< Hesabu 10 >

1 Bwana akamwambia Mose:
Gospod je spregovoril Mojzesu, rekoč:
2 “Tengeneza tarumbeta mbili za fedha ya kufua, uzitumie kwa kuita jumuiya pamoja na wakati wa kuvunja makambi ili kuondoka.
»Naredi si dve srebrni trobenti. Iz celega kosa ju boš izdelal, da ju boste lahko uporabljali za sklic zbora in za potovanje taborov.
3 Tarumbeta zote mbili zikipigwa, jumuiya yote itakusanyika mbele yako katika ingilio la Hema la Kukutania.
Ko bodo z njima zatrobili, se bo ves zbor zbral k tebi pri vratih šotorskega svetišča skupnosti.
4 Kama tarumbeta moja tu ikipigwa, viongozi, yaani wakuu wa koo za Israeli, ndio watakaokusanyika mbele yako.
Če bodo trobili samo z eno trobento, potem se bodo princi, ki so poglavarji tisočerih Izraelovih, skupaj zbrali k tebi.
5 Wakati mlio wa kujulisha hatari ukipigwa, makabila yaliyo na makambi upande wa mashariki yataondoka.
Kadar zatrobite alarm, potem bodo tabori, ki taborijo na vzhodnih delih, odšli naprej.
6 Ukisikika mlio wa pili wa jinsi hiyo, walioko kwenye makambi ya kusini wataondoka. Mlio huo wa kujulisha hatari utakuwa ishara ya kuondoka.
Kadar drugič zatrobite alarm, potem se bodo tabori, ki taborijo na južni strani, odpravili na svoje potovanje; zaradi njihovih potovanj bodo trobili alarm.
7 Ili kukusanya kusanyiko, piga tarumbeta zote, lakini siyo kwa mlio wa kujulisha hatari.
Toda ko naj bi se skupnost zbrala skupaj, boste trobili, toda ne boste razglasili alarma.
8 “Wana wa Aroni, makuhani, ndio watakaopiga hizo tarumbeta. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu na kwa vizazi vijavyo.
Aronovi sinovi, duhovniki, bodo trobili s trobentami in oni vam bodo za odredbo na veke skozi vaše rodove.
9 Wakati mtakapopigana vita katika nchi yenu wenyewe dhidi ya adui anayewaonea, piga tarumbeta kwa mlio wa kujulisha hatari. Ndipo utakumbukwa na Bwana Mungu wenu na kuokolewa kutoka kwa adui zenu.
Če greste v svoji deželi na vojno zoper sovražnika, ki vas zatira, potem boste s trobentami trobili alarm in Gospod, vaš Bog, se vas bo spomnil in rešeni boste pred svojimi sovražniki.
10 Pia nyakati za furaha yenu, yaani sikukuu zenu zilizoamriwa na sikukuu za Mwezi Mwandamo, mtapiga tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za amani, nazo zitakuwa ukumbusho kwa ajili yenu mbele za Mungu wenu. Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.”
Tudi na dan vašega veselja in na vaše slovesne dneve in ob začetkih mesecev boste s trobentami trobili nad svojimi žgalnimi daritvami in nad žrtvovanji svojih mirovnih daritev, da vam bodo za spomin pred vašim Bogom. Jaz sem Gospod, vaš Bog.«
11 Katika siku ya ishirini ya mwezi wa pili wa mwaka wa pili, wingu liliinuka kutoka juu ya maskani ya Ushuhuda.
Pripetilo se je na dvajseti dan drugega meseca, v drugem letu, da je bil oblak dvignjen iznad šotorskega svetišča pričevanja.
12 Ndipo Waisraeli wakaondoka kutoka Jangwa la Sinai wakasafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine mpaka wingu lilipotua katika Jangwa la Parani.
Izraelovi otroci so se odpravili na svoja potovanja iz Sinajske divjine in oblak je obstal v Paránski divjini.
13 Waliondoka kwa mara ya kwanza kwa agizo la Bwana kupitia kwa Mose.
Prvič so se odpravili na svoje potovanje glede na Gospodovo zapoved, po Mojzesovi roki.
14 Vikosi vya kambi ya Yuda vilitangulia kwanza chini ya alama yao. Nashoni mwana wa Aminadabu alikuwa kiongozi wao.
Prvi je odšel prapor tabora Judovih otrok, glede na njihove vojske in nad njegovo vojsko je bil Aminadábov sin Nahšón.
15 Nethaneli mwana wa Suari alikuwa kiongozi wa kabila la Isakari,
Nad vojsko rodu Isahárjevih otrok je bil Cuárjev sin Netanél.
16 naye Eliabu mwana wa Heloni alikuwa kiongozi wa kabila la Zabuloni.
Nad vojsko rodu Zábulonovih otrok je bil Helónov sin Eliáb.
17 Ndipo Maskani iliposhushwa, nao wana wa Gershoni na wana wa Merari ambao waliibeba wakaondoka.
Šotorsko svetišče je bilo podrto, in Geršónovi sinovi in Meraríjevi sinovi so se odpravili naprej, noseč šotorsko svetišče.
18 Vikosi vya kambi ya Reubeni vilifuata, chini ya alama yao. Elisuri mwana wa Shedeuri alikuwa kiongozi wao.
Prapor Rubenovega tabora se je odpravil naprej, glede na njihove vojske in nad njegovo vojsko je bil Šedeúrjev sin Elicúr.
