< Hesabu 13 >

1 Bwana akamwambia Mose,
And there, the Lord spoke to Moses, saying:
2 “Watume baadhi ya watu wakaipeleleze nchi ya Kanaani, ambayo ninawapa Waisraeli. Kutoka kwa kila kabila la baba zao, tuma mmoja wa viongozi wao.”
“Send men, who may examine the land of Canaan, which I will give to the sons of Israel, one from the rulers of each tribe.”
3 Hivyo kwa agizo la Bwana Mose akawatuma kutoka Jangwa la Parani. Wote walikuwa viongozi wa Waisraeli.
Moses did what the Lord had commanded, sending, from the desert of Paran, leading men, whose names are these:
4 Haya ndiyo majina yao: kutoka kabila la Reubeni, Shamua mwana wa Zakuri;
from the tribe of Ruben, Shammua the son of Zaccur;
5 kutoka kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori;
from the tribe of Simeon, Shaphat the son of Hori;
6 kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune;
from the tribe of Judah, Caleb the son of Jephunneh;
7 kutoka kabila la Isakari, Igali mwana wa Yosefu;
from the tribe of Issachar, Igal the son of Joseph;
8 kutoka kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Nuni;
from the tribe of Ephraim, Hosea the son of Nun;
9 kutoka kabila la Benyamini, Palti mwana wa Rafu;
from the tribe of Benjamin, Palti the son of Raphu;
10 kutoka kabila la Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi,
from the tribe of Zebulon, Gaddiel the son of Sodi;
11 kutoka kabila la Manase (kabila la Yosefu), Gadi mwana wa Susi;
from the tribe of Joseph, of the scepter of Manasseh, Gaddi the son of Susi;
12 kutoka kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemali;
from the tribe of Dan, Ammiel the son of Gemalli;
13 kutoka kabila la Asheri, Sethuri mwana wa Mikaeli;
from the tribe of Asher, Sethur the son of Michael;
14 kutoka kabila la Naftali, Nabi mwana wa Wofsi;
from the tribe of Naphtali, Nahbi the son of Vophsi;
15 kutoka kabila la Gadi, Geueli mwana wa Maki.
from the tribe of Gad, Guel the son of Machi.
16 Haya ndiyo majina ya watu ambao Mose aliwatuma kuipeleleza nchi. (Mose akampa Hoshea mwana wa Nuni jina Yoshua.)
These are the names of the men, whom Moses sent to examine the land. And he called Hosea, the son of Nun, Joshua.
17 Mose alipowatuma wakaipeleleze Kanaani, alisema, “Pandeni kupitia Negebu, mwende mpaka nchi ya vilima.
And so, Moses sent them to examine the land of Canaan, and he said to them: “Ascend by the south side. And when you arrive at the mountains,
18 Mwone nchi ni ya namna gani, na kama watu waishio humo wana nguvu au ni wadhaifu, iwapo ni wachache au wengi.
consider the land, as to what kind it may be, and the people, who are its inhabitants, whether they may be strong or weak, whether they may be few in number or many,
19 Wanaishi katika nchi ya namna gani? Je, ni nzuri au mbaya? Wanaishi katika miji ya namna gani? Je, haina kuta au ngome?
and the land itself, whether it is good or bad, what kind of cities, walled or without walls,
20 Ardhi iko aje? Ina rutuba au la? Je, kuna miti ndani yake au la? Jitahidini kadiri mwezavyo kuleta baadhi ya matunda ya nchi.” (Ulikuwa msimu wa kuiva zabibu za kwanza.)
the soil, rich or barren, forested or without trees. Be strong, and bring us some of the fruits of the land.” Now it was the time when the first ripe grapes were ready to be eaten.
21 Hivyo wakapanda na kuipeleleza nchi kutoka Jangwa la Sini hadi Rehobu, kuelekea Lebo-Hamathi.
And when they had ascended, they explored the land from the desert of Sin, all the way to Rehob, as one enters into Hamath.
