< Hesabu 13 >

1 Bwana akamwambia Mose,
And the LORD spoke unto Moses, saying:
2 “Watume baadhi ya watu wakaipeleleze nchi ya Kanaani, ambayo ninawapa Waisraeli. Kutoka kwa kila kabila la baba zao, tuma mmoja wa viongozi wao.”
'Send thou men, that they may spy out the land of Canaan, which I give unto the children of Israel; of every tribe of their fathers shall ye send a man, every one a prince among them.'
3 Hivyo kwa agizo la Bwana Mose akawatuma kutoka Jangwa la Parani. Wote walikuwa viongozi wa Waisraeli.
And Moses sent them from the wilderness of Paran according to the commandment of the LORD; all of them men who were heads of the children of Israel.
4 Haya ndiyo majina yao: kutoka kabila la Reubeni, Shamua mwana wa Zakuri;
And these were their names: of the tribe of Reuben, Shammua the son of Zaccur.
5 kutoka kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori;
Of the tribe of Simeon, Shaphat the son of Hori.
6 kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune;
Of the tribe of Judah, Caleb the son of Jephunneh.
7 kutoka kabila la Isakari, Igali mwana wa Yosefu;
Of the tribe of Issachar, Igal the son of Joseph.
8 kutoka kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Nuni;
Of the tribe of Ephraim, Hoshea the son of Nun.
9 kutoka kabila la Benyamini, Palti mwana wa Rafu;
Of the tribe of Benjamin, Palti the son of Raphu.
10 kutoka kabila la Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi,
Of the tribe of Zebulun, Gaddiel the son of Sodi.
11 kutoka kabila la Manase (kabila la Yosefu), Gadi mwana wa Susi;
Of the tribe of Joseph, namely, of the tribe of Manasseh, Gaddi the son of Susi.
12 kutoka kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemali;
Of the tribe of Dan, Ammiel the son of Gemalli.
13 kutoka kabila la Asheri, Sethuri mwana wa Mikaeli;
Of the tribe of Asher, Sethur the son of Michael.
14 kutoka kabila la Naftali, Nabi mwana wa Wofsi;
Of the tribe of Naphtali, Nahbi the son of Vophsi.
15 kutoka kabila la Gadi, Geueli mwana wa Maki.
Of the tribe of Gad, Geuel the son of Machi.
16 Haya ndiyo majina ya watu ambao Mose aliwatuma kuipeleleza nchi. (Mose akampa Hoshea mwana wa Nuni jina Yoshua.)
These are the names of the men that Moses sent to spy out the land. And Moses called Hoshea the son of Nun Joshua.
17 Mose alipowatuma wakaipeleleze Kanaani, alisema, “Pandeni kupitia Negebu, mwende mpaka nchi ya vilima.
And Moses sent them to spy out the land of Canaan, and said unto them: 'Get you up here into the South, and go up into the mountains;
18 Mwone nchi ni ya namna gani, na kama watu waishio humo wana nguvu au ni wadhaifu, iwapo ni wachache au wengi.
and see the land, what it is; and the people that dwelleth therein, whether they are strong or weak, whether they are few or many;
19 Wanaishi katika nchi ya namna gani? Je, ni nzuri au mbaya? Wanaishi katika miji ya namna gani? Je, haina kuta au ngome?
and what the land is that they dwell in, whether it is good or bad; and what cities they are that they dwell in, whether in camps, or in strongholds;
20 Ardhi iko aje? Ina rutuba au la? Je, kuna miti ndani yake au la? Jitahidini kadiri mwezavyo kuleta baadhi ya matunda ya nchi.” (Ulikuwa msimu wa kuiva zabibu za kwanza.)
and what the land is, whether it is fat or lean, whether there is wood therein, or not. And be ye of good courage, and bring of the fruit of the land.' — Now the time was the time of the first-ripe grapes. —
21 Hivyo wakapanda na kuipeleleza nchi kutoka Jangwa la Sini hadi Rehobu, kuelekea Lebo-Hamathi.
So they went up, and spied out the land from the wilderness of Zin unto Rehob, at the entrance to Hamath.
