< Hesabu 11 >
1 Basi watu wakalalamika kwa habari ya taabu zao masikioni mwa Bwana, naye alipowasikia, hasira yake ikawaka. Ndipo moto kutoka kwa Bwana ukawaka miongoni mwao na kuteketeza baadhi ya viunga vya kambi.
As pessoas estavam reclamando nos ouvidos de Yahweh. Quando Javé ouviu isso, sua raiva queimou; e o fogo de Javé queimou entre eles, e consumiu alguns dos arredores do acampamento.
2 Watu walipomlilia Mose, akamwomba Bwana, nao moto ukazimika.
O povo chorou a Moisés; e Moisés orou a Javé, e o fogo diminuiu.
3 Hivyo mahali pale pakaitwa Tabera, kwa sababu moto kutoka kwa Bwana uliwaka miongoni mwao.
O nome daquele lugar foi chamado Taberah, porque o fogo de Iavé queimou entre eles.
4 Umati wa watu wenye zogo waliokuwa miongoni mwao walitamani sana chakula kingine, Waisraeli wakaanza kulia tena na kusema, “Laiti tungekuwa na nyama tule!
A multidão mista que estava entre eles cobiçava demais; e os filhos de Israel também choraram novamente, e disseram: “Quem nos dará carne para comer?
5 Tunakumbuka wale samaki tuliokula huko Misri bila gharama, pia yale matango, matikitimaji, mboga, vitunguu, na vitunguu saumu.
Recordamos o peixe, que comemos no Egito por nada; os pepinos, e os melões, e os alhos-porros, e as cebolas, e o alho;
6 Lakini sasa tumepoteza hamu ya chakula; hatuoni kitu kingine chochote isipokuwa hii mana!”
mas agora perdemos o apetite. Não há nada além deste maná para se olhar”.
7 Mana ilifanana kama mbegu za giligilani, nayo ilikuwa na rangi ya manjano iliyopauka.
O maná era como uma semente de coentro, e parecia bdellium.
8 Hao watu walikwenda kukusanya, kisha waliisaga kwa mawe ya kusagia ya mkono au kuitwanga kwenye vinu. Waliipika vyunguni au kutengeneza maandazi. Ladha yake ilikuwa kama kitu kilichotengenezwa kwa mafuta ya zeituni.
As pessoas foram em volta, o colheram e o moeram em moinhos, ou o bateram em argamassas, e o cozeram em panelas, e fizeram bolos com ele. Seu sabor era como o sabor do óleo fresco.
9 Umande ulipoanguka kambini wakati wa usiku, pia mana ilianguka pamoja nao.
Quando o orvalho caiu no acampamento durante a noite, o maná caiu sobre ele.
10 Mose akasikia watu wa kila jamaa wakilia, kila mmoja kwenye mlango wa hema lake. Bwana akakasirika mno, naye Mose akafadhaika.
Moisés ouviu as pessoas chorando em suas famílias, cada homem à porta de sua tenda; e a raiva de Javé ardeu muito; e Moisés ficou descontente.
11 Akamuuliza Bwana, “Kwa nini umeleta taabu hii juu ya mtumishi wako? Nimekufanyia nini cha kukuchukiza hata ukaweka mzigo huu wa watu hawa wote juu yangu?
Moisés disse a Javé: “Por que você tem tratado tão mal seu servo? Por que não encontrei favor em sua visão, que você me impôs o fardo de todo este povo?
12 Je, watu hawa wote mimi ndiye niliyewatungisha mimba? Je, ni mimi niliyewazaa? Kwa nini unaniambia niwachukue mikononi mwangu, kama vile mlezi abebavyo mtoto mchanga, hadi kwenye nchi uliyowaahidi baba zao?
Será que eu concebi todo este povo? Se os trouxe para fora, que me diga: 'Carregue-os em seu seio, como uma enfermeira carrega uma criança amamentada, para a terra que você jurou aos pais deles'?
13 Nitapata wapi nyama kwa ajili ya watu wote hawa? Wanaendelea kunililia wakisema, ‘Tupe nyama tule!’
Onde eu poderia conseguir carne para dar a todas essas pessoas? Pois eles choram diante de mim, dizendo: 'Dê-nos carne, para que possamos comer'.