19 Shelumieli mwana wa Surishadai aliongoza kikosi cha kabila la Simeoni,
Nad vojsko rodu Simeonovih otrok je bil Curišadájev sin Šelumiél.
20 naye Eliasafu mwana wa Deueli aliongoza kikosi cha kabila la Gadi.
Nad vojsko rodu Gadovih otrok je bil Deguélov sin Eljasáf.
21 Kisha Wakohathi wakaondoka, wakichukua vitu vitakatifu. Maskani ilikuwa isimamishwe kabla wao hawajafika.
Kehátovci so se odpravili naprej, noseč svetišče, drugi pa so postavili šotorsko svetišče preden so ti prišli.
22 Vikosi vya kambi ya Efraimu vilifuata, chini ya alama yao. Elishama mwana wa Amihudi alikuwa kiongozi wao.
Prapor tabora Efrájimovih otrok se je odpravil naprej glede na njihove vojske in nad njegovo vojsko je bil Amihúdov sin Elišamá.
23 Gamalieli mwana wa Pedasuri aliongoza kikosi cha kabila la Manase,
Nad vojsko rodu Manásejevih otrok je bil Pedacúrjev sin Gamliél.
24 naye Abidani mwana wa Gideoni alikuwa kiongozi wa kikosi cha kabila la Benyamini.
Nad vojsko rodu Benjaminovih otrok je bil Gideoníjev sin Abidán.
25 Mwishowe, kama kikosi cha nyuma cha ulinzi wa vikosi vyote, vikosi vya kambi ya Dani viliondoka chini ya alama yao. Ahiezeri mwana wa Amishadai alikuwa kiongozi wao.
Prapor tabora Danovih otrok se je odpravil naprej, ki je bil zadnja straža vseh taborov po njihovih vojskah. In nad njegovo vojsko je bil Amišadájev sin Ahiézer.
26 Pagieli mwana wa Okrani aliongoza kikosi cha kabila la Asheri,
Nad vojsko rodu Aserjevih otrok je bil Ohránov sin Pagiél.
27 naye Ahira mwana wa Enani aliongoza kikosi cha kabila la Naftali.
Nad vojsko rodu Neftálijevih otrok je bil Enánov sin Ahirá.
28 Huu ndio ulikuwa utaratibu wa kuondoka wa vikosi vya Waisraeli walipokuwa wanaondoka.
Takšna so bila potovanja Izraelovih otrok glede na njihove vojske, ko so se odpravili naprej.
29 Basi Mose akamwambia Hobabu mwana wa Reueli, Mmidiani, mkwewe Mose, “Tunaondoka kwenda mahali ambapo Bwana amesema ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’ Twende pamoja nasi tutakutendea mema, kwa maana Bwana ameahidi mambo mema kwa Israeli.”
Mojzes je rekel Hobábu, sinu Midjánca Reguéla, Mojzesovega tasta: »Potujemo proti kraju, o katerem je Gospod rekel: ›Jaz vam ga bom dal.‹ Pridi z nami in mi ti bomo storili dobro, kajti Gospod je dobro govoril glede Izraela.«
30 Akajibu, “Hapana, sitakwenda; nitarudi kwenye nchi yangu mwenyewe na watu wangu mwenyewe.”
Ta pa mu je rekel: »Ne bom šel, temveč bom odšel k svoji lastni deželi in k svojemu sorodstvu.«
31 Lakini Mose akasema, “Tafadhali usituache. Wewe unajua mahali ambapo yatupasa kupiga kambi jangwani, nawe unaweza kuwa macho yetu.
Rekel je: »Ne zapusti nas, prosim te, ker veš kako naj taborimo v divjini in ti si nam lahko namesto oči.
32 Ikiwa utafuatana nasi, tutashirikiana nawe mema yoyote tutakayopewa na Bwana.”
In zgodilo se bo, če greš z nami, da, zgodilo se bo, da kakršna bo Gospodova dobrota do nas, isto bomo mi storili tebi.«
33 Hivyo waliondoka kutoka mlima wa Bwana, nao wakasafiri kwa siku tatu. Sanduku la Agano la Bwana liliwatangulia kwa zile siku tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika.
Odpravili so se od Gospodove gore tri dni potovanja in skrinja Gospodove zaveze je šla pred njimi na tridnevno potovanje, da zanje poišče počivališče.
34 Wingu la Bwana lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka kambini.
Gospodov oblak je bil nad njimi podnevi, ko so odšli iz tabora.
35 Wakati wowote Sanduku lilipoondoka, Mose alisema, “Ee Bwana, inuka! Watesi wako na watawanyike; adui zako na wakimbie mbele zako.”
Kadar je skrinja krenila na pot, se je pripetilo, da je Mojzes rekel: »Vstani, Gospod in razkrope naj se tvoji sovražniki in tisti, ki te sovražijo, naj zbežijo pred teboj.«
36 Wakati wowote Sanduku liliposimama, alisema, “Ee Bwana, rudi, kwa maelfu ya Waisraeli wasiohesabika.”
Ko pa je ta počivala, je rekel: »Vrni se, oh Gospod, k mnogim Izraelovim tisočerim.«

< Hesabu 10 >