou non. Ayez bon courage, et prenez des fruits du pays. » C'était le temps des premiers raisins.
21 Hivyo wakapanda na kuipeleleza nchi kutoka Jangwa la Sini hadi Rehobu, kuelekea Lebo-Hamathi.
Ils montèrent et explorèrent le pays, depuis le désert de Sin jusqu'à Rohob, sur le chemin d'Emath.
22 Wakapanda kupitia Negebu hadi wakafika Hebroni, mahali ambapo Ahimani, Sheshai na Talmai, wazao wa Anaki, waliishi. (Hebroni ulikuwa umejengwa miaka saba kabla ya mji wa Soani ulioko Misri.)
Ils montèrent dans le Négeb et allèrent jusqu'à Hébron, où étaient Achiman, Sisaï et Tholmaï, enfants d'Enac. Hébron avait été bâtie sept ans avant Tanis d'Egypte.
23 Walipofika katika Bonde la Eshkoli, walivunja tawi lililokuwa na kishada kimoja cha zabibu. Wawili wao wakalichukua lile tawi kwenye mti, pamoja na komamanga na tini.
Arrivés à la vallée d'Escol, ils coupèrent une branche de vigne avec sa grappe de raisin, et ils la portèrent à deux au moyen d'une perche; ils prirent aussi des grenades et des figues.
24 Eneo lile likaitwa Bonde la Eshkoli kwa sababu ya kile kishada cha zabibu ambacho Waisraeli walikikata huko.
On donna à ce lieu le nom de vallée d'Escol, à cause de la grappe que les enfants d'Israël y coupèrent.
25 Mwishoni mwa siku arobaini wakarudi kutoka kuipeleleza nchi.
Au bout de quarante jours, ils revinrent d'explorer le pays.
26 Wakarudi kwa Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli huko Kadeshi kwenye Jangwa la Parani. Hapo ndipo walipotoa habari kwao na kwa kusanyiko lote na kuwaonyesha matunda ya hiyo nchi.
Ils allèrent et se rendirent auprès de Moïse et d'Aaron, et de toute l'assemblée des enfants d'Israël, à Cadès, dans le désert de Pharan. Ils leur firent un rapport, ainsi qu'à toute l'assemblée, et leur montrèrent les fruits du pays.
27 Wakampa Mose taarifa hii: “Tuliingia katika nchi uliyotutuma, nayo inatiririka maziwa na asali! Hili hapa tunda lake.
Voici le récit qu'ils firent à Moïse: « Nous sommes allés dans le pays où tu nous as envoyés. C'est vraiment un pays où coulent le lait et le miel, et en voici les fruits.
28 Lakini watu wanaoishi huko ni wenye nguvu, na miji yao ina ngome na ni mikubwa sana. Huko tuliona hata wazao wa Anaki.
Mais le peuple qui habite le pays est puissant, et les villes sont fortifiées et très grandes; nous y avons même vu des enfants d'Enac.
29 Waamaleki wanaishi Negebu; Wahiti, Wayebusi na Waamori wanaishi katika nchi ya vilima; nao Wakanaani wanaishi karibu na bahari na kando ya Yordani.”
Amalec habite la contrée du Négeb; le Héthéen, le Jébuséen et l'Amorrhéen habitent dans la montagne, et le Chananéen habite au bord de la mer et le long du Jourdain. »
30 Kisha Kalebu akawanyamazisha watu mbele ya Mose na kusema, “Imetupasa kupanda na kuimiliki nchi, kwa maana hakika tunaweza kufanya hivyo.”
Caleb fit taire le peuple au sujet de Moïse: « Montons, dit-il, emparons-nous du pays, car nous pouvons nous en rendre maîtres. »
31 Lakini watu waliokuwa wamepanda pamoja naye wakasema, “Hatuwezi kuwashambulia wale watu; wana nguvu kutuliko sisi.”
Mais les hommes qui y étaient montés avec lui, dirent: « Nous ne sommes pas capables de monter contre ce peuple: il est plus fort que nous. »
32 Wakaeneza taarifa mbaya miongoni mwa Waisraeli kuhusu nchi waliyoipeleleza. Wakasema, “Nchi tuliyoipeleleza hula watu waishio ndani yake. Watu wote tuliowaona huko ni majitu.
Et ils décrièrent devant les enfants d'Israël le pays qu'ils avaient exploré, en disant: « Le pays que nous avons parcouru pour l'explorer, est un pays qui dévore ses habitants; tout le peuple que nous y avons vu est formé de gens de haute taille;
33 Tuliwaona Wanefili huko (wazao wa Anaki wanatokana na Wanefili.) Tulijiona kama panzi machoni petu wenyewe, nao ndivyo walivyotuona.”
et nous y avons vu les géants, fils d'Enac, de la race des géants: nous étions à nos yeux et aux leurs comme des sauterelles. »

< Hesabu 13 >