< Hesabu 10 >

1 Bwana akamwambia Mose:
Yahvé parla à Moïse, et dit:
2 “Tengeneza tarumbeta mbili za fedha ya kufua, uzitumie kwa kuita jumuiya pamoja na wakati wa kuvunja makambi ili kuondoka.
« Fais deux trompettes d'argent. Tu les feras en travail battu. Tu t'en serviras pour appeler l'assemblée et pour la marche des camps.
3 Tarumbeta zote mbili zikipigwa, jumuiya yote itakusanyika mbele yako katika ingilio la Hema la Kukutania.
Lorsqu'on en soufflera, toute l'assemblée se rassemblera auprès de toi à l'entrée de la tente de la Rencontre.
4 Kama tarumbeta moja tu ikipigwa, viongozi, yaani wakuu wa koo za Israeli, ndio watakaokusanyika mbele yako.
Si l'on n'en fait retentir qu'une seule, les princes, les chefs des milliers d'Israël, se rassembleront auprès de toi.
5 Wakati mlio wa kujulisha hatari ukipigwa, makabila yaliyo na makambi upande wa mashariki yataondoka.
Lorsque tu sonneras l'alarme, les camps qui se trouvent à l'est avanceront.
6 Ukisikika mlio wa pili wa jinsi hiyo, walioko kwenye makambi ya kusini wataondoka. Mlio huo wa kujulisha hatari utakuwa ishara ya kuondoka.
Lorsque tu sonneras une seconde fois, les camps qui se trouvent au sud avanceront. Ils sonneront l'alarme pour leurs déplacements.
7 Ili kukusanya kusanyiko, piga tarumbeta zote, lakini siyo kwa mlio wa kujulisha hatari.
Mais quand l'assemblée se réunira, tu sonneras, mais tu ne sonneras pas.
8 “Wana wa Aroni, makuhani, ndio watakaopiga hizo tarumbeta. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu na kwa vizazi vijavyo.
« Les fils d'Aaron, les prêtres, sonneront des trompettes. Ce sera pour vous une loi à perpétuité, de génération en génération.
9 Wakati mtakapopigana vita katika nchi yenu wenyewe dhidi ya adui anayewaonea, piga tarumbeta kwa mlio wa kujulisha hatari. Ndipo utakumbukwa na Bwana Mungu wenu na kuokolewa kutoka kwa adui zenu.
Lorsque tu iras à la guerre dans ton pays contre l'adversaire qui t'opprime, tu sonneras des trompettes. Alors on se souviendra de toi devant Yahvé ton Dieu, et tu seras sauvé de tes ennemis.
10 Pia nyakati za furaha yenu, yaani sikukuu zenu zilizoamriwa na sikukuu za Mwezi Mwandamo, mtapiga tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za amani, nazo zitakuwa ukumbusho kwa ajili yenu mbele za Mungu wenu. Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.”
« Au jour de ta joie, à tes fêtes et aux débuts de tes mois, tu sonneras des trompettes sur tes holocaustes et sur les sacrifices d'actions de grâces, et ils seront pour toi un mémorial devant ton Dieu. Je suis Yahvé ton Dieu. »
11 Katika siku ya ishirini ya mwezi wa pili wa mwaka wa pili, wingu liliinuka kutoka juu ya maskani ya Ushuhuda.
La deuxième année, au deuxième mois, le vingtième jour du mois, la nuée se retira de dessus le tabernacle de l'alliance.
12 Ndipo Waisraeli wakaondoka kutoka Jangwa la Sinai wakasafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine mpaka wingu lilipotua katika Jangwa la Parani.
Les enfants d'Israël partirent du désert du Sinaï, et la nuée resta dans le désert de Paran.
13 Waliondoka kwa mara ya kwanza kwa agizo la Bwana kupitia kwa Mose.
Ils s'avancèrent d'abord selon le commandement de Yahvé par Moïse.
14 Vikosi vya kambi ya Yuda vilitangulia kwanza chini ya alama yao. Nashoni mwana wa Aminadabu alikuwa kiongozi wao.
D'abord, l'étendard du camp des fils de Juda s'avança selon leurs armées. Nachshon, fils d'Amminadab, était à la tête de son armée.
15 Nethaneli mwana wa Suari alikuwa kiongozi wa kabila la Isakari,
Nethaneel, fils de Zuar, était à la tête de l'armée de la tribu des fils d'Issacar.
16 naye Eliabu mwana wa Heloni alikuwa kiongozi wa kabila la Zabuloni.
Eliab, fils de Hélon, était à la tête de l'armée de la tribu des fils de Zabulon.
17 Ndipo Maskani iliposhushwa, nao wana wa Gershoni na wana wa Merari ambao waliibeba wakaondoka.
Le tabernacle fut démonté; les fils de Gershon et les fils de Merari, qui portaient le tabernacle, partirent en avant.
18 Vikosi vya kambi ya Reubeni vilifuata, chini ya alama yao. Elisuri mwana wa Shedeuri alikuwa kiongozi wao.
La bannière du camp de Ruben s'avança, selon leurs armées. Elizur, fils de Shedeur, était à la tête de son armée.
