< Hesabu 11 >
1 Basi watu wakalalamika kwa habari ya taabu zao masikioni mwa Bwana, naye alipowasikia, hasira yake ikawaka. Ndipo moto kutoka kwa Bwana ukawaka miongoni mwao na kuteketeza baadhi ya viunga vya kambi.
Poslije stade se tužiti narod da mu je teško; a to ne bi po volji Gospodu; i kad Gospod èu, razgnjevi se; i raspali se na njih oganj Gospodnji, i sažeže krajnje u okolu.
2 Watu walipomlilia Mose, akamwomba Bwana, nao moto ukazimika.
Tada zavapi narod k Mojsiju, a Mojsije se pomoli Gospodu, i ugasi se oganj.
3 Hivyo mahali pale pakaitwa Tabera, kwa sababu moto kutoka kwa Bwana uliwaka miongoni mwao.
I prozva se ono mjesto Tavera, jer se raspali na njih oganj Gospodnji.
4 Umati wa watu wenye zogo waliokuwa miongoni mwao walitamani sana chakula kingine, Waisraeli wakaanza kulia tena na kusema, “Laiti tungekuwa na nyama tule!
A svjetina što bijaše meðu njima, bješe vrlo lakoma, te i sinovi Izrailjevi stadoše plakati govoreæi: ko æe nas nahraniti mesa?
5 Tunakumbuka wale samaki tuliokula huko Misri bila gharama, pia yale matango, matikitimaji, mboga, vitunguu, na vitunguu saumu.
Opomenusmo se riba što jeðasmo u Misiru zabadava, i krastavaca i dinja i luka crnoga i bijeloga.
6 Lakini sasa tumepoteza hamu ya chakula; hatuoni kitu kingine chochote isipokuwa hii mana!”
A sada posahnu duša naša, nema ništa osim mane pred oèima našima.
7 Mana ilifanana kama mbegu za giligilani, nayo ilikuwa na rangi ya manjano iliyopauka.
A mana bješe kao sjeme korijandrovo, a boja mu bješe kao boja u bdela.
8 Hao watu walikwenda kukusanya, kisha waliisaga kwa mawe ya kusagia ya mkono au kuitwanga kwenye vinu. Waliipika vyunguni au kutengeneza maandazi. Ladha yake ilikuwa kama kitu kilichotengenezwa kwa mafuta ya zeituni.
I izlažaše narod, te kupljahu, i meljahu na žrvnjima ili tucahu u stupama, i kuhahu u kotlu, ili miješahu pogaèe; a kus joj bijaše kao kus od novoga ulja.
9 Umande ulipoanguka kambini wakati wa usiku, pia mana ilianguka pamoja nao.
I kad padaše rosa po okolu noæu, padaše s njom i mana.
10 Mose akasikia watu wa kila jamaa wakilia, kila mmoja kwenye mlango wa hema lake. Bwana akakasirika mno, naye Mose akafadhaika.
I èu Mojsije gdje narod plaèe u porodicama svojim, svaki na vratima od šatora svojega; i Gospod se razgnjevi vrlo, i Mojsiju bi teško.
11 Akamuuliza Bwana, “Kwa nini umeleta taabu hii juu ya mtumishi wako? Nimekufanyia nini cha kukuchukiza hata ukaweka mzigo huu wa watu hawa wote juu yangu?
Pa reèe Mojsije Gospodu: zašto uèini tako zlo sluzi svojemu? i zašto ne naðoh milosti pred tobom, nego metnu na me teret svega naroda ovoga?
12 Je, watu hawa wote mimi ndiye niliyewatungisha mimba? Je, ni mimi niliyewazaa? Kwa nini unaniambia niwachukue mikononi mwangu, kama vile mlezi abebavyo mtoto mchanga, hadi kwenye nchi uliyowaahidi baba zao?
Eda li ja zaèeh sav ovaj narod? eda li ga ja rodih, kad mi kažeš: iznesi ga u naruèju svojem, kao što nosi dojilja dijete, u onu zemlju za koju si se zakleo ocima njihovijem.
13 Nitapata wapi nyama kwa ajili ya watu wote hawa? Wanaendelea kunililia wakisema, ‘Tupe nyama tule!’
Otkuda meni mesa da dam svemu ovom narodu? jer plaèu preda mnom govoreæi: daj nam mesa da jedemo.
