< Hesabu 10 >
Puis l'Eternel parla à Moïse, en disant:
2 “Tengeneza tarumbeta mbili za fedha ya kufua, uzitumie kwa kuita jumuiya pamoja na wakati wa kuvunja makambi ili kuondoka.
Fais-toi deux trompettes d'argent, fais-les d'ouvrage battu au marteau; et elles te serviront pour convoquer l'assemblée, et pour faire partir les compagnies.
3 Tarumbeta zote mbili zikipigwa, jumuiya yote itakusanyika mbele yako katika ingilio la Hema la Kukutania.
Quand on en sonnera, toute l'assemblée s'assemblera vers toi à l'entrée du Tabernacle d'assignation.
4 Kama tarumbeta moja tu ikipigwa, viongozi, yaani wakuu wa koo za Israeli, ndio watakaokusanyika mbele yako.
Et quand on sonnera d'une seule, les principaux, qui sont les chefs des milliers d'Israël, s'assembleront vers toi.
5 Wakati mlio wa kujulisha hatari ukipigwa, makabila yaliyo na makambi upande wa mashariki yataondoka.
Mais quand vous sonnerez avec un retentissement bruyant, les compagnies qui sont campées vers l'Orient partiront.
6 Ukisikika mlio wa pili wa jinsi hiyo, walioko kwenye makambi ya kusini wataondoka. Mlio huo wa kujulisha hatari utakuwa ishara ya kuondoka.
Et quand vous sonnerez la seconde fois avec un retentissement bruyant, les compagnies qui sont campées vers le Midi partiront; on sonnera avec un retentissement bruyant, quand on voudra partir.
7 Ili kukusanya kusanyiko, piga tarumbeta zote, lakini siyo kwa mlio wa kujulisha hatari.
Et quand vous convoquerez l'assemblée, vous sonnerez, mais non point avec un retentissement bruyant.
8 “Wana wa Aroni, makuhani, ndio watakaopiga hizo tarumbeta. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu na kwa vizazi vijavyo.
Or les fils d'Aaron Sacrificateurs, sonneront des trompettes; et ceci vous sera une ordonnance perpétuelle en vos âges.
9 Wakati mtakapopigana vita katika nchi yenu wenyewe dhidi ya adui anayewaonea, piga tarumbeta kwa mlio wa kujulisha hatari. Ndipo utakumbukwa na Bwana Mungu wenu na kuokolewa kutoka kwa adui zenu.
Et quand vous marcherez en bataille dans votre pays contre votre ennemi, venant vous attaquer; vous sonnerez des trompettes avec un retentissement bruyant, et l'Eternel votre Dieu se souviendra de vous, et vous serez délivrés de vos ennemis.
10 Pia nyakati za furaha yenu, yaani sikukuu zenu zilizoamriwa na sikukuu za Mwezi Mwandamo, mtapiga tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za amani, nazo zitakuwa ukumbusho kwa ajili yenu mbele za Mungu wenu. Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.”
Aussi dans vos jours de joie, dans vos fêtes solennelles, et au commencement de vos mois, vous sonnerez des trompettes sur vos holocaustes, et sur vos sacrifices de prospérités, et elles vous serviront de mémorial devant votre Dieu; je [suis] l'Eternel, votre Dieu.
11 Katika siku ya ishirini ya mwezi wa pili wa mwaka wa pili, wingu liliinuka kutoka juu ya maskani ya Ushuhuda.
Or il arriva le vingtième jour du second mois de la seconde année, que la nuée se leva de dessus le pavillon du Témoignage.
12 Ndipo Waisraeli wakaondoka kutoka Jangwa la Sinai wakasafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine mpaka wingu lilipotua katika Jangwa la Parani.
Et les enfants d'Israël partirent selon leurs traittes, du désert de Sinaï, et la nuée se posa au désert de Paran.
13 Waliondoka kwa mara ya kwanza kwa agizo la Bwana kupitia kwa Mose.
Ils partirent donc pour la première fois, suivant le commandement de l'Eternel, déclaré par Moïse.
14 Vikosi vya kambi ya Yuda vilitangulia kwanza chini ya alama yao. Nashoni mwana wa Aminadabu alikuwa kiongozi wao.
Et la bannière des compagnies des enfants de Juda partit la première, selon leurs troupes; et Nahasson, fils de Hamminadab, conduisait la bande de Juda;
15 Nethaneli mwana wa Suari alikuwa kiongozi wa kabila la Isakari,
Et Nathanaël, fils de Tsuhar, conduisait la bande de la Tribu des enfants d'Issacar.
16 naye Eliabu mwana wa Heloni alikuwa kiongozi wa kabila la Zabuloni.
Et Eliab, fils de Hélon, conduisait la bande de la Tribu des enfants de Zabulon.
17 Ndipo Maskani iliposhushwa, nao wana wa Gershoni na wana wa Merari ambao waliibeba wakaondoka.
Et le pavillon fut désassemblé; puis les enfants de Guerson, et les enfants de Mérari, qui portaient le pavillon, partirent.
18 Vikosi vya kambi ya Reubeni vilifuata, chini ya alama yao. Elisuri mwana wa Shedeuri alikuwa kiongozi wao.
Puis la bannière des compagnies de Ruben partit, selon leurs troupes; et Elitsur, fils de Sédéur, conduisait la bande de Ruben.
