< Hesabu 10 >

1 Bwana akamwambia Mose:
Et l'Éternel parla à Moïse en ces termes:
2 “Tengeneza tarumbeta mbili za fedha ya kufua, uzitumie kwa kuita jumuiya pamoja na wakati wa kuvunja makambi ili kuondoka.
Fais-toi deux trompettes d'argent; tu leur donneras la façon d'ouvrage fait autour; elles te serviront pour convoquer l'Assemblée, et indiquer le décampement.
3 Tarumbeta zote mbili zikipigwa, jumuiya yote itakusanyika mbele yako katika ingilio la Hema la Kukutania.
Et quand on en sonnera [des deux], toute l'Assemblée se réunira auprès de toi à la porte de la Tente du Rendez-vous.
4 Kama tarumbeta moja tu ikipigwa, viongozi, yaani wakuu wa koo za Israeli, ndio watakaokusanyika mbele yako.
Et quand on sonnera d'une seule, les Princes, les chefs des divisions d'Israël se réuniront auprès de toi.
5 Wakati mlio wa kujulisha hatari ukipigwa, makabila yaliyo na makambi upande wa mashariki yataondoka.
Et quand vous sonnerez la charge, ceux-là lèveront le camp, qui campent à l'orient.
6 Ukisikika mlio wa pili wa jinsi hiyo, walioko kwenye makambi ya kusini wataondoka. Mlio huo wa kujulisha hatari utakuwa ishara ya kuondoka.
Et quand vous sonnerez la charge pour, la seconde fois, ceux-là lèveront le camp, qui campent au midi; vous sonnerez la charge lors de votre décampement.
7 Ili kukusanya kusanyiko, piga tarumbeta zote, lakini siyo kwa mlio wa kujulisha hatari.
Mais pour convoquer l'Assemblée, vous sonnerez des trompettes, mais non pas la charge.
8 “Wana wa Aroni, makuhani, ndio watakaopiga hizo tarumbeta. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu na kwa vizazi vijavyo.
Et ce sont les fils d'Aaron, les Prêtres, qui sonneront des trompettes; elles sont instituées à perpétuité chez vous pour vos âges futurs.
9 Wakati mtakapopigana vita katika nchi yenu wenyewe dhidi ya adui anayewaonea, piga tarumbeta kwa mlio wa kujulisha hatari. Ndipo utakumbukwa na Bwana Mungu wenu na kuokolewa kutoka kwa adui zenu.
Et quand vous vous mettrez en campagne dans votre pays contre vos agresseurs qui vous attaqueront, vous sonnerez la charge avec les trompettes, et votre souvenir sera rappelé devant l'Éternel, votre Dieu, et vous serez délivrés de vos ennemis.
10 Pia nyakati za furaha yenu, yaani sikukuu zenu zilizoamriwa na sikukuu za Mwezi Mwandamo, mtapiga tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za amani, nazo zitakuwa ukumbusho kwa ajili yenu mbele za Mungu wenu. Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.”
Et dans vos jours de réjouissance, et dans vos solennités et à vos Nouvelles Lunes vous sonnerez des trompettes en offrant vos holocaustes et vos sacrifices pacifiques, afin qu'elles rappellent votre souvenir devant votre Dieu. Je suis l'Éternel, votre Dieu.
11 Katika siku ya ishirini ya mwezi wa pili wa mwaka wa pili, wingu liliinuka kutoka juu ya maskani ya Ushuhuda.
Et la seconde année, au second mois, le vingtième jour du mois, la nuée s'éleva de dessus la Résidence du Témoignage.
12 Ndipo Waisraeli wakaondoka kutoka Jangwa la Sinai wakasafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine mpaka wingu lilipotua katika Jangwa la Parani.
Et les enfants d'Israël partirent, selon l'ordre de leurs départs, du désert de Sinaï, et la nuée s'arrêta dans le désert de Paran.
13 Waliondoka kwa mara ya kwanza kwa agizo la Bwana kupitia kwa Mose.
Ils firent ce premier décampement sur l'ordre de l'Éternel transmis par Moïse,
14 Vikosi vya kambi ya Yuda vilitangulia kwanza chini ya alama yao. Nashoni mwana wa Aminadabu alikuwa kiongozi wao.
et d'abord partit la bannière du camp des fils de Juda rangés par divisions, et leur corps d'armée était sous Nahesson, fils de Amminadab,
15 Nethaneli mwana wa Suari alikuwa kiongozi wa kabila la Isakari,
et le corps d'armée de la Tribu des fils d'Issaschar, sous Nethanéel, fils de Tsuhar,
16 naye Eliabu mwana wa Heloni alikuwa kiongozi wa kabila la Zabuloni.
et le corps d'armée de la Tribu des fils de Zabulon, sous Eliab, fils de Hélon.
17 Ndipo Maskani iliposhushwa, nao wana wa Gershoni na wana wa Merari ambao waliibeba wakaondoka.
Puis la Résidence fut démontée, et partirent les fils de Gerson, et les fils de Merari, portant la Résidence.
