< Hesabu 10 >

1 Bwana akamwambia Mose:
上主訓示梅瑟說:「
2 “Tengeneza tarumbeta mbili za fedha ya kufua, uzitumie kwa kuita jumuiya pamoja na wakati wa kuvunja makambi ili kuondoka.
你要製造兩個喇叭,用銀打成,用為召集會眾,為遷疑營幕。
3 Tarumbeta zote mbili zikipigwa, jumuiya yote itakusanyika mbele yako katika ingilio la Hema la Kukutania.
幾時吹兩個喇叭,全會眾都應集合在會幕門口,來到你跟前。
4 Kama tarumbeta moja tu ikipigwa, viongozi, yaani wakuu wa koo za Israeli, ndio watakaokusanyika mbele yako.
若只吹一個喇叭,以色列的千夫長,作首領的應集合到你跟前。
5 Wakati mlio wa kujulisha hatari ukipigwa, makabila yaliyo na makambi upande wa mashariki yataondoka.
若吹緊急號,紮在東方的營就起程;
6 Ukisikika mlio wa pili wa jinsi hiyo, walioko kwenye makambi ya kusini wataondoka. Mlio huo wa kujulisha hatari utakuwa ishara ya kuondoka.
第二次吹緊急號時,紮在南方的營就起程:吹緊急號是為叫他們起程;
7 Ili kukusanya kusanyiko, piga tarumbeta zote, lakini siyo kwa mlio wa kujulisha hatari.
但為召集會眾,只吹號,不應緊急吹。
8 “Wana wa Aroni, makuhani, ndio watakaopiga hizo tarumbeta. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu na kwa vizazi vijavyo.
亞郎的子孫作司祭的應吹號:這為你們世世代代是條永久的規定。
9 Wakati mtakapopigana vita katika nchi yenu wenyewe dhidi ya adui anayewaonea, piga tarumbeta kwa mlio wa kujulisha hatari. Ndipo utakumbukwa na Bwana Mungu wenu na kuokolewa kutoka kwa adui zenu.
幾時你們在本國要出去作戰,攻打來侵的仇敵,應吹緊急號,使上主你們的天主,記得你們,救你們脫離仇敵。
10 Pia nyakati za furaha yenu, yaani sikukuu zenu zilizoamriwa na sikukuu za Mwezi Mwandamo, mtapiga tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za amani, nazo zitakuwa ukumbusho kwa ajili yenu mbele za Mungu wenu. Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.”
此外,在你們的慶日、節日、月朔之日,獻全燔祭及和平祭時,還應吹號,使你們的天主記得你們:我是上主,你們的天主。」
11 Katika siku ya ishirini ya mwezi wa pili wa mwaka wa pili, wingu liliinuka kutoka juu ya maskani ya Ushuhuda.
第二年二月二十日,雲彩由會幕升起,
12 Ndipo Waisraeli wakaondoka kutoka Jangwa la Sinai wakasafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine mpaka wingu lilipotua katika Jangwa la Parani.
以色列子民就從西乃曠野循序起程出發。以後雲採在帕蘭曠野停住了。
13 Waliondoka kwa mara ya kwanza kwa agizo la Bwana kupitia kwa Mose.
他們初次依照上主藉梅瑟所出的命令起程。
14 Vikosi vya kambi ya Yuda vilitangulia kwanza chini ya alama yao. Nashoni mwana wa Aminadabu alikuwa kiongozi wao.
首先依隊起程的,是猶大子孫的營旗,率領軍隊的,是阿米納達布的兒子納赫雄;
15 Nethaneli mwana wa Suari alikuwa kiongozi wa kabila la Isakari,
率領依撒加爾子孫支派軍隊的,是族阿爾的兒子乃塔乃耳;
16 naye Eliabu mwana wa Heloni alikuwa kiongozi wa kabila la Zabuloni.
率領則步隆子孫支派軍隊的,是厄隆的兒子厄里雅布。
17 Ndipo Maskani iliposhushwa, nao wana wa Gershoni na wana wa Merari ambao waliibeba wakaondoka.
拆下帳幕後,革爾雄的子孫和默辣黎的子孫,就抬著帳幕起程出發。
18 Vikosi vya kambi ya Reubeni vilifuata, chini ya alama yao. Elisuri mwana wa Shedeuri alikuwa kiongozi wao.
以後依隊出發的,是勒烏本的營旗,率領軍隊的是,舍德烏爾的兒子厄里族爾;
19 Shelumieli mwana wa Surishadai aliongoza kikosi cha kabila la Simeoni,
率領西默盎子孫支派軍隊的,是族黎沙待的兒子舍路米耳;
20 naye Eliasafu mwana wa Deueli aliongoza kikosi cha kabila la Gadi.