14 Mimi siwezi kuwabeba watu hawa wote peke yangu, mzigo ni mzito sana kwangu.
Não sou capaz de suportar toda esta gente sozinha, porque é muito pesada para mim.
15 Kama hivi ndivyo unavyonitendea, uniue sasa hivi, yaani kama nimepata kibali machoni pako, wala usiniache nione maangamizi yangu mwenyewe.”
Se você me tratar desta maneira, por favor, mate-me agora mesmo, se eu encontrei favor em sua vista; e não me deixe ver minha miséria”.
16 Bwana akamwambia Mose: “Niletee wazee sabini wa Israeli, unaowafahamu kama viongozi na maafisa miongoni mwa watu. Walete katika Hema la Kukutania, ili waweze kusimama huko pamoja nawe.
Yahweh disse a Moisés: “Reuni a mim setenta homens dos anciãos de Israel, que vós sabeis ser os anciãos do povo e oficiais sobre eles; e levai-os à Tenda da Reunião, para que estejam ali convosco.
17 Nami nitashuka na kusema nawe huko. Nami nitachukua sehemu ya Roho iliyo juu yako na kuiweka juu yao. Watakusaidia kubeba mzigo wa watu hao ili usije ukaubeba peke yako.
Eu descerei e falarei com vocês lá. Tomarei do Espírito que está sobre vós, e o porei sobre eles; e eles carregarão o fardo do povo convosco, para que não o carregueis sozinhos.
18 “Waambie hao watu: ‘Jiwekeni wakfu wenyewe kwa ajili ya kesho, wakati mtakapokula nyama. Bwana aliwasikia mlipolia, mkisema, “Laiti tungekuwa na nyama tule! Tulikuwa na hali nzuri zaidi katika nchi ya Misri!” Sasa Bwana atawapa nyama, nanyi mtaila.
“Digam ao povo: 'Santificai-vos em preparação para o amanhã, e comereis carne; pois chorastes aos ouvidos de Javé, dizendo: “Quem nos dará carne para comer? Pois foi bom para nós no Egito”. Portanto, Javé vos dará carne e vós comereis.
19 Hamtaila kwa siku moja tu, au siku mbili, au tano, kumi au siku ishirini,
Você não comerá apenas um dia, ou dois dias, ou cinco dias, ou dez dias, ou vinte dias,
20 bali kwa mwezi mzima mpaka iwatokee puani, nanyi mtaichukia kabisa, kwa kuwa mmemkataa Bwana, ambaye yupo miongoni mwenu, nanyi mmelia mbele zake, mkisema, “Hivi kwa nini tulitoka Misri?”’”
mas um mês inteiro, até que saia em suas narinas, e é repugnante para você; porque você rejeitou Yahweh que está entre vocês, e chorou diante dele, dizendo: “Por que saímos do Egito””.
21 Lakini Mose alisema, “Mimi niko hapa miongoni mwa watu 600,000 wanaotembea kwa miguu, nawe umesema, ‘Nitawapa nyama ya kula kwa mwezi mzima!’
Moisés disse: “O povo, entre os quais estou, são seiscentos mil homens a pé; e você disse: 'Eu lhes darei carne, para que possam comer um mês inteiro'.
22 Je, wangeweza kupata nyama ya kuwatosha hata kama makundi ya kondoo na ya ngʼombe yangechinjwa kwa ajili yao? Je, wangetosheka hata kama samaki wote wa baharini wangevuliwa kwa ajili yao?”
Shall rebanhos e rebanhos são abatidos para eles, para que sejam suficientes para eles? Todos os peixes do mar devem ser reunidos para eles, para que sejam suficientes para eles”?
23 Bwana akamjibu Mose, “Je, mkono wa Bwana ni mfupi sana? Sasa utaona kama jambo nililolisema litatimizwa kwa ajili yako au la.”
Yahweh disse a Moisés: “A mão de Yahweh ficou curta? Agora você vai ver se minha palavra vai acontecer com você ou não”.
24 Kwa hiyo Mose akatoka na kuwaambia watu lile ambalo Bwana alikuwa amesema. Akawakusanya wazee wao sabini, akawasimamisha kuzunguka Hema.