19 Shelumieli mwana wa Surishadai aliongoza kikosi cha kabila la Simeoni,
Shelumiel, fils de Zurishaddai, commandait l'armée de la tribu des fils de Siméon.
20 naye Eliasafu mwana wa Deueli aliongoza kikosi cha kabila la Gadi.
Eliasaph, fils de Deuel, était à la tête de l'armée de la tribu des fils de Gad.
21 Kisha Wakohathi wakaondoka, wakichukua vitu vitakatifu. Maskani ilikuwa isimamishwe kabla wao hawajafika.
Les Kehathites s'avancèrent, portant le sanctuaire. Les autres ont monté le tabernacle avant leur arrivée.
22 Vikosi vya kambi ya Efraimu vilifuata, chini ya alama yao. Elishama mwana wa Amihudi alikuwa kiongozi wao.
L'étendard du camp des fils d'Éphraïm s'avançait selon leurs armées. Élischama, fils d'Ammihud, était à la tête de son armée.
23 Gamalieli mwana wa Pedasuri aliongoza kikosi cha kabila la Manase,
Gamaliel, fils de Pedahzur, était à la tête de l'armée de la tribu des fils de Manassé.
24 naye Abidani mwana wa Gideoni alikuwa kiongozi wa kikosi cha kabila la Benyamini.
Abidan, fils de Gideoni, était à la tête de l'armée de la tribu des fils de Benjamin.
25 Mwishowe, kama kikosi cha nyuma cha ulinzi wa vikosi vyote, vikosi vya kambi ya Dani viliondoka chini ya alama yao. Ahiezeri mwana wa Amishadai alikuwa kiongozi wao.
L'étendard du camp des fils de Dan, qui était l'arrière-garde de tous les camps, se mit en marche selon leurs armées. Ahiezer, fils d'Ammishaddai, était à la tête de son armée.
26 Pagieli mwana wa Okrani aliongoza kikosi cha kabila la Asheri,
Pagiel, fils d'Ochran, commandait l'armée de la tribu des fils d'Aser.
27 naye Ahira mwana wa Enani aliongoza kikosi cha kabila la Naftali.
Ahira, fils d'Enan, était à la tête de l'armée de la tribu des fils de Nephtali.
28 Huu ndio ulikuwa utaratibu wa kuondoka wa vikosi vya Waisraeli walipokuwa wanaondoka.
Tels furent les déplacements des enfants d'Israël, selon leurs armées, et ils partirent.
29 Basi Mose akamwambia Hobabu mwana wa Reueli, Mmidiani, mkwewe Mose, “Tunaondoka kwenda mahali ambapo Bwana amesema ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’ Twende pamoja nasi tutakutendea mema, kwa maana Bwana ameahidi mambo mema kwa Israeli.”
Moïse dit à Hobab, fils de Réuel, le Madianite, beau-père de Moïse: « Nous sommes en route pour le lieu dont Yahvé a dit: « Je te le donnerai ». Viens avec nous, et nous te traiterons bien, car Yahvé a dit du bien d'Israël. »
30 Akajibu, “Hapana, sitakwenda; nitarudi kwenye nchi yangu mwenyewe na watu wangu mwenyewe.”
Il lui dit: « Je n'irai pas, mais je m'en irai dans mon pays et dans ma famille. »
31 Lakini Mose akasema, “Tafadhali usituache. Wewe unajua mahali ambapo yatupasa kupiga kambi jangwani, nawe unaweza kuwa macho yetu.
Moïse dit: « Ne nous quitte pas, je t'en prie, car tu sais comment nous devons camper dans le désert, et tu peux être nos yeux.
32 Ikiwa utafuatana nasi, tutashirikiana nawe mema yoyote tutakayopewa na Bwana.”
Il en sera, si tu pars avec nous - oui, il en sera ainsi - que tout le bien que Yahvé nous fera, nous vous en ferons autant. »
33 Hivyo waliondoka kutoka mlima wa Bwana, nao wakasafiri kwa siku tatu. Sanduku la Agano la Bwana liliwatangulia kwa zile siku tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika.
Ils partirent de la montagne de Yahvé pour trois jours de marche. L'arche de l'alliance de l'Éternel les précéda de trois jours de marche, pour leur chercher un lieu de repos.
34 Wingu la Bwana lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka kambini.
La nuée de l'Éternel était sur eux pendant le jour, lorsqu'ils quittèrent le camp.
35 Wakati wowote Sanduku lilipoondoka, Mose alisema, “Ee Bwana, inuka! Watesi wako na watawanyike; adui zako na wakimbie mbele zako.”
Lorsque l'arche s'avança, Moïse dit: « Lève-toi, Yahvé, et que tes ennemis soient dispersés! Que ceux qui te haïssent fuient devant toi! »
36 Wakati wowote Sanduku liliposimama, alisema, “Ee Bwana, rudi, kwa maelfu ya Waisraeli wasiohesabika.”
Quand elle s'est reposée, il a dit: « Reviens, Yahvé, vers les dix mille des milliers d'Israël. »

< Hesabu 10 >