14 Mimi siwezi kuwabeba watu hawa wote peke yangu, mzigo ni mzito sana kwangu.
Ne mogu ja sam nositi svega naroda ovoga, jer je teško za mene.
15 Kama hivi ndivyo unavyonitendea, uniue sasa hivi, yaani kama nimepata kibali machoni pako, wala usiniache nione maangamizi yangu mwenyewe.”
Ako æeš tako èiniti sa mnom, ubij me bolje, ako sam našao milost pred tobom, da ne gledam zla svojega.
16 Bwana akamwambia Mose: “Niletee wazee sabini wa Israeli, unaowafahamu kama viongozi na maafisa miongoni mwa watu. Walete katika Hema la Kukutania, ili waweze kusimama huko pamoja nawe.
A Gospod reèe Mojsiju: saberi mi sedamdeset ljudi izmeðu starješina Izrailjevijeh, koje znaš da su starješine narodu i upravitelji njegovi, i dovedi ih k šatoru od sastanka, neka ondje stanu s tobom.
17 Nami nitashuka na kusema nawe huko. Nami nitachukua sehemu ya Roho iliyo juu yako na kuiweka juu yao. Watakusaidia kubeba mzigo wa watu hao ili usije ukaubeba peke yako.
Tada æu siæi i govoriti ondje s tobom, i uzeæu od duha koji je na tebi i metnuæu na njih, da nose s tobom teret narodni i da ne nosiš ti sam.
18 “Waambie hao watu: ‘Jiwekeni wakfu wenyewe kwa ajili ya kesho, wakati mtakapokula nyama. Bwana aliwasikia mlipolia, mkisema, “Laiti tungekuwa na nyama tule! Tulikuwa na hali nzuri zaidi katika nchi ya Misri!” Sasa Bwana atawapa nyama, nanyi mtaila.
A narodu reci: pripravite se za sjutra da jedete mesa, jer plakaste da Gospod èu, i rekoste: ko æe nas nahraniti mesa? jer nam dobro bijaše u Misiru. Daæe vam dakle Gospod mesa i ješæete.
19 Hamtaila kwa siku moja tu, au siku mbili, au tano, kumi au siku ishirini,
Neæete jesti jedan dan, ni dva dana, ni pet dana, ni deset dana, ni dvadeset dana;
20 bali kwa mwezi mzima mpaka iwatokee puani, nanyi mtaichukia kabisa, kwa kuwa mmemkataa Bwana, ambaye yupo miongoni mwenu, nanyi mmelia mbele zake, mkisema, “Hivi kwa nini tulitoka Misri?”’”
Nego cio mjesec dana, dokle vam na nos ne udari i ne ogadi vam se, zato što odbaciste Gospoda koji je meðu vama i plakaste pred njim govoreæi: zašto izidosmo iz Misira?
21 Lakini Mose alisema, “Mimi niko hapa miongoni mwa watu 600,000 wanaotembea kwa miguu, nawe umesema, ‘Nitawapa nyama ya kula kwa mwezi mzima!’
A Mojsije reèe: šest stotina tisuæa pješaka ima naroda, u kojem sam, pa ti kažeš: daæu im mesa da jedu cio mjesec dana.
22 Je, wangeweza kupata nyama ya kuwatosha hata kama makundi ya kondoo na ya ngʼombe yangechinjwa kwa ajili yao? Je, wangetosheka hata kama samaki wote wa baharini wangevuliwa kwa ajili yao?”
Eda li æe im se poklati ovce i goveda da im dostane? ili æe im se pokupiti sve ribe morske da im bude dosta?
23 Bwana akamjibu Mose, “Je, mkono wa Bwana ni mfupi sana? Sasa utaona kama jambo nililolisema litatimizwa kwa ajili yako au la.”
A Gospod reèe Mojsiju: zar ruka Gospodnja neæe biti dovoljna? Vidjeæeš hoæe li biti što ti rekoh ili neæe.
24 Kwa hiyo Mose akatoka na kuwaambia watu lile ambalo Bwana alikuwa amesema. Akawakusanya wazee wao sabini, akawasimamisha kuzunguka Hema.
