< Hesabu 11 >

1 Basi watu wakalalamika kwa habari ya taabu zao masikioni mwa Bwana, naye alipowasikia, hasira yake ikawaka. Ndipo moto kutoka kwa Bwana ukawaka miongoni mwao na kuteketeza baadhi ya viunga vya kambi.
Le peuple se plaignait aux oreilles de l'Éternel. Lorsque l'Éternel l'entendit, sa colère s'enflamma; le feu de l'Éternel brûla au milieu d'eux et consuma une partie des abords du camp.
2 Watu walipomlilia Mose, akamwomba Bwana, nao moto ukazimika.
Le peuple cria à Moïse; Moïse pria l'Éternel, et le feu s'apaisa.
3 Hivyo mahali pale pakaitwa Tabera, kwa sababu moto kutoka kwa Bwana uliwaka miongoni mwao.
On donna à ce lieu le nom de Tabérah, parce que le feu de Yahvé brûlait au milieu d'eux.
4 Umati wa watu wenye zogo waliokuwa miongoni mwao walitamani sana chakula kingine, Waisraeli wakaanza kulia tena na kusema, “Laiti tungekuwa na nyama tule!
La multitude mélangée qui était au milieu d'eux se livra à des excès de luxure; et les enfants d'Israël pleurèrent de nouveau, et dirent: Qui nous donnera de la viande à manger?
5 Tunakumbuka wale samaki tuliokula huko Misri bila gharama, pia yale matango, matikitimaji, mboga, vitunguu, na vitunguu saumu.
Nous nous souvenons du poisson que nous avons mangé pour rien en Égypte, des concombres, des melons, des poireaux, des oignons et de l'ail;
6 Lakini sasa tumepoteza hamu ya chakula; hatuoni kitu kingine chochote isipokuwa hii mana!”
mais maintenant nous avons perdu l'appétit. Il n'y a rien du tout, sauf cette manne, à regarder ».
7 Mana ilifanana kama mbegu za giligilani, nayo ilikuwa na rangi ya manjano iliyopauka.
La manne était semblable à de la graine de coriandre, et elle ressemblait à du bdellium.
8 Hao watu walikwenda kukusanya, kisha waliisaga kwa mawe ya kusagia ya mkono au kuitwanga kwenye vinu. Waliipika vyunguni au kutengeneza maandazi. Ladha yake ilikuwa kama kitu kilichotengenezwa kwa mafuta ya zeituni.
Le peuple la parcourait, la ramassait, la broyait dans des moulins, la battait dans des mortiers, la faisait bouillir dans des marmites et en faisait des gâteaux. Son goût était comme celui de l'huile fraîche.
9 Umande ulipoanguka kambini wakati wa usiku, pia mana ilianguka pamoja nao.
Lorsque la rosée tombait sur le camp pendant la nuit, la manne y tombait.
10 Mose akasikia watu wa kila jamaa wakilia, kila mmoja kwenye mlango wa hema lake. Bwana akakasirika mno, naye Mose akafadhaika.
Moïse entendit le peuple pleurer dans toute sa famille, chacun à l'entrée de sa tente; la colère de Yahvé s'enflamma, et Moïse fut mécontent.
11 Akamuuliza Bwana, “Kwa nini umeleta taabu hii juu ya mtumishi wako? Nimekufanyia nini cha kukuchukiza hata ukaweka mzigo huu wa watu hawa wote juu yangu?
Moïse dit à Yahvé: « Pourquoi as-tu traité ton serviteur si mal? Pourquoi n'ai-je pas trouvé grâce à tes yeux, pour que tu fasses peser sur moi le poids de tout ce peuple?
12 Je, watu hawa wote mimi ndiye niliyewatungisha mimba? Je, ni mimi niliyewazaa? Kwa nini unaniambia niwachukue mikononi mwangu, kama vile mlezi abebavyo mtoto mchanga, hadi kwenye nchi uliyowaahidi baba zao?
Ai-je conçu tout ce peuple? Les ai-je fait sortir pour que tu me dises: Porte-les dans ton sein, comme une nourrice porte un nourrisson, jusqu'au pays que tu as juré à leurs pères?
13 Nitapata wapi nyama kwa ajili ya watu wote hawa? Wanaendelea kunililia wakisema, ‘Tupe nyama tule!’
Où pourrais-je trouver de la viande pour donner à tous ces gens? Car ils pleurent devant moi en disant: « Donne-nous de la viande, que nous puissions manger.