率領加得子孫支派軍隊的,是勒烏耳的兒子厄里亞撒夫。
21 Kisha Wakohathi wakaondoka, wakichukua vitu vitakatifu. Maskani ilikuwa isimamishwe kabla wao hawajafika.
此後刻哈特人抬著聖所之物起程;當他們達到時,人應已豎起帳幕。
22 Vikosi vya kambi ya Efraimu vilifuata, chini ya alama yao. Elishama mwana wa Amihudi alikuwa kiongozi wao.
以後依隊出發的,是厄弗辣因子孫的營旗,率領軍隊的,是阿米胡得的兒子厄里沙瑪;
23 Gamalieli mwana wa Pedasuri aliongoza kikosi cha kabila la Manase,
率領默納協子孫支派軍隊的,是培達族爾的兒子加默里耳;
24 naye Abidani mwana wa Gideoni alikuwa kiongozi wa kikosi cha kabila la Benyamini.
率領本雅明子孫支派軍隊的,是基德敖尼的兒子阿彼丹。
25 Mwishowe, kama kikosi cha nyuma cha ulinzi wa vikosi vyote, vikosi vya kambi ya Dani viliondoka chini ya alama yao. Ahiezeri mwana wa Amishadai alikuwa kiongozi wao.
以後依隊出發的,是作全營後衛的丹子孫的營旗,率領軍隊的,是阿米沙待的兒子阿希厄則爾;
26 Pagieli mwana wa Okrani aliongoza kikosi cha kabila la Asheri,
率領阿協爾子孫支派軍隊的,是敖革蘭的兒子帕革厄耳;
27 naye Ahira mwana wa Enani aliongoza kikosi cha kabila la Naftali.
率領納斐塔里子孫支派軍隊的,是厄南的兒子阿希辣。
28 Huu ndio ulikuwa utaratibu wa kuondoka wa vikosi vya Waisraeli walipokuwa wanaondoka.
這是以色列子民出發時,依隊起程的次序。
29 Basi Mose akamwambia Hobabu mwana wa Reueli, Mmidiani, mkwewe Mose, “Tunaondoka kwenda mahali ambapo Bwana amesema ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’ Twende pamoja nasi tutakutendea mema, kwa maana Bwana ameahidi mambo mema kwa Israeli.”
梅瑟對自己的岳父,米德楊人勒烏耳的兒子曷巴布說:「我們正要起程往上主曾說:「我要給你們的那地方」去;你同我們一起去罷! 我們必要好待你,因為上主對以色列許下了幸福。」
30 Akajibu, “Hapana, sitakwenda; nitarudi kwenye nchi yangu mwenyewe na watu wangu mwenyewe.”
曷巴布回答他說:「我不去,我要回到故鄉我的老家去。」
31 Lakini Mose akasema, “Tafadhali usituache. Wewe unajua mahali ambapo yatupasa kupiga kambi jangwani, nawe unaweza kuwa macho yetu.
梅瑟說請你不要離開我們! 因為你知道我們在曠野安營的地方,你要給我們當響導。
32 Ikiwa utafuatana nasi, tutashirikiana nawe mema yoyote tutakayopewa na Bwana.”
你若同我們一起去,我們必使你分享上主要賜給我們的幸福。」
33 Hivyo waliondoka kutoka mlima wa Bwana, nao wakasafiri kwa siku tatu. Sanduku la Agano la Bwana liliwatangulia kwa zile siku tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika.
他們就由上主的山起程出發,行了三天的路程;三天的路程中,上主的約櫃走在他們的前面,為他們尋求休息的地方。
34 Wingu la Bwana lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka kambini.
白天他們移營前行時,上主的雲彩常在他們頭上。
35 Wakati wowote Sanduku lilipoondoka, Mose alisema, “Ee Bwana, inuka! Watesi wako na watawanyike; adui zako na wakimbie mbele zako.”
當約櫃起行時,梅瑟就說:「上主,請你起來,使你的仇敵潰散,使懷恨你的由你面前逃走。」
36 Wakati wowote Sanduku liliposimama, alisema, “Ee Bwana, rudi, kwa maelfu ya Waisraeli wasiohesabika.”
在約櫃停留時,他就說:「上主,請歸來,住在以色列千家萬戶中。」

< Hesabu 10 >