I Mojsije izide i reèe narodu rijeèi Gospodnje; i sabra sedamdeset ljudi izmeðu starješina narodnijeh, i postavi ih oko šatora.
25 Kisha Bwana akashuka katika wingu na kunena na Mose, naye akachukua sehemu ya Roho iliyokuwa juu ya Mose na kuiweka juu ya wale wazee sabini. Roho aliposhuka juu yao, wakatoa unabii, lakini hawakufanya hivyo tena.
I Gospod siðe u oblaku, i govori k njemu, i uzevši od duha koji bješe na njemu metnu na onijeh sedamdeset ljudi starješina; i kad duh doðe na njih, prorokovahu, ali više nikad.
26 Lakini, watu wawili, ambao majina yao ni Eldadi na Medadi, walibaki kambini. Walikuwa wameorodheshwa miongoni mwa wale wazee sabini, lakini hawakutoka kwenda kwenye Hema. Lakini Roho pia alishuka juu yao, nao wakatabiri huko kambini.
A dva èovjeka ostaše u okolu, jednom bješe ime Eldad, a drugom Modad, na koje doðe duh, jer i oni bijahu zapisani ali ne doðoše k šatoru, i stadoše prorokovati u okolu.
27 Mwanaume mmoja kijana alikimbia na kumwambia Mose, “Eldadi na Medadi wanatoa unabii kambini.”
I dotrèa momak, te javi Mojsiju govoreæi: Eldad i Modad prorokuju u okolu.
28 Yoshua mwana wa Nuni, ambaye alikuwa msaidizi wa Mose tangu ujana wake, akajibu akasema, “Mose bwana wangu, wanyamazishe!”
A Isus sin Navin, sluga Mojsijev, jedan od momaka njegovijeh, reèe govoreæi: Mojsije gospodaru moj, zabrani im.
29 Lakini Mose akajibu, “Je, unaona wivu kwa ajili yangu? Ningetamani watu wote wa Bwana wangekuwa manabii na kwamba Bwana angeweka Roho yake juu yao!”
A Mojsije mu odgovori: zar zavidiš mene radi? kamo da sav narod Gospodnji postanu proroci i da Gospod pusti duh svoj na njih!
30 Ndipo Mose na wale wazee wa Israeli wakarudi kambini.
Potom se vrati Mojsije u oko sa starješinama Izrailjevijem.
31 Kisha ukatokea upepo kutoka kwa Bwana, nao ukawaletea kware kutoka baharini. Ukawaangusha kwenye eneo lote linalozunguka kambi na kujaa ardhini kimo cha mita moja hivi kutoka ardhini kwenye eneo la umbali wa mwendo wa siku moja kila upande.
Tada se podiže vjetar od Gospoda, i potjera od mora prepelice, i razasu ih po okolu, na dan hoda odovuda i na dan hoda odonuda oko okola, na dva lakta od zemlje.
32 Mchana kutwa na usiku kucha pamoja na siku nzima iliyofuata watu walitoka kwenda kuokota kware. Hakuna mtu yeyote aliyekusanya chini ya homeri kumi. Kisha wakazianika kuzunguka kambi yote.
I ustavši narod vas onaj dan i svu noæ i vas drugi dan kupljaše prepelice: i ko nakupi najmanje nakupi deset gomora; i povješaše ih sebi redom oko okola.
33 Lakini walipokuwa wakila nyama, ilipokuwa ingali kati ya meno yao na kabla hawajamaliza kula, hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya watu, naye akawapiga kwa tauni.
Ali meso još im bijaše u zubima, jošte ga ne pojedoše, a Gospod se razgnjevi na narod, i udari Gospod narod pomorom vrlo velikim.
34 Kwa hiyo mahali hapo pakaitwa Kibroth-Hataava, kwa sababu huko ndiko walipowazika watu ambao walitamani sana chakula kingine.
I prozva se ono mjesto Kivrot-Atava jer ondje ukopaše narod koji se bješe polakomio.
35 Kutoka Kibroth-Hataava watu wakasafiri mpaka Haserothi na kukaa huko.
I poðe narod od Kivrot-Atave u Asirot, i stadoše u Asirotu.