14 Mimi siwezi kuwabeba watu hawa wote peke yangu, mzigo ni mzito sana kwangu.
Je ne suis pas capable de porter tout ce peuple tout seul, car c'est trop lourd pour moi.
15 Kama hivi ndivyo unavyonitendea, uniue sasa hivi, yaani kama nimepata kibali machoni pako, wala usiniache nione maangamizi yangu mwenyewe.”
Si tu me traites ainsi, tue-moi tout de suite, si j'ai trouvé grâce à tes yeux, et ne me laisse pas voir ma misère. »
16 Bwana akamwambia Mose: “Niletee wazee sabini wa Israeli, unaowafahamu kama viongozi na maafisa miongoni mwa watu. Walete katika Hema la Kukutania, ili waweze kusimama huko pamoja nawe.
Yahvé dit à Moïse: « Rassemble auprès de moi soixante-dix hommes parmi les anciens d'Israël, que tu connais comme étant les anciens du peuple et ses dirigeants, et amène-les à la tente de la Rencontre, afin qu'ils s'y tiennent avec toi.
17 Nami nitashuka na kusema nawe huko. Nami nitachukua sehemu ya Roho iliyo juu yako na kuiweka juu yao. Watakusaidia kubeba mzigo wa watu hao ili usije ukaubeba peke yako.
Je descendrai et je vous parlerai là. Je prendrai de l'Esprit qui est sur toi et je le mettrai sur eux; ils porteront avec toi le fardeau du peuple, afin que tu ne le portes pas seul.
18 “Waambie hao watu: ‘Jiwekeni wakfu wenyewe kwa ajili ya kesho, wakati mtakapokula nyama. Bwana aliwasikia mlipolia, mkisema, “Laiti tungekuwa na nyama tule! Tulikuwa na hali nzuri zaidi katika nchi ya Misri!” Sasa Bwana atawapa nyama, nanyi mtaila.
« Dis au peuple: « Sanctifiez-vous en prévision de demain, et vous mangerez de la viande; car vous avez pleuré aux oreilles de Yahvé, en disant: « Qui nous donnera de la viande à manger? Car vous avez pleuré aux oreilles de Yahvé, en disant: « Qui nous donnera de la viande à manger, car nous étions bien en Égypte? ». C'est pourquoi l'Éternel vous donnera de la viande, et vous mangerez.
19 Hamtaila kwa siku moja tu, au siku mbili, au tano, kumi au siku ishirini,
Vous ne mangerez pas un jour, ni deux jours, ni cinq jours, ni dix jours, ni vingt jours,
20 bali kwa mwezi mzima mpaka iwatokee puani, nanyi mtaichukia kabisa, kwa kuwa mmemkataa Bwana, ambaye yupo miongoni mwenu, nanyi mmelia mbele zake, mkisema, “Hivi kwa nini tulitoka Misri?”’”
mais un mois entier, jusqu'à ce qu'elle vous vienne aux narines et qu'elle vous soit répugnante; car vous avez rejeté l'Éternel qui est au milieu de vous, et vous avez pleuré devant lui, en disant: « Pourquoi sommes-nous sortis d'Égypte? »".
21 Lakini Mose alisema, “Mimi niko hapa miongoni mwa watu 600,000 wanaotembea kwa miguu, nawe umesema, ‘Nitawapa nyama ya kula kwa mwezi mzima!’
Moïse dit: « Le peuple au milieu duquel je suis est composé de six cent mille hommes à pied; et tu as dit: « Je leur donnerai de la viande, pour qu'ils mangent un mois entier ».
22 Je, wangeweza kupata nyama ya kuwatosha hata kama makundi ya kondoo na ya ngʼombe yangechinjwa kwa ajili yao? Je, wangetosheka hata kama samaki wote wa baharini wangevuliwa kwa ajili yao?”
Abattra-t-on pour eux des brebis et des bœufs, pour qu'ils en aient assez? Est-ce qu'on rassemblera pour eux tous les poissons de la mer, pour qu'ils en aient assez? ».
23 Bwana akamjibu Mose, “Je, mkono wa Bwana ni mfupi sana? Sasa utaona kama jambo nililolisema litatimizwa kwa ajili yako au la.”
Yahvé dit à Moïse: « La main de Yahvé est-elle devenue courte? Tu verras maintenant si ma parole s'accomplira pour toi ou non. »
24 Kwa hiyo Mose akatoka na kuwaambia watu lile ambalo Bwana alikuwa amesema. Akawakusanya wazee wao sabini, akawasimamisha kuzunguka Hema.
