< Hesabu 11 >

1 Basi watu wakalalamika kwa habari ya taabu zao masikioni mwa Bwana, naye alipowasikia, hasira yake ikawaka. Ndipo moto kutoka kwa Bwana ukawaka miongoni mwao na kuteketeza baadhi ya viunga vya kambi.
Cependant il s’éleva un murmure du peuple contre le Seigneur, comme se plaignant de la fatigue. Le Seigneur l’ayant entendu, fut irrité; et le feu du Seigneur allumé contre eux, dévora l’extrémité du camp.
2 Watu walipomlilia Mose, akamwomba Bwana, nao moto ukazimika.
Alors, comme le peuple cria vers Moïse, Moïse pria le Seigneur, et le feu s’éteignit.
3 Hivyo mahali pale pakaitwa Tabera, kwa sababu moto kutoka kwa Bwana uliwaka miongoni mwao.
Et il appela ce lieu du nom d’Embrasement, parce que le feu du Seigneur s’y était allumé contre eux.
4 Umati wa watu wenye zogo waliokuwa miongoni mwao walitamani sana chakula kingine, Waisraeli wakaanza kulia tena na kusema, “Laiti tungekuwa na nyama tule!
Car une foule de gens de toute espèce, qui étaient montés avec eux, s’enflamma de convoitise, s’asseyant et pleurant, et les enfants d’Israël s’étant joints aussi à elle, elle dit: Qui nous donnera de la chair à manger?
5 Tunakumbuka wale samaki tuliokula huko Misri bila gharama, pia yale matango, matikitimaji, mboga, vitunguu, na vitunguu saumu.
Nous nous souvenons des poissons que nous mangions en Egypte pour rien: ils nous viennent à l’esprit, les concombres, les melons, les poireaux, les ognons et les aulx.
6 Lakini sasa tumepoteza hamu ya chakula; hatuoni kitu kingine chochote isipokuwa hii mana!”
Notre âme est aride: nos yeux ne voient que la manne.
7 Mana ilifanana kama mbegu za giligilani, nayo ilikuwa na rangi ya manjano iliyopauka.
Or la manne était comme de la graine de coriandre, de la couleur du bdellium.
8 Hao watu walikwenda kukusanya, kisha waliisaga kwa mawe ya kusagia ya mkono au kuitwanga kwenye vinu. Waliipika vyunguni au kutengeneza maandazi. Ladha yake ilikuwa kama kitu kilichotengenezwa kwa mafuta ya zeituni.
Et le peuple allait autour du camp, et la recueillant, il la brisait sous la meule, ou il la pilait dans le mortier, la cuisant dans la marmite, et en faisant de petites miches d’une saveur semblable à celle du pain pétri avec de l’huile.
9 Umande ulipoanguka kambini wakati wa usiku, pia mana ilianguka pamoja nao.
Et lorsque la rosée descendait pendant la nuit sur le camp, la manne aussi descendait pareillement.
10 Mose akasikia watu wa kila jamaa wakilia, kila mmoja kwenye mlango wa hema lake. Bwana akakasirika mno, naye Mose akafadhaika.
Moïse entendit donc le peuple pleurant dans les familles, chacun à la porte de sa tente. Alors la fureur du Seigneur fut extrêmement irritée; et la chose parut aussi à Moïse insupportable.
11 Akamuuliza Bwana, “Kwa nini umeleta taabu hii juu ya mtumishi wako? Nimekufanyia nini cha kukuchukiza hata ukaweka mzigo huu wa watu hawa wote juu yangu?
Et il dit au Seigneur: Pourquoi avez-vous affligé votre serviteur? pourquoi ne trouvé-je point grâce devant vous? et pourquoi avez-vous mis le poids de tout ce peuple sur moi?
12 Je, watu hawa wote mimi ndiye niliyewatungisha mimba? Je, ni mimi niliyewazaa? Kwa nini unaniambia niwachukue mikononi mwangu, kama vile mlezi abebavyo mtoto mchanga, hadi kwenye nchi uliyowaahidi baba zao?
Est-ce moi qui ai conçu toute cette multitude, ou qui l’ai engendrée, pour que vous me disiez: Porte-les dans ton sein, comme la nourrice a coutume de porter son petit enfant, et conduis-les dans la terre au sujet de laquelle vous avez juré à leurs pères?