22 Wakapanda kupitia Negebu hadi wakafika Hebroni, mahali ambapo Ahimani, Sheshai na Talmai, wazao wa Anaki, waliishi. (Hebroni ulikuwa umejengwa miaka saba kabla ya mji wa Soani ulioko Misri.)
And they went up into the South, and came unto Hebron; and Ahiman, Sheshai, and Talmai, the children of Anak, were there. — Now Hebron was built seven years before Zoan in Egypt. —
23 Walipofika katika Bonde la Eshkoli, walivunja tawi lililokuwa na kishada kimoja cha zabibu. Wawili wao wakalichukua lile tawi kwenye mti, pamoja na komamanga na tini.
And they came unto the valley of Eshcol, and cut down from thence a branch with one cluster of grapes, and they bore it upon a pole between two; they took also of the pomegranates, and of the figs. —
24 Eneo lile likaitwa Bonde la Eshkoli kwa sababu ya kile kishada cha zabibu ambacho Waisraeli walikikata huko.
That place was called the valley of Eshcol, because of the cluster which the children of Israel cut down from thence. —
25 Mwishoni mwa siku arobaini wakarudi kutoka kuipeleleza nchi.
And they returned from spying out the land at the end of forty days.
26 Wakarudi kwa Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli huko Kadeshi kwenye Jangwa la Parani. Hapo ndipo walipotoa habari kwao na kwa kusanyiko lote na kuwaonyesha matunda ya hiyo nchi.
And they went and came to Moses, and to Aaron, and to all the congregation of the children of Israel, unto the wilderness of Paran, to Kadesh; and brought back word unto them, and unto all the congregation, and showed them the fruit of the land.
27 Wakampa Mose taarifa hii: “Tuliingia katika nchi uliyotutuma, nayo inatiririka maziwa na asali! Hili hapa tunda lake.
And they told him, and said: 'We came unto the land whither thou sentest us, and surely it floweth with milk and honey; and this is the fruit of it.
28 Lakini watu wanaoishi huko ni wenye nguvu, na miji yao ina ngome na ni mikubwa sana. Huko tuliona hata wazao wa Anaki.
Howbeit the people that dwell in the land are fierce, and the cities are fortified, and very great; and moreover we saw the children of Anak there.
29 Waamaleki wanaishi Negebu; Wahiti, Wayebusi na Waamori wanaishi katika nchi ya vilima; nao Wakanaani wanaishi karibu na bahari na kando ya Yordani.”
Amalek dwelleth in the land of the South; and the Hittite, and the Jebusite, and the Amorite, dwell in the mountains; and the Canaanite dwelleth by the sea, and along by the side of the Jordan.'
30 Kisha Kalebu akawanyamazisha watu mbele ya Mose na kusema, “Imetupasa kupanda na kuimiliki nchi, kwa maana hakika tunaweza kufanya hivyo.”
And Caleb stilled the people toward Moses, and said: 'We should go up at once, and possess it; for we are well able to overcome it.'
31 Lakini watu waliokuwa wamepanda pamoja naye wakasema, “Hatuwezi kuwashambulia wale watu; wana nguvu kutuliko sisi.”
But the men that went up with him said: 'We are not able to go up against the people; for they are stronger than we.'
32 Wakaeneza taarifa mbaya miongoni mwa Waisraeli kuhusu nchi waliyoipeleleza. Wakasema, “Nchi tuliyoipeleleza hula watu waishio ndani yake. Watu wote tuliowaona huko ni majitu.
And they spread an evil report of the land which they had spied out unto the children of Israel, saying: 'The land, through which we have passed to spy it out, is a land that eateth up the inhabitants thereof; and all the people that we saw in it are men of great stature.
33 Tuliwaona Wanefili huko (wazao wa Anaki wanatokana na Wanefili.) Tulijiona kama panzi machoni petu wenyewe, nao ndivyo walivyotuona.”
And there we saw the Nephilim, the sons of Anak, who come of the Nephilim; and we were in our own sight as grasshoppers, and so we were in their sight.'

< Hesabu 13 >