< Hesabu 11 >
1 Basi watu wakalalamika kwa habari ya taabu zao masikioni mwa Bwana, naye alipowasikia, hasira yake ikawaka. Ndipo moto kutoka kwa Bwana ukawaka miongoni mwao na kuteketeza baadhi ya viunga vya kambi.
Or le peuple fut comme des gens qui se plaignent d'un malheur, aux oreilles de l'Éternel; et l'Éternel l'entendit, et sa colère s'embrasa, et le feu de l'Éternel s'alluma parmi eux et dévora à l'extrémité du camp.
2 Watu walipomlilia Mose, akamwomba Bwana, nao moto ukazimika.
Alors le peuple cria à Moïse, et Moïse pria l'Éternel, et le feu s'arrêta.
3 Hivyo mahali pale pakaitwa Tabera, kwa sababu moto kutoka kwa Bwana uliwaka miongoni mwao.
Et l'on nomma ce lieu Thabéera (incendie), parce que le feu de l'Éternel s'était allumé parmi eux.
4 Umati wa watu wenye zogo waliokuwa miongoni mwao walitamani sana chakula kingine, Waisraeli wakaanza kulia tena na kusema, “Laiti tungekuwa na nyama tule!
Et le ramassis d'étrangers qui était parmi eux se livra à la convoitise; et même les enfants d'Israël se mirent de nouveau à pleurer, et dirent: Qui nous fera manger de la chair?
5 Tunakumbuka wale samaki tuliokula huko Misri bila gharama, pia yale matango, matikitimaji, mboga, vitunguu, na vitunguu saumu.
Il nous souvient des poissons que nous mangions en Égypte, pour rien; des concombres, des melons, des poireaux, des oignons et des aulx.
6 Lakini sasa tumepoteza hamu ya chakula; hatuoni kitu kingine chochote isipokuwa hii mana!”
Et maintenant, notre âme est desséchée; il n'y a rien du tout! Nos yeux ne voient que la manne.
7 Mana ilifanana kama mbegu za giligilani, nayo ilikuwa na rangi ya manjano iliyopauka.
Or la manne était comme de la semence de coriandre, et sa couleur, comme celle du bdellion.
8 Hao watu walikwenda kukusanya, kisha waliisaga kwa mawe ya kusagia ya mkono au kuitwanga kwenye vinu. Waliipika vyunguni au kutengeneza maandazi. Ladha yake ilikuwa kama kitu kilichotengenezwa kwa mafuta ya zeituni.
Le peuple se dispersait et la ramassait; puis il la broyait avec les meules, ou la pilait dans un mortier, et la faisait cuire dans un chaudron, et en faisait des gâteaux; et le goût en était semblable à celui d'un gâteau à l'huile.
9 Umande ulipoanguka kambini wakati wa usiku, pia mana ilianguka pamoja nao.
Et quand la rosée tombait la nuit sur le camp, la manne descendait dessus.
10 Mose akasikia watu wa kila jamaa wakilia, kila mmoja kwenye mlango wa hema lake. Bwana akakasirika mno, naye Mose akafadhaika.
Moïse entendit donc le peuple qui pleurait dans ses familles, chacun à l'entrée de sa tente; et la colère de l'Éternel s'embrasa fortement, et Moïse en fut affligé.
11 Akamuuliza Bwana, “Kwa nini umeleta taabu hii juu ya mtumishi wako? Nimekufanyia nini cha kukuchukiza hata ukaweka mzigo huu wa watu hawa wote juu yangu?
Et Moïse dit à l'Éternel: Pourquoi as-tu affligé ton serviteur; et pourquoi n'ai-je pas trouvé grâce devant tes y eux, que tu aies mis sur moi la charge de tout ce peuple?
12 Je, watu hawa wote mimi ndiye niliyewatungisha mimba? Je, ni mimi niliyewazaa? Kwa nini unaniambia niwachukue mikononi mwangu, kama vile mlezi abebavyo mtoto mchanga, hadi kwenye nchi uliyowaahidi baba zao?
Est-ce moi qui ai conçu tout ce peuple, ou l'ai-je engendré, que tu me dises: Porte-le dans ton sein, comme le nourricier porte l'enfant qui tète, jusqu'au pays que tu as promis par serment à ses pères?
13 Nitapata wapi nyama kwa ajili ya watu wote hawa? Wanaendelea kunililia wakisema, ‘Tupe nyama tule!’
D'où aurais-je de la chair pour en donner à tout ce peuple? Car il pleure après moi, en disant: Donne-nous de la chair, que nous mangions.
