< Hesabu 1 >
1 Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
L'Éternel parla à Moïse, au désert de Sinaï, dans le tabernacle d'assignation, au premier jour du second mois, la seconde année de leur sortie du pays d'Égypte, en disant:
2 “Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
Faites le compte de toute l'assemblée des enfants d'Israël, selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, en comptant par tête les noms de tous les mâles,
3 Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
Depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux d'Israël qui peuvent aller à la guerre; vous les dénombrerez selon leurs armées, toi et Aaron.
4 Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
Et il y aura avec vous un homme par tribu, le chef de la maison de ses pères.
5 Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
Et voici les noms des hommes qui vous assisteront: Pour la tribu de Ruben, Elitsur, fils de Shedéur;
6 kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
Pour celle de Siméon, Shelumiel, fils de Tsurishaddaï;
7 kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
Pour celle de Juda, Nahasshon, fils d'Amminadab;
8 kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
Pour celle d'Issacar, Nathanaël, fils de Tsuar;
9 kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
Pour celle de Zabulon, Eliab, fils de Hélon;
10 kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
Pour les enfants de Joseph, pour la tribu d'Éphraïm, Elishama, fils d'Ammihud; pour celle de Manassé, Gamaliel, fils de Pédahtsur;
11 kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
Pour la tribu de Benjamin, Abidan, fils de Guideoni;
12 kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
Pour celle de Dan, Ahiézer, fils d'Ammishaddaï;
13 kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
Pour celle d'Asser, Paguiel, fils d'Ocran;
14 kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
Pour celle de Gad, Eliasaph, fils de Déhuël;
15 kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
Pour celle de Nephthali, Ahira, fils d'Enan.
16 Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
C'étaient là ceux qu'on appelait pour tenir l'assemblée, les princes des tribus de leurs pères, les chefs des milliers d'Israël.
17 Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
Moïse et Aaron prirent donc ces hommes qui avaient été désignés par leurs noms;
18 wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
Et ils convoquèrent toute l'assemblée, le premier jour du second mois, et on les enregistra d'après leurs familles, selon la maison de leurs pères, en les comptant par leurs noms, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, et par têtes;
19 kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
Comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse, il les dénombra au désert de Sinaï.
20 Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Les fils de Ruben, premier-né d'Israël, enregistrés selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, en les comptant par leurs noms et par tête, tous les mâles depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre:
21 Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
Ceux de la tribu de Ruben, qui furent dénombrés, furent quarante-six mille cinq cents.
22 Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Les fils de Siméon, enregistrés selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, ceux qui furent dénombrés, en les comptant par leurs noms et par tête, tous les mâles depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre:
23 Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
Ceux de la tribu de Siméon, qui furent dénombrés, furent cinquante-neuf mille trois cents.
24 Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Les fils de Gad, enregistrés selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, en les comptant par leurs noms, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre:
25 Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
Ceux de la tribu de Gad, qui furent dénombrés, furent quarante-cinq mille six cent cinquante.
26 Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Les fils de Juda, enregistrés selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, en les comptant par leurs noms, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre:
27 Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
Ceux de la tribu de Juda, qui furent dénombrés, furent soixante-quatorze mille six cents.
28 Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Les fils d'Issacar, enregistrés selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, en les comptant par leurs noms, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre:
29 Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
Ceux de la tribu d'Issacar, qui furent dénombrés, furent cinquante-quatre mille quatre cents.
30 Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Les fils de Zabulon, enregistrés selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, en les comptant par leurs noms, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre:
31 Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
Ceux de la tribu de Zabulon, qui furent dénombrés, furent cinquante-sept mille quatre cents.
32 Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Quant aux fils de Joseph: les fils d'Éphraïm, enregistrés selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, en les comptant par leurs noms, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre:
33 Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
Ceux de la tribu d'Éphraïm, qui furent dénombrés, furent quarante mille cinq cents.
34 Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Les fils de Manassé, enregistrés selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, en les comptant par leurs noms, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre:
35 Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
Ceux de la tribu de Manassé, qui furent dénombrés, furent trente-deux mille deux cents.
36 Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Les fils de Benjamin, enregistrés selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, en les comptant par leurs noms, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre:
37 Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
Ceux de la tribu de Benjamin, qui furent dénombrés, furent trente-cinq mille quatre cents.
38 Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Les fils de Dan, enregistrés selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, en les comptant par leurs noms, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre:
39 Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
Ceux de la tribu de Dan, qui furent dénombrés, furent soixante-deux mille sept cents.
40 Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Les fils d'Asser, enregistrés selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, en les comptant par leurs noms, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre:
41 Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
Ceux de la tribu d'Asser, qui furent dénombrés, furent quarante et un mille cinq cents.
42 Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Les fils de Nephthali, enregistrés selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, en les comptant par leurs noms, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à la guerre:
43 Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
Ceux de la tribu de Nephthali, qui furent dénombrés, furent cinquante-trois mille quatre cents.
44 Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
Tel est le dénombrement que firent Moïse et Aaron, et les douze princes d'Israël; il y avait un homme pour chaque maison des pères.
45 Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
Ainsi tous ceux des enfants d'Israël qui furent dénombrés, selon les maisons de leurs pères, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, tous les Israélites qui pouvaient aller à la guerre,
46 Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
Tous ceux qui furent dénombrés, furent six cent trois mille cinq cent cinquante.
47 Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
Mais les Lévites, selon la tribu de leurs pères, ne furent point dénombrés avec eux.
48 Bwana alikuwa amemwambia Mose:
Car l'Éternel avait parlé à Moïse, en disant:
49 “Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
Tu ne dénombreras point la tribu de Lévi seulement, et tu n'en feras point le compte au milieu des enfants d'Israël;
50 Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
Mais donne aux Lévites la charge de la Demeure du Témoignage, et de tous ses ustensiles, et de tout ce qui lui appartient. Ce sont eux qui porteront la Demeure et tous ses ustensiles, et qui en feront le service; et ils camperont autour de la Demeure.
51 Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
Et quand la Demeure partira, les Lévites la démonteront; et quand la Demeure campera, les Lévites la dresseront; et l'étranger qui en approchera sera puni de mort.
52 Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
Or, les enfants d'Israël camperont chacun dans son camp, et chacun près de sa bannière, selon leurs armées.
53 Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
Mais les Lévites camperont autour de la Demeure du Témoignage, afin qu'il n'y ait point d'indignation contre l'assemblée des enfants d'Israël; et les Lévites auront la garde de la Demeure du Témoignage.
54 Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.
Et les enfants d'Israël firent tout ce que l'Éternel avait commandé à Moïse; ils firent ainsi.