13 Nitapata wapi nyama kwa ajili ya watu wote hawa? Wanaendelea kunililia wakisema, ‘Tupe nyama tule!’
D’où aurai-je de la chair pour en donner à une si grande multitude? ils pleurent contre moi, disant: Donne-nous de la chair, afin que nous en mangions.
14 Mimi siwezi kuwabeba watu hawa wote peke yangu, mzigo ni mzito sana kwangu.
Je ne puis seul soutenir tout ce peuple; parce qu’il est lourd pour moi.
15 Kama hivi ndivyo unavyonitendea, uniue sasa hivi, yaani kama nimepata kibali machoni pako, wala usiniache nione maangamizi yangu mwenyewe.”
S’il ne vous en semble pas autrement, je demande instamment que vous me fassiez mourir, et que je trouve grâce à vos yeux, pour que je ne sois pas accablé de tant de maux.
16 Bwana akamwambia Mose: “Niletee wazee sabini wa Israeli, unaowafahamu kama viongozi na maafisa miongoni mwa watu. Walete katika Hema la Kukutania, ili waweze kusimama huko pamoja nawe.
Et le Seigneur répondit à Moïse: Assemble-moi soixante dix hommes d’entre les anciens d’Israël, que tu sais être les anciens du peuple et les maîtres; et tu les conduiras à la porte du tabernacle d’alliance, et tu les feras rester là avec toi,
17 Nami nitashuka na kusema nawe huko. Nami nitachukua sehemu ya Roho iliyo juu yako na kuiweka juu yao. Watakusaidia kubeba mzigo wa watu hao ili usije ukaubeba peke yako.
Pour que je descende et que je te parle, que je prenne ton esprit et que je leur donne, afin qu’ils soutiennent avec toi le fardeau du peuple, et que toi seul, tu ne sois pas surchargé.
18 “Waambie hao watu: ‘Jiwekeni wakfu wenyewe kwa ajili ya kesho, wakati mtakapokula nyama. Bwana aliwasikia mlipolia, mkisema, “Laiti tungekuwa na nyama tule! Tulikuwa na hali nzuri zaidi katika nchi ya Misri!” Sasa Bwana atawapa nyama, nanyi mtaila.
Tu diras aussi au peuple: Sanctifiez-vous, demain vous mangerez de la chair. Car moi-même je vous ai entendu dire: Qui nous donnera des aliments de chair? Nous étions bien en Egypte. Ainsi le Seigneur vous donnera de la chair, afin que vous en mangiez,
19 Hamtaila kwa siku moja tu, au siku mbili, au tano, kumi au siku ishirini,
Non pas un jour, ni deux, ni cinq, ni dix, ni même vingt.
20 bali kwa mwezi mzima mpaka iwatokee puani, nanyi mtaichukia kabisa, kwa kuwa mmemkataa Bwana, ambaye yupo miongoni mwenu, nanyi mmelia mbele zake, mkisema, “Hivi kwa nini tulitoka Misri?”’”
Mais pendant un mois de jours, jusqu’à ce qu’elle sorte par vos narines, qu’elle devienne nauséabonde, parce que vous avez rejeté le Seigneur, qui est au milieu de vous, et que vous avez pleuré devant lui, disant: Pourquoi sommes-nous sortis de l’Egypte?
21 Lakini Mose alisema, “Mimi niko hapa miongoni mwa watu 600,000 wanaotembea kwa miguu, nawe umesema, ‘Nitawapa nyama ya kula kwa mwezi mzima!’
Et Moïse dit: Il y a six cent mille hommes de pied dans ce peuple, et vous dites: Je leur donnerai des aliments de chair pendant un mois entier.
22 Je, wangeweza kupata nyama ya kuwatosha hata kama makundi ya kondoo na ya ngʼombe yangechinjwa kwa ajili yao? Je, wangetosheka hata kama samaki wote wa baharini wangevuliwa kwa ajili yao?”
Est-ce qu’une multitude de brebis et de bœufs sera tuée, pour suffire à leur nourriture? ou bien tous les poissons de la mer seront-ils réunis, afin de les rassasier?
23 Bwana akamjibu Mose, “Je, mkono wa Bwana ni mfupi sana? Sasa utaona kama jambo nililolisema litatimizwa kwa ajili yako au la.”
Le Seigneur lui répondit: Est-ce que la main du Seigneur est impuissante? Dès à présent tu verras si ma parole se réalisera.
24 Kwa hiyo Mose akatoka na kuwaambia watu lile ambalo Bwana alikuwa amesema. Akawakusanya wazee wao sabini, akawasimamisha kuzunguka Hema.