14 Mimi siwezi kuwabeba watu hawa wote peke yangu, mzigo ni mzito sana kwangu.
Je ne puis, moi seul, porter tout ce peuple; car il est trop pesant pour moi.
15 Kama hivi ndivyo unavyonitendea, uniue sasa hivi, yaani kama nimepata kibali machoni pako, wala usiniache nione maangamizi yangu mwenyewe.”
Que si tu agis ainsi à mon égard, tue-moi, je te prie, si j'ai trouvé grâce à tes yeux; et que je ne voie point mon malheur.
16 Bwana akamwambia Mose: “Niletee wazee sabini wa Israeli, unaowafahamu kama viongozi na maafisa miongoni mwa watu. Walete katika Hema la Kukutania, ili waweze kusimama huko pamoja nawe.
Alors l'Éternel dit à Moïse: Assemble-moi soixante et dix hommes, d'entre les anciens d'Israël, que tu connais pour être les anciens du peuple, et préposés sur lui; amène-les au tabernacle d'assignation, et qu'ils se tiennent là avec toi.
17 Nami nitashuka na kusema nawe huko. Nami nitachukua sehemu ya Roho iliyo juu yako na kuiweka juu yao. Watakusaidia kubeba mzigo wa watu hao ili usije ukaubeba peke yako.
Puis je descendrai, et là je parlerai avec toi; je mettrai à part de l'esprit qui est sur toi, et je le mettrai sur eux, afin qu'ils portent avec toi la charge du peuple, et que tu ne la portes pas toi seul.
18 “Waambie hao watu: ‘Jiwekeni wakfu wenyewe kwa ajili ya kesho, wakati mtakapokula nyama. Bwana aliwasikia mlipolia, mkisema, “Laiti tungekuwa na nyama tule! Tulikuwa na hali nzuri zaidi katika nchi ya Misri!” Sasa Bwana atawapa nyama, nanyi mtaila.
Et tu diras au peuple: Sanctifiez-vous pour demain et vous mangerez de la chair. Parce que vous avez pleuré aux oreilles de l'Éternel, en disant: Qui nous fera manger de la chair? car nous étions bien en Égypte; l'Éternel vous donnera de la chair et vous en mangerez.
19 Hamtaila kwa siku moja tu, au siku mbili, au tano, kumi au siku ishirini,
Vous n'en mangerez pas un jour, ni deux jours, ni cinq jours, ni dix jours, ni vingt jours;
20 bali kwa mwezi mzima mpaka iwatokee puani, nanyi mtaichukia kabisa, kwa kuwa mmemkataa Bwana, ambaye yupo miongoni mwenu, nanyi mmelia mbele zake, mkisema, “Hivi kwa nini tulitoka Misri?”’”
Mais jusqu'à un mois entier, jusqu'à ce qu'elle vous sorte par les narines, et que vous en soyez dégoûtés, parce que vous avez rejeté l'Éternel qui est au milieu de vous, et que vous avez pleuré devant lui, en disant: Pourquoi donc sommes-nous sortis d'Égypte?
21 Lakini Mose alisema, “Mimi niko hapa miongoni mwa watu 600,000 wanaotembea kwa miguu, nawe umesema, ‘Nitawapa nyama ya kula kwa mwezi mzima!’
Et Moïse dit: Il y a six cent mille hommes de pied dans ce peuple, au milieu duquel je suis; et tu as dit: Je leur donnerai de la chair, et ils en mangeront un mois entier.
22 Je, wangeweza kupata nyama ya kuwatosha hata kama makundi ya kondoo na ya ngʼombe yangechinjwa kwa ajili yao? Je, wangetosheka hata kama samaki wote wa baharini wangevuliwa kwa ajili yao?”
Leur égorgera-t-on des brebis et des bœufs, en sorte qu'il y en ait assez pour eux? ou leur assemblera-t-on tous les poissons de la mer, en sorte qu'il y en ait assez pour eux?
23 Bwana akamjibu Mose, “Je, mkono wa Bwana ni mfupi sana? Sasa utaona kama jambo nililolisema litatimizwa kwa ajili yako au la.”
Et l'Éternel répondit à Moïse: La main de l'Éternel est-elle raccourcie? Tu verras maintenant si ce que je t'ai dit, arrivera ou non.
24 Kwa hiyo Mose akatoka na kuwaambia watu lile ambalo Bwana alikuwa amesema. Akawakusanya wazee wao sabini, akawasimamisha kuzunguka Hema.
