< Hesabu 10 >

1 Bwana akamwambia Mose:
HERREN talede fremdeles til Moses og sagde:
2 “Tengeneza tarumbeta mbili za fedha ya kufua, uzitumie kwa kuita jumuiya pamoja na wakati wa kuvunja makambi ili kuondoka.
Du skal lave dig to Sølvtrompeter; i drevet Arbejde skal du lave dem. Dem skal du bruge, når Menigheden skal kaldes sammen, og når Lejrene skal bryde op.
3 Tarumbeta zote mbili zikipigwa, jumuiya yote itakusanyika mbele yako katika ingilio la Hema la Kukutania.
Når der blæses i dem begge to, skal hele Menigheden samle sig hos dig ved Indgangen til Åbenbaringsteltet.
4 Kama tarumbeta moja tu ikipigwa, viongozi, yaani wakuu wa koo za Israeli, ndio watakaokusanyika mbele yako.
Blæses der kun i den ene, skal Øversterne, Overhovederne for Israels Stammer, samle sig hos dig.
5 Wakati mlio wa kujulisha hatari ukipigwa, makabila yaliyo na makambi upande wa mashariki yataondoka.
Når I blæser Alarm med dem, skal Lejrene på Østsiden bryde op;
6 Ukisikika mlio wa pili wa jinsi hiyo, walioko kwenye makambi ya kusini wataondoka. Mlio huo wa kujulisha hatari utakuwa ishara ya kuondoka.
blæser Alarm anden Gang, skal Lejrene på Sydsiden bryde op: tredje Gang skal Lejrene mod Vest bryde op, fjerde Gang Lejrene mod Nord; der skal blæses Alarm, når de skal bryde op.
7 Ili kukusanya kusanyiko, piga tarumbeta zote, lakini siyo kwa mlio wa kujulisha hatari.
Men når Forsamlingen skal sammenkaldes skal I blæse på almindelig Vis, ikke Alarm.
8 “Wana wa Aroni, makuhani, ndio watakaopiga hizo tarumbeta. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu na kwa vizazi vijavyo.
Arons Sønner, Præsterne, skal blæse i Trompeterne; det skal være eder en evig gyldig Anordning fra Slægt til Slægt.
9 Wakati mtakapopigana vita katika nchi yenu wenyewe dhidi ya adui anayewaonea, piga tarumbeta kwa mlio wa kujulisha hatari. Ndipo utakumbukwa na Bwana Mungu wenu na kuokolewa kutoka kwa adui zenu.
Når I drager i Krig i eders Land mod en Fjende, der angriber eder, og blæser Alarm med Trompeterne, skal I ihukommes for HERREN eders Guds Åsyn og frelses fra eders Fjender.
10 Pia nyakati za furaha yenu, yaani sikukuu zenu zilizoamriwa na sikukuu za Mwezi Mwandamo, mtapiga tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za amani, nazo zitakuwa ukumbusho kwa ajili yenu mbele za Mungu wenu. Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.”
Og på eders Glædesdage, eders Højtider og Nymånedage, skal I blæse i Trompeterne ved eders Brændofre og Takofre; så skal de tjene eder til Ihukommelse for eders Guds Åsyn. Jeg er HERREN eders Gud!
11 Katika siku ya ishirini ya mwezi wa pili wa mwaka wa pili, wingu liliinuka kutoka juu ya maskani ya Ushuhuda.
Den tyvende Dag i den anden Måned af det andet År løftede Skyen sig fra Vidnesbyrdets Bolig.
12 Ndipo Waisraeli wakaondoka kutoka Jangwa la Sinai wakasafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine mpaka wingu lilipotua katika Jangwa la Parani.
Da brød Israeliterne op fra Sinaj Ørken, i den Orden de skulde bryde op i, og Skyen stod stille i Parans Ørken.
13 Waliondoka kwa mara ya kwanza kwa agizo la Bwana kupitia kwa Mose.
Da de nu første Gang brød op efter Guds Bud ved Moses,
14 Vikosi vya kambi ya Yuda vilitangulia kwanza chini ya alama yao. Nashoni mwana wa Aminadabu alikuwa kiongozi wao.
var Judæernes Lejr den første, der brød op under sit Felttegn, Hærafdeling for Hærafdeling; deres Hær førtes af Nahasjon, Amminadabs Søn.
15 Nethaneli mwana wa Suari alikuwa kiongozi wa kabila la Isakari,
Issakariternes Stammes Hær førtes af Netanel, Zuars Søn,
16 naye Eliabu mwana wa Heloni alikuwa kiongozi wa kabila la Zabuloni.
og Zebuloniternes Stammes Hær af Eliab, Helons Søn.
17 Ndipo Maskani iliposhushwa, nao wana wa Gershoni na wana wa Merari ambao waliibeba wakaondoka.
Da derpå Boligen var taget ned, brød Gersoniterne og Merariterne op og bar Boligen.
18 Vikosi vya kambi ya Reubeni vilifuata, chini ya alama yao. Elisuri mwana wa Shedeuri alikuwa kiongozi wao.
Så brød Rubens Lejr op under sit Felttegn, Hærafdeling for Hærafdeling; deres Hær førtes af Elizur, Sjedeurs Søn.