Moïse vint donc et rapporta au peuple les paroles du Seigneur, rassemblant soixante-dix hommes d’entre les anciens d’Israël, qu’il plaça autour du tabernacle.
25 Kisha Bwana akashuka katika wingu na kunena na Mose, naye akachukua sehemu ya Roho iliyokuwa juu ya Mose na kuiweka juu ya wale wazee sabini. Roho aliposhuka juu yao, wakatoa unabii, lakini hawakufanya hivyo tena.
Alors le Seigneur descendit dans la nuée, et parla à Moïse, prenant de l’esprit qui était en lui, et le donnant aux soixante-dix hommes. Or, lorsque l’Esprit se fut reposé en eux, ils prophétisèrent et ne cessèrent plus.
26 Lakini, watu wawili, ambao majina yao ni Eldadi na Medadi, walibaki kambini. Walikuwa wameorodheshwa miongoni mwa wale wazee sabini, lakini hawakutoka kwenda kwenye Hema. Lakini Roho pia alishuka juu yao, nao wakatabiri huko kambini.
Mais il était demeuré dans le camp deux hommes, dont l’un s’appelait Eldad, et l’autre Médad: l’Esprit se reposa sur eux; car ils avaient été enregistrés, et ils n’étaient pas sortis pour aller au tabernacle.
27 Mwanaume mmoja kijana alikimbia na kumwambia Mose, “Eldadi na Medadi wanatoa unabii kambini.”
Et, comme ils prophétisaient dans le camp, un enfant courut et l’annonça à Moïse, disant: Eldad et Médad prophétisent dans le camp.
28 Yoshua mwana wa Nuni, ambaye alikuwa msaidizi wa Mose tangu ujana wake, akajibu akasema, “Mose bwana wangu, wanyamazishe!”
Aussitôt Josué, fils de Nun, serviteur de Moïse, et choisi dans le plus grand nombre, dit: Mon seigneur Moïse, empêchez-les.
29 Lakini Mose akajibu, “Je, unaona wivu kwa ajili yangu? Ningetamani watu wote wa Bwana wangekuwa manabii na kwamba Bwana angeweka Roho yake juu yao!”
Mais Moïse: Pourquoi, dit-il, es-tu jaloux pour moi? Plût à Dieu que tout le peuple prophétisât, et que le Seigneur leur donnât son esprit!
30 Ndipo Mose na wale wazee wa Israeli wakarudi kambini.
Et Moïse revint, ainsi que les anciens d’Israël, dans le camp.
31 Kisha ukatokea upepo kutoka kwa Bwana, nao ukawaletea kware kutoka baharini. Ukawaangusha kwenye eneo lote linalozunguka kambi na kujaa ardhini kimo cha mita moja hivi kutoka ardhini kwenye eneo la umbali wa mwendo wa siku moja kila upande.
Mais un vent envoyé par le Seigneur, saisissant des cailles au-delà de la mer, les porta et les abattit dans le camp, de tout côté autour du camp, dans l’espace du chemin qu’on peut faire en un jour; et elles volaient en l’air à la hauteur de deux coudées au-dessus de la terre.
32 Mchana kutwa na usiku kucha pamoja na siku nzima iliyofuata watu walitoka kwenda kuokota kware. Hakuna mtu yeyote aliyekusanya chini ya homeri kumi. Kisha wakazianika kuzunguka kambi yote.
Le peuple, se levant donc durant tout ce jour-là, toute la nuit, et le jour suivant, amassa des cailles, chacun au moins dix mesures; et ils les firent sécher autour du camp.
33 Lakini walipokuwa wakila nyama, ilipokuwa ingali kati ya meno yao na kabla hawajamaliza kula, hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya watu, naye akawapiga kwa tauni.
La chair était encore en leurs dents, et cet aliment n’était pas achevé; et voilà que la fureur du Seigneur excitée contre le peuple, le frappa d’une très grande plaie.
34 Kwa hiyo mahali hapo pakaitwa Kibroth-Hataava, kwa sababu huko ndiko walipowazika watu ambao walitamani sana chakula kingine.
Aussi ce lieu fut-il appelé: Sépulcres de la concupiscence; là, en effet, on ensevelit le peuple qui avait désiré de la chair. Mais sortis des Sépulcres de la concupiscence, ils vinrent à Haséroth et y demeurèrent.
35 Kutoka Kibroth-Hataava watu wakasafiri mpaka Haserothi na kukaa huko.

< Hesabu 11 >