18 Vikosi vya kambi ya Reubeni vilifuata, chini ya alama yao. Elisuri mwana wa Shedeuri alikuwa kiongozi wao.
Alors partit la bannière du camp de Ruben rangé par divisions, et son corps d'armée était sous Elitsur, fils de Sedéur,
19 Shelumieli mwana wa Surishadai aliongoza kikosi cha kabila la Simeoni,
et le corps d'armée de la Tribu des fils de Siméon, sous Selumiel, fils de Tsurisaddaï,
20 naye Eliasafu mwana wa Deueli aliongoza kikosi cha kabila la Gadi.
et le corps d'armée de la Tribu des fils de Gad, sous Eliasaph, fils de Deguel.
21 Kisha Wakohathi wakaondoka, wakichukua vitu vitakatifu. Maskani ilikuwa isimamishwe kabla wao hawajafika.
Puis partirent les Kahathites portant le Sanctuaire; et [les premiers] dressaient la Résidence en attendant leur arrivée.
22 Vikosi vya kambi ya Efraimu vilifuata, chini ya alama yao. Elishama mwana wa Amihudi alikuwa kiongozi wao.
Alors partit la bannière du camp des fils d'Ephraïm rangés par divisions, et leur corps d'armée était sous Elisamah, fils de Ammihud,
23 Gamalieli mwana wa Pedasuri aliongoza kikosi cha kabila la Manase,
et le corps d'armée de la Tribu des fils de Manassé, sous Gamliel, fils de Pedahtsur,
24 naye Abidani mwana wa Gideoni alikuwa kiongozi wa kikosi cha kabila la Benyamini.
et le corps d'armée de la Tribu des fils de Benjamin, sous Abidan, fils de Gidéoni.
25 Mwishowe, kama kikosi cha nyuma cha ulinzi wa vikosi vyote, vikosi vya kambi ya Dani viliondoka chini ya alama yao. Ahiezeri mwana wa Amishadai alikuwa kiongozi wao.
Ensuite partit la bannière du camp des fils de Dan fermant la marche de tous les campements et rangés par divisions, et leur corps d'armée était sous Ahiézer, fils de Aramisaëdaï,
26 Pagieli mwana wa Okrani aliongoza kikosi cha kabila la Asheri,
et le corps d'armée de la Tribu des fils d'Asser, sous Paghiel, fils de Hochram,
27 naye Ahira mwana wa Enani aliongoza kikosi cha kabila la Naftali.
et le corps d'armée de la Tribu des fils de Néphthali, sous Ahira, fils de Einan.
28 Huu ndio ulikuwa utaratibu wa kuondoka wa vikosi vya Waisraeli walipokuwa wanaondoka.
Tel fut l'ordre du décampement des enfants d'Israël selon leurs divisions, c'est ainsi qu'ils se mirent en marche.
29 Basi Mose akamwambia Hobabu mwana wa Reueli, Mmidiani, mkwewe Mose, “Tunaondoka kwenda mahali ambapo Bwana amesema ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’ Twende pamoja nasi tutakutendea mema, kwa maana Bwana ameahidi mambo mema kwa Israeli.”
Alors Moïse dit à Hobab, fils de Reguel, le Madianite, beau-père de Moïse: Nous marchons vers le lieu dont l'Éternel a dit: Je veux vous le donner; viens avec nous, et nous te ferons du bien; car l'Éternel a promis de faire du bien à Israël.
30 Akajibu, “Hapana, sitakwenda; nitarudi kwenye nchi yangu mwenyewe na watu wangu mwenyewe.”
Et il lui répondit: Je n'irai point; mais je veux regagner mon pays et ma patrie.
31 Lakini Mose akasema, “Tafadhali usituache. Wewe unajua mahali ambapo yatupasa kupiga kambi jangwani, nawe unaweza kuwa macho yetu.
Et Moïse reprit: Ne nous quitte donc pas, puisque en effet tu connais les lieux propres à nos campements dans le désert: sois donc notre œil.
32 Ikiwa utafuatana nasi, tutashirikiana nawe mema yoyote tutakayopewa na Bwana.”
Et si tu viens avec nous, et quand sera arrivé ce bien que l'Éternel veut nous faire, nous te ferons du bien.
33 Hivyo waliondoka kutoka mlima wa Bwana, nao wakasafiri kwa siku tatu. Sanduku la Agano la Bwana liliwatangulia kwa zile siku tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika.
Ils partirent ainsi de la montagne de l'Éternel, et firent trois journées de marche, et l'Arche de l'alliance de l'Éternel avait sur eux l'avance de trois journées de marche pour leur découvrir une station.
34 Wingu la Bwana lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka kambini.
Et la nuée de l'Éternel était au-dessus d'eux pendant le jour, lorsqu'ils partaient de leur campement.
35 Wakati wowote Sanduku lilipoondoka, Mose alisema, “Ee Bwana, inuka! Watesi wako na watawanyike; adui zako na wakimbie mbele zako.”
Et au départ de l'Arche Moïse disait: Lève-toi, Éternel! et que tes ennemis soient dissipés, et ceux qui te haïssent, mis en fuite devant toi.
36 Wakati wowote Sanduku liliposimama, alisema, “Ee Bwana, rudi, kwa maelfu ya Waisraeli wasiohesabika.”
Et quand elle s'arrêtait, il disait: Ramène, Éternel, les myriades des divisions d'Israël.

< Hesabu 10 >