Moisés saiu e contou ao povo as palavras de Javé; e reuniu setenta homens dos anciãos do povo, e os colocou em torno da Tenda.
25 Kisha Bwana akashuka katika wingu na kunena na Mose, naye akachukua sehemu ya Roho iliyokuwa juu ya Mose na kuiweka juu ya wale wazee sabini. Roho aliposhuka juu yao, wakatoa unabii, lakini hawakufanya hivyo tena.
Yahweh desceu na nuvem, falou com ele, tomou do Espírito que estava sobre ele, e o colocou sobre os setenta anciãos. Quando o Espírito descansou sobre eles, eles profetizaram, mas eles não o fizeram mais.
26 Lakini, watu wawili, ambao majina yao ni Eldadi na Medadi, walibaki kambini. Walikuwa wameorodheshwa miongoni mwa wale wazee sabini, lakini hawakutoka kwenda kwenye Hema. Lakini Roho pia alishuka juu yao, nao wakatabiri huko kambini.
Mas dois homens permaneceram no acampamento. O nome de um era Eldad, e o nome do outro Medad; e o Espírito repousou sobre eles. Eles eram daqueles que foram escritos, mas não tinham saído para a Tenda; e profetizaram no acampamento.
27 Mwanaume mmoja kijana alikimbia na kumwambia Mose, “Eldadi na Medadi wanatoa unabii kambini.”
Um jovem correu, disse a Moisés, e disse: “Eldad e Medad profetizam no acampamento”.
28 Yoshua mwana wa Nuni, ambaye alikuwa msaidizi wa Mose tangu ujana wake, akajibu akasema, “Mose bwana wangu, wanyamazishe!”
Josué, filho de Freira, o servo de Moisés, um de seus escolhidos, respondeu: “Meu senhor Moisés, proíbe-os”!
29 Lakini Mose akajibu, “Je, unaona wivu kwa ajili yangu? Ningetamani watu wote wa Bwana wangekuwa manabii na kwamba Bwana angeweka Roho yake juu yao!”
Moisés lhe disse: “Você está com ciúmes por minha causa? Gostaria que todo o povo de Javé fosse profetas, que Javé colocasse seu Espírito sobre eles”!
30 Ndipo Mose na wale wazee wa Israeli wakarudi kambini.
Moisés foi para o campo, ele e os anciãos de Israel.
31 Kisha ukatokea upepo kutoka kwa Bwana, nao ukawaletea kware kutoka baharini. Ukawaangusha kwenye eneo lote linalozunguka kambi na kujaa ardhini kimo cha mita moja hivi kutoka ardhini kwenye eneo la umbali wa mwendo wa siku moja kila upande.
Um vento de Javé saiu e trouxe codornizes do mar, e as deixou cair junto ao acampamento, cerca de um dia de viagem deste lado, e um dia de viagem do outro lado, ao redor do acampamento, e cerca de dois cúbitos acima da superfície da terra.
32 Mchana kutwa na usiku kucha pamoja na siku nzima iliyofuata watu walitoka kwenda kuokota kware. Hakuna mtu yeyote aliyekusanya chini ya homeri kumi. Kisha wakazianika kuzunguka kambi yote.
O povo levantou-se todo aquele dia, e toda aquela noite, e todo o dia seguinte, e juntou as codornizes. Aquele que menos reuniu dez pessoas, e as espalhou por si mesmo ao redor do acampamento.
33 Lakini walipokuwa wakila nyama, ilipokuwa ingali kati ya meno yao na kabla hawajamaliza kula, hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya watu, naye akawapiga kwa tauni.
Enquanto a carne ainda estava entre seus dentes, antes de ser mastigada, a raiva de Yahweh queimou contra o povo, e Yahweh atingiu o povo com uma praga muito grande.
34 Kwa hiyo mahali hapo pakaitwa Kibroth-Hataava, kwa sababu huko ndiko walipowazika watu ambao walitamani sana chakula kingine.
O nome daquele lugar se chamava Kibroth Hattaavah, porque ali enterraram as pessoas que cobiçavam.
35 Kutoka Kibroth-Hataava watu wakasafiri mpaka Haserothi na kukaa huko.
De Kibroth Hattaavah, as pessoas viajaram para Hazeroth; e ficaram em Hazeroth.