19 Shelumieli mwana wa Surishadai aliongoza kikosi cha kabila la Simeoni,
Et Sélumiel, fils de Tsurisaddaï, conduisait la bande de la Tribu des enfants de Siméon.
20 naye Eliasafu mwana wa Deueli aliongoza kikosi cha kabila la Gadi.
Et Eliasaph, fils de Déhuël, conduisait la bande des enfants de Gad.
21 Kisha Wakohathi wakaondoka, wakichukua vitu vitakatifu. Maskani ilikuwa isimamishwe kabla wao hawajafika.
Alors les Kéhathites, qui portaient le Sanctuaire, partirent; cependant on dressait le Tabernacle, tandis que ceux-ci venaient.
22 Vikosi vya kambi ya Efraimu vilifuata, chini ya alama yao. Elishama mwana wa Amihudi alikuwa kiongozi wao.
Puis la bannière des compagnies des enfants d'Ephraïm partit, selon leurs troupes; et Elisamah, fils de Hammihud, conduisait la bande d'Ephraïm.
23 Gamalieli mwana wa Pedasuri aliongoza kikosi cha kabila la Manase,
Et Gamaliel, fils de Pédatsur, conduisait la bande de la Tribu des enfants de Manassé.
24 naye Abidani mwana wa Gideoni alikuwa kiongozi wa kikosi cha kabila la Benyamini.
Et Abidan, fils de Guidhoni, conduisait la bande de la Tribu des enfants de Benjamin.
25 Mwishowe, kama kikosi cha nyuma cha ulinzi wa vikosi vyote, vikosi vya kambi ya Dani viliondoka chini ya alama yao. Ahiezeri mwana wa Amishadai alikuwa kiongozi wao.
Enfin la bannière des compagnies des enfants de Dan, qui faisait l'arrière-garde, partit, selon leurs troupes; et Ahihézer, fils de Hammisaddaï, conduisait la bande de Dan.
26 Pagieli mwana wa Okrani aliongoza kikosi cha kabila la Asheri,
Et Paghiel, fils de Hocran, conduisait la bande de la Tribu des enfants d'Aser.
27 naye Ahira mwana wa Enani aliongoza kikosi cha kabila la Naftali.
Et Ahirah, fils de Hénan, conduisait la bande de la Tribu des enfants de Nephthali.
28 Huu ndio ulikuwa utaratibu wa kuondoka wa vikosi vya Waisraeli walipokuwa wanaondoka.
Tels étaient les décampements des enfants d'Israël selon leurs troupes, quand ils partaient.
29 Basi Mose akamwambia Hobabu mwana wa Reueli, Mmidiani, mkwewe Mose, “Tunaondoka kwenda mahali ambapo Bwana amesema ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’ Twende pamoja nasi tutakutendea mema, kwa maana Bwana ameahidi mambo mema kwa Israeli.”
Or Moïse dit à Hobab, fils de Réhuel Madianite, son beau-père: Nous allons au lieu duquel l'Eternel a dit, je vous le donnerai. Viens avec nous, et nous te ferons du bien; car l'Eternel a promis de faire du bien à Israël.
30 Akajibu, “Hapana, sitakwenda; nitarudi kwenye nchi yangu mwenyewe na watu wangu mwenyewe.”
Et Hobab lui répondit: Je n'y irai point, mais je m'en irai en mon pays, et vers ma parenté.
31 Lakini Mose akasema, “Tafadhali usituache. Wewe unajua mahali ambapo yatupasa kupiga kambi jangwani, nawe unaweza kuwa macho yetu.
Et Moïse lui dit: Je te prie, ne nous quitte point; car tu nous serviras de guide, parce que tu connais les lieux où nous aurons à camper dans le désert.
32 Ikiwa utafuatana nasi, tutashirikiana nawe mema yoyote tutakayopewa na Bwana.”
Et il arrivera que quand tu seras venu avec nous, et que le bien que l'Eternel nous doit faire sera arrivé, nous te ferons aussi du bien.
33 Hivyo waliondoka kutoka mlima wa Bwana, nao wakasafiri kwa siku tatu. Sanduku la Agano la Bwana liliwatangulia kwa zile siku tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika.
Ainsi ils partirent de la montagne de l'Eternel, [et ils marchèrent] le chemin de trois jours; et l'Arche de l'alliance de l'Eternel alla devant eux pendant le chemin de trois jours pour chercher un lieu où ils se reposassent.
34 Wingu la Bwana lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka kambini.
Et la nuée de l'Eternel était sur eux le jour, quand ils partaient du lieu où ils avaient campé.
35 Wakati wowote Sanduku lilipoondoka, Mose alisema, “Ee Bwana, inuka! Watesi wako na watawanyike; adui zako na wakimbie mbele zako.”
Or il arrivait qu'au départ de l'Arche, Moïse disait: Lève-toi, ô Eternel, et tes ennemis seront dispersés, et ceux qui te haïssent s'enfuiront de devant toi.
36 Wakati wowote Sanduku liliposimama, alisema, “Ee Bwana, rudi, kwa maelfu ya Waisraeli wasiohesabika.”
Et quand on la posait, il disait: Retourne, ô Eternel, aux dix mille milliers d'Israël.