19 Shelumieli mwana wa Surishadai aliongoza kikosi cha kabila la Simeoni,
Simeoniternes Stammes Hær førtes af Sjelumiel, Zurisjaddajs Søn,
20 naye Eliasafu mwana wa Deueli aliongoza kikosi cha kabila la Gadi.
og Gaditernes Stammes Hær af Eljasaf, Deuels Søn.
21 Kisha Wakohathi wakaondoka, wakichukua vitu vitakatifu. Maskani ilikuwa isimamishwe kabla wao hawajafika.
Så brød Kehatiterne, der bar de hellige Ting, op; og før deres Komme havde man rejst Boligen.
22 Vikosi vya kambi ya Efraimu vilifuata, chini ya alama yao. Elishama mwana wa Amihudi alikuwa kiongozi wao.
Så brød Efraimiternes Lejr op under sit Felttegn, Hærafdeling for Hærafdeling; deres Hær førtes af Elisjema, Ammihuds Søn.
23 Gamalieli mwana wa Pedasuri aliongoza kikosi cha kabila la Manase,
Manassiternes Stammes Hær førtes af Gamliel, Pedazurs Søn,
24 naye Abidani mwana wa Gideoni alikuwa kiongozi wa kikosi cha kabila la Benyamini.
og Benjaminiternes Stammes Hær af Abidan, Gidonis Søn.
25 Mwishowe, kama kikosi cha nyuma cha ulinzi wa vikosi vyote, vikosi vya kambi ya Dani viliondoka chini ya alama yao. Ahiezeri mwana wa Amishadai alikuwa kiongozi wao.
Så brød Daniternes Lejr op under sit Felttegn som Bagtrop i hele Lejrtoget, Hærafdeling for Hærafdeling; deres Hær førtes af Ahiezer, Ammisjaddajs Søn.
26 Pagieli mwana wa Okrani aliongoza kikosi cha kabila la Asheri,
Aseriternes Stammes Hær førtes af Pagiel, Okrans Søn,
27 naye Ahira mwana wa Enani aliongoza kikosi cha kabila la Naftali.
og Naftalitemes Stammes Hær af Ahira, Enans Søn.
28 Huu ndio ulikuwa utaratibu wa kuondoka wa vikosi vya Waisraeli walipokuwa wanaondoka.
Således foregik Israelitternes Opbrud, Hærafdeling for Hærafdeling. Så brød de da op.
29 Basi Mose akamwambia Hobabu mwana wa Reueli, Mmidiani, mkwewe Mose, “Tunaondoka kwenda mahali ambapo Bwana amesema ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’ Twende pamoja nasi tutakutendea mema, kwa maana Bwana ameahidi mambo mema kwa Israeli.”
Men Moses sagde til Midjaniten Hobab, Reuels Søn, Moses's Svigerfader: "Vi bryder nu op for at drage til det Sted, HERREN har lovet at give os; drag med os! Vi skal lønne dig godt, thi HERREN har stillet Israel gode Ting i Udsigt."
30 Akajibu, “Hapana, sitakwenda; nitarudi kwenye nchi yangu mwenyewe na watu wangu mwenyewe.”
Men han svarede ham: "Jeg vil ikke drage med; nej, jeg drager til mit Land og min Slægt."
31 Lakini Mose akasema, “Tafadhali usituache. Wewe unajua mahali ambapo yatupasa kupiga kambi jangwani, nawe unaweza kuwa macho yetu.
Da sagde han: "Forlad os ikke! Du kender jo de Steder, hvor vi kan slå Lejr i Ørkenen; vær Øje for os!
32 Ikiwa utafuatana nasi, tutashirikiana nawe mema yoyote tutakayopewa na Bwana.”
Drager du med os, skal vi give dig Del i alt det gode, HERREN vil give os."
33 Hivyo waliondoka kutoka mlima wa Bwana, nao wakasafiri kwa siku tatu. Sanduku la Agano la Bwana liliwatangulia kwa zile siku tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika.
Derpå brød de op fra HERRENs Bjerg og vandrede tre Dagsrejser frem, idet HERRENs Pagts Ark drog i Forvejen for at søge dem et Sted, hvor de kunde holde Hvil.
34 Wingu la Bwana lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka kambini.
Og HERRENs Sky svævede over dem om Dagen, når de brød op fra Lejren.
35 Wakati wowote Sanduku lilipoondoka, Mose alisema, “Ee Bwana, inuka! Watesi wako na watawanyike; adui zako na wakimbie mbele zako.”
Og hver Gang Arken brød op, sagde Moses: "Stå op, HERRE, at dine Fjender må splittes og dine Avindsmænd fly for dit Åsyn!"
36 Wakati wowote Sanduku liliposimama, alisema, “Ee Bwana, rudi, kwa maelfu ya Waisraeli wasiohesabika.”
Og hver Gang den standsede, sagde han: "Vend tilbage, HERRE, til Israels Stammers Titusinder!"

< Hesabu 10 >