Moïse sortit, et rapporta au peuple les paroles de Yahvé. Il rassembla soixante-dix hommes parmi les anciens du peuple, et les plaça autour de la Tente.
25 Kisha Bwana akashuka katika wingu na kunena na Mose, naye akachukua sehemu ya Roho iliyokuwa juu ya Mose na kuiweka juu ya wale wazee sabini. Roho aliposhuka juu yao, wakatoa unabii, lakini hawakufanya hivyo tena.
Yahvé descendit dans la nuée et lui parla; il prit de l'Esprit qui était sur lui et le mit sur les soixante-dix anciens. Lorsque l'Esprit reposa sur eux, ils prophétisèrent, mais ils ne le firent plus.
26 Lakini, watu wawili, ambao majina yao ni Eldadi na Medadi, walibaki kambini. Walikuwa wameorodheshwa miongoni mwa wale wazee sabini, lakini hawakutoka kwenda kwenye Hema. Lakini Roho pia alishuka juu yao, nao wakatabiri huko kambini.
Mais deux hommes restèrent dans le camp. Le nom de l'un était Eldad, et le nom de l'autre Médad; et l'Esprit reposa sur eux. Ils étaient de ceux qui avaient été écrits, mais qui n'étaient pas sortis pour aller à la Tente; et ils prophétisaient dans le camp.
27 Mwanaume mmoja kijana alikimbia na kumwambia Mose, “Eldadi na Medadi wanatoa unabii kambini.”
Un jeune homme courut en informer Moïse, et dit: « Eldad et Médad prophétisent dans le camp! »
28 Yoshua mwana wa Nuni, ambaye alikuwa msaidizi wa Mose tangu ujana wake, akajibu akasema, “Mose bwana wangu, wanyamazishe!”
Josué, fils de Nun, serviteur de Moïse, l'un de ses hommes d'élite, répondit: « Mon seigneur Moïse, interdis-leur! »
29 Lakini Mose akajibu, “Je, unaona wivu kwa ajili yangu? Ningetamani watu wote wa Bwana wangekuwa manabii na kwamba Bwana angeweka Roho yake juu yao!”
Moïse lui dit: « Es-tu jaloux à cause de moi? Je voudrais que tout le peuple de Yahvé soit prophète, que Yahvé mette son Esprit sur eux! ».
30 Ndipo Mose na wale wazee wa Israeli wakarudi kambini.
Moïse entra dans le camp, lui et les anciens d'Israël.
31 Kisha ukatokea upepo kutoka kwa Bwana, nao ukawaletea kware kutoka baharini. Ukawaangusha kwenye eneo lote linalozunguka kambi na kujaa ardhini kimo cha mita moja hivi kutoka ardhini kwenye eneo la umbali wa mwendo wa siku moja kila upande.
Un vent de Yahvé sortit et fit sortir de la mer des cailles qu'il laissa tomber près du camp, à environ un jour de marche de ce côté et un jour de marche de l'autre côté, autour du camp, et à environ deux coudées au-dessus de la surface de la terre.
32 Mchana kutwa na usiku kucha pamoja na siku nzima iliyofuata watu walitoka kwenda kuokota kware. Hakuna mtu yeyote aliyekusanya chini ya homeri kumi. Kisha wakazianika kuzunguka kambi yote.
Le peuple se leva tout ce jour-là, toute cette nuit-là et tout le lendemain, et il ramassa les cailles. Celui qui en ramassait le moins en ramassait dix, et ils se les répartirent autour du camp.
33 Lakini walipokuwa wakila nyama, ilipokuwa ingali kati ya meno yao na kabla hawajamaliza kula, hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya watu, naye akawapiga kwa tauni.
Comme la viande était encore entre leurs dents, avant qu'ils l'aient mâchée, la colère de l'Éternel s'enflamma contre le peuple, et l'Éternel frappa le peuple d'une très grande plaie.
34 Kwa hiyo mahali hapo pakaitwa Kibroth-Hataava, kwa sababu huko ndiko walipowazika watu ambao walitamani sana chakula kingine.
On donna à ce lieu le nom de Kibroth Hattaavah, parce qu'on y enterra le peuple qui avait eu de la convoitise.
35 Kutoka Kibroth-Hataava watu wakasafiri mpaka Haserothi na kukaa huko.
De Kibroth Hattaavah, le peuple se rendit à Hatséroth, et il resta à Hatséroth.

< Hesabu 11 >