Moïse sortit donc et rapporta au peuple les paroles de l'Éternel; et il assembla soixante et dix hommes d'entre les anciens du peuple, et les plaça tout autour du tabernacle.
25 Kisha Bwana akashuka katika wingu na kunena na Mose, naye akachukua sehemu ya Roho iliyokuwa juu ya Mose na kuiweka juu ya wale wazee sabini. Roho aliposhuka juu yao, wakatoa unabii, lakini hawakufanya hivyo tena.
Alors l'Éternel descendit dans la nuée, et lui parla, et il mit à part de l'esprit qui était sur lui, et le mit sur les soixante et dix anciens. Et dès que l'esprit reposa sur eux, ils prophétisèrent; mais ils ne continuèrent pas.
26 Lakini, watu wawili, ambao majina yao ni Eldadi na Medadi, walibaki kambini. Walikuwa wameorodheshwa miongoni mwa wale wazee sabini, lakini hawakutoka kwenda kwenye Hema. Lakini Roho pia alishuka juu yao, nao wakatabiri huko kambini.
Or il en était demeuré deux au camp, dont l'un s'appelait Eldad, et l'autre Médad, et l'esprit reposa sur eux; or ils étaient de ceux qui avaient été inscrits, mais ils n'étaient point sortis vers le tabernacle; et ils prophétisèrent dans le camp.
27 Mwanaume mmoja kijana alikimbia na kumwambia Mose, “Eldadi na Medadi wanatoa unabii kambini.”
Et un jeune garçon courut le rapporter à Moïse, et dit: Eldad et Médad prophétisent dans le camp.
28 Yoshua mwana wa Nuni, ambaye alikuwa msaidizi wa Mose tangu ujana wake, akajibu akasema, “Mose bwana wangu, wanyamazishe!”
Et Josué, fils de Nun, serviteur de Moïse, dès sa jeunesse, répondit, et dit: Moïse, mon seigneur, empêche-les!
29 Lakini Mose akajibu, “Je, unaona wivu kwa ajili yangu? Ningetamani watu wote wa Bwana wangekuwa manabii na kwamba Bwana angeweka Roho yake juu yao!”
Et Moïse lui répondit: Es-tu jaloux pour moi? Plût à Dieu de tout, que le peuple de l'Éternel fût prophète, et que l'Éternel mît son esprit sur eux!
30 Ndipo Mose na wale wazee wa Israeli wakarudi kambini.
Et Moïse se retira au camp, lui et les anciens d'Israël.
31 Kisha ukatokea upepo kutoka kwa Bwana, nao ukawaletea kware kutoka baharini. Ukawaangusha kwenye eneo lote linalozunguka kambi na kujaa ardhini kimo cha mita moja hivi kutoka ardhini kwenye eneo la umbali wa mwendo wa siku moja kila upande.
Alors l'Éternel fit lever un vent, qui enleva des cailles de la mer, et les répandit sur le camp, environ le chemin d'une journée, d'un côté et de l'autre, tout autour du camp, et presque deux coudées de haut sur la terre.
32 Mchana kutwa na usiku kucha pamoja na siku nzima iliyofuata watu walitoka kwenda kuokota kware. Hakuna mtu yeyote aliyekusanya chini ya homeri kumi. Kisha wakazianika kuzunguka kambi yote.
Et le peuple se leva, tout ce jour-là, et toute la nuit, et tout le jour suivant, et ils amassèrent les cailles; celui qui en amassa le moins, en avait dix homers, et ils les étendirent pour eux, tout autour du camp.
33 Lakini walipokuwa wakila nyama, ilipokuwa ingali kati ya meno yao na kabla hawajamaliza kula, hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya watu, naye akawapiga kwa tauni.
La chair était encore entre leurs dents, elle n'était pas encore mâchée, que la colère de l'Éternel s'embrasa contre le peuple, et l'Éternel frappa le peuple d'une très grande plaie.
34 Kwa hiyo mahali hapo pakaitwa Kibroth-Hataava, kwa sababu huko ndiko walipowazika watu ambao walitamani sana chakula kingine.
Et l'on nomma ce lieu-là Kibroth-Hatthaava (tombeaux de la convoitise); car on ensevelit là le peuple qui avait convoité.
35 Kutoka Kibroth-Hataava watu wakasafiri mpaka Haserothi na kukaa huko.
De Kibroth-Hatthaava le peuple partit pour Hatséroth; et ils s'arrêtèrent à Hatséroth.