< Hesabu 13 >

1 Bwana akamwambia Mose,
And the Lord spoke unto Moses, saying,
2 “Watume baadhi ya watu wakaipeleleze nchi ya Kanaani, ambayo ninawapa Waisraeli. Kutoka kwa kila kabila la baba zao, tuma mmoja wa viongozi wao.”
Send thou out some men that they may spy out the land of Canaan, which I give unto the children of Israel: one man each of every tribe of their fathers shall ye send, every one who is a prince among them.
3 Hivyo kwa agizo la Bwana Mose akawatuma kutoka Jangwa la Parani. Wote walikuwa viongozi wa Waisraeli.
And Moses sent them out from the wilderness of Paran by the order of the Lord: they all were men, [who] were heads of the children of Israel.
4 Haya ndiyo majina yao: kutoka kabila la Reubeni, Shamua mwana wa Zakuri;
And these are their names: Of the tribe of Reuben, Shammua the son of Zaccur.
5 kutoka kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori;
Of the tribe of Simeon, Shaphat the son of Chori.
6 kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune;
Of the tribe of Judah, Caleb the son of Yephunneh.
7 kutoka kabila la Isakari, Igali mwana wa Yosefu;
Of the tribe of Issachar, Yigal the son of Joseph.
8 kutoka kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Nuni;
Of the tribe of Ephraim, Hoshea, the son of Nun.
9 kutoka kabila la Benyamini, Palti mwana wa Rafu;
Of the tribe of Benjamin, Palti the son of Raphu.
10 kutoka kabila la Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi,
Of the tribe of Zebulun, Gaddiel the son of Sodi.
11 kutoka kabila la Manase (kabila la Yosefu), Gadi mwana wa Susi;
Of the tribe of Joseph, of the tribe of Menasseh, Gaddi the son of Sussi.
12 kutoka kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemali;
Of the tribe of Dan, 'Ammiel the son of Gemalli.
13 kutoka kabila la Asheri, Sethuri mwana wa Mikaeli;
Of the tribe of Asher, Sethur the son of Michael.
14 kutoka kabila la Naftali, Nabi mwana wa Wofsi;
Of the tribe of Naphtali, Nachbi the son of Vophsi.
15 kutoka kabila la Gadi, Geueli mwana wa Maki.
Of the tribe of Gad, Geuel the son of Machi.
16 Haya ndiyo majina ya watu ambao Mose aliwatuma kuipeleleza nchi. (Mose akampa Hoshea mwana wa Nuni jina Yoshua.)
These are the names of the men whom Moses sent to spy out the land; and Moses called Hoshea the son of Nun, Joshua [[Yehoshua']].
17 Mose alipowatuma wakaipeleleze Kanaani, alisema, “Pandeni kupitia Negebu, mwende mpaka nchi ya vilima.
And Moses sent them to spy out the land of Canaan, and he said unto them, Go you up this way at the south side, and go up into the mountain;
18 Mwone nchi ni ya namna gani, na kama watu waishio humo wana nguvu au ni wadhaifu, iwapo ni wachache au wengi.
And see the land, what it is; and the people that dwell therein, whether they be strong or weak, whether they be few or many;
19 Wanaishi katika nchi ya namna gani? Je, ni nzuri au mbaya? Wanaishi katika miji ya namna gani? Je, haina kuta au ngome?
And what the land is on which they dwell, whether it be good or bad; and what the cities are in which they dwell, whether in open places, or in strongholds;
20 Ardhi iko aje? Ina rutuba au la? Je, kuna miti ndani yake au la? Jitahidini kadiri mwezavyo kuleta baadhi ya matunda ya nchi.” (Ulikuwa msimu wa kuiva zabibu za kwanza.)
And what the land is, whether it be fat or lean, whether there be trees therein, or not; and take ye courage, and take away some of the fruit of the land. Now the time was the season of the first ripening of grapes.
21 Hivyo wakapanda na kuipeleleza nchi kutoka Jangwa la Sini hadi Rehobu, kuelekea Lebo-Hamathi.
And they went up, and spied out the land from the wilderness of Zin unto Rechob, on the road to Chamath.