22 Wakapanda kupitia Negebu hadi wakafika Hebroni, mahali ambapo Ahimani, Sheshai na Talmai, wazao wa Anaki, waliishi. (Hebroni ulikuwa umejengwa miaka saba kabla ya mji wa Soani ulioko Misri.)
And they ascended by the south side. And they arrived at Hebron, where there were Ahiman and Shishai and Talmai, the sons of Anak. For Hebron was founded seven years before Tanis, the city of Egypt.
23 Walipofika katika Bonde la Eshkoli, walivunja tawi lililokuwa na kishada kimoja cha zabibu. Wawili wao wakalichukua lile tawi kwenye mti, pamoja na komamanga na tini.
And continuing on as far as the Torrent of the Cluster of Grapes, they cut off a vine with its grapes, which two men carried on a board. Likewise, they took from the pomegranates and the figs of that place,
24 Eneo lile likaitwa Bonde la Eshkoli kwa sababu ya kile kishada cha zabibu ambacho Waisraeli walikikata huko.
which was called Nehel Eshcol, that is, the Torrent of the Cluster of Grapes, because the sons of Israel had carried a cluster of grapes from there.
25 Mwishoni mwa siku arobaini wakarudi kutoka kuipeleleza nchi.
And those exploring the land returned after forty days, having circulated through the entire region.
26 Wakarudi kwa Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli huko Kadeshi kwenye Jangwa la Parani. Hapo ndipo walipotoa habari kwao na kwa kusanyiko lote na kuwaonyesha matunda ya hiyo nchi.
And they went to Moses and Aaron, and to the entire assembly of the sons of Israel in the desert of Paran, which is in Kadesh. And speaking to them, and to the entire multitude, they showed them the fruits of the land.
27 Wakampa Mose taarifa hii: “Tuliingia katika nchi uliyotutuma, nayo inatiririka maziwa na asali! Hili hapa tunda lake.
And they explained, saying: “We went into the land, to which you sent us, which, it is true, flows with milk and honey, as one can know by these fruits.
28 Lakini watu wanaoishi huko ni wenye nguvu, na miji yao ina ngome na ni mikubwa sana. Huko tuliona hata wazao wa Anaki.
But it has very strong occupants, and the cities are great and also walled. We saw the race of Anak there.
29 Waamaleki wanaishi Negebu; Wahiti, Wayebusi na Waamori wanaishi katika nchi ya vilima; nao Wakanaani wanaishi karibu na bahari na kando ya Yordani.”
Amalek lives in the south. The Hethite, and the Jebusite, and the Amorite live in the mountains. And truly, the Canaanite stays near the sea and around the streams of the Jordan.”
30 Kisha Kalebu akawanyamazisha watu mbele ya Mose na kusema, “Imetupasa kupanda na kuimiliki nchi, kwa maana hakika tunaweza kufanya hivyo.”
During these events, Caleb, to restrain the murmuring of the people who rose up against Moses, said, “Let us ascend and possess the land, for we will be able to obtain it.”
31 Lakini watu waliokuwa wamepanda pamoja naye wakasema, “Hatuwezi kuwashambulia wale watu; wana nguvu kutuliko sisi.”
Yet truly, the others, who had been with him, were saying, “By no means are we able to ascend to this people, because they are stronger than we are.”
32 Wakaeneza taarifa mbaya miongoni mwa Waisraeli kuhusu nchi waliyoipeleleza. Wakasema, “Nchi tuliyoipeleleza hula watu waishio ndani yake. Watu wote tuliowaona huko ni majitu.
And before the sons of Israel they disparaged the land, which they had inspected, saying: “The land, which we viewed, devours its inhabitants. The people, upon whom we gazed, were of lofty stature.
33 Tuliwaona Wanefili huko (wazao wa Anaki wanatokana na Wanefili.) Tulijiona kama panzi machoni petu wenyewe, nao ndivyo walivyotuona.”
There, we saw some monsters among the sons of Anak, of the race of giants; by comparison with them, we seemed like locusts.”

< Hesabu 13 >