22 Wakapanda kupitia Negebu hadi wakafika Hebroni, mahali ambapo Ahimani, Sheshai na Talmai, wazao wa Anaki, waliishi. (Hebroni ulikuwa umejengwa miaka saba kabla ya mji wa Soani ulioko Misri.)
And they ascended on the south side, and came unto Hebron; and there were Achiman, Sheshai, and Talmai, the children of 'Anak; [now Hebron had been built seven years before Zoan in Egypt.]
23 Walipofika katika Bonde la Eshkoli, walivunja tawi lililokuwa na kishada kimoja cha zabibu. Wawili wao wakalichukua lile tawi kwenye mti, pamoja na komamanga na tini.
And they came unto the valley of Eshcol, and they cut down from there a branch with one cluster of grapes, and they bore it upon a barrow between two; and [they took some] of the pomegranates and of the figs.
24 Eneo lile likaitwa Bonde la Eshkoli kwa sababu ya kile kishada cha zabibu ambacho Waisraeli walikikata huko.
That place was called the valley of Eshcol, on account of the cluster which the children of Israel cut down from there.
25 Mwishoni mwa siku arobaini wakarudi kutoka kuipeleleza nchi.
And they returned from spying out the land at the end of forty days.
26 Wakarudi kwa Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli huko Kadeshi kwenye Jangwa la Parani. Hapo ndipo walipotoa habari kwao na kwa kusanyiko lote na kuwaonyesha matunda ya hiyo nchi.
And they went and came to Moses, and to Aaron, and to all the congregation of the children of Israel, unto the wilderness of Paran, to Kadesh; and they brought back word unto them, and unto all the congregation, and showed them the fruit of the land.
27 Wakampa Mose taarifa hii: “Tuliingia katika nchi uliyotutuma, nayo inatiririka maziwa na asali! Hili hapa tunda lake.
And they told him, and said, We came unto the land whither thou didst send us, and truly doth it flow with milk and honey; and this is its fruit.
28 Lakini watu wanaoishi huko ni wenye nguvu, na miji yao ina ngome na ni mikubwa sana. Huko tuliona hata wazao wa Anaki.
Nevertheless the people are strong that dwell in the land, and the cities are very strongly walled, and great; and the children of 'Anak also have we seen there.
29 Waamaleki wanaishi Negebu; Wahiti, Wayebusi na Waamori wanaishi katika nchi ya vilima; nao Wakanaani wanaishi karibu na bahari na kando ya Yordani.”
The Amalekites dwell in the southern country; and the Hittites, and the Jebusites, and the Emorites, dwell in the mountains; and the Canaanites dwell by the sea, and by the margin of the Jordan.
30 Kisha Kalebu akawanyamazisha watu mbele ya Mose na kusema, “Imetupasa kupanda na kuimiliki nchi, kwa maana hakika tunaweza kufanya hivyo.”
And Caleb stilled the people toward Moses, and he said, We can easily go up, and take possession of it; for we are well able to overcome it.
31 Lakini watu waliokuwa wamepanda pamoja naye wakasema, “Hatuwezi kuwashambulia wale watu; wana nguvu kutuliko sisi.”
But the men who had gone up with him said, We are not able to go up against the people; for they are stronger than we.
32 Wakaeneza taarifa mbaya miongoni mwa Waisraeli kuhusu nchi waliyoipeleleza. Wakasema, “Nchi tuliyoipeleleza hula watu waishio ndani yake. Watu wote tuliowaona huko ni majitu.
And they brought up an evil report of the land which they had spied out unto the children of Israel, saying, The land through which we have passed to spy it out, is a land that consumeth its inhabitants; and all the people that we saw in it are men of a great stature.
33 Tuliwaona Wanefili huko (wazao wa Anaki wanatokana na Wanefili.) Tulijiona kama panzi machoni petu wenyewe, nao ndivyo walivyotuona.”
And there we saw the giants, the sons of 'Anak, of the giants' [family]: and we were in our own eyes as grasshoppers, and so were we in their eyes.

< Hesabu 13 >